NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3
SEHEMU YA 18
mwisho
Kabla mke wangu hajajibu jamaa akampiga tena Kofi la uso ,,,aisee,,,
Hapo nikajikuta mapigo ya moyo yapo kasi sana nikashuka kwenye gari nikajikuta namkunja yule jamaa na kuanza kupigana nae huku namwambia kwanini unampiga mke wangu , nilipandwa hasira tu , afande akaja kutuamua ,mke wangu ye alikuwa analia tu , yule jamaa aliondoka huku akitoa maneno machafu na kusema atakuja tena kudai mtoto wake ,
Nilimwangalia mke wangu kwa huruma sana nikawa najisemea mimi ndio nnamakosa sikupaswa kumdanganya mke wangu , maana haya yote yametokea kwa sababu mimi nilimdanganya kuwa nimefukuzwa kazi kumbe bado nipo kazini , afande akaniambia unajua huyu mwanaume amempiga mkeo mpaka roho yangu ikaniuma sana ,nikamjibu sasa tunafanyaje akaniambia kwa kitu alichokufanyia mkeo twende tumtafutie chumba halafu tukampokonye yule jamaa duka tumrudishie mkeo halafu muachane na mkeo kwa amani , nikamuuliza tutampokonya vip ,? Akaniambia kwani tin namba si ya lile duka si ni yamkeo ,? Nikamjibu ndio , akaniambia si una mashine ya risiti nikamjibu ndio ,akaniambia basi mchezo umeisha , mwambie mkeo aingize mabegi ndani tukamtafutie chumba ,
Nikamwambia mke wangu aingize mabegi ndani yaani hakuamini ,alipiga magoti na kunishukuru , mi nikatoka na afande mpaka kituon akachukua mafaili fulani na akaniambia nitaje namba ya duka lamke wangu akayachapisha , tukaenda mpaka dukani kwa mke wangu huku tukiwa na polisi kama sita , na ukumbuke mke wangu hajui chochote, tulipofika tukamkuta yule jamaa akiwa na wafanyakazi wake wawili na duka limejaa si mchezo , alipotuona akastuka akauliza kuna nini afande akatoa makaratasi na kumuoneshea jamaa na kumwambia mwenye jina hili ndio mmiliki wa duka hili kihalali kabisa na kila kitu kinajionesha kwahiyo funga duka twende kituoni , jamaa akajitetea kuwa ameuziwa duka hilo na mke wangu , afande akamwambia tuoneshe hati ya makbiziano na vielelezo vya mauziano ,jamaa hana , akapigwa pingu tukamuweka kwenye gar mpaka kituoni, akaambiwa achague moja afunguliwe kosa la utapeli au aachie duka , jamaa akasema anaachia duka ,
Basi akaachiwa na hakufanikiwa kutoka hata na rosheni ,
Tukatafuta dalali na akatutafutia chumba tukakilipia , na tukamnunulia mke wangu kitanda na godoro tukamuwekea , tukarudi nyumbani , nikamwambia mke wangu kwanza naomba unisamehe sana kama kuna kosa nimekosea ila kwa sasa nataka nianze maisha mapya nimefanikiwa kurudisha duka lako na utaenda kuuza , lakini utaenda kukaa sehemu niliyokupangishia yaani hatutakaa pamoja tena ,mke wangu alilia sana akaniambia nashukuru sana na nakuomba afande umtunze mume wangu najua nimekosea sana ila naomba iwe fundisho kwa wanawake wenzangu , usije mdharau mumeo eti hana kazi maana hakuna aijuae kesho ,basi tuka mpa ufunguo wa duka na tukampeleka kwenye chumba chake cha kupanga , aisee alilia sana na kujutia aliyoyafanya , na mimi na afande penzi likawa Moto moto ,tukahamia kwenye nyumba yangu mpya ,na ile nyumba ya zamani nikaweka wapangaji , afande nae nyumba yake akaweka wapangaji ,akahamia kwangu mambo yakaenda sawa,
Nikarudishwa kazini maisha yakawa mazuri tu na mke wangu alijifungua akanijulisha tukaenda mimi na afande kumuona mtoto ki ukweli yule mtoto alikuwa sio wa kwangu , ila mke wangu akatuomba tusimwambie jamaa aliempa mimba kwani yule jamaa ni mkorofi mtoto atamlea mwenyewe, basi tulibaki hivyo mimi na afande mke wangu akabaki kama rafiki tu wa familia akiwa na shida anatuambia tuna msaidia , afande akashika mimba akajifungua katoto ka kike kazuri aisee kalifanana na mimi nikafurahi sana kumuona mwanangu origino,
Nikajifunza kuwa uongo ni m baya sana haswa kwenye familia zetu ,
Story hii hatujataja majina ya watu ,kwa kuwa watu hulalamika kuwa tumeweka wazi maisha yao , yaani wao ndio walipatwa na mkasa huo kwahiyo walipwe ,
Na tunaomba radhi kama mkasa huu umekugusa kwa namna moja ama nyingine ????
MWISHO.