????CHUMBA CHA MPANGAJI
ILIPOISHIA.....
Nyie mabinti wa mjini mnajidai mnajua kuchezea watoto wa watu kwa kuwaloga ili mmiliki mali zao.. Sasa kwa huyu Mgongo wa Dodoma naomba usahau hilo.. Mali ya mwanangu hakuna mpuuzi wa kuichukua.. Nakupa siku saba mwanagu arudi kwenye hali yake..
Aliongea yule mama na kuinuka kisha kuondoka zake....
Dalali sele aliinuka pia na kuwatazama akina Nasra na Saidi kisha kuondoka zake....
Nasra aliinamisha kichwa huku anawaza na kububujikwa na machozi kama maji..
Alitegemea huenda mama wa Saidi kaja angeweza kusaidiana nae kurejesha hali ya mwanae sawa kumbe ndio matatizo mapya yanaanza..
"" "" " Eeeeehhh Mwenyezi Mungu. Ni mtihani gani umenipa mimi mja wako.. Au kuna sehemu nimekukosea muumba wangu.??? Naomba msamaha wako ewe muweza wa yote....
Aliongea Mwenyewe Nasra na kuchukua kitambaa fulani kwenye kochi na kujifuta machozi pamoja na makamasi yaliyokuwa yanambubujika kwa pamoja...
"" "" Dada Chiku. Huyu mama anatoka wapi,.?? Mbona anawaka kiasi hiki huyu mama.??? Aliongea saidi na kusogea karibu na Nasra kisha kuanza kumbembeleza..
Saidi alikuwa anapenda sana kumuita Nasra kwa jina la Chiku..
Nasra aliingia tena ndani na kunawa uso kisha kupaka mafuta upya na kutoka...
Alimkuta Saidi bado amekaaa tu Sebuleni anaangalia Tv huku anacheka...
"" "" Saidi. Naomba ukae hapa nyumbani kwa kutulia.. Kama hupendi niendelee kuteseka na kulia, basi nakuomba sana usitoke humu ndani..
"" " Mimi natoka sasaivi kwenda kazini. Nakuomba basi njoo ufunge Geti na urudi ndani utulie Saidi.. Nakuomba sana...
" "" " Sawa dada Chiku.. Nakutakia kila Kheri mbele ya mboni ya macho yako.. Usifikirie mengi sana juu ya nyota inayong'aa upande wa kusini mwa Dunia..
Angalia nyota ya Magharibi ndio inayomulika ulimwengu kwa uangavu wa hali ya juu..
Haya unaweza kwenda..
Aliongea Saidi na kuinuka kisha kumshika Nasra Mkono na kuelekea nae hadi lilipo gari..
Nasra alipanda na alifunguliwa vyema tu gati na Saidi kisha gari likatoka..
Saidi alirudishia geti na kurudi Sebuleni..
Saidi alishusha pumzi na kutulia kimya utadhani hana matatizo ya akili, aliwasha TV na kuanza kuangalia baadhi ya vipindi...
Alishika rimoti na kuweka chaneli ya wanyama kwasababu alikuwa mpenzi sana wa kuangalia mambo hayo...
Saidi aliinuka tena na kwenda kufunga vizuri mlango wa Sebuleni na kuingia chumbani kwake..
Alifungua begi lake na kuangalia hati zake za nyumba....
Aliziona zote zipo sawa..
Aliendelea pekua zaidi ndani ya begi na kuchukua simu yake ndogo iliyokuwa silent kisha kumpigia mmoja wa wafanyakazi kwenye duka lake la Jumla..
"" "" Rojas, mambo vipi mzee, aliongea Saidi na kuiweka ile simu Laud speaker..
"" " Poa brother.. Unaendeleaje.. Alijibu huyo Rojas
""" mimi nipo poa kabisa.. Nimepata nafasi ndogo hapa nikaona nikucheki..
Vipi pesa za mapato yote unaingiza kwenye account.??
Hakikisha na wafanyakazi unawalipa kwa wakati.. Kama kuna tatizo nitumie tu ujumbe. Kama sintokujibu kwa wakati basi ujue nipo bize.. Lakini nikiwa Free nitakuwa nakupigia...
Aliongea Saidi huku anachungulia Dirishani kama kuna mtu anatokea au laa...
"" " Sawa Broo...
Usijali kila kitu kipo sawa. Nakutakia kila la kheri katika kumpata mke mwema..
Aliongea Rojaz na kukata sim...
*******
Kumbe saidi hakuwa na Tatizo lolote la Akili lakini ukweli ni kwamba Dalali sele alikuwa na mpango wa kumharibu mwenzie na inasemekana kuwa ni tabia yake hapo mtaani..
******
Siku ya Tukio iliyo pelekea Saidi kujipatisha ile ajali Makusudi ilikuwa hiviiiiiiii
****
**
Mara tu baada ya Dalali sele kutoka Ndachi kwa mganga na kufanya mambo yake kama alivyohitaji yawe.....
Yule mganga alishika simu yake na kumpigia mwanae Rojas, kumbe Rojas yule mfanyakazi na msimamizi wa maduka ya Saidi alikuwa ni mtoto wa yule Mganga lakini Dalali sele hakuwa anajua kitu chochote...
"" "" Mwanangu Rojas, nakuomba sana mjulishe Boss wako kuwa kuna kijana fulani kaja hapa kwa nia ya kutaka kumfanyia dawa awe kichaa kisa ugomvi wa mwanamke...
Huyo jamaa nilimsikiliza tu na kumwambia kuwa nitamfanya Saidi kuwa kichaa..
Amelipa pesa yule jamaa na mimi nilifanya kazi ya uongo tu hapa...
Aliongea yule Mzee..
"" "" " Hembu ngoja baba... Nampigia Saidi ili asikie yote haya..
Aliongea Rojaz na kumpigia Saidi pia..
Ziliunganishwa simu tatu na walikuwa wakisikilizana Vyema tu...
" "" Mwanangu Saidi upo wapi.. Aliongea mzee baada ya Saidi kupokea simu na kujiunga na Mjadala huo.....
"" "" " Shkamoo mzee. Nipo nyumbani kwasasa ila nilikuwa nampango wa kurudi kijiweni kuokoteza tena mzee wangu...
Saidi aliongea kwa upole huku anawaza kuna tatizo gani hadi simu ziunganishwe vile....
ITAENDELEA...SEHEMU YA 09
CHUMBA CHA MPANGAJI
ILIPOISHIA.....
"" "" " Shkamoo mzee. Nipo nyumbani kwasasa ila nilikuwa nampango wa kurudi kijiweni kuokoteza tena mzee wangu...
Saidi aliongea kwa upole huku anawaza kuna tatizo gani hadi simu ziunganishwe vile....
" "" Sasa kijana. Kuna bwana mmoja anaitwa Sele ni Dalali mkubwa tu hapo mjini..
Leo kaja hapa kwa sababu za kumharibu binti mmoja anaitwa Nasra..
Lakini baada ya mimi kutazama kwa undani nilibaini kuwa huyo Nasra tayari ulishiriki naye kimapenzi..
Aliongea yule mzee...
"" "" Enheee mzee wangu.....
Saidi aliongea na kutulia ili kumsikiliza mzee vyema..
"" "" "" Yule dalali huwa namsaidia kwenye kazi zake nyingi sana hata dawa nyingi za kuoga ili apate mvuto kwenye kazi zake huwa nampa...
Pia huwa anakuja hapa akiwa na Dhumuni la kuwaharibu wake za watu wenye mali ili apendwe na apewe pesa..
Hayo yote huwa namsaidia na huwa anakuja kunipa majibu kuwa mambo yake yanaenda sawa..
Aliendelea kuongea mzee yule
"" "" Sasa leo kaja hapa kwa shida ya kukuharibu..
Daaahh hilo niliona hapana. Niliona haliwezekani kabisa kukufanyia ubaya mtu usiye na Hatia...
Saidi wewe ulimsaidia mwanangu kwa kumpa kazi na kumlipa vizuri bila hiyana yeyote..
Na mimi ndiye nilikutengenezea kinga yako inayokulinda na nilikusafisha hadi ukashinda hiyo bahati nasibu ya mpira na kupata mamilioni yale..
Sasa kwanini nikuharibu kijana wangu pasina sababu yeyote...
Aliendelea kuongea yule mzee..
"" "" " Saidi nakuheshim mwanangu na kama kuna tatizo uwe unanitafuta...
Nimejaribu kumuangalia huyo binti anayo nyota kali ya pesa..
Pia binti huyo nje na kazi yake anayo ifanya, anaonekana kama mpelelezi na huenda anayo kazi ingine ya siri ambayo ni ngumu mtu yeyote kuijua..
Nakuomba mpime huyo binti uone kama anayo mapenzi ya kweli na Umuoe.. Utaona mafanikio yatakavyo kumiminikia..
Alizidi kuongea yule mganga.....
Muda huo Saidi alikuwa kimya akisikiliza kwa umakini sana huku anawaza ni kazi gani ya siri ambayo huenda mpenzi wake anayo..
"" "" "" "
Mwanangu Saidi mimi nakupa moyo wa kuendelea kupiga kazi zako na kujiamini.. Hakuna ubaya wowote. Lakini huyo dalali atakuwa na mwisho mbaya sana aliongea mzee..
Saidi alitulia kimya huku anatafakari nini cha kufanya..
" "" " Basi Mzee wangu. Nimekuelewa.. Mimi leo nikiwa natoka hapa, nitajipatisha ajali ambayo haitoniumiza alafu nitajidai nimekuwa kichaa..
Nataka nipime uvumilivu wa huyu mwanamke. Je ananipenda kweli au kafuata pesa tu.??
Aliongea Saidi..
" "" "" Hilo ni wazo zuri sana.. Hata ukibaini mapungufu yake basi utaniambia tu na mimi nitamtengeneza atatulia sana...
Aliongea yule mzee..
"" "" Dogo Rojas. Kwasasa nitakuwa napatikana kwa sim ndogo tu..
Nitaiweka Silent na nitaificha mbali..
Kama kuna tatizo utakuwa unanitumia ujumbe na nitakujibu ninapo pata muda....
Aliongea Saidia na Mawasiliano yalikatwa na kila mtu aliendelea na Shughuli zake......
*****
Baada ya maongezi yale.. Saidi alishika sim na kumpigia mama yake kumwambia nini anataka kukifanya...
Saidi hakutaka kufanya kwa siri kwasababu aliogopa kumsababishia matatizo mama yake....
Na pia Saidi alikuwa wapekee na msaada mkubwa kwa mama yake.. Aliogopa kumficha mama yake kwasababu mama angesikia kuwa mwanae ni kichaa basi yule mama angepata hata Presha au matatizo mengine ya kiafya...
Saidi aliliamua kumwambia kila kitu mama yake mzazi..
Kwahiyo hata Siku dalali Sele anaenda kwa mama yake Saidi kumwambia habari zile. Yule mama alikuwa anaelewa mchezo wote...
Ni Sele tu ndio alikuwa haelewi nini anakifanya kwasababu kila mmoja alikuwa anamchora tu..
Dalali Sele kwa umbea na akijua anaenda kumkomoa Nasra, alimua kwenda kumwambia mama yake Saidi. Na ndio sababu mama yake Saidi kwenda kumtishia Nasra, Yote ilikuwa ni kumpima tu msimamo wa binti yule..
*******
Huo ulikuwa mpango wote wa Saidi hadi kuwa kichaa...
**********
**********
Siku ya leo baada ya Saidi kujua namna gani maduka yake yanaendelea, aliizima sim na kuirudisha chini kabisa ya begi lake kisha kurudi Sebuleni..
Kabla ya kukaa.. Alipata wazo la kwenda kukagua mabegi ya Nasra..
Aliingia chumbani na kufungua moja ya begi kubwa la Nasra..
Alianza kutoa nguo taratibu hadi chini kabisa ya begi...
Alikutana na mkoba fulani mdogo.. Aliutoa ule mkoba na kuanza kuupekua,
Aliingiza mkono na kushika kitu fulani kigumu cha Plastiki..
Saidi alishtuka na kutoa mkono wake haraka..
Aliingiza tena na kukishika hicho kitu kisha kukitoa...
Alikitazama na kuona ni Bastola...
"" "" Mungua wangu.. Saidi aliongea kwa hofu na kutetemeka sana hadi bastola ikadondoka chini...
"" " Huyu mwanamke ni jambazi jamani... Aliwaza Saidi na kuiokota bastola kuirudisha kwenye Begi..
Alifungua baadhi ya Zipu za kibegi kile na kukuta kitambulisho fulani kidogo kilikaribia kufanana na kitambulisho cha mpiga Kura..
Saidi alikitoa na kukisoma..
" "" " TANZANIA INTELLIGENCE AND SECURITY SERVICE (TISS) ...
Saidi alishtuka baada ya kukuta maandishi hayo na nembo ya taifa pamoja na picha ya Nasra kwenye kitambulisho kile..
" "" " Inamaana huyu Dada ni usalama wa Taifa..??? Aliongea Saidi na haraka alianza kurudisha vitu kwenye Begi kwa hofu...
Full 1000
Whatsp 0784468229.