Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3 SEHEMU YA 15

1st Jun, 2025 Views 36

NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3

SEHEMU YA 15

Nilimwangalia mke wangu alivyokonda na nikaona ngoja nifanye maamuzi ya kiume tu LIWALO NA LIWE,
Nikasogea pale mbele na nikatoa maelezo yangu , na maelezo hayakutofautiana sana na mke wangu , hakimu akaniuliza kwanini uliamua kumdanganya mkeo,? Nikamjibu ni kwasababu nilikuwa na mpenda sana na nilitaka kuona kama na yeye ananipenda na anaweza kunivumilia kipindi sina pesa ? Yule Hakim akasema kabla hatujatoa maamuzi kakae tumsikilize mlalamikaji , yule mlalamikaji akaanza kutoa maelezo jinsi ilivyokuwa , akasema alimtongoza mke wangu na mke wangu akamkubalia wakawa wapenzi ,akamuuliza mke wangu kama anamume mke wangu akamjibu hana wameshaachana , ndo jamaa akafanya maamuzi ya kujazia duka na kubadirisha baazi ya lesen na duka likawa lake , sasa jamaa alipogundua kuwa kumbe mke wangu anamume ndo akamwambia waachane na duka sio lake tena ndo mke wangu akaenda kufanya fujo dukani , hakimu akaniuliza je uko tayali kumsamehe mkeo ?
Mi nikamjibu nimemsamehe lakini siwezi kuishi nae tena kama mke wangu , mke wangu alianza kulia na kusema mi naomba tuishi kama zamani ,mi nikasema hapana kwa kuwa tayari nimeshaoa nikamwambia afande asimame akasimama nikamwambia huyu ndo mke wangu mpya ,mke wangu akalia pale mahakamani kama mtoto,
Hakim akasema mke wangu anatakiwa alipe mali alizoharibu dukani kwa yule jamaa au kifungo cha nje cha miezi sita , mke wangu alilia sana afande akasema mlipie tu ,nami nikamlipia akawa huru ,
Tukarudi nyumbani lakini sikumpakiza kwenye gari yangu ,ndani ya gari tulikuwa mi na afande , afande akaniuliza sasa we umenitambulisha kama mkeo na wewe umesema huwezi kuoa tutafanyaje , mi nikamjibu leo tutaenda kulala nyumbani lakini tusifanye kitu halafu kesho utaondoka ili mke wangu asinisumbue leo, afande alikubali na alivyokuwa na sifa si tukanunua na chakula cha kupika usiku , tukarudi nyumbani tukamkuta mke wangu kajiinamia tu , sikumsemesha tukapita zetu mpaka chumbani , afande akachukua maji yakuoga akaniwekea bafuni huku mke wangu akiwa bado kajiinamia tu huku analia kilio cha kwikwi,
Mi nikaenda zangu kuoga afande akaingia jikoni ,kumbuka mpaka hapo tulikuwa tunaigiza tu na afande wala mi sikuwa na mpango wa kumuoa afande ,
Nilipotoka nikabadilisha nguo kisha nikaenda kucheza na mwanangu , chakula kiliiva tukakaa tukala mi na mwanangu pamoja na afande , ilikuwa nikama familia tu , mtoto akaniuliza mbona mama haji kula nikamwambia atakula tu baadae kwani anaumwa, mtoto akalizika , aliposhiba nikampeleka kulala na mimi na afande tukaingia zetu chumbani , tulipiga story mbili tatu huku tumelala lakini gafra nikamuona afande kanikumbatia nikajaribu kujitoa lakini sikuweza akanipa mdomo nikaupokea , sasa hapo sijui ilikuwaje tukajikuta katikati ya mahaba mazito , ilikuwa ni mshike mshike yaani huyu afande nyiee aaah ,
Kuna muda kama nilihisi kupaa nikawa napiga tu kelele na kunamuda hata sijui ilikuwaje yaani nyie kuna wanawake mafundi , kwa mbaali sana nilisikia kama mlango unagongwa ila kwa vile tulizama katikati ya mapenzi sikusikia , simu pia iliita mpaka ikakata sms zikaingia kama zote ,yaani mi sikuwa na habari kabisa yaani nyie huyu afande huyu mmh ,
Nilistuka saa11 alfajili nikaangalia saa kwenye simu ndo nikakuta simu zilizopigwa zilikuwa kama 18 sms ndo usiseme zote zilikuwa za mke wangu , sikuzijali nikatoka zangu ili niende uwani ,ile nafungua mlango nikamuona mke wangu kalala mlangoni kwangu , nikamwangalia tu nikampita nikaenda uwani nikarudi zangu ndani ,
Afande nae alijiandaa huku akinipiga mabusu na kiukweli hata mimi nilianza kumuelewa huyu afande ,
Afande akaniuliza mbona mkeo kalala mlangoni halafu nimepita hata hajastuka na nimerudi ndani hata hajastuka , nikawaza nikasema hata mimi nilipita hakustuka na nikarudi pia alikuwa kalala vile vile , ikabidi nitoke nimwamshe , nilipomgeuza nikashangaa anatoa mapovu mdomoni haraka nikamwita afande , tulimwangalia tukagundua amekunywa sumu ,
Upesi na haraka nikawasha gari tukampakia na kuondoka nae kwenda hospital, afande akaona naendesha gari huku natetemeka akaniambia hebu simamisha gari akaendesha yeye , aliendesha kwa spidi mpaka na mimi nilianza kuogopa lakini alikuwa makini ,tukafika hospital na haraka akanza matibabu doctor akasema yaani mngechelewa kidogo tu mngemkosa , nilianza tena kuingiwa na roho ya huruma kila nikimuangalia mke wangu anavyopumulia gesi huku anamipira ya kutolea sumu mwilini ,aisee alikuwa anatia huruma ,
Afande alinipa moyo na kuniambia atapona nisiwaze sana , afande akasema anakwenda kazini hali itakavyokuwa nimjulishe ,nikabaki pale hospital sasa ndo nikaanza kusoma sms za mke wangu zilikuwa nyingi ila moja ndo ilinisikitisha ikanifanya niwaze sana aliandika hivi,
" Najua huwezi nisamehe mume wangu kwa nilichokufanyia hata mimi siwezi jisamehe ndo maana nakunywa sumu ili nife , najua unajua kuwa chanzo niwewe kwa kunidanganya kuwa umeacha kazi kumbe bado upo kazini ni kweli umefanya la maana sana maana kupitia kunidanganya kwako nimeona nikwambie tu ukweli kuwa huyo mtoto sio wako , baba wa huyo mtoto aliikataa mimba kipindi mimba inamwezi mmoja na wewe ndo ukanioa kwahiyo ulinioa nikiwa na mimba ya mwezi mmoja ,na ungekuwa makini kipindi kile ungegundua kwa kuhesabu miez tuliyokaa mpaka kupata mtoto,
Nisameha sana mume wangu , nimekuachia mtoto sio wako ,,,,,

Aisee sikuweza kuimalizia hii sms nikakaa chini kama mzigo ,,,,


Usikose kifuatacho,,,,,
Je jamaa atachukua hatua gani , ?

Tupe maoni yako jamaa afukuze yeye na mtoto au mtoto abaki amlee japo sio wake ,,?
Au amsamehe tu ? NASOMA KOMENT ????

ITAENDELEA.
   

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

side chick episode 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

SIDE CHICK EPisode 2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY???15

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 18

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 17

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 8

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA Sehemu ya 32

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA? Sehemu 13.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY ???11

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

BOYCHILD PART 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 4.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 29

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

LOVE Part 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 28

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA Sehemu nne.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 26

mrindia rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 25

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest