VYOTE NDANI GONGA94
MAHABA YA MZOA TAKA 23 ππ
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Nilifika nyumbani na baada ya mda mzoa taka nae alifika na kwakuwa karibu kila kitu kilikuwa changu sikutaka tena kuendelea kuishia na mzoa taka.
"Damian ondoka mbele ya macho yangu sihitaji kukuona tena" niliongea pasipo kumuangalia usoni.
"Siwezi kuondoka mpaka unipe nafasi ya kujieleza" mzoa taka aliongea.
"Uniambie nini!? yani uchepuke alafu uniambie nikupe nafasi ya kujieleza!?" nilimuuliza huku nikiwa bado na hasira.
"Najua nimekosea lakini mbona na wewe ulikuwa ukichepuka kipindi cha ndoa yako na ulikolezwa na penzi langu Irene!?" alijichanganya na kuongea kitu kingine kilichozidi kunikasilisha zaidi.
"Kwahiyo kumbe ndiyo sababu iliyokufanya utembee na huyo mwanamke wako!?"
"No sio hivyo Irene" Damian alijitahidi kujitetea ila sikutaka kumwelewa siku hiyo, niliamua kumtimua pia niliamua kuchukua funguo za dukani maana zilitumika pesa zangu kwenye biashara yake.
Kiukweli sikutaka kujali kama ndiye baba wa binti yangu.
Maisha mapya yalianza bira ya uwepo wa mzoa taka na sikujua ni wapi alipokuwa akiishia Damian.
Baada ya wiki mbili kupita nilipigiwa simu na Alex.
"Huyu mpuuzi anataka nini tena!?" niliongea huku nikiwa najifikiria nipokee simu yake au niiache lakini baada ya kuita mda mrefu niliamua kuipokea.
Ile naipokea nilikutana na kicheko kutoka kwa Alex "hahahahahahahahahahah" Alex alicheka kwa mda mrefu bira kuchoka na mimi niliamua kuikata simu.
Baada ya mda alipiga tena na niliipokea huku nikiwa na hasira.
"Una matatizo gani!? mbona unapenda kunisumbua!?" nilimuuliza Alex.
"Nilikuahidi Irene kuwa lazima mtaachana na huyo mzoa taka wako, kiko wapi Irene??? hahahahaha nilijua tu hawezi kuchomoka mbele ya mtaro" Alex aliongea na mimi nilianza kujumlisha matukio na moja kwa moja wazo nililopata ni huenda Suzi alitumwa na Alex kwa ajili ya kuja kuvunja mahusiano yangu na mzoa taka.
"Umelizika sasa Alex sio!?" nilimuuliza baada ya kuutambua ukweli.
"Bado mpaka ujute kwanini ulikuwa msaliti wakati wa ndoa yetu" Alex aliongea na mimi niliamua kumkatia simu.
Licha ya kumkatia simu bado aliendelea kunitumia jumbe za kila aina akiniambia kuwa bado hajatosheka na mpaka nitajuta kumfahamu.
Kiukweli nilikuwa sijui niwe upande gani kwa kipindi hicho kwani niliutambua ukweli kuwa mzoa taka aliingizwa kwenye mtego na yeye akaingia.
"Lakini ata kama ulikuwa ni mtego kwanini Damian alikubali kunisaliti!?" niliongea mwenyewe huku nikiwa nawaza cha kufanya.
Wiki mbili zilipita nikiwa naishi mwenyewe pamoja na mwanangu na mfanyakazi wangu wa ndani, siku hiyo nilipigiwa simu na dada yangu na aliniuliza kama nipo nyumbani na mimi nilimkubalia kuwa nipo nyumbani. sikujua alikuwa na lengo gani ila aliniambia atafika ndani ya mda mfupi hivyo niliamua kubaki nyumbani na kumsubiri.
Dada alifika na ujuo wake ulinichanganya kwani alionekana ni mtu mwenye mawazo sana.
"Dada kuna tatizo!?" nilimuuliza ili nipate kujua na dada aliniambia.
"Ndio mdogo wangu kuna tatizo tena sio dogo"
"Tatizo gani hilo!?" ilibidi nimuulize kwa mara nyingine na dada alianza kunielezea tatizo lililokuwa likimsibu.
"Mdogo wangu mimi dada yako tayari nimeisha na Alex aliyekuwa mmeo ameamua kunimaliza kabisa" Dada aliongea huku machozi yakimlenga lenga na mimi mda huo nilikuwa bado sijamwelewa kile alichokuwa akimaanisha.
Nilimuuliza kwa mara nyingine na dada alianza kunifafanulia kwa kunieleza ukweli kuwa ameshafanya mapenzi na Alex zaidi ya mara tatu na mara zote alikuwa akimwingilia nyuma ya maumbile au waswali wanasema kwa kumzibua mtaro na tayari alikuwa ni mwathirika na alidai kuwa Alex ndiye aliyemwambukiza.
"Dada kwanini lakini na wewe ulikubali kumbinulia na yule mpuuzi!?" nilimuuliza Dada.
"Niliingia kwenye mtego wake Irene sikuwa na njia nyingine ata mimi sikutarajia kama nitafanya nae mapenzi Alex japo alikuwa ni mmeo" Aliongea na mimi nilibaki nikimtia moyo kuwa wapo wengi tuΒ wenye ugonjwa aliokuwa ameupata kwa wakati huo huku nikimsisitizia kuwa afate taratibu zote za utumiaji wa dawa ili maisha mengine yaendeleee.
Baada ya maongezi ya mda mrefu Dada aliamua kuniuliza.
"Irene mbona simuoni mzoa taka wako!?" Dada ilibidi aniulize baada ya kutokumuona Damian nyumbani kwangu.
"Hayupo nimeshamtimua tayari na tumeachana mimi na yeye" niliongea mbele ya dada na hakuacha kuniuliza sababu ya sisi kuachana na mimi nilimwambia ni kwa sababu ya uchepukaji wake aliokuwa nao japo sikutaka kumwambia kama Alex ndiye chanzo na ndiye aliyetengeneza mipango ya kututenganisha mimi na Damian.
Siku hiyo dada alishinda nyumba na siku iliyofata aliondoka na siku mbili zilipita tangu dada aondoke na siku hiyo nilipigiwa simu na mama hivyo ilinibidi niipokee.
"Irene huyu mzoa taka wako bado upo nae mpaka sasa!?" mama aliniuliza.
"Hapana sipo nae" nilimjibu baada ya yeye kuniuliza.
"Hapo sawa maana ningeshangaa na umefanya la maana kuachana nae maana nimemuona huku akizoa taka" mama aliniambia na baada ya maongezi alikata simu.
Kiukweli moyo wangu ulishituka baada ya kuambiwa kuwa Damian amerudi kwenye kazi yake ya zamani ya kuzoa taka kwa mara nyingine hasa ukizingatia ndiye mwanaume aliyekuwa akinilizisha vizuri kwenye mapenzi.........ITAENDELEA.
Umesoma kwa utulivu Β· dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mahaba-ya-mzoa-taka

