????NAEMA KWA MAMA*
*SEHEMU YA 36, 37,
*
*ILIPOISHIA*
**
" "" "Muhusika hapa ni Boss wangu.. Lazima awajibike...
Lidya aliwaza kimya kimya na kurudi ndani kisha kupita moja kwa moja hadi kwenye Meza za VIP walipokuwa wamekaa mabosi...
*ENDELEANAYO*
Alifika mbele kabisa na kusimama mbele ya boss wake.. watu walianza kumshangaa Lidya badala ya kuangalia Show ya uchekeshaji iliyokuwa mbele yao..
Kuna baadhi waliohisi ni msichna mlevi tu kaenda kule mbele au ni miongoni mwa wachekeshaji kaenda kwa kusudi la kutoa burudani pia.
Lidya aliendelea kumtazama bosi wake kwa sekunda kadhaa,
""" vipi mrembo mbona unakuja VIP wakati ulikuwa huko nyuma kwenye siti za buku tano.??
Mbona unaangalia kwa huruma au hujala chakula haya chukua pesa.. Aliongea Boss huku anamtazama Lidya kwa dharau sana na kutoa kibunda kidogo cha pesa na kumkabidhi..
Lidya alikasirika sana kwa zile dharau lakini hakuwa na jinsi.. Alipokea zile pesa na kuweka kwenye mkoba wake mdogo aliokuwa ameushika,
Lidya kwa kujiamini alimsogelea zaidi boss wake na kumshika kabalia kisha kuanza kumshushia kipondo...
Zilikuwa ni ngumi kama tatu tu zimetua kwenye uso wa biss lakini alikuwa amelegea utadhani kapigwa zaidi ya ngumi 30.
Walinzi wa boss waliinuka kwa haraka baada ya kuona hali siyo ya kawaida.. Ukumbi mzima watu waliinuka pia.
Waliokuwa VIP walianza kurudi nyuma kwa hofu...
""""Jamaaani mtulie.. Kila mmoja akae sehemu yake.. Aliongea MC baada ya kuona shuguli ni kama imeingia dosari..
Watu waliendelea kurudi nyuma wakati huo lidya ameshikwa na walinzi....
"""" Mwambieni boss wenu anielekeze alipo Mama Dayana.. Tofauti na hapo hakuna kitakacho fanyika hapa.. Aliongea Lidya huku anawatazama wale walinzi.....
Baadhi ya walinzi walisogea na kuanza kumfuta Boss wao damu usoni na kumuinua ili wamtoe njee kwaajili ya kumpeleka hospitali usiku ule.....
"""Nimesema huyu mwanaume hawezi kabisa kutoka hapa.. Mniambie kwa amani tu ni wapi alipo mama yake Dayana...
Aliongea lidya...
Walinzi kama wanne walikuwa wamemshika Lidya na mmoja wao alikuwa anatoa kamba ili amfunge lidya mikono..
Lidya baada ya kuona vile aliinuka kwa nguvu na kuwasukuma pembeni walinzi wote wanne..
Alianza kuwatembezea kipigo na sekunde kadhaa hakukuwa na mtu karibu yake zaidi ya boss pekeee....
Hata wanyabi waliokuwa wahusika na shughuli walishakimbia pia.
******
Baadhi ya walinzi wenye silaha na askari baadhi walikuwa wameanza kusogelea ukumbi kwa kujihami sana kwasababu walishajua mtu wanae enda kumkamata siyo wakawaida....
Lidya hakutaka kuchelewa pia akiwa ndani ya ukumbi alitazamakila kona ya chumba na kubaini kuna milango ya usalama pia...
Kwenye kumbi kubwa au ndani ya majengo makubwa kama mlimani City ni vyema kukawa na milango ya siri kwaajili ya dharura..
Milango ile hakuna mtu wa kawaida anaeweza kujua labda awe na mafunzo ya usalama..
Kuna alama maalum huwa zinawekwa kwenye maeneo ya dharura ili waokoaji na watu wausalama waweze kujua na kuzitumia wakati wakuokoa watu...
Lidya aliona miongoni mwa sehemu za kujiokoa au kutorokea ni pale.
Alisogea hadi kwenye pembe ya ukuta kulipokuwa na alama.
Lidya alichukua meza nakuanza kubamiza kwenye ule ukuta sehemu yenye alama.
Mara nyingi ukuta kwenye sehemu zile huwa ni mlaini kuvunjwa na ndani yake kuna njia za kupitia chini kwenda kutokea sehemu nyingine kabisa njeee ya ukumbi..
**
Wakati huo walinzi pamoja na baadhi ya askari waliokuwa na silaha walikuwa wakinyata kuukaribia mlango wa ukumbi..
Walifika hadi mlangoni ila kila mmoja alikuwa anaogopa kuingia japokuwa walikuwa na silaha mkononi.
Mmoja alijitosa na kuingia huku anaangalia kila pande akiwa tayari ameikoki silaha yake tayari kufyatua risasi..
Wenzake pia waliingia kwa pamoja wakiwa wameshika silaha zao...
Waligawanyika na kuanza kukagua kila pande ya ukumbi ule mkubwa wenye meza za kutosha na viti vingi...
Kila mmoja alikuwa na hofu sana kwasababu hakuna aliekuwa anajua ni wapi lidya kajificha...
Walianza kupekua kila kona lakini hawakufanikiwa kumuona Lidya wala Boss wake...
ENDELEA.......
*37*
Wakiwa wale walinzi na askari wanaendelea kumtafuta Lidya na boss wake, ilikuwa ni kama nafasi kwa akina Lidya kuendelea kufika mbali ndani ya njia ile ya siri..
Ilikuwa ni njia ndefu sana... '''Wakiwa wanatembea waliona kama wameanza kukanyaga maji machafu na harufu kali ilianza kutoka, ghafla hewa ilikuwa nzito na kuwafanya waheme kwa taabu sana..
Giza la chini ya mfumo huo ulikuwa ukiwafanya wazidi kuwa na hofu na wapi wanaelekea....
"" Lidya tunaenda wapi jamani.. Nisamehe mimi.. Nitoe humu tutakufa hakuna hewa, nakuomba nitoe jamani, najua ni wapi alipo huyo mama na nikitoka tu nitaamrisha aachiwe na sintojaribu tena kukufuatilia jamani....
Aliongea kwa shida sana boss..
Lidya alitulia kama hamsikii aliendelea kumvuta hadi wakafika kwenye ukingo fulani..
Kulikuwa na kizibo cha chuma juu ya njia ile ya chini..
Kazi iliyokuwa ngumu kwa wakati ule ilikuwa ni kuifungua kizibo kile cha chuma..
Lidya aliinua mikono yake na kujaribu kuusukuma ule mfuniko wa chumu lakini haikuwa rahisi kama alivyo dhani. Ulikuwa ni mfuniko wa kuzungushwa ili ufunguliwe na siyo kuusukuma tu.
Lidya alijisachi na kutoa simu yake mfukoni.. Alitaka kuwapigia maafisa wenzie ili wapate msaada lakini mtandao ulikuwa ukigoma kuruhusu simu kupigwa..
Kila akipiga alikuwa akiambiwa network fail..
Lidya alichoka na kubaki anamtazama tu mzee aliekuwa amechoka sana pia kwa kupita njia ya shida na kukosa hewa nzuri kwa muda mrefu.
Dakika kama mbili zilipita huku kila mmoja akiwa amechoka..
Hali ya hewa ilizidi kuwa nzito sana mule ndani..
"" Uuuuhhhh.. Hapana jamani Mbona kifo kinatufikia kabisa hapa.. Aliwaza lidya...
Au turudi tutokee kule kule jamani.... Aliendelea kuwaza lidya.....
Umbalia wa kutoka walipo na kurudi hadi mlango walio ingilia ulikuwa ni mrefu sana.. Lazima ingewagharimu uhai......
Kwa haraka lidya alikishika tena kile kizibo cha chuma kilichokuwa juu yao na kuanza kukisukuma kwa nguvu.
Alitumia nguvu sana lakini bado kilimshinda..
""""" Hembu sogea hapa we mzee. Unaleta uboss hadi kwenye mazingira kama haya. Tutakufa shenzi wewe..
Aliongea Lidya akimuelekeza boss wake aliekuwa amesimama tu pembeni badala ya kutoa msaada kwa mwenzie..
Mzee alijisogeza karibu na lidya na kuanza kusukuma kile kizibo...
Wakiwa wanaendelea kukisuma, Ghafla walianza kusikia vishindo vya watu vikikanyaga kizibo, vilikuwa kama vinakimbia vile...
Ilionekana ni watu wengi kiasi fulani waliokuwa wakikimbia..
Kwambalia sana Lidya alisikia.. """Mbagala Rangi tatu ya Mwisho hii.. Mjipange vizuri, kama hutaki shida ya daladala nunua yako.. Ilikuwa sauti ya Konda wa daladala akiongea..
Hapo lidya alitambua huenda wakawa kwenye kituo cha daladala hivyo wakitumia nguvu kugonga kile kizibo huenda watu wa njee wangesikia na kupata msaada..
Lilikuwa ni wazo la haraka alilowaza Lidya..
Lidya alianza kubamiza kile kizibo kwa mikono yake migumu iliyokomaa kwa mazoezi makali ya jeshi..
""" msaada jamani tunakufaa... Aliongea lidya huku akiendelea kubamiza kile kizibo..
Kimya kilitawala kwenye eneo lile na hakukuwa na kelele tena za daladala..
Lidya aliendelea kugonga kwanguvu sana,
Baada ya Muda kidogo alikia kama kile kizibo kinafunguliwa...
Lidya alishusha pumzi zito na kuendelea kugonga ili kuomba msaada..
Kizobo kiliendelea kufunguliwa kwa nguvu sana hadi kikatolewa...
Hewa nzuri ya njee iliingia ndani na kufanya wauone uhai kwa mara nyingine...
"" Wewe ni nani.?? Mnatoka wapi huku.???
Aliongea mtu mmoja aliekuwa akiwamulika kwa tochi... Muda huo watu walikuwa wakiongezeka kuzunguka lile shimo la mfumo wa maji taka kuona maajabu..
ENDELEA.....
Full 1000
Whatsp 0784468229.