WATOTO MAPACHA
sehemu ya 15
Celena aliendelea kulala huku amepakatwa na mama yake Stefano ,tena Cha ajabu aliuchapa usingizi kabisa ,
Sasa kumbuka mama Celena bado alikuwa anamtafuta yule mama kichaa , Nia yake amwangalie Kama bado kichaa anacho au amekaribia kupona , maana Kama anaweza kukumbuka vitu inamaana anakaribia kupona , Sasa akawa anauliza uliza mpaka akaelekezwa anapopatikana , akaja mpaka kwenye mtaa huo ,kumbe mtaa huo ndio anaokaa , mama Stefano na tena yupo nje kwenye kibaraza amempakata Celena , mama Celena yeye alikuwa kwenye gari huku akiangalia huku na kule Kama atamuona yule mama kichaa gafra akaona Kuna mama amekaa kibarazani ,na kampakata mtoto, alipomuangalia vzr mtoto mwenyewe akagundua ni Celena,
" He huyu si ni Celena huyu , au ndio yule mtoto aliefanana na Celena ,"?
Alijiuliza maswali Sasa kumbuka gari ya mama Celena inatinted yaani sio rahis wa nje amuone wa ndani lakin wa ndani anamuona wa nje , mama Stefano yeye alikuwa anaangalia tu ile gar nakuishangaa maana ilipaki mbele ya nyumba yake na dereva hata hatelemki ,
Sasa ule mlio wa gari ukamstua Celena na alipoamka akaliona gari la mama yake , akamwambia mama Stefano " huyo aliesimamisha gari ni mama yangu , " mama Stefano akashangaa , "ni mama yako kivipi ,"?
Mama Stefano alimuuliza Celena ,
" Ni mama yangu mzazi ,"
Sasa wakati wanaongea mama Celena hakuwasikia maana alikuwa ndani ya gari , lakin alikuwa anawaona , Sasa kosa alilofanya mama Celena akaona ngoja aende shule kwa kina Celena ,halafu amchukue Celena aje nae mpaka hapa kwa kwa kina Stefano ,ili awakutanishe na huyu mtoto anaefanana na mwanae, na amuulize mama Stefano kuwa kwanini Hawa watoto wamefanana kiasi hiki au Kama ni mapacha ajue ni wanani Kama ni wakwake au ni wanani ,"?
Akaondoka haraka eneo Hilo ,
Celena akamwambia mama Stefano kuwa mama yake atakuwa amemuona na hapo anakwenda shuleni kwao ,ili kuhakikisha Kama yupo ,
Celena akanyanyuka upesi upesi akaenda ndani na kuvaa nguo zake za shule na akamuaga mama Stefano kuwa anaondoka zake kurudi nyumbani maana mama yake akimkosa shule lazima atakuja nyumbani kumuangalia ,
Sasa huku shuleni kwa kina Celena, kumbe Celina alikuja hapo shuleni ili aonane na Celena , na ukumbuke Celena hajaenda shule alienda kule kwa kina Stefano ili asubilie Celina akitoka shule amuone yaan waonane ,
Sasa huku kwa Celina akaanza kuuliza wanafunzi Kama wamemuona Celena , wanafunzi wenzake wakaanza kumcheka , " yaani we unajitafuta mwenyewe, "
Wanafunzi walicheka walijua ni Celena ,
" Jamani Mimi sio Celena Mimi naitwa Celina namtafuta Celena ,"
Aliongea Celina lakin bado wanafunzi wenzake hawamuelewi ,ndio kwanza walicheka na kumuona Kama amechanganyikiwa ,
" Yaani Celena sijui anamawazo Gani eti anamtafuta Celena wakati Celena ni yeye ,"
Waliongea wanafunzi huku wakiondoka ,
Sasa wakati Celina anashangaa akamuona mama yake na Celena kumbuka yeye hamjui ila anajua huyu mama ndie yule aliepigana na mama yake kichaa kule hospital, Sasa alivyomuona akaogopa na kukimbia ,
Mama Celena akashangaa kumuona mwanawe anamkimbia , kumbuka yeye mama Celena anajua huyu ndie Celena ,kumbe huyo ni Celina ,
" Huyu mtoto vip au sio yeye ,?
Bado mama Celena alijiuliza maswali huku akiendelea kumsaka shuleni hapo bila mafanikio ,
Mama Celena aliamua kurudi nyumbani huku akiwa amechukia ,
Celina akarudi nyumbani baada ya kumkosa Celena kule shuleni kwao ,kumbuka Celina anakaa pale kwa kina Stefano baada ya wazazi wa Stefano kuamua kumsaidia yeye na mama yake kichaa , na ukumbuke kuwa mama Stefano ameamua kumsaidia Celina kwa sababu anampenda Kama mwanae , na hajui Kama ni mwanae , na kinachomchanganya ni kwamba hao watoto wapo mapacha, na kwanini mmoja yupo kule kwa matajiri na mwingine yupo huku kwa kichaa , Hilo ndio swali analojiuliza na hajapata jibu ,
Celina na Stefano wakafika nyumbani ,wakamsalimia mama Stefano na kuingia ndani ,
Wakashangaa ndani kumevurgika ,kumbuka Celena ndio kavuruga vuruga humo ndani , yaan makoch katupa tupa ,nguo chumbani katupa tupa ,
" Mama mbona kuko hivi huku ndani ,"?
Celina alimuuliza mama Stefano na kumbuka Celina anamuita tu mama Stefano MAMA kutokana na heshima tu ila anajua sio mama yake ,anajua mama yake ni yule kichaa ,
" Amekuja Celena ameshinda hapa ,"
Mama Stefano alimjibi Celina ,
'celena alikuja hapa nyumbani,"?
Celina aliuliza huku akishangaa ,
" Ndio tena ameondoka muda sio mlefu Kama masaa mawili yamepita ,"
Aliongea mama Stefano ,
" Jamani mama si ungemzuia mi nikaja kumuona ,"?
Aliongea Celina ,
Kumbuka mama Stefano akiitwa mama na Celina au Celena moyo wake hustuka na hujihisi tofauti kabisa ,
Kule kwa mama Celena alirudi nyumbani huku akiwa na mawazo tele ,kwanza kwanini Hawa watoto wako wawili , pili kwanini yule mama kichaa anakaribia kupona , Cha tatu kwanini Celena amemuona kule shuleni akamkimbia ,
Sasa wakati anaingia kwake akamuona Celena ameshavua nguo za shule tena amekaa mezan anakula ,
" He huyu mtoto vip amefikaje huku mala hii ,"
Alijiuliza huku anamuangalia Celena ,
Celena yeye alikuwa anakula bila hata wasiwasi ,
"Au nilizaa mapacha ,"?
Bado alijiuliza bila jibu ,
" Vip mke wangu mbona umesimama unashangaa ,"?
Alikuwa Mr Benson akimuuliza mkewe ,
Mama Celena akastuka na kukaa kwenye sofa ,
" Hapana ni mawazo tu ,"
Aliongea mama Celena ,
Wakati wanaongea akaja Celena na kumuuliza baba yake ,
" Baba eti Celina ni nani mbona nimefanana nae ,"?
Swali Hilo likawastua wote , maana ni kweli Celena anahaki ya kujua kwanini amefanana na Celina ,swali ambalo hata wazazi wake hawana jibu la kumpa ,
" Baba na mbona Mimi nimefanana na mama yake Stefano au sisi ni ndugu ,"?
Celena aliuliza tena swali ambalo hawakuwa na majibu yake ,
" Kama ni ndugu zetu mi nataka kwenda kuishi kule ,"
Celena bado aliwaumiza vichwa wazazi wake ,
Kumbuka story hii utaipata yote mwanzo mwisho kwa elf moja tu namba ni 0655772653 njoo whtsap
Je itakuwaje hapo ndani , wazazi watajibu nini , na Je watamruhus aende , na Je itakuwaje wakigundua ni mapacha ,na Je mama Stefano akigundua ni watoto wake itakuwaje , na Je ukichaa wa yule mama kichaa ilikuwaje ,
Usikose Leo saa 12 jion
Itaendelea.