ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ:26
Nikamuuliza βkwanini uniite boss.β
Hakujibu badala yake akaendesha gari nami nikishangaa jiji lilivyo zuri.
Kisha tukafika mahali akasimamisha gari na kusema βNdeana, Nakupenda. Kuwa mpenzi wangu tafadhali. Siwezi kujizuia kwako. Hisia hizi ni kweli na ndiyo. Nipo tayari kufanya lolote kwaajili yako.
Nipo tayari kufanya kila kitu kwaajili yako kwasababu wewe ndiyo furaha yangu. Nakupenda na nasikia furaha ambayo sijawahi kuwa nayo kabla.β
Nikamtazama. Yeye akatanitazama na kutabasamu halafu akashuka na kuja kunifungulia mlango. Mimi mwenzenu nilizoea super market moja tu, Mliman city pale nikichoka nibebane na wenzangu tukasafishe macho.
Huyu mwanaume alinipeleka moja kati ya supermarket nzuri na kubwa sana huko maeneo ya Posta. Tena alinishika mkono wangu na tuliingia kwa kushikana mikono. Huku akiwa ana furaha sana. Baada ya kufika ndani akaniuliza βUnataka nini totoo?β
Nikamtazama tu kwa maana mimi sikuwa nimejipanga. Akatabasamu na kusema βwakati unafikiria Icecream kwanza.β
Mimi huyu napelekwa sehemu ya icecream wakati mimi nikinunua icecream nimejitahidi ni koni ya buku au huku jero zaidi ni zile ukwaju, mara maziwa na vitu kama hivyo.
Leo hii nanunuliwa kubwa sana na ya gharama tena aliniuliza βNyumbani si kuna friji totoo.β
Sasa friji la nyumbani kwetu lilivyo, leo linawaka kesho linazima. Nikamwambia tu βMoja inatosha zaidi zitaharibika.β
Alinitazama na kusema βnimeelewa. Haya chagua utakayo kisha sasa useme tununue nini kwenye soko hili.β
Nikamtazama tu usoni. Akatabasamu na kusema βhujanizoea tu. Basi sawa nanunua mahitaji ya nyumbani.β
Nikasema βwanajua sina pesa sasa nitasemaje?β
Akanitazama na kusema βkama ukishindwa kusema mpenzi wangu kanunua basi useme mtoto wa Mungu kanunua.β
Akaanza kucheka na mimi nikajikuta nacheka. Basi akanunua vyakula pale vya nyumbani. Na mafuta mara maziwa ya kopo, sukari na vingine vingi tu. Kisha akaninunulia vitu vya kitoto kama chocolate na pipi nzuri na vingine vingi. Tukaenda kulipia nakumbuka alilipa kwa kadi na kisha aliniambia βnaomba nikupeleke nyumbani.β
Nikamuuliza βnyumbani?β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ:27
Akanijibu βina maana hutaki nipajue kwenu?β
Nikamtazama na kusema βhapana ila sio sasa. Naomba tuongee kuhusu kazi.β
Stewart aliniambia βnilikuahidi kazi, na nitakupa kazi. Ila nami ninaomba uwe mpenzi wangu. Kazi hata ukisema Jumatatu utaanza ila uwe mpenzi wangu nakuomba sana. Sitaweza kukaa na wewe kazini ukinikataa mimi.β
Nikavuta pumzi na kuuliza βunataka penzi langu kwa mara moja au unanipenda?β
Nikamuona Stewart akinitazama kwa kushangaa. Na kisha aliniuliza βNdeana ina maana unaona mimi wale vijana wa kula na kukimbia. Mimi nakupenda nataka penzi lako maisha yote.β
Nikamwambia kwa upole βmimi siwezi kuwa mpenzi wako Stewart. Ninazo sababu nyingi sana. β
Akatabasamu na kusema huku akiwasha gari βHutaki kuwa mpenzi wangu ila unaweza kunipa penzi upate kazi si ndiyo Ndeana.β
Nikainamisha kichwa na kusema βsina maana hiyo, kwa maana siwezi kutoa utu wangu kwaajili ya kazi.β
Akacheka na kusema βbasi unatakiwa kunipenda. Nipende Ndeana hutojuta kunipenda mimi. Utafurahia sana. Tafadhali nipende.β
Nikanyamaza tu.
Aliendesha gari tukiwa kimya sana na alipofika mahali nikamwambia βniache hapa nitachukua bajaji mpaka nyumbani.β
Akatabasamu na kusimamisha gari. Kisha mimi nikawa nataka kushuka. Akanishika mkono akiitazama mikono yangu akisema kwa hisia βNdeana nimekuelewa, kuwa hunipendi na hunitaki. Nakuahidi nitakaa mbali na wewe. Ila nitafanya hivyo walau ukinibusu hata kidogo tu. Ndeana naomba busu lako, please nakuomba sana.β
Namna anaongea kwa hisia mpaka nasisimka. Nikajikuta nasema βStewart.β
Stewart akaniambia kwa sauti ya mahaba βplease kiss me beutiful. Usiwe mchoyo please.β
Akasema hivyo wakati tayari amegonganisha vichwa vyetu, yaani komwe langu na lake vimegongana na mimi nimeinama tu siwezi hata kuinuka yeye ananiita kwa mahaba βNdeana, Ndeana please kiss me, sitaki unipende, siwezi kukulazimsha but please. β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ:28
Alikuwa anaongea hivyo huku akiwa amenifikia kwenye midomo yangu. Na hapo ndipo alipoanza kunibusu tena kwa ufundi sana. Niliyafumba macho yangu ni kelele za midomo ndizo zilizosikika huku akichukua mkono wangu akiweka juu ya zipu ya suruali yake kunionesha namna pale juu palivyo tuna. Nilisisimka sana kwa maana ilikuwa inaonekana kubwa.
Sijui hata alifanyaje aliitoa palepale nami nikshtuka kwa maana sikuwahi kuona mtu mwenye sehemu nene na kubwa kubwa namna ile. Nilijikuta nazidi sisimka. Na yeye akionekana kunogewa aliniambia βNdeana Suck me Please!!β
Nikashtuka, ina maana huyu mwanaume anataka afanye mapenzi na mimi kirahisi hivi, nikajikuta nasema βno inatosha, inatosha naomba kushuka.β
Akanifungulia mlango, kisha akaniambia βNdeana, kesho nataka nikupeleke mahali, kama hutojali niambie na Nitafanya maandalizi yote Jumatatu uanze kazi. Ndeana Asante.β
Nikamtazama tu, kusema ukweli wa moyoni mwangu sikuwa nimechukia kabisa. Yaani anajua kubusu huyu Boss. Siwezi kusema ni mubaba, wala siwezi kusema kaka ila yupo hapo katikati. Namna alinibusu mimi Ndeana ninakiri kuwa ilikuwa ni kwa namna ya pekee sana.
Nilishuka, na yeye pia baada ya muda akashuka huku akinitazama kwa upendo sana. Akashusha mizigo yangu. Na kisha akawa ananipa mkono hivi kuagana. Nami nikampa mkono wangu vizuri tu, ila aliniachia pesa mkononi. Na kisha aliingia kwa gari na kuniacha pale. Nilipokunjua mkono wangu ilikuwa ni elfu 50.
Nikatabasamu huku moyoni nikisema βkajuaje kama sikuwa hata na nauli sasa maana hizi safari za kuonana nao zinanimaliza Pesa.β
Nikabeba vifurushi vyangu mpaka kwa bajaji. Sasa nipo kwa bajaji nawaza lile jambo nimetoka kufanya ndani ya gari. Inajirudia vilevile yaani mpaka najikuta ninasema kwa sauti βunafanya nini Ndeana acha ujinga ulishindwa kujizuia walau hata kidogo.β
Abiria mwenzangu akanitazama na akaniuliza βdada upo sawa kweli?, unaongea mwenyewe.β
Nikajisikia aibu, nikatabasamu ba kusema βnipo sawa nipo sawa.β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ:29
Basi nikawa ninatamani tu ifike sehemu nishuke na ndivyo ilikuwa. Ilifika mahali mimi nikashuka na kuendelea na safari kidogo tu maana ninaposhukia sio mbali na nyumbani kwetu.
Nimefika tu nyumbani nakuta dada yangu amejilaza sebuleni. Aliponiona na mizigo akainuka na kusema βmdogo wangu, umerudi, karibu. β
Nami nikamuitikia βasante mama wa mimi.β
Akaniambia βmbona vifurushi tena.β
Nikamtazama na kutabasamu tu. Kisha nikapeleka jikoni. Na kurudi sebuleni.
Nilipofika niliketi huku nikivuta pumzi na kusema βdada yangu mbona kulala tena kuna shida gani?β
Dada yangu akaniambia βmdogo wangu tumbo linanisumbua sana. Yaani ninateseka acha tu.β
Nikamtazama na kusema βpole sana dada yangu. Tutafute pesa tu inabidi utibiwe hilo tumbo sio kawaida ujue kuumwa mara kwa mara.β
Dada alinitazama na kusema βni kweli mdogo wangu, ni kweli kabisa. Niambie imekuaje huko.β
Nikajikuta natabasamu.
Dada akaguna na kusema βunatabasamu tena. Niambie umepata kazi au hujapata maana umeenda huko unarudi usiku na unacheka tu hapa.β
Nikasema kwa upole βdada si unaumwa wewe sasa mbona mkali.β
Akacheka na kusema βunanikera ujue, niambie basi.β
Nikamtazama na kusema βyaani dada kabla sijasema habari za kazi. Nataka nikuambie kitu.β
Dada yangu akasema βunajizungusha ujue, si useme sasa.β
Nikavuta pumzi na kusema βdada, eti ananipenda.β
Dada akanitazama na kuniuliza βnani anakupenda?β
Nikajibu βBoss, Boss wangu ameniambia ananipenda sana. Anataka tuwe wapenzi na ana lengo la kunioa.β
Dada akaniuliza βna ndiyo kakununulia vyakula.β
Nikaitikia kwa kichwa.
Dada yangu akakaa vizuri, kisha akanoa sauti yake saafi kabisa nami nikawa na hofu ninamtazama tu. Akaniambia kwa upole akiniuliza βNdeana nikuulize kitu?β
Nikasema kwa upole tu βniulize dada?β
Akaniambia kwa upole βushawahi kuona au kusikia mwanaume anamtaka mwanamke akamwambia ninataka kukuchezea tu sitakuoa?β
Nikajikuta nasema βhaiwezekani, kivipi sasa dada?β
Dada akacheka kidogo na kusema β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ:30
βmdogo wangu hakuna mwanaume mbaya anapomtaka mwanamke. Kama ni mlevi akijua wewe hupendi pombe basi ataacha akupate, akiwa mwizi atajificha usijue, akiwa malaya hutojua kwa mwanzo. Tabia zote mbaya huwa zinajificha kabisa mpaka pale atakapokumiliki na kukuweka kwa viganja vyake.
Mimi sijasoma hata kama wewe, wewe mwenzangu kidogo umesoma unaelewa. Ni nani amekuambia unaweza kuwa na uhisiano na Boss. Najua utasema wapo na wanaolewa na wanaishi.
Ni kweli mdogo wangu ila ni moja ya kumi. Ndeana huyo mwanaume utafanya naye vipi kazi mkiwa wapenzi?, utaishi vipi kazini mkiwa wapenzi. Na vipi kama humpendi na yeye akawa anakutumia tu kisa kakupa kazi ukimkataaa anakutishia au anakufukuza kazi. Kwanini akupende wewe mdogo wangu kwanini wewe.
Ile ni Hotel kubwa, wewe una uzuri gani wa ajabu kuwashinda wageni wanaofika pale, wafanyakazi wa pale. Mdogo wangu Ndeana. Kama mtu huyo humpendi muache akunyime kazi mbona tunaishi tu.
Au Lah kama anakupenda kweli inabidi akuelewe kuwa wewe humpendi ndiyo muwe wapenzi. Sitaki kabisa masuala ya kukutumua kingono na wakati hujalelewa hivyo. Sijui unanielewa mdogo wangu?, sasa nakuuliza swali, Unampenda huyo mwanaume na upo tayari kumpa penzi ili akupe kazi?β
Nikasema kwa upole nikimdanganya dada yangu βdada kazi amenipa tayari tu amekiri upendo.β
Dada alinitazama na kusema βmimi siwezi kukupangia nani wa kuwa naye na nani usiwe naye. Wewe ni mtu mzima sasa. Ila ninachoweza kusema ni kuwa usitoe penzi kisa sisi. Kinachokuja kirahisi huwa hakidumu siku zote. Kama anakupenda utajua na kama hakupendi pia utajua. Maisha haya ni yetu na yametukuza sisi wote. β
Nikatabasamu. Dada yangu akatabasamu na kuanza kucheka akisema βnimefurahi sana umepata kazi ya ndoto yako. Ina maana jumatatu kazini. Nimefurahi sana sana mdogo wangu ndoto imetimia.β
Nilimkumbatia huku nikisema βasante sana dada yangu. Ni wewe umesababisha. Nakushukuru sana.β
Dada alisema βwacha nimshukuru Mar kwakweli nimefurahi sana mdogo wangu amefanikiwa mno. Asante Mungu.β
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ:31
Mimi na wewe sasa tunajua ukweli. Ukweli ni kuwa natakiwa kutoa penzi jumatatu niingie kazini. Yaani sielewi kabisa. Dada yangu alipotaka kumpigia Martha mimi nikamuulizia baba wakati yeye anatafuta namba. Dada akaniambia βbaba si unajua afya yake, leo kalala mapema.β
Nikasema βWacha nikamuone.β
Basi nikatembea na nikafika sehemu nikasimama nikawa namsikia dada yangu akisema βMartha ndugu yangu asante sana. Mdogo wangu amepata kazi kwasababu yako nashukuru sana.β
Sasa sikuwa nasikia ya upande mwingine, nikawa nasikia tu cheko huku dada akisema βnakuja kesho ndugu yangu tuzungumze. Nakuja.β
Basi mimi nikafumba macho kinyonge na kuvuta pumzi nikiwa nimechoka sana.
Taratibu nilianza kutembea kuelekea chumbani kwa baba. Nilibisha hodi bila mafanikio. Ikabidi nichungulie, baba yangu alikuwa amelala. Hivyo ilinibidi nirudi chumbani kwangu.
Nilipokuwa hata sijafika ujumbe ukaingia. Ulitoka kwa dada Martha. Nikasoma na yeye aliandika βSaafi sana mdogo wangu. Kiukweli ningekushangaa sana kuacha hii nafasi kubwa na nzuri. Hongera sana kwa kupata kazi naamini hutoniangusha.β
Sikuweza hata kujibu kiukweli. Nikaingia chumbani. Nikatupa simu kitandani ili nikaoge nichangamshe mwili wangu maana na lile busu najisikia sio vizuri yaani alijua kunichanganya.
Mara simu yangu kwa mara nyingine tena ujumbe ukaingia kwa simu yangu. Kama nisiseme nani alinitumia ujumbe. Alikuwa ni Boss kubwa, Stewart ndiye alinitumia ujumbe.
Nakumbuka aliandika βMidomo yako, totoo, midomo yako mizuri, na laini sana. Natamani nikuambie namna nimejisikia pale tulipokutanisha midomo yetu kwa mara ya kwanza.
Wewe ni wa pekee totoo, mtu mzima hapa nishavurugwa, natamani nirudi tena walau unibusu mara ya mwisho. Ladha yako bado imebaki katika moyo na midomo yangu.
Ni kama upo kando yangu, please, Please totoo kesho naweza kukuona tena, nakuomba nikuone tena nipate muda wa kutazama kwa uzuri uumbaji wa Mungu. Sema ndiyo basi nikupe zawadi. One, Two, Threee.... Yeees!!
ππππππ ππππ ππ πππππ ππππ πππ:32
Si nikajikuta nashika midomo yangu tena taratibu na kuketi kitandani. Nikawa nataka kumjibu kila nikiandika nafuta, kila ninachoandika nafuta. Ujumbe mwingine tena ukaingia kutoka kwa boss kubwa, aliniulizwa swali βhivi totoo unajisikia kama ninavyojisikia?. No ungekuwa unajisikia hivi ningejua. Mwenzako nipo tayari kuuza hata Hotel yenyewe nikupe niwe na weweπ€£π€£π€£π€£.β
Alimalizia hivyo na emoji za kucheka na mimi nikajikuta nacheka kwa emoji βπππ.β
Akaniambia kwa upole βFinally, totoo amecheka. Niambie basi kesho upo tayari kutoka na mimi?β
Maneno ya dada yangu yakawa yanapita moyoni mwangu kwa kasi. Lakini nataka kwaajili yetu na familia. Hata hivyo mwanaume mwenyewe sio wa kutisha.
Nikawa najiuliza βhivi ni kweli nina hisia naye, hapana sitaki kutoa penzi sasa nifanye nini.β
Kumbuka kazi nataka hivyo sitaki kumuudhi tajiri hapa nacheza sitaki nataka. Nikamuuliza βtunaenda wapi sasa boss?β
Akaniambia kwa ujumbe βsiwezi kusema kwasababu ni for you totoo. Nikikuambia itakuwa mbaya. Kesho utapaona.β
Nikaanza βmimi sitaki kwenda mbali, baba anaumwa na dada pia hajisikii vizuri.β
Boss akajibu βNdeana, Ndeana kwahiyo kesho tunatoka mimi na wewe?β
Nikavuta pumzi na kuuliza βsi ni kutoka tu kwani kuna lingine boss?β
Nakumbuka akaniambia βsipendi neno boss, kuwa huru kwangu nakuomba sana. Pia Ndeana acha utoto. Kesho nakufuata hapo mida ya saa 6 hivi naomba upendeze sana.β
Nikamuuliza kwa kushangaa βkupendeza tena?β
Akaniambia βHata hivyo wewe ni mzuri.β
Nikavuta pumzi na kuweka simu pembeni bila kujibu, nikajiuliza βnafanya nini sasa Mungu wangu. Hivi inawezekana kweli?β
Simu yangu ikaita. Nikatazama simu, alikuwa boss. Nikashusha pumzi na kusema βkazi ipo.β
Nikapokea ile simu.Nilipopokea tu sauti tamu ya mapenzi iliniita kwa upole βSweetheart!!!β
Nikanyamaza. Akaniambia βHivi si unajua Mungu hapendi kumnunia mtu anaye kupenda hiyo si ni dhambi totoo!!!β
Nikajikuta natabasamu. Na kusema βsamahani nilikuwa nataka nikaoge.β
Basi akaniambia βOoh jamani, i wish nipae. Kwahiyo umejiandaa unaenda kuoga.β
π€£π€£π€£ ila penzi jipyaπ€£π€£π€£π€£πππ
Soma muendelezo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005


Maoni