NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3
SEHEMU YA 09
Aliongea vile huku akileta mdomo wake ugusane na mdomo wangu sasa mke wangu akatukuta tukiwa kwenye hali ile,,
Mke wangu akastuka akasimama huku anatutazama , alionekana anawasiwasi maana nilimuona ametoa macho,
Sasa yule afande nae akajifanya kama hajamuona maana tuligusanisha midomo tu huku tumekumbatiana lakini gafra tu akatoa ulimi wake na kuutumbukiza mdomoni kwangu , nikajitahidi kutaka kuutoa maana niliona kama mke wangu anapandwa na hasira, sasa wakati nahangaika kujitoa ndivyo yule afande alivyozidi kuuingiza ulimi wake sasa nikajikuta namimi namkumbatia , mke wangu hakuvumilia akaja mbio na kunivuta lakini wakati anataka kumshika yule afande akachoropoka na kuingia kwenye gar, mke wangu akawahi ili afungue mlango lakini tayali yule afande akawa amerock na yupo ndani,
" Huyu ninani nakuulizaa ,,??
Mke wangu aliniuliza kwa hasira, na yule afande akaondoa gari nakuondoka zake, nikashindwa cha kumjibu , mke wangu akachukua jiwe na kulirusha kule lilipoelekea gari huku akitukana mshenzi ww na nikikujua utanitambua , halafu akarudi tena kwangu ,niambie yule ninani ,?? Sasa mimi kwanza nilishindwa kumjibu mke wangu kwa sababu kwanza sikujua yule afande alikuwa na nia gani , halafu sikuwahi kuchepuka tokea nimuoe mke wangu sasa kile kitendo cha mimi kunyonywa mate mbele ya mke wangu kilinipa kama ganzi fulani hiv,
Mke wangu akazid kuniuliza huku ananisukuma ikabidi na mimi nimuulize na wewe uliekuja nae ninani ,,? Akanijibu eti ni dereva wa tax , nikamwambia dereva wa tax wakati mmekumbatiana hebu niache ," niliongea kwa ukali huku naingia zangu ndani,
Yaani nikama yule afande amenipa ujasiri fulani hivi maana hata nilipomjibu mke wangu nilimuona kama amenywea hivi ,
Nilimuacha kule nje akiwa na yule jamaa wa kwenye gar na wala sikutaka hata kuwafuatilia ,nikaingia ndani jikoni nikapakua chakula nikakaa pale sebuleni nikaanza kula ,lakini moyoni nilikuwa naumia sana maana nilimuacha mke wangu kule nnje akiwa na mwanaume mwingine , wakati nawaza nikasikia muungurumo wa gari ukiondoka nikamuona mke wangu anafungua mlango na kuingia ndani akanikuta nimekaa chin nakula , akaanza kusema "wewe si unajifanya mjanja sasa naondoka ili ukae na hao malaya zako , na tuone kama huyo malaya atakupenda ukiwa huna kazi ,
Kweli mke wangu akatoa begi lake languo na akaliweka pale sebuleni akaingia tena chumbani akatoka na mkoba huku akisema utanikumbuka tu labda sio mimi , yaani mi nakuvumilia huna kazi mimi ndo natoa pesa za matumiz bado unaniona mi mjinga sasa subiri niondoke zangu ,,
Mi nilipoona vile nikatamani kumuomba msamaha ili asiondoke lakini moyo mwingine ukaniambia muache kwanza ingia chumbani , nikaingia chumbani huku nnawasi wasi kweli ,
Kule chumbani niliufunga mlango nikawa namchungulia mke wangu kwenye tundu la funguo , maana nilitaka nione kama ataondoka kweli basi nimfuate nimwombe samahani,
Nikamuona ametoa begi lingine lakini alipoangalia pale nilipokaa hakuniona , nikamuona amejishika kiuno kasimama anaangalia huku kwenye mlango wangu , alisimama kama dakika mbili hivi akawa kama anawaza jambo , akaanza kutembea taratibu huku akiwa kama anawaza sana , nikamuona amerudisha yale mabegi ndani ,nikajua kumbe alikuwa anatingisha kiberiti,
Mi nikalala zangu , kesho yake asubuhi nikaamka lakini sikumkuta mke wangu nikajua kaenda kazini , nikamuandaa mtoto nikampeleka shule , nikarudi nyumbani ili nijiandae niende kule sait ,
Wakati najiandaa akaja mke wangu na wanaume watatu , walikuwa wameshika makaratasi kama mafaili wakajitambulisha kuwa wao ni watu kutoka mahakamani na mke wangu alikwenda kudai nimpe taraka kisha mali zigawanywe , nikashangaa , nikawaambia mi sina mali zozote zaidi ya hii nyumba ,wakaniambia hiyo hiyo nyumba inatakiwa iuzwe halafu mimi nitapewa asilimia 20 halafu mke wangu atapewa asilimia 80 kwa vile anamtoto, au mi niondoke nimwachie nyumba akae na mtoto,
Nikamwangalia mke wangu na nikamuuliza mbona umefikia huko ,? Akanijibu we si unajifanya mjanja unakuja na wanawake zako sasa nataka tuone mimi nawewe nani mjanja , nilisikia uchungu sana na mke wangu akawa haon hata aibu ,
Mi nikawajibu basi wanipe mwezi mmoja tu mimi ntakuwa nishaondoka , wakaniambia unatakiwa uwandike talaka leo tena hii ndoa ivunjwe na mahakama mkeo ndo kataka hivyo , nikapiga magoti na kumuomba kama kuna kosa basi anisamehe lakini mke wangu akasisitiza niandike talaka , basi nikaandika talaka nikamkabidhi mke wangu lakini kishingo upande , na wale jamaa wakasema unamwezi mmoja tu wa kukaa hapa nyumbani ukiisha unatakiwa kuhama , niliumia sana , na wale jamaa wakaondoka , mke wangu nae akajiandaa akaondoka ,nilikaa nikampigia simu yule afande nikamwambia mambo yote yaliyojitokeza , yule afande akaniambia nimsubilie anakuja ,
Kweli akaja na nikaanza kumlaumu na kumwambia lile tukio la jana ndo limemfanya mke wangu aniache , akaniambia unachotakiwa ww ni kusimama kwenye nafasi yako kama mwanaume , akaniuliza pale kazin kwa mkeo si kuna duka pembeni nikamwambia ndio , akaniambia nataka nimuoneshe mkeo kuwa wewe unathamani , nikamwambia kivp ,? Akanijibu twende , tulienda mpaka kwenye duka la nguo , akaninunulia Jens Kali pamoja na fulana nzuri kubwa kubwa ,kisha akaninunulia na viatu vya kisasa kama wanavyovaaga wasanii , daah nilipendeza sana ,akaninunulia na miwani nyeusi , nilionekana kama msanii fulani ,
Akaniambia sasa twende pale dukani karibu na mkeo , tulifika na kabla hatuja shuka yule afande akavaa kofia na miwani nyeusi na nywele zake kazilaza kwa nyuma nae alipendeza na alikuwa mzuri si mchezo na kwa haraka huwez mjua kama ni yule afande maana alivaa nguo suruali ya Jens na Sweta la bruu kisha akapiga kofia na miwani weee,,
Basi tukashuka huku tumeshikana mikono , sasa wakati tunaenda pale dukani pembeni ya duka hilo ndiko kuna duka la mke wangu halafu kuna saloon , mke wangu alikuwa kakaa kwa nje ya duka lake anachezea simu yake sijui ndo alikuwa anachati , sasa aliponyanyua kichwa akatuona , akashangaa akaamka huku akiwa bado anatuangalia , alikuwa ni kama mtu aliekuwa haamini anachokiona mbele yake , akaanza kusogea kutufuata , sasa yule afande akajifanya eti anamuogopa mke wangu akauwachilia mkono wangu kwa nguvu na kukimbilia kwenye gari , nikamuona mke wangu anamkimbiza , yule afande akarock gari mke wangu akawa anaipiga piga ile gari huku anamwambia fungua nikuoneshe malaya mkubwa wewe ,, sasa namimi nikarudi fasta na nikazunguuka upande mwingine na kufungua mlango nikazama kwenye gari ,mke wangu nae akazunguuka fasta lakini nikawa nishaingia kwenye gari akabaki anapiga piga gari nakusema fungua nimuoneshe huyo malaya wako mshenzi wa tabia huyo mwizi wa waume za watu , yule afande akawasha gari tukaondoka eneo hilo tukamuona mke wangu anatukimbiza lakini hakufika mbali akasimama na kutoa simu yake na gafra nikaona simu yangu inaita , mpigaji alikuwa ni mke wangu , tukaangaliana na afande tukacheka na afande akanipiga busu la shavuni kisha akaniambia lete hiyo simu niipokee ,
Nini kitaendelea na si amedai talaka mwenyewe,,???????
ITAENDELEA.... FULL.