We Kula Tu Binamu
Sehemu 1
Kwa miaka mingi, familia yetu ilikuwa imegawanyika kwa sababu ya kazi na maisha ya mjini. Mimi nilizaliwa Dar es Salaam, lakini kila likizo, nilikuwa nikipenda kwenda kijijini kwa bibi, Kijiji hicho kilikuwa pembezoni mwa milima ya Lushoto.
Siku moja, mama aliniambia kuwa msimu huu wa likizo hatungeenda peke yetu. "Binamu zako wa Tanga nao watakuwepo," alinitangazia kwa furaha. Sikutilia maanani sana, kwa sababu tangu utoto sikuwa nimewahi kuwa na ukaribu nao lakini sasa nilikuwa kijana wa miaka ishirini na mbili, na dunia yangu ilikuwa imejaa hisia tofauti.
Tulipofika kijijini, maisha yalirudi polepole: kunywa maji ya kisima, kula ndizi mbivu, kucheza bao na kusikiliza hadithi za wazee. Ilikuwa dunia nyingine kabisa kutoka kelele za jiji.
Ndipo nikamuona Asha binamu yangu wa pili, binti wa shangazi yangu mdogo. Alikuwa amekua! Hakika hakufanana na yule msichana mdogo aliyekuwa akikimbia mitaani akiwa peku. Sasa alikuwa na umbo la kuvutia, ngozi laini ya kahawia na tabasamu lililoweza kuyeyusha hasira yoyote.
Kwa siku chache za mwanzo, Asha na mimi tulikwepa kukutana sana. Iliibuka ile aibu ya asili ya binamu kukutana baada ya muda mrefu. Tulionana kwa mbali, tukitupiana tabasamu za haraka na kuendelea na shughuli.
Lakini hatimaye kijiji kidogo kilitufanya tusalimiane zaidi kwenye kisimani, msikitini, au sokoni tunapotumwa. Urafiki ulianza kuchanua taratibu kama maua ya porini baada ya mvua.
Siku ya Jumamosi mchana, bibi aliandaa sherehe ndogo ya familia. Kulikuwa na wali wa nazi, mbuzi wa kuchoma, na maandazi yaliyopikwa kwa mikono ya shangazi. Tuliketi wote kwenye kivuli cha mti mkubwa wa mwembe, tukicheka na kuhadithiana.
Wakati wa kugawa chakula, bibi alimtuma Asha aniletee chakula changu. Alikuja huku akicheka, akining'iniza sinia la chakula kwa mkono mmoja.
"We kula tu binamu," alisema kwa sauti ya kucheka, akiweka sahani mbele yangu.
Nilitabasamu. “Asante mama,” nikasema kwa mzaha.
Aliketi karibu nami, tukaanza kula pamoja. maisha ya shule, marafiki wa utotoni, ndoto za baadaye. Kila dakika ilipoendelea, nilihisi ukaribu wa ajabu ukimea kati yetu ule wa kirafiki, lakini pia wa hisia za ajabu zilizojaa hewani.
Baada ya chakula, watu walikimbilia kucheza kiduku mbele ya bibi. Lakini Asha na mimi tulibaki chini ya mwembe, tukibembea kwenye matawi madogo.
"Umemiss sana kijiji au umekuja kwasababu ya maandazi ya bibi?" alinicheka.
"Nimekuja kwa sababu yako," nilijikuta nikisema bila kufikiri. Nikakuna kichwa changu kwa aibu.
Asha alinitazama kwa jicho la kuibia, halafu akageuza macho chini kana kwamba hajalisikia lile neno..