MY WANGU sehemu ya 41 na 42
Akanmbia unanijibu hivyo mm nakuuliza ww unanijibu mm hivyo. Nikasema ndio kwan wewe nani . Kwani unzani nakuogopa mm. Ilikuwa zamani sio sasa sikuogopi ata kidogo. Mlige akaningalia kwa hasira. Akaniilukia alinipiga mabao ya maana. Mpka nilipiga kelele mana nilihisi anataka kuniua. Kwa bahati mlango ukafunguliw akaingia sir . Akakuta nimekwidwa nadundwaa. Sir tupa ndo akamzuia mlige. Akamshika akamwambia nn sasa mlige utauua. Shida nn. Yani kanipiga kweli ila sikulia lia mie. Machozi tu yalikuwa yanashuka na mm nilikuwa na hasira nae sana. Mlig na yeye hakuweza ata kuongea. Anatwetwa kwa mahasira yake
Sir meja akanmbia nenda darasani farida. Mi nikanyanyuka nikaondoka nikawaacha. Yani mi ata darasani sikukaa nilienda kuchukua begi na mda uo uo mi nikaludi home kwanza kanipiga mno. Unajua ni ule ujeuri tu wa kukaza ila kanidunda aswaa mwili mpaka umetutumuka yani . Umejaa na kuvimba mnoo. Mie mdogo mdogo mpaka home. Nilivyofika nikamkuta mama alivyoniona akashangaa akasema we mbona umevimba sula.imekuwajee. nikasema kichwa kinauma ndo nimepewa ruksa niludi nyumbani . Mh wapi mangumi ya mlige ayoo. Mama akasema mh kichwa kinauma mpaka umevimba farida. Nikasema ndio mimi naenda kulala. Mama akabaki ananaishangaa tu. Nilivyoingia ndani ndio nililila sasa. Moyo unauma naona ata sijielewi. Na mkono ukawa unauma alinidunda mnoo. Kunipiga tu alinipiga jamani. Basi mie nikalia mnoo. Mpaka nikalala zangu. Mama akaja kuniamsha jioni sana . Akanmbia kaoge nishakuchemshia maji kisha uje kula. Basi mie nikajivuta na nikaelekea choon kuoga nilipotoka nakala . Nikameza dawa kisha nikapumzika.
Basi asubuh na mapema .mama ndo aliniamsha akaniuliza vp leo umeamkaje mana umekuwa mbovu siku hizi faridah. Kuumwa kil siku mwanangu nikasema mam mi nendele powa. Mama akambia shule unaendaa. Nikasema ndio mama naenda nimeamka swa. Mama akanambia sawa .aya jiandae sasa. Jiandae haraka mwanangu usije ukaenda kupigwa na uzingatie zaidi masomo si mnaona mpo kipindi cha mwisho .nikasema ndio mama naelewa hakuna shida
Basi harka nikainuka nikaanza kujiandaa kwa ajili ya shul.na niliwahi tu nikampitia yusta tukaanza kuelekea shule . Basi tukiwa njiani yusta akanambia ww kwani jana na ofisini na mlige imekuwaje .mana umekuja umechukua tu begi lako umeondoka kwa hasira. Nikamuonesha tu mkono. Bado ulivimba. Akanmbia mh ndo alikupiga hivi. Nikamuuliza na dua huoni imevimba ni yeye alinipiga mangumi ya maana. Ila wala sikulia nimemuonesha jeuri ya mwaka hakuamini mbona. Kunipiga kanipiga mimi kisha kalia yeye. Yust akasem shoga kuna mda namuonea huruma mlige. Jana kaja darasan kukuita tena . Sindo haukuwepo.nikamwambia kaondoka kaniita mieee. Anaanza kunihoji kwa hasra ni nani kakuandikia ile barua. Shoga mie kila nikimwambia sijuh ataki ata kunielewa. Mpaka nikabaki tu kimya .nikamuacha anaongea kwa hasiraa. Na kasema leo utamueleza nani alikupa ruksa ya kuondoka nyumbani ule mda. Nikasema ataangaika sana na ndo simtaki.
Basi tukafika mpaka shule.. ile tunaingia tu .getini kakaa yeye. Kaja mnoo. Mh mie natka kumpita .akanita we faridah simama apo. Mie nikasimama aknmbia njooo ofisini. Nlitaka kugoma ila yust akanioneshea ishara ya kwamba niende.basi mie nikaenda na yeye ananifaa nyuma.tumefika yupo serious mnoo. Na mie ndo nikazidi kujinunisha.her kavuta droo kanitupia barua nenda kamuite mzazi wako. Looooh mie nilivyojeuri nikaiokot ile barua sikumuuliza hii barua ya nn. Sikumuuliza kwa nn nikaite mzazi. Yani sikumuuliza chochote. Nikachukua barua nikasema.sawa. aknmbia hakuna kwenda darasni. Wala kurudi mstalini. Naomba uende nyumbani kuleta mzazi sas hivi. Nataka tujadili tabia zako . Umekuwa mtovu wa nidhamu. Na ukifanya masihara ntakufukuza na shulee . Kheee anatumia madaraka kwenye mapenzi. Mie nikasema sawa. Nikatoka zangu jee..ila nilivurugwa kuita wazazi tena. Kwa ajili ya utovu wa nidhamu
Mh basi niikuta yust ananisubir nje ya ofisi akaniuliza vp. Nikamwambiua knipa barua.nikamuite mzazi. Yust akasema toba mbona mambo yanataka kuwa mengi we kamuombe msamaha. Nikasema mm siendi kumuomba msamaha ata dunia ianguke. Ye si kasema nikaite mzazi sawa mi naenda kumuita baba. Yust akanmbia mh ebu kaongee na mlig yaishe. Nikasema.siendi . Kisha uyo nikaludi zangu mpkaa nyumbani. Nyiee mama alivyoniona . Akasema vp umezidiwa nikasema hapana . Nimepewa barua na sir mlig mnaitwa shule. Nyie mama akasema umefanyaje shule tena farida .nikasema mie wala sijafanya kitu. Mama akasema ngoja nimwambia baba yako ndo aende mie nikienda ntakudunda uko uko. Nyieee kweli mama akingia ndani akaongea na baba. Baba alivyotoka mie nikampa ila barua ya wito. Baba aknmbia umechelewa na leo nikasema hapana bbaa mie wala.sijachelewa baba akanmbia twende mama yangu. Tutajua uko uko. Na kweli mie mpaka shule na mzee msukuma.
Basi kukafika tukakalibishwa ndani na mlige.. mlige akamkaribisha baba vizuri. Mzee akasema nimekalibia kijana wangu .eeeh mtoto wetu kafanya nn tena. Au kuna nn. Mana namjua faridah nae .au kachelewa na leo. Mlige akanikata jicho na mie nikamuangalia vizuri wala sikumuogopa. Heeee mlige akasema mzee nimekuita .kwa sasa binti yako amekuwa mtovu wa nidahamu. Anajibidhana na walimu wa kike sana . Ana dharau mno mtoto wko. Amekuw ana tabia mbaya mnoo. Yani kwanza ata kunijibu mm haoni shida mtoto wako. Hana adabu ata kidogo na mabaya zaidi jana kakamatwa na barua ya mapenzi. Nyie akatoa ile barua akampa baba. Ambyo nilikamatwa nayo jana.kheeee baba akaanza kuisoma mh niliogopa . Mana mimi sikuwahi kuwa na tabia za hivi kabisa. Nyiee mlige akuishia apoo. Alijaza maneno mpaka yasiyokuwepo. Et mpaka nataka kupigana na walimu. Et sina adabu . Natukana mpaka wenzangu darasani. Jamani mi skuelewa nia ya uyu baba. Alafu akamalizia kwa tabia zake hizo . Ntamsimamisha shule mpka skku ya mtihani wa nec ndo nimuone apa..khaaaaaa mpaka nilishangaa
💗💗💗💗💗💗💗💗💗
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi