MY WANGU❤️ sehemu ya 56 na 57
Mh basi nikajitahidi tu pale. Kusoma mpaka saa 5 ndo prepo .inaisha tukauruhusiwa sasa kuludi bwenini. Basi tumefika bwenini. Akaanza zaituni akasema nyiee mmemuona yule mkaka wa kiarabu mzuri yule mmemuona. Au nimemuona mwenyewe. Mie nikacheka nikasema na mm nimemuoa . Prisca akasema ahaaa mnamzungumzia zayd. Mi nna story zake.nna rafiki yangu wa form six. kanisimulia.si mnamzungumzia yule zayd wa form six. Prisca akadakia akasema ndio ndo uyo. Ndo kafanyaje
Zai akasema yule bwana . Ndo kaja jana . Nasikia alipewa suspension. Alikamatwa. Na barua za wanawake za mapenzi . Mh mbona nikaanza kuchoka. Nikasema mh makubwa. Zaituni akasema yule kaka wanamsimulia ni maraya kweli kweli. Ila sasa ni anagombaniwa mnoo. Ao form six mpaka wanapigana na mwenyewe ni ana dharau kwanza asalimini na mtu na hamjibu mtu salamu ukimsalimia pale alipo..na hana mda na mtu..watu wanampigania apoo anawacha anasepa zake. Alafu sasa kwao wana pesa chafu . Wanapesa kweli kweli. Nasikia ni mtu wa dar. .mh mimi nikashangaa mbona nimekutana nae na kanaichangamkia mno. Tena mpka kaniokotea na na vitabu vyangu na msamaha kaniomba kwa kunigonga. Alafu uku nasikia story nyengine. Basi prisca akasema mh ila yule mkaka ni mzuri jamani. Uwiiii mungu kamuumba na ana nywele mpamka ana bana na shule wanamuachia
Zai akasema wee nae waarabu si wana asiri ya nywele nasikia yule ata akinyolewa leo baada ya siku 5. Nywele teali. Ndo mana anaambiwa azibane tu. Mh kwa uhandsime ata mm nilikubali. Yni hii siku tulimjadili sana zayd yani aswaaa. Kila kitu tulimchambua. Basi tukalala.saa 8 kwa kumzungumzia zayd tu. Na asubuh na mapema tukaendelea na ratiba za masomo. Nilikuwa namuona sana zayd mstarini. .mana mstarini ndo form five tunachanganyika na form six. Ila sasa darasani ni story za zayd tu. Ni anavutia sana uyu kaka .lazima umeongeleeee tu. Yani sio sisi tu tukiokuwa tunamsifia zayd kuwa ni mzuri .ila ni wadada wengi
Basi siku iyo bwana nilikuwa nipo na shoga zangu cafe. Apo kuna sehemu wanauza chipsi kabisa.na sie hatukutamani kula ugali siku iyo. Na mie pesa baby si ananipa sina ata shaka.so tukaamua tukanunue chipsi. Basi tukafika tukaagiza na kila kutu pale. Tukawa tu tunasubilia pale. Mh tukiwa pale.akaingia zayd na mkaka mmoja kaongozana nae .kwa jinsi walikuwa wanaongea na kucheka. Ni kwamba alikuwa ni mshikaji wake yule. Basi walivyofika pale yule zayd akaningaalia ssna kisha akatabasamu. Nyie ana tabasamu zuri like woow. Akanmbia ahaa nakukimbuka unaitwaga faridah si. Ndio. Nikasema ndio akanmbia ahaa powa . Ngoja nikulipie chipsi apa.akachomoa pochi yake kisha akatoa elfu 30 akanipa. Et shika utalolipoa chipsi hiii. Mh nilisita kupokea kabisa ile pesa mm. Yani kma nilizubaa hivo. Zaituni ndo akanistua akanmbia we faridah si unapewa pesa ww. Basi mie nikaipokea ile pesa kisha nikasema asante. Akanmbia usikonde. Kisha uyo na rafiki yake wakaondoka. Mh wanafunzi wa kike walokuwa pale waliniangalia jamani. Mnajua waliniangalia mpka nikawa naona aibu sasa
Basi mi nikachukua ile pesa yote nikampa zai nikamwambia lipia tu chipsi ili tule wote. Na kweli shoga akalipia tukaongezaa na vipaja vya kuku na sooda ila pesa ilibaki. Tukala kimya kimya kisha tukaludi doom. Tulivyoludi tu prisca akaniuliza we kumbe unajuna na yule zayd. Nikasema hapana awala hatujuani ila ni siku moja tu ndo tulionana . Tiligongana akaniangushia madaftari yangu. Akaniokotea na akaniuliza na jina. Mh prksca akanambia we ukute anakutaka uyu kaka. Mana sio kwa kujichekesha kule leo alipokuona na pesa yake kakupa.bila ya kumumba. Mh nikasema kunitaka tena.mi sitaki mahusiano shuleni. Zai akanmbia we tulia bwana kwani kakutongoza. Si kakupa kwa upemdo tu ile pesa. Kwaiyo wla usimind bwana. Basi mie nikanyamaza kimya.
Basi jioni nikiwa najiandaa kwenda prepo. Mala akaingia mdada mmoja ata simjuh ila nahisi ni mdada wa form six. Nyieeee alikuja kishari uyu dada mmpaka niliogiopa. Aksema nataka kujua umu katika room anaitwa faridaha ndo nani kwanza .uyo anayejiona yeye ni mrembo . Ana tako sana nataka kumjua. Mie nikasem.a ndo mm kwani vp. Basi yule dada akanisogelea akanmbia naitwa shamira nasoma kidato kimoja na zayd .mie ndo mrs zayd orggg. Shule nzima wananijua kuanzia walimu. Matrani
Patroni .wapishi na kila mtu .binti kaa. Mbali na mwanaume wangu. We ni mgeni sana ata miez 3 hujamaliza shuleni apa. Nitakufanya kitu kibaya kweli kweli. Unaelewa we maraya mtoto. .zai akaingilia akasema ada uyu umaraya wake uko
Wapi?? Wewe ndo ukaongee na zayd .mana zaud ndo alimfata uyu akampa elfu 30 akanunue chipsi sasa ulitaka ukatae. Au waambea wako hawajakipa taarifa vizuri. Mana uyo zayd ndo kamshobokea faridah
Yule dada aksema unajifanya unajua kuongea sana binti. Wewe ni mdogo sana . Sisi ndo. Wakongwe wa hii shule my dear ntakufanya kitu kibaya. Mh zai akkakaa kimya. Prisca akasema sikia dada we nenda uyu tutaongea nae na atakaaa mbali na mwanaume wako mambo yasiwe mengi apa. Akasema naondoka ila ww farida h nikisikia tena umeonwa onaongea na mwanaume wangu . Itakuea kesi kubwa. Mie nikanyamaza kimya . Yule dada akaondoka. Zai akasema si niliwaambia mm. Uyo zayd ni marya apo shoga utatishwa na wadada wa form six wote kwa ajili ya uyo zayd. Wakati kakupa pesa mwenyee wala hujamuomba. Mie nikabaki kuguna tu. Kisha nikajiandaa nikaingia prepo. Aseee kwani manazani masihara .nikafatwa na wadada wawili tena . Wakaja kunichamba ey nikae mbali na mwanaume wao rooh .niliona uyo zayd ni maraya mh. Yani siku moja nimefatwa na wadada wattu . Wananitishia khaaaaa apa kazi ipo . Alafu wote ni wakubwa kwangu form six wenzie .nikaona uyu kaka mie nikae. Nae mbali kabissaa
Basi zikpita week mbili apo naongea na mlige kila week end basi ananisisitiza sana kusoma na kujitunza . Pesa ye ananitumia wla hakuna shida. Ila tu nipambane kusoma. Basi nikawa pia nikipata mda na simu .nawasalimu na wazazi. na. maisha ya shule yanaenda. Na tulikuwaa na walimu wazuri sana. Yani walimu wazuri mnoo mpaka rahaaa. Basi bwana ikakata miezi 3 mimi nipo zangu shule na apa rkkizo ndogo au fupi haturudi tunaludi kubwa ya mwez wa 6 na 12. Kwaiyo nikawa napamabana na shhule tu .
Hamuwezi amini. Ata mama mkwe alikuwa ananipigia kabisa siku za week end . Et ananisalimia. Mpaka rahaa yani . Basi .bwana siku iyo sasa ilikuwa ni j pili shiue ilitulia sana mana hii shile ina wakristi wengi kwaoyo. Wengi walikuwa kanisani.mie nikaona ebu ngoja nikajisomeee. Basi nikajiandaa kisha nikabeba vitu vuangu nikawa naelekea darasani. Nikasome kidogo. Mh ila naangaliaa mbele namuona na zayd nae anakuja uku nnapotoka mm. Basi mie nikajifanya kama.simuoni. nikataka kumpita kimya kimya ila zayd alinisemesha. Akasema ahaa mambo mrembo farida. Ila sikumjibu kabisa. Nilishajua kuwa karibu na uyu kaks ni kujitafutia matatizo na kutoikukaa na amani apa shuleni kwaiyo mm binafsi sikutaka kabisaa. Yani nikampita. Na moja kwa moja nikaingia clss. Nikaweka vitabu vyangu mezani na nikatoa sasa ili nianze kujisomea
Mh naona zayd nae akaingi darasani. Khaa kumbe alikuwa ananifatalia kwa nyuma et.. ila uyu kaka.
🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴🔴
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi