Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  gonga94 official track

๐‰๐€๐Œ๐€๐๐ˆ ๐๐Ž๐’๐’ ๐Œ๐ˆ ๐๐€๐Ž๐๐€ ๐€๐ˆ๐๐” ๐Ÿ’๐Ÿ™ˆ๐Ÿ’ž: 76

9th Aug, 2025 Views 103

Akacheka akisema โ€œkwa ulivyonichosha sitaki hata ufanye nini.โ€ Nikasema โ€œya kweli hayo?โ€ Akacheka akisema โ€œkwanza haramu. โ€œ Tukacheka nikisema โ€œunajua nasubiriwa na leo nawahi kutoka kwaajili ya maandalizi ya kesho.โ€ Akanitazama akasema โ€œhata mimi nawahi kutoka naenda msaidia totoo kujiandaa. Sasa sikia ukitoka fanya unaloweza kanisubiri pale kona ya kanisani. Mimi nakufuata hapo chapu nakupeleka saluni nzuri mama yangu nilikuwa nampeleka hapo. Ukapendeze.โ€ Nikamuuliza โ€œtunaenda wote saluni?โ€ Akaniambia akicheka โ€œhaya nenda ubishi ni haramu.โ€ Nikacheka na kuanza kutoka. Wakati natoka tu, nikakutana na mfanyakazi mwingine mlangoni na yeye ndiyo alikuwa anaingia. Natamani ungemuona alivyokuwa ananitazama. Nikasema wewe usinitanie, mimi nikarudi tena ndani kwa Boss. Nilipofika tu. Boss alimuuliza yule dada โ€œUnahitahi nini?โ€ Yule dada alinitazama jicho kali, kisha alisema โ€œsamahani naomba kuzungumza na wewe.โ€ Boss alinitazama na kisha alimwambia โ€œmara ngapi nikuambie hii sio sehemu ya kuja ovyo kila unapojisikia. Shida na malalamiko yenu nayapata kwa meneja. Haya nenda kamwambie matatizo yako ndiyo kisha utajibiwa na meneja.โ€ Huyu dada alijisikia aibu sana. Alinitazama kwa hasira akatoka. Alipotoka nikauliza โ€œkwani huyu kafuata nini?โ€ Akaniambia akitabasamu โ€œusijali baby, najua namna ya kumalizana mambo madogo madogo.โ€ Nikamtazama kwa jicho, akatabasamu akasema โ€œbaby kununa ni haramu wallahi nakuambia, dini zote haikubaliki.โ€ Nikatabasamu tu na kutoka. Nilipotoka nilikwenda moja kwa moja kwa Joan. Joan aliponiona aliniambia โ€œndugu yangu muda wote huo?โ€ Moyoni nasema angejua huyu mwenzake nimetoka kuchangamsha damu asingeniuliza maswali. Basi nikamwambia โ€œnisamehe kipenzi, kuna maagizo ya Boss nikatoka kabisa hapa ndiyo narudi na nina njaa hatari, si unajua hata simu hatuna nikashindwa kukuambia rafiki yangu.โ€ Joan akasema โ€œmimi nishakula, nimekubakishia. Kula basi haraka haraka tuondoke.โ€ Basi wakati nataka kula yule dada nimekutana naye kwa Boss akapita na kusonya. Joan akashangaa na kusema โ€œkachanganyikiwa nini?โ€

...
๐‰๐€๐Œ๐€๐๐ˆ ๐๐Ž๐’๐’ ๐Œ๐ˆ ๐๐€๐Ž๐๐€ ๐€๐ˆ๐๐” ๐Ÿ’๐Ÿ™ˆ๐Ÿ’ž: 77 Nikamuuliza โ€œkwani ni vipi huyu dada, nimekutana naye muda ule natoka kwa Boss. Basi alinitazama kwa jicho hilo nikaogopa.โ€ Joan alianza kucheka alicheka akisema โ€œhao ndiyo wanaohangaika waolewe na Boss. Boss mwenyewe hacheki na kima, yeye akikupitia tu tayari si bora watulie kama mimi hapa?โ€ Nikashtuka na kuuliza โ€œhata wewe pia?โ€ Akasema โ€œndugu yangu kupata kazi sio rahisi hivyo, mtu mwenyewe ana dharau kama nini unaweza nenda naye room akaishia kukutazama tu. Ya nini mimi.โ€ Nikacheka tu, nikisema โ€œtuondoke, nitakula tu nyumbani.โ€ Joan alisema โ€œyamekuwa hayo, au unampenda Boss ndugu yangu. Kama unampenda bora usahau tu. Yile sijui hana Moyo.โ€ Nikacheka tu nikisema โ€œnitamuanzia wapi mimi, na usikute anaye mke nyie mnahangaika tu.โ€ Naongea hapo moyoni kuna waka moto. Nachukia kusikia hayo maneno sana, ila nitafanyaje sasa na mtu kakiri. Nilichukia ila moyoni nasema โ€œMungu anajua.โ€ Basi tulienda kuchukua simu, na kubadili nguo. Nilipowasha tu simu nilikuta na semeji zake zimejipanga. Honey babe Hunny bunny Honey pot My sweet person Totooo Kipenzi Ndeana wangu, na maneno matamu matamu mengi. Nikacheka tu. Na kisha ujumbe mwingine aliandika โ€œ Nisubiri nilipokuambia, tunaenda saluni pamoja leo.โ€ Kiukweli siku hii sikuwa na story nyingi na Joan. Basi tulipotoka tu tuliagana vizuri tu. Nilitembea mpaka hiyo sehemu aliyoniambia. Nilimtumia ujumbe kuwa nipo hapo. Hakuchelewa ndani ya muda mfupi tu alifika. Niliingia ndani ya gari na alinitazama na kuniambia โ€œUnaonekana umenuna kuna nini totoo!!!โ€ Nikamtazama na kumuuliza โ€œKwani kazini umetembea na wanawake wangapi?โ€ Akasimamisha gari na kusema โ€œNdeana nilijua umenielewa na yameisha. Ina maana unataka nilie tena. Mumy mimi mtu mzima ujue, please nipe muda. Ningekuwa sikupendi nisingekuwa nahangaika hivi. Please jiweke mbali na hayo mambo kama ni hivyo basi uache kazi.โ€

...
๐‰๐€๐Œ๐€๐๐ˆ ๐๐Ž๐’๐’ ๐Œ๐ˆ ๐๐€๐Ž๐๐€ ๐€๐ˆ๐๐” ๐Ÿ’๐Ÿ™ˆ๐Ÿ’ž: 78 Nikamtazama na kusema โ€œNiache kazi kivipi sasa?โ€ Akavuta pumzi na kuniuliza โ€œunanipenda mimi?โ€ Nikamtazama tu, akaniambia โ€œnisikilize mimi, mimi nakupenda peke yako wewe tu.โ€ Nikaitikia kwa kichwa. Akaniita โ€œNdeana!!!โ€ Nikaitikia โ€œabee!!โ€ Akaniuliza โ€œunajua kwanini napenda kukubusu?โ€ Nikamtazama kwa aibu na kusema โ€œHapana, sijui?โ€ Akniambia โ€œkwasababu kila busu lako linaanzisha maisha mapya ndani ya moyo wangu. Mwili wote unasisimuka na kuwa na furaha. Nakupenda Ndeana.โ€ Nikasema kwa upole โ€œTuachane na hayo sasa tuendelee na safari.โ€ Akatabasamu. Basi akaweka nyimbo zake kama kawaida, kwa mara ya kwanza, tangu nitoke kwenye tumbo la mama yangu. Ninaonaga kwa tv tu, ila sasa hivi yananitokea mimi mwenyewe katika maisha yangu. Nilishuka kwa gari, na Boss akashuka. Kapendeza mwenyewe, anavutia yaani hata ukisimama ukisema huyu ni mpenzi wangu, lazima upewe maua yako. Alinishika mkono, alinibebea pochi yangu. Nilikuwa najisikia aibu sana. Tulitembea mpaka saluni. Ile tunaingia tu, wadada wote wa saluni wakaacha walichokuwa wanafanya wakatutazama. Kisha Boss wangu, aliita kwa sauti ya wote kusikia โ€œAunt, nimekuletea mkweo leo, maana kila siku unanipigia kelele haya huyu hapa, anaitwa Ndeana, ni mke wangu mtarajiwa.โ€ Aunt sasa akashangaa akisema โ€œStewart, usinambie unanitania, mbona mrembo hivi, nitambulishe vizuri.โ€ Mwanaume wangu sasa, alivyo anajiachia kwa raha, si mwenzenu nilianza kutambulishwa alianza kwakusema โ€œAunt, she is my sweet person.โ€ Aunt sasa โ€œumh!!, uhm!!โ€ Aliendelea akisema โ€œMimi namuitaga totoo, Aunt huyu sasa ndiyo roho yangu, nampenda sana huyu mrembo anaitwa Ndeana. Ni mwanamke wa pekee sana kwangu. Ndeana huyu ni aunt yangu. Rafiki kipenzi wa mama yangu. โ€œ Mimi sasa mpaka aibu wadada wengine wanavyoshangaa yaani huku moyoni nasema โ€œNdeana mimi, sijawahi kupendwa hivi, zamani nilikuwa kama hawa wanaoshangaa.โ€ Basi nikasalimiana na Aunt kwa furaha na kisha Boss wangu alisema โ€œNakaaa hapa nataka nione anavyopendeza. Naomba mtengeneze vizuri sana. Vyovyote ili mradi apendeze. Totoo enjoy kipenzi.โ€ ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œna leo mkikoment kama jana kesho mpaka mia๐Ÿ’ƒ๐Ÿป

...
๐‰๐€๐Œ๐€๐๐ˆ ๐๐Ž๐’๐’ ๐Œ๐ˆ ๐๐€๐Ž๐๐€ ๐€๐ˆ๐๐” ๐Ÿ’๐Ÿ™ˆ๐Ÿ’ž: 79 Nikacheka. Akasema โ€œBaby kwani kukusubiri hapa ni haramu.โ€ Nikamjibu nikicheka โ€œni haramu baby dini zote zinakataza.โ€ Akacheka akisema โ€œumoja wa mataifa uingilie kati nakusubiri kipenzi.โ€ Watu wakajikuta wanacheka na kuanza kunongโ€™onezana. Mimi na yeye tunatazamana na kukonyezana huku akiwa na pochi pembeni. Nyie mapenzi matamu mjue, mimi ndeana nawaambia. Basi tena, Aunt mkwe tena kajua mimi ni mkwe wake. Basi ananifurahia mwenyewe, ananitengeneza nywele akiwa na furaha sana.Boss wangu amekaa tu anachezea simu yake hana habari, wadada mule ndani wanapiga story wanamuangalia Boss wangu napata wivu maana wasije niibia njiwa wangu akapeperukia mbali sana. Nilipendeza sana, unajua kuna kule kupendeza mpaka wewe mwenyewe unajua wazi ya kuwa umependeza. Basi nilipomaliza Aunt mkwe alisema โ€œmkwe wangu umependeza mno, yaani hapa sasa kila mawimbi yakivurugika njoo tunatengeneza mtindo mwingine. Hili wiki ni kama lilitengenezwa maalumu kwaajili yako. Stewart unasemaje, umemuona mwenzio.โ€ Boss alitabasamu na kusema โ€œnimemuona aunt, ni mzuri sana. Amependeza sana.โ€ Akanisogelea na kisha akanishika mkono tulienda kukaa kwenye sofa pamoja. Akawa ananishika nywele zangu huku ananiambia โ€œbaby hawa wadada wanaona wivu, itakuwa hawapendwi hawa.โ€ Nikajikuta nacheka na akaniziba mdomo watu wanatutazama. Mimi nikamwambia โ€œhuna akili kabisa.โ€ Akatabasamu na kusena โ€œNdeana wewe ni mzuri sana. Umependeza sana. Umependeza vibaya mno.โ€ Nikamwambia โ€œNashukuru sana. Haya uliza basi gharama nilipie.โ€ Boss wangu alitabasamu na kusema โ€œuna matatizo wewe. Nikusifie na Bill ulipe wewe. Hii ni juu yangu. Mwanaume akikusifia ahakikishe yeye ndiyo ana gharamia. Yaani akikusifia umevaa nguo mpya umependeza, viatu vipya ama chochote na yeye hana tatizo lolote lile, yupo tu kukuonea, anakufanyia makusudi mbinafsi.โ€ Nikamtazama na kusema โ€œbaby lakini mwingine kipato kidogo?โ€ Akatabasamu akisema โ€œkipato kidogo pia kuna vitu vidogo vya kunogesha penzi lao. Sasa baby niwe sina hela hata kijola ukose, hata kukupeleka kula mihogo nishindwe, masihara sasa.โ€ Nikacheka na kusema โ€œuna maneno kama nini?โ€
...
๐‰๐€๐Œ๐€๐๐ˆ ๐๐Ž๐’๐’ ๐Œ๐ˆ ๐๐€๐Ž๐๐€ ๐€๐ˆ๐๐” ๐Ÿ’๐Ÿ™ˆ๐Ÿ’ž: 80 Aliinuka na kisha alienda kwa Aunt yake. Walizungumza kidogo kisha Aunt alinifuata na kusema โ€œKipenzi, sasa usiwaze kuhusu nywele. Wewe njoo hapa kila ukiona nywele haifai. Njoo hapa na utengeneze. Ushalipiwa kabisa, na bill ikiisha mpenzi wako analipa hana shida.โ€ Nikamtazama Boss na kutabaasamu kwa kushangaa yaani, kisha akaniuliza โ€œUtanishangaa tu totoo, hutonikumbatia?โ€ Nikacheka na kwa aibu nilikumbatia nikisema โ€œAsante sana, Mungu akubariki.โ€ Basi alinishika mkono mpaka kwenye kioo eti akaniambia โ€œhaya baby jishaue kidogo nakuchukua video hapa.โ€ Huyu mwanaume ana vituko yaani nikajikuta ninacheka. Basi tukapigana picha na tukiwa timekumbatiana huku tunaonesha picha na video za hapa na pale. Tukamaliza basi nakuambia nikabebewa pochi tena tukamuaga Aunt huku msalimie mama zikiwa nyingi, nitakuja na vitu kama hivyo. Nikafunguliwa mlango totoo mie tukaingia ndani ya gari. Mimi mwenzenu nimepata dereva binafsi, napelekwa nyumbani na nimepata furaha ndani ya muda mchache. Huyu mwanaume amenifanya nifurahie mapenzi ndani ya muda mfupi sana. Hata wiki hatujamaliza ila ananidekeza ananijali na kunitunza ni kama yaani tumejuana kwa muda mrefu sana. Ni kama vile tunajua miaka na miaka. Amenifanya nimzoee na amenifanya nijihisi huru kwake. Ninampenda, ila naona aibu nami kufunguka nahisi bado ni mapema sana. Basi mwenyewe kwa gari humo nilikuwa na furaha sana. Maana nasifiwa na kutaniwa tu huku na yeye akijisifia kuwa katika wanaume wamepata wanawake wazuri basi na yeye ni mmoja kati ya hao wanaume. Tulifika mpaka mitaa karibu na nyumbani. Alisimamisha gari na baada ya hapo alinitazama na kusema โ€œTotoo, nimesimamisha kukuambia kuwa jambo ambalo linaenda kutokea kesho ni jambo kubwa sana. Ni jambo ambalo sikumbuki kama katika hotel yetu limewahi kutokea. Kwanza hotel itakuwa busy, kuanzia vyumba, na hata upande wa chakula. Pesa zitaingia za kutosha. Pia itatangazwa sana Hotel hii na tutapata watu wapya wengi sana. Yote haya ni kwasababu yako. Natamani nikufanyie kila kitu kizuri ndiyo uwezo sina.

Soma muendelezo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

๐‰๐€๐Œ๐€๐๐ˆ ๐๐Ž๐’๐’ ๐Œ๐ˆ ๐๐€๐Ž๐๐€ ๐€๐ˆ๐๐” ๐Ÿ’๐Ÿ™ˆ๐Ÿ’ž: 76   >>> https://gonga94.com/semajambo/jamani-boss-mi-naona-aibu-76
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

gonga94 official track
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

RATIBA YA SIMULI ZETU

Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.


Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest