ðºððððð ððð 81 - 89.. ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð:
...
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 82 Baada ya hapo nilikuwa natabasamu tu ila nilikuwa nikikumbuka Joan na yeye amelala na mwanaume wangu nachoka yaani moyo wangu unaniuma sana. Natamani hata nisiwe rafiki wa Joan. Ila nakumbuka dada yangu, na hata mwanaume amesema ukweli isije ikanifanya nikaanza kuchukia Hotel nzima. Nikajikuta ninasema âHekima ni muhimu sana, Hekima. Nilikuwa nimechoka kusema ukweli, usingizi haukuniacha, nikasinzia pale kitandani. Nilikuja kushtushwa na dada yangu. Baada ya mimi kuamka tu dada alianza kusema âwacha weee!!, wacha weee!!.â Sasa mimi nimesahau hata kama nimependeza kichwani nikawa nashangaa tu.Nikasema âdada kuna nini kwani?â Dada alisema âHivi unqjua kuwa umependeza sana. Mdogo wangu nywele ya gharama umetoa wapi?, nywele imenyooka hii unajua.â Nikamtazama na kujikuta nimeanza kucheka kwa sauti. Nilicheka nikisema âMambo ya shemeji yako hayo.â Dada akasema âweee, boss wako huyo?â Nami natamba nikisema ânani tena?â Dada akaniambia âinuka twende sebuleni kwanza nimekuja na miguu ya kuku, utumbo na chips, najua unapenda huwezi kukataa.â Nikasema ânakaaa vipi kwa mfano dada.â Dada alicheka akisema âumbea wa leo hatari eenh.â Basi tulifika wenyewe tukawa tunakula namwambia âbasi dada yangu, nikapelekwa saluni.â Dada sasa anasema âwee!!!, ikawajeâ Namuambia namna alivyobeba pochi na kunitambulisha. Dada alicheka akisema âsasa huo ndiyo utambulisho, sio ile kutana na huyu ndiyo mwenzangu ninayekuambiaga, tunaimba wote kwaya, pale kazini tupo wote.â Nilicheka nikisema âdada bora hiyo ina maneno mengi. Unakumbuka yule mjinga alivyokuwa ananifanyia yaani tukienda mahali linasema âHuyu mshikaji wangu, anaitwa Ndeana.â Basi tukacheka mno. Nikamsimulia dada pia kuhusu yote yaliyotokea na alivyonielezea na kisha nilisema âkusema ukweli nashindwa kujizuia nampenda sana dada. Ila naogopa na mimi kuwa wazi kwake si ataniacha si eti?â Dada alisema âhuo ni ubinafsi mdogo wangu. Mapenzi ya upande mmoja yanauma na yanachosha sana. Fikiria ungekuwa wewe, unafanya anavyokufanyia na huwezi hata kusema nakupenda.
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 83
Si unaona unasababisha matatizo. Na umekaa hapa unazungumzia wanawake wanavyohangaika wapate mahusiano. Mdogo wangu kuna zaidi katika mapenzi. Mapenzi ni kujaliana, kupendana, kuelewana, kufurahiana, kuombana msamaha na mambo mengi kama hayo.
Katika mapenzi kila dakika ina maana, kila sekunde ina maana. Unavyofanya hivi mwenzako anaumia ni vile hawezi kusema na pengine kakupa muda kuwa zikifikika wiki mbili au wiki hasemi kama ananipenda basi nitamuacha.
Mdogo wangu. Unatakiwa kufurahia sasa kuachwa, au kuolewa ni mipango ya Mungu. Huwezi kusema sitamwambia mpenzi wangu namna nampenda kwanza sio mume wangu, wewe unajuaje?.
Wewe furahia sio kwaajili yake pekee. Hata wewe utakuwa na furaha hata ukiachwa utakuwa na kitu cha kusema, na ukiolewa pia utasimulia namna pendo lenu lilivyo.
Ndeana kama unampenda leo na wewe mwambie namna unampenda, mwambie namna alivyo wa muhimu kwako. Utaona namna anavyofurahia na hapo ndiyo utajua namna gani alivyokuwa anatamani kusikia maneno kama hayo.â
Nilivuta pumzi na kusema âdada unajua una hekima sana kwenye suala la mapenzi. Mungu akujalie mwanaume mzuri.â
Dada alitabasamu akisema âSina papara mdogo wangu ni suala la muda tu.â
Nikatabasamu na kisha dada aliniambia tuendelee kula huku akikumbushia eti huyu mshikaji wangu anaitwa Ndeana basi tunacheka mpaka baba anaingia alitukuta na hali hiyo.
Alikuwa na mfuko akitushangaa kwa kusema âwanangu wanangu, nini kimetokea mbona furaha namna hiyo.â
Tukacheka tu tukisema âkaribu baba. Karibu basi nikainuka na kumpokea mfuko. Baba alisema âKuna zawadi zenu humo, sasa sijui nimepatia.â
Tukatazama na kusema kwa pamoja âZawadi, eenh baba zawadi gani tena.â
Baba alisema tufungue ili tujionee. Waooo!!, waoo!!, baba alikuwa ametuletea viatu, sendozi za chini chini. Tulifurahia sana na kusema âbaba asante, baba asante sana tunakupenda.â
Baba alitabasamu tu, tulimkumbatia baba yetu na yeye alikuwa amefurahia akisema ânimepita sehemu nikatamani. Sasa mmpendeza.â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 84
Tukacheka. Kiuhalisi hivi viatu vilikuwa ni vya kawaida, bei yake ni ndogo sana, ila namna vimekuja kwetu, vimekuja na upendo pesa haiwezi kununua. Nikavipenda sana, nikavifurahia sana.
Kusema ukweli baba alitushangaza na kitu kama hiki boss alisema kuwa hata kama sio tajiri kuna vitu tu vya hadhi yenu vinaleta furaha ili mradi tu vimekuja na upendo kama ambavyo dada kaniletea miguu ya kuku.
Kumbe kila mmoja anaweza kufurahia kwa hadhi yake bila kuumia. Turidhike na hali zetu na kufurahia nini mazingira yanatupa.
Baba yangu pia hakupitwa na kupendeza kwangu. Alinisifia akisema âunaonekana kama bibi harusi leo.â
Dada alicheka akisema ânimemwambia mimi.â
Nyumba ikawa na vicheko juu ya vicheko na kisha nami nikawaelezea kuhusu kazi ambayo tunayo kuanzia kesho. Hakuna ambaye alipinga, wote walinipa baraka zao. Huku baba yangu akionekana mwenye furaha akisema âMungu ambaye tunamuomba amejibu maombi.
Nilitabasamu na kisha kama familia tuliongea hili na lile huku baba akimuuliza na dada biashara yake. Dada naye alisema yake basi familia ikafurahi.
Mimi niliwahi kuingia chumbani. Dada naye alinifuata na kusema âmdogo wangu nimesahau kitu ingawa nakujua mdogo wangu huna marafiki. Ila muweke mpenzi wako mbali na marafiki. Wasimzoee wewe ndiyo mlinzi weka mipaka. Usije ukathubutu kujinadi kwa unayofanyiwa naamiji kitu kizuri wao wenyewe wataona. Wewe kazi yako ni kupendwa na kupenda tu.â
Nikatabasamu, nikamkalisha dada kitandani nikisema âasante sana dada.Nakupenda. Ila nina kitu. Nataka dada yangu uende hospitali ukaangalie hilo tumbo kwanza. Nilipewa pesa kidogo ya maandalizi. Nakupa laki mbili sawa dada. Nataka upone na usijitese kufanya kazi ngumu. Ukichoka acha. Pia pesa kidogo baba yetu apate dawa nami nikiwa kazini nikipata kidogo nakuwa natuma kwaajili ya familia yetu. Sawa dada.â
Dada yangu alinishangaa na kunikumbatia akisema âuna roho nzuri sana mdogo wangu. Wewe sio mbinafsi. Na unaipenda familia yako. Mungu akubariki sana. Mungu azidi kukufungulia mdogo wangu. Sina neno nakupenda tu.â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 85
Nilimwambia kwa upole âdada huna sababu ya kulia kwasababu jukumu la familia yetu ni letu pamoja. Wewe ndiyo rafiki yangu, ndugu yangu, ni kama mama. Dada nakupenda sana.â
Tulikumbatiana na nilimpatia pesa. Dada alifurahi sana. Alifurahi mno. Niliona hilo.
Basi dada yangu alitoka chumbani na aliniacha nikiwa na amani sana moyoni. Nilishika simu yangu, sikuona ujumbe wowote. Nikakumbuka maneno ya dada yangu nikaona ni heri nami nimuoneshe upendo. Sijui ninafanya nini ila nitazoea. Ndipo na mimi kwa mara ya kwanza, nilichukua simu yangu na kuanza kuandika.
Nilikuwa na mengi moyoni ila siku hii nilisema âStewart, Asante kwa kila kitu. Wewe ni mwanaume mzuri sana. Kuelezea ninavyokupenda peke yake haitoshi. Ninatafuta kitu cha kuubebea upendo ambao ninao kwako nakosa kabisa.
Mapenzi yangu kwako ni makubwa. Asante unanipenda nw unanijali. Sina kitu cha kukupatia zaidi ya penzi langu la dhati na la kweli. Nakupenda sana Stewart wangu, natamani kungekuwa na neno kubwa zaidi ya neno nakupenda ila hakuna na sijui nifanye nini ujue namna nakupenda. NAKUPENDA.â
Nikasoma huu ujumbe, nikasema âMungu wangu sijui nimeweza, sijui sasa nifanye nini. Nifute nianze upya au nifanye nini. Nikaituma ule ujumbe na kuweka simu yangu pembeni. Kwasababu nilikuwa naona aibu yaani. Nawaza sijui atapokeaje ule ujumbe.
Basi mimi nikaenda kuoga, na niliporudi simu yangu niliikuta ikiita. Niliitazama alikuwa ni Boss wangu. Nilitabasamu na kujisema âMy boss.â
Basi Nikapokea, Boss aliniambia âNdeana ni wewe?â
Nikamuuliza âvipi mbona sielewi, unauliza kuhusu nini tena.â
Akaniuliza kwa kimuhemuhe âumesema unanipenda si ndiyo, unanipenda sana. Umesema unanipenda.â
Nikatabasamu na kujibu kwa sauti ya chini âNakupenda sana.â
Akacheka sana akisema âNdeana unanipenda kweli, kama ambavyo mimi Nakupenda.â
Nikamwambia kwa masihara âumeniambia niwahi kulala leo ujue!!â
Akasema âacha utani Ndeana hapa serikali iingilie kati. Nakuacha vipi ulale na ndiyo kwanza penzi limeanza upya.â
Nikacheka sana.
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 86
Ni kweli inaonekana alikuwa anasubiri kwa hamu sana siku hii itokee. Alifurahi sana na hata aliniruhusu nilale kwa maana kazi ya kesho ni muhimu kwa maslahi ya Hotel yetu tunayofanyia kazi. Nilikuwa natabasamu tu muda wote. Moyoni ni kama nimetua mzigo mzito sana baada ya hili kutokea. Ninafuraha sana.
Ninakumbuka sana asubuhi hii, niliamka nikajiandaa vizuri sana. Wakati natoka nilikutana na baba na dada pale nje. Baba yangu alinitania akisema âsasa ndiyo nakuona vizuri zaidi. Binti yangu umependeza sana.â
Nilitabasamu na kisha baba alisema âDada yako amenielezea mwanangu. Mungu akubariki uwe na moyo huo huo. Asante sana. Nafurahi kuona mnapendana. Nafurahi sana.â
Nilitabsamu na kusema âNashukuru baba, kila kitu kitakuwa sawa.â
Baba alisema âNi furaha kuona mmoja kati ya familia hii anafanya kazi katika hotel ya ufahari. Nimekuombea usiku wote mwanangu ikawe heri kwako.â
Nikatabasamu na kusema âKila siku unanibariki baba yangu. Ina maana leo hutoshika kichwa changu.â
Baba akacheka na kusema âNjoo binti yangu.â
Nilimsogelea, nikainama mbele yake akabibariki. Na dada yangu pia alinibariki. Nikafurahi sana na kuondoka zangu.
Nilifika katika geti la Hotel, wakati naingia simu yangu ikaita. Alikuwa ni Boss na yeye aliniambia âNdeana kabla hujaingia ndani naomba njoo parking, ninataka kukuona.â
Nikashangaa nikisema âtunaweza kuonekana lakinu.â
Aliniambia âsijali nani ataona kwa maana mwisho wa siku kila kitu kitakuwa wazi. Hata hivyo kwanini tunajificha?, please njoo.â
Nikavuta pumzi yangu na kuelekea aliposema. Baada ya kufika tu alinionesha ishara nami nikamfuata. Alinifungulia mlango wa gari, nilipoingia tu alisalimia vizuri na kisha aliniambia âNakuomba geukia upande wangu, nataka nione sura yako nzuri.â
Nikatabasamu tu, nakumbuka alichukua mkono wake akanishika uso wangu kwa upendo.
Huku ananitazama usoni, kwa utulivu na mahaba mazito aliniambia âNdeana unaweza?, unaweza kusema tena yale maneno ya jana nikiwa nakutazama, unaweza kusema unanipenda sana ukinitazama, unaweza kusema mimi ni mwanaume wa pekee kwako ukinitazama.
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 87
Tafadhali totoo, niambie unanipenda. Nataka kuona midomo yako mizuri na laini yenye muonekano wa kupendeza ukiniambia namna unanipenda, Please niambie baby, nataka kukusikia, nataka kukuona, niangalie usoni na uniambie unanipenda, please baby.â
Mimi sijawahi kuwa na mwanaume mtulivu namna hii. Anaongea maneno unasisimuka mpaka unahisi kujikojolea kwa furaha. Nilijikuta namtazama machozi kwa mbali na nikasema nikimtazama usoni tena kwa kumaanisa. Nilisema âYes, Nakupenda sana Stewart, Nashindwa kujizuia hisia zangu. Kila nikitaka nikae mbali na wewe upendo unazidi. Your so sweet, Romantic, lovely, wewe ni waajabu sana. Ni kama vile mapenzi yameumbwa kwaajili yako. Unanifundisha kupenda, Nakupenda.â
Alinitazama kwa hisia, akisema âDont stop, usiache kuongea, usiache kunipenda. Endelea kuongea. Ndeana maneno yako yameumba kitu kipya moyoni. Maneno matamu yanayotoka kwenye kinywa na moyo wa mwanamke mwenye heshima, mtulivu, na mpole kama wewe ni sababu mpya ya mwanaume kuishi maisha marefu. Ndeana, usiache kuniambia namna unanipenda, ili niweze kuishi maisha marefu na kukupenda zaidi unatakiwa uumbe maisha mapya kwa kuniambia Nakupenda kila siku. Nakupenda Ndeana, nimefurahi sana na nakutakia kila jema katika kazi yako. Mungu akubariki.â
Nikamtazama na kusema âAsante sana, basi naomba niende.â
Akanishika mkono na kusema âtotoo si tukikubaliana uchoyo ni haramu.â
Nikacheka na kusema ândiyo baby dini hairuhusu ni haramu.â
Akasema âsasa mbona unaninyima busu langu.â
Nikacheka lakini nilimbusu na kisha nilitoka huku akiniambia âNakupenda.â
Tena wakati sijafika hata mbali alinitumia ujumbe akisema âNdeana wangu, umependeza sana. Umependeza.â
Nikatazama nyuma na kucheka tu kisha nikaelekea sehemu nahitajika.
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 88
Basi niliingia ndani nikasalimia baadhi ya wafanyakazi wenzangu wakawa wananitazama tu wananipandisha wananishusha. Moyoni nikawa najiuliza tatizo hata sielewi. Basi ilinibidi nitulie tu nimtafute Joan, aliniambia yupo chumba cha kubadilishia nguo na vitu kama hivyo. Nikapanda mpaka sehemu ya kubadili nguo. Nilipofika tu kitu cha kwanza nikauliza âKuna nini jamani, ninasalimia watu huko chini hawanijibu wananinyari tu.â
Joan alimtazama yule dada mwingine na kusema âVumilia tu, na itafika muda utazoea. Watu wamechukia kwanini wewe ndiyo usimamie hili na wakati kuna wakongwe na hawajapata nafasi.â
Nikavuta pumzi na kusema âMakubwa haya, sasa mimi hapa kosa langu nini?â
Yule dada mwingine akasema âhata sisi tumewaambia badala yake wakaanza kutusema na sisi na vitu kama hivyo yaani maneno kibao.â
Nikavuta pumzi na kusema âni sawa hata hivyo hapa ni kazini. Kazi yetu ni kufanya kazi na kurudi nyumbani. Mahusiano mazuri ya wafanyakazi ni muhimu ila hatuwezi lazimisha tusipotakiwa. Hatupaswi kukasirika ila kufanya kazi nzuri. Tuvae tukaanze kazi. Wanatakiwa kujifunza kutoka kwetu na sio kulalamika.â
Joan alitabasamu na kusema âsahihi kabisa.â
Basi tulivaa na baada ya muda ilikuja taarifa Boss anatuhitaji chumba cha dharula nasi tulitii. Baada ya kufika mule, ile naingia tu macho yetu yakagongana na kisha akatabasamu kiwizi.
Kisha akawa ananitazama na kunikonyeza. Wale wenye mahusiano ya hivi hapa wanaelewana, na mimi natabasamu ili mradi tu kumchanganya. Kisha nacheka kidogo unajua tena kunogesha penzi letu eenh.
Basi alitoa maelekezo yake kikubwa ilikuwa ni kuhusu wageni, hivyo usafi, utulivu na mambo kama hayo. Basi ndiyo hivyo alipomaliza macho yote kwangu, meneja naye alisema yake kisha walipomaliza wengine wote waliondoka, akabaki meneja, Boss na sisi watatu.
Mimi nilikuwa namsikiliza huku tunakonyezana na baada ya hapo sasa wakati anatoka si akajichanganya akasema âTotoo, Ooh sorry!!, sorry!!, Ndeana all the best na Team yako.â
Nikashtuka na kisha kuzuga nikajibu âasante sana boss.â
ðððððð ðððð ðð ððððð ðððð ððð: 89
Na wengine wakajibu hivyo, kisha Joan akanitazama na kusema âtotoo!!â
Nikacheka nikisema âYes, dada yangu aliyeniunganisha hapa. Anapenda kuniita hivyo, anapenda sana sasa na Boss kazoea hivyo kutoka kwa dada.â
Nikazuga zuga pale, meneja akatoa maelekezo na akatuacha. Basi tukabaki tunacheka tu huku nikisifiwa nimependeza nywele ya gharama na vitu kama hivyo huku wakifikiri nimetoka familia nzuri kumbe kumbe familia yangu inanitegemea nipambane mambo yaende sawa.
Chuki, wivu, majungu na vitu kama hivi havikosekani kazini. Kwasababu nimepitapita mahali basi hili halinipi shida kabisa. Halinisumbui mimi watajua wenyewe.
Wageni walianza kufika, nasi tuliwapokea. Wageni hawa walikuwa ni wengi sana. Yaani tofauti na ambavyo tulikuwa tunategemea. Kulikuwa na viongozi wa nchi, kulikuwa na watu wa mataifa mbali mbali. Tulifanya kazi sana siku hii, tulifanya sana kazi. Nakumbuka kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja ndiyo mkutano wao ulikuwa unaisha.
Basi wakati watu wanatawanyika, ninakumbuka niliitwa na huyu mtu mkubwa sana kwenye ule mkutano. Ni mmoja kati ya viongozi wakubwa sana.
Alinisimamisha na aliniambia âAsante sana kwa huduma nzuri, hakika sikuwaza kama Tanzania kuna huduma nzuri kama hizi.â
Nikatabasamu na kusema âkaribu sana, na sisi pia tunayo furaha kufanya kazi nanyi.â
Akatabasamu na kusema âhuu hautakuwa mwisho, tutafanya kazi pamoja na nitaleta na wengine. Mnastahili pongezi.â
Nikatabasamu na kumjibu âtutafurahi sana.â
Akacheka akisema âUnaitwa nani muhudumu mrembo kuliko wote.â
Nikacheka na kumjibu âNdeana, naitwa Ndeana.â
Akasema âwaoo!!, Waoo!!, jina zuri kama wewe ulivyo. Wewe ni mzuri sana. Natumai tutazunguka zaidi. Naitwa Mr Tarick. Here is my busness Card.â
Nikapokea na kusema tu âNashukuru sana. Asante.â
Akatabasamu na kuanza kuondoka. Ile mimi nageuka nyuma ili nibebe vitu vyangu nakutana na uso wa Boss, hakuwa na furaha. Niliita âBoss!!â
Alinitazama na kusema bila hata tabasamu âNifuate Ndeana.â
ð€£ð€£ð€£ð€£kivumbi leoððmjue leo ilikuwa nisipost nimebanana hatari ila nilipokumbuka ni haramu weee nikakurupukað€£ð€£ð€£ð€£ðð»ðð»ðð»ðð»
MWISHO WA SEASON TWO
SEASON THREE IPO WHATSAPP KWA SH 1000 UNAISOMA
ðµðððð ðð ðððððð ðœðð ðððð ðŽ ðððð 0743433005 ðððð ðšð®ð¶ðºð»ð°ðµð¶
ðŒðððððð ððððððð ðŸðððððšðð ððððððð ððððð +255743433005 ððððððð ðððð
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni