Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3 Sehemu ya 03

1st Jun, 2025 Views 36

NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3

Sehemu ya 03

Nilisoma harakaharaka hapo ndipo nilipochanga nyikiwa nikajikuta na tetemeka mikono,
Kwanza sikuamini kama mke wangu angeweza kufanya vile , nikajiuliza mbona ni muda mfupi tu , yaani tokea nimwambie NIMEFUKUZWA kazi ni wiki ya 3 tu , leo nakuta meseg chafu mesegi inayoniliza , mke wangu kafanya mapenzi ,yaani kanisaliti ,unajua sikuamini , ile mesegi ilipita kwenye kichwa changu kama muvi ya kutisha , ASANTE BEBY KWA PENZI TAMUU !????
Hyo mesegi ilijirudia rudia kichwani , nilijikuta nalia aisee ,! Msomaji nakwambia kweli mapenzi yanauma ,nilipandwa na hasira nikajisemea ngoja akitoka nitampa kipigo halafu ntamwambia ukweli kuwa mimi sijafukuzwa kazi , maana nahisi kabisa amesaliti kwa kujua mimi sina kazi ,
Wakati anarudi kuoga moyo wangu ukaniambia vumilia tu kwani miez mi 3 sio mingi ndo kwanza wiki ya 3 ,
Nikairudishia ile simu haraka kwenye pochi yake nikajifuta machozi upesi nikajilaza kitandani , akaingia na kujifuta maji kisha akachukua simu yake na kwenda sebuleni akawa anaangalia tv huku anachati ,
Inahitaji hekima ya hali ya juu kuvumilia haswa ukijua kabisa mkeo anachati na mchepuko huku anazuga anaangalia tv ,
Niliwaza Sana nikatoka chumbani na kumfuata sebuleni nikaa karibu nae na kumwambia , mkewangu kama nimekosa basi naomba unisamehe, naomba tuishi kama zamani , kufukuzwa kazi sio tatizo la kufanya wewe unichukie kiasi hicho , niliongea kwa uchungu wa kweli ila nilichunga tu kumwambia ukweli , na sikumwambia kama nimeona mesegi zake ,
Mke wangu aliniangalia mala moja tu kisha akaniambia , kwani nani amekuchukia ? Ingekuwa mimi nakuchukia nisingetoa pesa ya chakula , au pesa ya chakula unatoa wewe humu ndani ,? Nikamjibu hapana sitoi mimi ,akaendelea tena kuongea , basi unachotakiwa kufanya wewe ni yale majukumu niliyokuwa nayafanya mwanzo yanatakiwa uyafanye wewe , nikamuuliza majukumu gani ,?
Akanijibu , majukumu yote ya nyumbani kama kuosha vyombo kufua , kupika , usafi wa nyumba , sio unisubilie mimi ndo nije nikufanyie wakati wewe huna kazi yoyote ,
Niliumia sana haswa mke wangu anapoongea kwa kujiamini kama Mimi siwezi kumfanya chochote, nikajiuliza kupika sawa ntapika lakini mimi nioshe vyombo kweli , ? Au sawa kufua nitafua lakini mimi eti nishike fagio nifagie uwanja huku mke anaenda kazini hii ni dharau kubwa sana , wakati natafakari nikaona simu yake inawaka na kuzima kuashiria kuna mesegi zilikuwa zinaingia ,yaani ametoa mlio wa mesegi, nikamuitikia tu sawa mke wangu huku nikiamka kwenye kochi na kumuacha mwenyewe, ila wakati naamka nikatupia jicho kwenye simu yake nikamuona akitoa rock halafu akawa anajibu sms , nikaijua rock yake ,
Nilienda kulala nikijifanya sijui kitu , aisee Acheni na msije mkajaribu huu mchezo nilioujaribu mimi, maumivu yake hayasimuliki , yaani mwanamke niliempenda nikampa mtaji wa duka la vipodozi , tukajenga nyumba ,tukapata mtoto wetu , eti leo ananisaliti kisa sina kazi ,
Sikupata usingizi mpaka mke wangu akaja na yeye akalala ,nikajifanya naamka na kumkumbatia ili tulale kama zamani , akanitoa mikono , kwa wale wanandoa wanajua ukiwa na mwenza ndani halafu ukihitaji tendo la ndoa utaona mwanaume amekukumbatia tu na wewe unajua kifuatacho , maana tendo landoa kwa wanandoa haliombwi ,
Basi alivyoitoa mikono yangu nikamwambia mke wangu naomba japo mala moja tu nimezidiwa na haswa ukiangalia mwezi unakatika , mke wangu akanijibu nimechoka naomba nilale , nikajifanya namshika shika lakini akanisonya na kuamka kabisa akaenda kulala kwenye Koch ,
Daah nilipata shida sana kuwaza , na siku hiyo sikulala , usiku muda kama saa Tisa usiku mke wangu akiwa sebuleni kwenye kochi kalala nikachukua simu yake na kuanza kupekua , nilisoma mesegi za kawaida na kila meseg nilidondosha choz ,siwez kukwambia ni mesegi gani lakini ziliniliza ,
Nikatoka chumbani nikaenda mpaka kule sebuleni na nikamwangalia mke wangu jinsi alivyolala pale kwenye Koch , machozi yalinitoka ,
Nikarudi kitandani nikalala zangu , asubuhi nikastuka nikaangalia saa ilikuwa saa moja moja na madakika , halafu mke hayupo yaani ameenda kazini hakuniaga na wala hakumuandaa hata mtoto ili aende shule , nikaamka upesi upesi nikamwandaa mtoto akaenda shule kisha nikampigia mke wangu kwa wema tu ili nimuulize mbona leo hujaniaga , ? Mke wangu akanijibu kwani ulitaka nikuamshe ili iweje ? Kwani unaenda kazini wewe ? Au kuna sehemu utaenda labda kuna pesa unafuatilia ? Wewe hata ukiamka saa sita ni sawa kwani kazi zako ni zanyumbani tu ,"
Mke wangu akanijibu kisha akakata simu ,
Nilifanya kazi za nyumbani kweli ,niliosha vyombo nikafua na nikapika , mtoto wangu akarudi tukala , na kwa vile ilikuwa mapema bado nikamchukua mwanangu tukaenda kutembea kule kwenye nyumba ninayojenga , nilimkuta mama mmoja niliempa pesa kwa ajili ya kumwagilia ukuta alikuwa anaifanya kazi yake , tulisalimiana nae na akawa anamtania mwanangu anamwambia hii nyumba ni yako jitahidi usome ,
Basi tulizunguuka na kuangalia nyumba huku mwanangu nae akiniuliza eti baba na hii nyumba ni yetu nikamwambia ndio mwanangu , bas tulikaa mpaka muda wa kurudi tukarudi nyumbani , nilipika chakula cha usiku na nikampa mtoto ale ili awahi kulala kesho shule ,
Nikabaki peke yangu pale sebuleni nikimsubilia mke wangu , mpaka saa 5 inafika alikuwa bado hajarudi, nikasikia muungurumo wa gari nje na nilipochungulia nikamuona mke wangu akiagana na jamaa mmoja na yeye akaingia ndani , ile gari ikaondoka , alipoingia cha kwanza kabisa nikamuuliza yule aliekuleta na gari ni nani ,? Akanijibu ile ni Tex nimeona nimechelewa nikachukua tax ,
Nikamwambia lakini sijaona ukimlipa pesa , mke wangu akanijibu kwa ukali kidogo ,kwani we shida yako nini lakini , mtu amerudi amechoka badala hata ya kumpa pole unakazana na maswali tu ,
Nikamwambia basi mke wangu yaishe , nikatenga chakula nikakaa namsubilia aje tule lakini alivyotoka kuoga akaenda chumbani akalala ,
Nikamfuata na kumwambia twende tukale nilikuwa nakusubili wewe , akanijibu ameshiba , nikamwambia leo ni siku ya 2 huli nyumbani na chakula kinabaki asubuh tunakimwaga sio vzr , akanijibu kwani anaetafuta hicho chakula ni nani ,? Nikamjibu ni wewe , akaniambia sasa mbona unakuwa kama mjinga , kama wewe sio unatafuta chakula hicho chakula ukikimwaga kinakuuma nini ,? Nikastuka sana aliponiambia nakuwa kama mjinga , na nikamwambia yaani mke wangu mimi ni mjinga ? Akanijibu sio mjinga bali ni mpumbavu sasa swali gani hilo unaniuliza ,?
Nilihisi Koo limekauka kwa muda gafra tu nikamvaa na kumtandika makofi mawili ya maana , na nikamwambia fanya yote ila usinitukane na ukirudia ntakunyoosha , mke wangu nae hakukubali akaanza kuongea tena kwa sauti yajuu , kama unaona nakukera ni bora tuachane kila mtu awe na maisha yake , kuliko kunipiga hujanizaa wewe tena ukome , na kuanzia kesho sitoi pesa ya matumizi tuone utakula wapi m bwa wewe , yaani nakulisha halafu unanipandishia kibes na kunipiga we msen *ngee nini ,
Mke wangu alitukana tusi lililopenya kwenye moyo likatokea chini ya unyayo , ikabidi niende kwanza chooni nikamwacha anaongea tena kwa sauti ile yajuu , na kwa taarifa yako tukiachana hii nyumba nitabaki nayo mimi kwa ajili ya mwanangu au iuzwe ,huwezi kunipiga kama mwanao mimi ,mke wangu aliendelea kuongea ,
Nilikaa kulechooni nilijihisi kuharisha ila sikuwa na hajakubwa ,

Nini kitaendelea
Twende wote sambamba ,

Jamani kuna watu wanalalamika siwatag na story zinawapita ila ukimtag mtu mwingine hapend ,

ITAENDELEA ....FULL .
   

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

side chick episode 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

SIDE CHICK EPisode 2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY???15

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 18

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 17

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 8

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA Sehemu ya 32

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA? Sehemu 13.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY ???11

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

BOYCHILD PART 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 4.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 29

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

LOVE Part 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 28

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA Sehemu nne.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 26

mrindia rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 25

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest