MY WANGU sehemu ya 36 & 37
Sitaki kukumbuka ata zile nguvu nilizipata wapi .Yani nilimpiga kibao cha maana. Mlige akashika shavu ata haamini. Akasema faridah please nisikilizeeee. Yani hajaongea lolote nikamtandika kibao cha pili.
Nyiee hii siku nilichafukwa mno. Mnajua uyu baba kanipita umri mnooo. Ila nilimuona kam mtoto. Nilikuwa na hasira sana. Niliumia sana .kiukweli nilimwambia mligi. Kuanzia leo mm na ww basi. Mligi akasema hapana sio kweli we nipige tu unavyotaka ila nataka tuelewana nakupenda farida ntakuelezea mengine mke wangu please . Mi sikutaka kumsikiliza nilimsukuma kw nguvu mpaka akaanguka chini
Kisha mimi sikugeuka tena nyuma nilikimbia sana kuelekea nyumbani nililia mnoo uko njiani . Moyo uliuma. Jamni niliumia moja kwa moja mi nilienda kwa kina yusta kwanza mana nilihisi namuhitaji kwa uo mda .nilimkuta nje kwao anaosha vyombo. Yani nilifika nikajibwaaga chini nikaanza kulia kwa nguvu. Tena kwa kwikwi mpaka natetemeka . Nyie yust alishanga akaniuliza farida vp .umefiwa kwani. Nikasema yust simtaki mlig. Simpendi na namchukia sana . Simtaki mimi ata kumsikia .nililia nyie yusta akiniinua kwa akuniburuza akainiingiza chumbani kwake. Nililia jamani . Mpaka yusta anambia taratibu basi utajiumiza kwani shida nn. Nilimwambia mlige mlige alikuwa ananidanganyaaa. Nyie nilimuelezea yista kwa kulia na nikiwa na mchungu sana moyoni yani nilikuwa nalia mnooo. Yust akasema yani uyu mlige kumbe ana date kweli na zahara na mimba ni yake. Nikasema ndio ni kweli kabisa
Mnajua ata yust alinionea huruma sana. Mana anaelewa kabisa ni kwa kiasi gani mm nampenda mlige. Yani yust anaelewa sana .ni kwa jinsi gani nampenda yule baba. Mapenzi yanauma sana. Nililia sana😭😭😭😭. Nikisema sitamini kuwa nae tena .namuona ni mwanaume muongo na. Asiyekuwa na msimamo. Mana mm na mlige tuna kama miez 6 tupo katika mahusiano. Alafu yule madame alisema mimba yake ni ya miezi 3.Nikajua kabisa kuwa mlig kanisaliti apa kati. Na wala sio mm nimewaingilia katika mahusiano yao. Niuliumia sana ila yust alinituliza sana ila kiukweli sikuwa sawa .jioni ilibidi niondoke tu. Mana nilijua mama yake yust ataludi na akinikuta katika hali ile itakuwa sio sawa. na yista akanisindikiza mpka kwetu.
Ase nilivyofika nyumbani nilijikaza mama asijue ila mama aliponiona alinliza shida nn mbona kama haupo sawa..Nikasema hamna mama mbona nipo powa tu . Ila wapi nyie . Niliingia chumbani kwngu nililia kweli kweli mpaka pressure jlikanipanda. Na pumu ikaja nikawa napumua kwa shida mnoo. Nyie kumfumania mwanaume au mwanamke unayempenda kunauma mnoo. .yani mpaka.kupumua kulikata.mama aliponiona alichanganikiwa. Akamuita mzee .bibie mimi nikabebwa mpka hospitali. Yani ile kufika tu .niliekewa dripu tatu za maji Apo apo. Nyiee nilibanwa aseee yani mlige alijua kunikomesha a. Wazazi waliangika na mimi pale siku nzima.na nikalazwa kabisa. Nikaja kutolewa kesho yake j pili jioni kabisaa. Ase bado sikuwa saw kabisa. Mpaka amma alisema mh hii homa kweli imekukamata mwanangu kesho nitampigia simu mwalimu wako mligi kumpa taarifa. Nyie nikamwambia mama ukimpigie mlige mwambie sipo nyumbani . Mana hapendi uteseke wakati upo nyumbani labda uwe hospital na ulazwe . Nilisema hivyo ili uyo mlige asije akaja kutaka kuniona apa nyumbani.
Basi bwana kma masihara shoga yenu sikuenda shule homa bado ilinikamata mno nikawa naendelea nayoo. Ila sasa jioni yusta ndio alikuja kuniona akanisalimia pale . Bado alikuwa sawa nilikuwa mnyonge mno. Akanmbia pole sana shoga. Ila lazima upige moyo konde na maisha yaende. Faridah ww ni mzuri sana . Yani ww ni mzuri aswaa una sura .una shepu na tabia nzuri huwezi kukosa mwanaume. Kama yeye anakuona cha nn wapo kina fahidi mwanajiuliza watakupata lini. Nikasema sawa bwana..akanmbia sikia mlige kaniita leo ofsini kwake..et ohhhh kwa nn shoga yako hajaj shule.
Wala.sijambakisha nimemchamba apo apo. Nimemwambia ukweli.nimemuacha ofisini mimacho kodo. Nimemwambia kabisa sababu ya ulichomfanyia kapata na homa..nikasema yan yust mimi simtaki tena yule mwanaume simtaki kabisa ni muuaji kabisa. Yani simtaki kabis kwenye maisha yangu. Apo naongea uku nalia . Basi yust akaanza kunibembeleza akanmbia bassi nyamaza haitajiyokea tena hii kuwa na amani. Basi nikatulia na jioni akaludi kwao.ila sasa usiku mzima nalia tuu
Yani kila nikikumbuka mahaba ya mlige mwenzenu nabaki kulia japo kimya kimya yani silalai nakula kwa tabu na kulia ndo sana.mama anshangaa kila nikiamka.naamka na homa..na sikuenda shule week 3Homa haishuki kabisa mapka mama akawa anachanganikiwa.
Basi baada ya week 1 . Ndo kidogo nikaona moyo umepoa . Yan apo na yust ndio alikuwa ananipa maneno ya furaha. Na alishanambia ntapata tu mwanume mwengine mzuri tu na tutapendana . So nikaona acha nisome bwana mapenz yashanishinda nisije nikaalibu na shule. Basi juma tatu ya iyo wiki ndo nikajikokote nikampitia yusta ila nilikuwa nimekonda sana .week 3 nilibaki kama mti yote mapenzi. Basi hii siku sasa ndo nikaingia shule ila kiukweli mi binafsi nilishajizatiti kuwa simtaki tena uyu mlig ..namuachia tu na mtu wake wazae. mpka washatiana mimba asa mimi nna nini. Akaa wala.sina . Sio siri nilionana na mlige uso kwa uso. Ila mlige ndio alikwepesha macho kunitazama .mi sikujali na wala sikumfatilia na mda wa darasani mi nikaingia zangu darasani. Yani ile tunaingia tu darasani. Kaja mwanafunzi anambia farida anakuita sir mlige ofisini kwake. Nikasema kamwambie faridah kasema hataki na ukome kumjua kama ulivyokoma katika zima la mama yako. Nyiee nilikuwa nna hasira nae kisha anakuja kuniita nini. nikaona yule mwanafunzi kama anagwaya kwenda kumwambia Nikamwambia unangoja nn ebu nenda kamwambie mlige hivyo. Mwambie ayo maneno kayasema faridah basi kale katoto kakaenda kwa mkuu. Sasa sijuh alimwambia aje laa. Sijuh kabisaa.
💗💗💗💗💗💗💗💗💗
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi