*GENERAL SILI SILALI JUU YAKO* *01--05* *__________________________________* *SEHEMU YA 01* "Kikosi namba saba, wote mnatakiwa pared, leo jioni kutakuwa na ugeni, hivyo mjiandae"
Tulitoka mbio na kuelekea pared, mara tuu baada ya kamanda kumaliza kuongea hivyo, tulikuwa kwenye mazoezi, vikosi vyote tulikutana hapo, na baada ya hapo tulifanya pared yanguvu kidogo, na kisha alisimama kiongozi wa vikosi vyote, tulimpa heshma kwa kutoa sarut, aliitikia nae kisha alisema:
"Vikosi vyote makamanda, tunapaswa kufanya maandalizi, kwani kesho kutakuwa na ugeni, General Ethane atakuwa hapa, nadhani mnamjuwa, huwa hapendi makosa, hivyo tukitoka hapa wakuu wa vikosi wote tukutane ukumbi wa mkutano sawa"?
Wakuu wa vikosi vyoote, waliitikia na kutii amli ya kiongozi, kisha tulipomaliza mazoezi ya pared, tuliruhusiwa tukaenda mabwenini, kwani muda wamazoezi pia ulikuwa umeisha, tukiwa bwenini dada Catrine alikuwa akiongea na wenzie, nilimsikia:
"General Ethane ni handsome jamani, hata kama ninamchumba, na akatokea General Ethane akanipenda, simkatai ninampenda sana"
Na wenzie wote walisapoti hayo maneno, nilibaki nikiwaona kama wemevurugwa, kwa maneno yale nilikuwa naona niujinga, kwanza katika maisha yangu kabisa siamini kitu mapenzi, na sipo tayari kuyapa nafasi kabisa, kwa hapa kambini, mimi nimgeni sinamuda sana tangu nimejiunga na jeshi, hivyo viongozi wetu wakubwa nawasikia tuu majina, wengi siwajui hata kwa sura, ninao wajua ni hawa wa kambini tu, ndio maana niliona wanaongea upuuzi tuu, muda kidogo, kamanda wa kikosi chetu, alikuja na kusema:
"Laura, kesho asubuhi unione, kunakazi nataka nikupe"
"Sawa mkuu"
Nilijibu kwa heshma, na kisha baada ya kuondoka, wakina Catrine waliendelea kupiga stori zao, ambazo mimi sikuwa muumini wa hizo stori, nilichukua kitabu changu kinachohusu historia ya nchi na kuanza kujisomea, huku nikiwa nimejiegesha kwenye kitanda changu, napenda sana kusoma historia ya nchi yangu, baada ya muda tulienda kula chakula cha usiku, tulipotoka kantini tuliludi bwenini, nilipofikatu nilipanda kitandani, na kuendelea kujisomea hapo, hadi nilipitiwa usingizi, kulipokucha kama kawaida, alfajiri namapema tunaamka na tizi la kufa mtu, kisha kukipambazuka tunakutana pared, na baada ya hapo ukaguzi unafanyika, kisha tunatuhusiwa kwenda kupata kifungua kinywa, ni dakika tuu kisha tunaenda mazoezini kwa vikosi, nilipotoka kupata breakfast nilimfuata kiongozi wa kikosi chetu, na kumuitikia wito, aliniambia jana usiku kuwa asubuhi nimuone, anakazi anataka kunipa,
"Mkuu nimeitika wito, ulioniambia jana nikuone asubuhi, kunakazi unataka unipe"
"Ok, ninakumbuka, nione mida ya saa sita mchana, baada ya kutoka kupata ranch, sawa"
"Sawa mkuu"
Kisha baada ya hapo tuliendelea na mazoezi kama kawaida, tulifanya mazoezi mbali mbali, mengine magumu acha tuu, tulikuwa mchanganyiko wanaume kwa wanawake, lakini nilikuwa nijitahidi sana sio wakulalamika lalamika, kwani mazoezi yalikuwa yapamoja hakuna kubagua, lilifika lile zoezi la kutambaa kwenye matope, nilifanya bila kuogopa kitu, na hivi nilivyo mwembamba na kisura changu chaupole, hadi kiongozi wetu huwa ananikubali sana, napenda kujitahidi kuhakikisha sishindwi kitu, hiyo ndio staili yangu mimi yamaisha, sinaga marafiki, pia sina boyfriend, sijaona haja ya kuwa naye kwa sasahivi, huwa nipo kivyangu tuu mkimya sana, tulifanya mazoezi ya kila aina hadi yakutembea kwenye kamba, muda ulienda hatimae saa sita ilifika, tulienda kupata chakula chamchana kantini, tukiwa huko tunakula nawenzangu alikuja mkuu wa kikosi chetu, kikosi namba saba alikuja moja kwa moja nilipokuwa mimi nakula, na kuniambia:
"Laura! ukimaliza kula njoo ofisini kwa mkuu wa vikosi vyote, utanikuta huko sawa?
"Sawa mkuu"
Kisha mkuu wa kikosi chetu aliondoka, wakina Catrine na marafiki zake wote walikuwa wakinitizama, na kisha walianza kunong'ona nog'ona, sikuwafuatilia, nilijisemea kimoyo moyo ni kawaida palipo na wasichana zaidi ya mmoja, huwa hapakosi maneno maneno, hivyo niliwapuuza mambo ambayo hayanichumbui ngozi, niliendelea kula mala tu filimbi ilipo lia, kila aliekuwa ana kula aliachia chakula, na kuludi kwenye maziezi, nami nilienda ofisini kwa mkuu wa vikosi vyote, na kumkuta mkuu wa kikosi changu pamoja na mkuu wa vikosi vyote hapo, walipo niona walinikaribisha:
"Karibu"
"Asante"
Aliongea mkuu wa kikosi namba saba mkuu wangu:
"Anaitwa Laura Lewis, ni kruta wakikosi namba saba, kati ya wale ulioniambia nitafute, kwaajili ya usafi na kusimamia mambo ya chakula cha General Ethane, huyu ni mmoja wapo"
"Ok, sawa haya unaweza kumpeleka eneo la tukio, atamkuta mwenzie huko, naomba Laura mfanye vizuri, na haraka kwani muda pia umeenda, sio muda mrefu atakuwa hapa, nimkali sana sawa"?
Niliitikia na kusimama haraka, tayari kwa kwenda kufanya kazi niliyopewa, mkuu wa kikosi namba saba, aliniongoza hadi kwenye chumba cha muheshimiwa General Ethane, tulipo fika tulimkuta kruta mwingine , alipiga sarut kutoa heshima kwa mkuu wangu wakikosi kisha alijitambulisha:
"Naitwa Nancy mkuu natoka kikosi namba tisa namba yangu ni namba tano, nipo hapa kwaajili ya kufanya usafi, nimaelekezo kutoka kwa mkuu wangu wa kikosi"
"Ok sawa Nancy, kutana na Laura nikikosi namba saba, namba yake ni saba, nae yupo hapa kusaidiana na wewe"
Kisha Nancy alinipigia sarut, nami nilimjibu kwa sarut, ndio salamu zetu masoja, baada ya hapo kiongozi wangu muheshimiwa Jeff, alituelekeza kilakitu chakufanya, kisha akatuacha wenyewe, na kwenda kwenye mazoezi kusimamia, tulianza kufanya kilicho tupeleka hapo, tukiwa tunashugulika Nancy aliniuliza:
"Laura, unamjua General Ethane?
"Hapana simjui"
"Wewe unamuda gani kambini, hadi usimjue General Ethane"
"Ninakaribia mwezi sasa, nafikili ni wiki ya tatu"
"Ndio maana, alikuwa kasafiri alienda nje ya nchi, ni mkali sana, lakini nimzuri sana yaani handsome, na anamoyo mzuri mno"
"Ok, kwanini kila mtu anamsifia hivyo kuwa ni hb, inawezekana ni hb, kweli haya tunamuona akija"
Tulifanya kazi kwa kushilikiana, kilakitu tuliweka sawa, na tulifanikiwa kumaliza, na tulimuita kiongozi wa kikosi namba saba, kuja kukagua, alifurahishwa na kazi yetu tuliyoifanya, na kutupongeza kisha tulienda kwenye mazoezi yetu na yavikosi, baada ya muda mchache viongozi walikusanyika, na kutuambia tufanye mazoezi bila kusimamiwe kwa muda, na kisha walienda kumpokea General Ethane, alikuwa tayari kaingia, walimkaribisa na kisha aliingia moja kwa moja kwenye ukaguzi wa mazoezi, alizungukia vikosi vyote, alipofika kikosi namba saba, tulisimama na kumpa sarut kama saram ya heshima kwa mkuu wetu, na kisha alitupa inshara tuendelee na mazoezi, tuliendelea kufanya mazoezi, wakati huo alikuwa bado anatutizama, nilikuwa nafanya zoezi la kuparamia ukuta, kwabahati mbaya nikaanguka, nilikuwa nimepanda vibaya, alikasirika sana General na kunifokea kwa nguvu kisha hapo hapo akanipa adhabu"
Je unatamani kujua nilipewa adhabu gani endelea kufuatilia.......
Namba ya malipo 0742133100
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi