NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3
SEHEMU YA 10
Tuliangaliana na afande akanipiga busu la shavuni kisha akaniambia lete hiyo simu niipokee,
Nikamwambia hapana ngoja iite mpaka ikate, nilianza kuhisi vitu fulani kama vya upendo hivi kwa afande ,maana ni kama alikuwa anafurahi zaidi vile tunavyomkomesha mke wangu , na yale mabusu daah , japo nilikuwa najihisi Raha kupigwa busu lakini kwa upande mwingine nilikuwa naona kama nazidi kujiweka mbali na mke wangu ,
Sim iliita ikakata mke wangu akapiga tena ikaita mpaka ikakata alipiga kama mala sita lakini sikupokea mpaka akaacha kupiga ,afande akasema hapo lazima aumie maana alikuwa anahisi wewe huwez pata mwanamke mwingine zaid yake , tulienda mpaka kwenye fukwe moja hapa mjini dar ,ilikuwa ni bichi nzuri sana na ilikuwa imetulia sana , tulikaa sehemu na tukaagiza madafu tukaanza kula huku tunapiga story za hapa na pale ,afande alinieleza history yake ya mahusiano kuwa nayeye alipitia changamoto nyingi sana , alimpenda sana kijana mmoja walikuwa nae chuo , na wakaahidiana kuowana pindi watakapopata kazi , akasema walieshimiana sana na kupendana sana nayeye afande akaweka matumaini yake kwa kijana huyo kuwa ndie atakaekuwa mumewe, lakini yule kijana alikuja kuoa mwanamke mwingine halafu yule kijana alimletea kadi ya mchango wa harusi yake , fikiria mpenzi wako anaoa halafu anakuletea kadi ya mchango wa harusi yake inauma kiasi gani ,? Afande aliongea huku akilia , nilimuonea huruma nikamfuta machozi , akaniambia tokea siku ile nikajua hakuna mwanaume mwenye mapenzi ya dhati kwa mwanamke sasa nilikuja kushangaa wewe jinsi unavyompenda mkeo licha ya mkeo kukufanyia visa kiasi kile, namimi nilimwambia kuwa yule mke wangu ndio mwanamke wangu wa kwanza na sijui kama nitamwacha kwa sababu nampenda sana , sijawahi kupenda mwanamke mwingine,
Nikamuona yule afande amebadirika sura akawa kama amechukia kusikia maneno yangu , akaniambia mi nilitamani kupata mwanaume mwenye upendo wa dhati kama uliokuwa nao wewe , maana kama ni mali ninazo ninanyumba na magari mawili ila sina mtu wa kunipenda kwa dhati wanaume wengi ni waongo waongo tu , mi nikampa pole na tukapiga story nyingi tu lakini kama alikuwa na kitu kinamsumbua ila hakutaka kuniambia ,
Tulitoka kule beach na akanipeleka mpaka nyumbani, nikamshukuru sana , akaniambia kama nnashida yeyote nimwambie tu nisiogope , nikamwambia nashukuru sana kwa msaada wake na Haina haja ya kuwasiliana tena ,nikamuona amebadirika na amepoteza uchangamfu ,sasa nikajiuliza huyu afande anashida gani mbona amechukia gafra , yule afande akaniuliza kwanini tusiwe tunawasiliana ,? Nikamwambia Haina haja wala sababu kwa kuwa nitajitahid kumludisha mke wangu awe kama zamani na naamini atanielewa tu, yule afande hakusema kitu akawasha gari nakuondoka ,
Niliifuta ile namba ya yule afande huku nikiamini mke wangu ndio kila kitu nitajitahidi tu nimrudishe kwenye mstari ,
Nakumbuka nilipika pilau nyama huku nikikata kachumbali nzuri niliamini kutokana na mke wangu alivyoniona na mwanamke mwingine anaweza kupoa na tukaombana msamaha , na mimi nilipanga kama ataniomba msamaha basi kesho nampeleka kule kwenye ile nyumba ,
Tulimsubilia mke wangu lakini nikaona mtoto anataka kulala ikabidi tupakue tu chakula tukaanza kula , wakati tunakula mke wangu akarudi akiwa na hasira sana , kwanza alianza kuongea tokea yupo kule mlangoni, unaniletea malaya zako mpaka kazini kwangu si ndio, nikamwambia akae kwanza tule, akanijibu ,,Nile upuuzi ?unahongwa na malaya halafu unakuja kumpikia mwanangu , sasa kuanzia leo iwe mwanzo na mwisho kumpikia mwanangu uchafu wako huu , mke wangu aliongea akamwaga kile chakula chini , huna kazi huna kibarua unahongwa na Malaya zako unakuja kumpikia mwanangu upuuzi ,bado aliendelea kuongea , kitendo kile kilinikera sana ila nikajikaza tu , maana alikuwa anaongea mbele ya mwanangu ,nikamjibu na kumwambia mke wangu mi sijahongwa pesa hizi pesa ni za kwangu nimeamua leo nipike pilau kwanini unakuwa hivyo,? Usiniambie upumbavu wako kumbuka wewe umefukuzwa kazi kwa ajili ya wizi wako hizo pesa unatoa wapi kama sio kuhongwa na Malaya zako , ? Au kwa vile anagari unajua gari kalitoa wapi yule ,? Kama anatoa nyuma na wewe ukatoe upate gari ,
Mke wangu aliendelea kutoa maneno machafu , nikajua kumbe sijatatua shida bali nimeongeza matatizo ,nilimlaumu sana yule afande kwa kunipa mbinu kama zile, nilitamani kumwambia ukweli kuwa hata yule mwanamke sio mke wangu , tulipanga tu iwe vile nikashindwa nikanyamaza tu,
Ukweli nampenda sana mke wangu na najitahid kila njia arudi kwenye mstari lakini nashindwa , mke wangu alitoka na mtoto akaenda kumnunulia chips mi nikaokota lile pilau nikarudisha kwenye sahani nikaendelea kula ,
Nilikula lakini chakula kilinishinda nikainama tu chini nakuanza kulia , nililia mpaka mke wangu alipokuja nikajifuta machozi nikajifanya silii , " unajua unamwezi mmoja tu wa kukaa hapa kwangu sasa kwa vile umenionesha upuuzi wako utakaa hapa siku tatu tu , na utaondoka uniachie mwanangu , " aliongea mke wangu , niliamua nijishushe maana niliona sina jinsi nikapiga magoti na kumwambia mke wangu nisamehe tu maana mimi ndio nilikosea , lakini mke wangu hakutaka hata kunisikiliza ,aliingia ndani na kufunga mlango,
Nilikaa pale nikajuta , nakwambia ndugu msomaji maumivu ya mapenzi hayafananishi na chochote hata msiba hauko hivi, chunguza utaniambia ,
Nilimsikia mke wangu anaongea na simu halafu akafungua mlango akatoka , nikamuuliza unakwenda wapi ? Akaniambia tusifuatiliane kwani tumeshaachana na talaka anayo, nikabaki kimya ,
Mke wangu alitoka nje nikaona hebu namimi nitoke nimuone anaongea na nanani , nilipochungulia nikamuona mke wangu kakumbatiwa na lijamaa huku wananyonyana mate , niliumia na hasira zikapanda nikazunguuka nyuma ya nyumba nikachukua shoka nilizamilia kuuwa , nilitoka mpaka pale nje waliposimama namimi nikasimama na kumwambia yule jamaa aisee muache mke wangu , yule jamaa akaanza kucheka huku ananiambia ,sasa wewe huna kazi huna kibarua yaan wewe ni mama wa nyumbani , unafikiri mkeo pesa za kukutunza anatoa wapi,? Au lile duka la vipodozi ungeweza kulijaza namna ile ,?
Nilipandwa na hasira nikanyanyua shoka ,,,,,
.