Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3 SEHEMU YA 14

1st Jun, 2025 Views 33

NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3

SEHEMU YA 14

Jamani mwambieni mume wangu anisamehe jamaaniiiii uuwiiii,,
Aliongea mke wangu huku akilia ,akapelekwa mahabusu , sasa tukabaki mimi na afande tukaangaliana na tukacheka, nikamwambia afande unajua lile busu limenisisimua yaani sikutarajia kabisa , afande akacheka akanitania akaniambia kwani mkeo hakupagi vitu kama hivi ,?nikamjibu aah sasa hivi sina hata hamu ya kumuona yaani sijui kwanini , yule afande akasogeza kiti karibu halafu akaniuliza unajua nimefanya vile kwa sababu gani ,? Nikamjibu sijui akaniambia kwa kuwa nakupenda , nikamjibu nikamwambia acha utani bana mi nilijua tunafanya vile kumkomoa mke wangu, akaniambia ni kweli ila nimegundua wewe ni mwanaume wa aina gani , kwanza unaupendo wa kweli kabisa ,yaan upendo uliokuwa nao wewe kwa mkeo nilitamani ningekuwa mimi ndio mkeo aisee ningelinga sana , nilicheka sana nikamwambia unajua kwasasa sitamani tena kumpenda mtoto wa mtu kwa sababu nimejitambua tena nimetambua nilikuwa mjinga sana , lakini hata nikimpenda mtu siwezi tena kumdanganya kama nilivyomdanganya mke wangu kuwa nimefukuzwa kazi kumbe bado Niko kazini hii imenifanya nione upande mwingine wa mke wangu,
, kuwa pamoja tutakuwa pamoja lakini siwezi kuoa tena ,
Nikamuona afande amefurahi sana akaniambia basi sawa nami nataka tuwe pamoja ,, tuongelee kesi ya mkeo, mkeo ameletwa hapa kisa amefanya fujo dukani kwa mtu na duka lenyewe ni la vipodozi,mkeo anadai duka hilo ni lake na huyo jamaa nae anadai duka hilo ni lakwake , tena jamaa mwenyewe ni yule tuliomfumania na mkeo siku ile , nikashangaa kdg nikajua itakuwa yule jamaa ndo amemzurum mke wangu ,nikamwambia afande sasa tutafanyaje ,? Afande akaniambia ingekuwa mkeo kaja yeye kushtaki ingekuwa sawa na tungeweza kulipata lile duka lakini kashtakiwa na mlalamikaji anataka kesi iende mahakamani kwa kuwa mkeo kavuruga duka na Katia hasara ,
Afande akaniambia tusubilie hiyo kesi iende mahakamani ndio tutajua tumsaidiaje , basi tuliagana na afande na wakati natoka mke wangu akawa ananiita aisee alikuwa anatia huruma kweli , nikamfuata mpaka kule ndani aliwekwa kwenye kachumba kadogo huku kukiwa na wasichana wengine kama 6 hivi na ndoo ya mikojo iko humo humo , nilisimama mlangoni mke wangu akawa analia tu huku akiniangalia ,nilihisi huruma inanijia nikamuuliza huyo jamaa imekuwaje anasema duka ni la kwake ,? Mke wangu hakuwa na jibu alikuwa analia tu ,nikaondoka zangu ,
Nilienda mpaka dukani kwa mke wangu ili nijue nini kimetokea ,nikweli nilikuta duka limebadilishwa kila kitu kwanza limejazwa vipodozi na mawigi marasta pamoja na mawiving yaani ni bonge la duka tatizo tu limebadilishwa mpaka jina ,yaani jina la mke wangu limetolewa ,limewekwa jina lingine , nikaondoka zangu wala hata sikuingia ,
Nilienda kwenye nyumba yangu maana leo nilikuwa navuta umeme ilikuwa nyumba ndogo lakini ya kisasa Sana yaani mtu angeiona angezani ya tajili mmoja ,
Nyumba ilikuwa tayari hata kuhamia ila nilisubilia ,
Ikapita siku mbili kesi ya mke wangu ikapelekwa mahakamani ,na mimi nilikuwepo tena tulikuwa na afande , aisee mke wangu alikonda yaani siku mbili tu za kuwekwa ndani zilitosha kabisa kumkondesha , kesi ikasomwa mke wangu anashtakiwa kwa kuvuruga duka la mtu na kutia hasara ya milion moja na laki mbili, akaulizwa je nikweli au sio kweli , mke wangu akajibu sio kweli lile duka ni langu huyu jamaa anataka kunidhurumu tu , akaulizwa duka ni lako kivipi hebu tuambie ,mke wangu akaanza kulia alilia mpaka akaambiwa sawa tuambie sasa ,
Nilipewa mtaji na mume wangu nikafungua duka la vipodozi,
duka japo halikuwa kubwa sana lakini lilitupatia kipato tukafanikiwa kujenga nyumba mimi na mume wangu , mke wangu akaanza kulia tena ,,akaambiwa anyamaze na aendelee na maelezo ,
Miezi mitatu iliyopita mume wangu aliniambia amefukuzwa kazi ,, sikujua kama ananidanganya , nilianza kumdharau na kumuona hana maana tena , nikaanza kufanya mambo yangu peke yangu , mume wangu naomba unisamehe jamanii , mke wangu bado aliendelea kulia ,
Watu wote tulikuwa tunasikiliza story ile ,
Niliweza kutembea na wanaume mbali mbali kwa kuwa nilijiona niko huru na nilitamani kuachana na mume wangu kwa kuwa niliona kama ananibana ,katika wanaume niliokutana nao mmoja wapo ni huyu alienishtaki , kiukweli nilijiona mwenye bahati kukutana na mwanaume huyu , alinibadirisha akalijaza duka langu , kisha akabadirisha kila kitu huku akiniambia niachane na mume wangu ili tuwe wote, jamani naombeni mnisamehe watu wote , nimekosea sana , mke wangu aliongea huku akilia aisee nami nilijikuta machozi yakinitoka , mke wangu akaendelea , huyu jamaa nilimwamini kwa vile alikuwa akinipa kila kitu na kwa vile niliona tutakaa pamoja baada ya kuachana na mume wangu nilimwachia mpaka lile duka ,
Sasa nikaja kugundua kuwa mume wangu alinidanganya yaani alikuwa ananipima upendo wangu ukoje juu yake , na wakati naujua ukweli huyu kaka alikuwa ndani yaani chumbani kwangu kwenye nyumba ya mume wangu, nilichomfanyia mume wangu hakisimuliki na najiona kabisa sina sababu ya kuishi kama asiponisamehe , mbele yako hakimu nakwambia mume wangu asiponisamehe nitakunywa sumu nife maana siwezi mwangalia usoni ,
Nilishangaa sana , na Hakim akasema aletwe mumewe hapa atoe maelezo, nikasogea huku najiuliza nimsamehe au nisimsamehe moyo ulikuwa unadunda si mchezo ,
Nilimwangalia mke wangu alivyokonda na jinsi anavyolia nikaona heri nifanye maamuzi ya kiume tu LIWALO NA LIWE ,

Heeeeeh ?maamuzi gani hayo ,,????

Tupige kura hapa amsamehe au asimsamehe ?

Usikose uhondo huu ?
ITAENDELEA.
   

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

side chick episode 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

SIDE CHICK EPisode 2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY???15

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 18

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 17

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 8

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA Sehemu ya 32

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA? Sehemu 13.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY ???11

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

BOYCHILD PART 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 4.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 29

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

LOVE Part 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 28

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA Sehemu nne.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 26

mrindia rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 25

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest