NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3
SEHEMU YA 07&08
Sasa badala nijitetee nikajikuta napiga magoti na kumwambia mke wangu,naomba unisamehe, wale polis wakasema aisee nyanyuka unatupotezea muda,
Nikapiga magoti na kumshika mke wangu miguu nakumwambia mke wangu angalia mtoto wetu anaumwa nawewe unaenda kazini sasa mi ukinipeleka huko polis mtoto atabaki nanani ,
Mke wangu hakunisikiliza ndo kwanza akasema mpelekeni mi nakuja ,wale polis kweli wakanipeleka kituon , niliwekwa ndani kama mwizi , nilikaa mule kituon nakujiona mi ni mpuuzi sana , nilianza kumchukia mke wangu na nikamuona ni mwanamke katili sana , kwanza nilimfumania na mesegi za mwanaume pili akamleta mwanaume ndani kwangu halafu akaiba vitu vya ndani na nilipomuuliza akaniweka ndani , kisa tu anaona mimi sina kazi ,
Siku hiyo mke wangu hakuja hata kuniletea chakula ,nilimchukia Sana nikasema ni bora tuachane tu liwalo na liwe hawezi kunifanya mi mpuuzi kiasi hiki ,
Asubuhi alikuja mkuu wa kituo akawa anaita mtu mmoja mmoja kwa ajili ya kusikiliza kesi zao na wengine walipelekwa mahakamani ,
Niliitwa mimi nikaenda ofis ya mkuu wa kituo nikamkuta mdada mdogo mdogo tu lakini ananyota zake ,yaani huyu dada ukikutana nae njiani hajavaa nguo za kazi unaweza kumtongoza au kumfanyia fujo , akaniambia kesi yako imeandikwa umempiga mkeo na unamnyanyasa kila siku na hutaki kazi mkeo ndio anahangaika kukutafutia pesa ya kula , sasa unaweza niambia nini ili kesi yako isiende mahakamani ,?
Nikaanza kumwambia afande kuwa mimi nikweli ninamakosa kwakuwa nilimdanganya mke wangu , naamini nisingemdanganya basi mpaka leo tungekuwa tunaishi kwa amani kabisa , yule afande akaniuliza umemdanganya kivipi ,?
Nikamwambia mimi sio kwamba sina kazi ,mimi ni muaniliwa kabisa wa shirika la Reli TAZARA, sasa nilipewa likizo ya miezi mi tatu na nikapewa na kiwanja , niliporudi nyumban nikamdanganya mke wangu nimefukuzwa kazi , sasa hapo ndipo visa vya mke wangu vilipoanza akijua ni kweli sina kazi ,yule polis akacheka na kuniambia aisee we kweli unamoyo wa chuma sasa ulimdanganya ili iweje, ? Nikamwambia nilitaka nione uvumilivu wake kwangu maana kuna nyumba naijenga ndio nilipanga nimpe kama zawadi na ninunue Kigali kidogo cha kutembelea nimpe mke wangu kama zawadi maana nampenda sana ,nikamwambia hata akija naomba umwambie kuwa nampenda sana nataka tuishi kama zamani , yule afande akasema hee haya makubwa ,
Nikarudishwa kule mahabusu , mke wangu alikuja tukaitwa wote kwenye chumba cha yule mkuu wa kituo , mke wangu akaanza kueleza vitu vingine ni vya uongo kuwa eti mi nampiga na mnyanyasa sasa anataka tuachane na ili akatafute maisha yake ,
Mi nikapiga magoti na kumwambia mke wangu naomba usiniache kwa sababu mimi sio kama sina kazi bali nilikudanganya tu kuwa nimefukuzwa kazi lakini mimi Niko likizo na kuna nyumba naijenga ntakupa ,
Mke wangu akacheka na kumgeukia yule mkuu wa kituo na kumwambia unamuona alivyo muongo ,? Yaani mtu hana kazi amefukuzwa kazini kwa ajili ya wizi wake eti anasema hajafukuzwa na kuna nyumba anajenga nyumba gani we kapuruu ,usie na kazi wala kibarua ,
Mke wangu aliongea bila hata kituo na alionekana haamini kile nilichomwambia ,nikasema hakyamungu tena ninanyumba najenga eti afande mwambie mke wangu kuwa nampenda asiniache , mke wangu akamwambia afande kuwa huyu amechanganyikiwa na kukaa huko ndani ndio maana anaropoka ropoka , nikamwambia mke wangu mimi sijaacha kazi na nikirudi kazini nitakununulia na gari ,
Sasa jinsi nolivyokuwa naongea wao wakaniona nikama naropoka tu na maneno yangu hayana ukweli wowote hata yule mkuu wa kituo akajua mimi nadanganya tu , nikarudishwa ndani huku mke wangu akidai atahakikisha tumeachana ,
Mule ndani nilijilaumu Sana kwa kumdanganya mke wangu maana sikufiri kabla sijatenda , wakati nimejiinamia nikaitwa tena nayule mkuu wa kituo , akaniambia anataka twende kwenye hiyo nyumba ninayojenga ili aamini maneno yangu , nikamuuliza tunaenda na mke wangu au ,akanijibu mke wangu ameshondoka ameenda kazini , nikamjibu sawa ,
Tulitoka na gari ya mkuu wa kituo akiwa yeye ndo anaendesha mpaka kule nnakojenga , tuliposhuka tu mafundi walikuja huku wakiwa na wasi wasi na kuniuliza vip bosi kuna shida gani ,? Nikawatuliza na kuwaambia hakuna shida huyu polis anataka aone ramani ya nyumba yangu , bas wakaendelea na kazi ,nasisi tukawa tunaizunguuka ile nyumba , yule polis alishangaa sana akaniangalia mala mbili mbili na kuniuliza unauhakika mkeo hajui kama unamjengea nyumba ,? Nikamwambia hajui na siunaona nilivyomwambia akadai naropoka tu ,
Bas akaniambia hapa nimeamini ni kwako sasa twende kazini kwako tukifika tu mi ntajua , tukapanda kwenye gari na kwenda mpaka kule kazini kwangu , tulipofika ilikuwa ni muda wa chakula wafanyakazi wote walikuwa sehemu moja wanakula , basi waliponiona wote wakaamka na kuja kunikumbatia huku wengine wakisema aisee tumekumisi Sana hiyo likizo si iishe tu, basi tulitafuta siti tukakaa na yule afande , vyakula vikaletwa tukala na tukanywa tukafurahi na wafanyakazi ,mpaka yule afande akawa ananishangaa ,
Muda wakazi ulifika na wafanyakazi wote wakarudi kazini na sisi tukaaga na kuondoka ,tukiwa kwenye gari yule afande akaniambia unajua siamini mpaka sasa ,? Nikamwambia kwanini ,? Akaniambia niwanawake wachache sana wanaoweza kufauru mtihani uliompa mkeo ,nikamwambia nikweli na ndio maana najaribu kumrudisha kwenye njia ili tuwe kama zamani lakini naona hanielewi , akaniambia basi twende kwanza hapo mnapoishi nikapaone halafu ndo ntajua nitoe maamuzi gani , nikamwambia sawa ila nakuomba umwambie ukweli mke wangu kuwa nampenda nataka tuishi kama zamani , yule afande akasema usijali ,
Tulifika nyumbani nikashangaa milango iko wazi inaonekana mke wangu hakwenda kazini , nilimklibisha yule afande tukaingia mpaka ndani lakini tulipofika sebuleni tukasikia sauti kama ya mke wangu akifanya mapenzi chumbani kwa mtoto wangu , yule afande akaniangalia tukaangaliana , nikaona aibu sikujua hata nisemeje , ikabidi niende nikagonge mlango haraka maana zile kelele zilianza kumuuzi yule afande, niligonga huku namuita mke wangu , tukasikia kimya halafu mke wangu akafungua mlango na kutoa kichwa tu ,akaanza kufoka nani kakutoa polis? Halafu si nilishakuambia nikiwa nimepunzika sipendi unisumbue ,? Mke wangu aliongea huku jasho linamtoka alionekana nikama kuna kazi alikuwa anaifanya maana hata nywele zake zilikuwa Tim Tim ,
Nilimwambia mke wangu anisamehe na nikamgeukia yule afande na kumwambia amwambie mke wangu asifanye anachofanya kwani naumia na amwambie ukweli kuwa nampenda ,
Mke wangu akastuka kumuona yule afande ,na yule afande akamwambia mke wangu, Mimi mwenyewe ni mwanamke lakini siwezi kufanya upumbavu kama unaoufanya wewe , nikamwambia yule afande kuwa asimtukane mke wangu kwani anaweza akakasirika akaondoka nyumbani ,
yule afande akanikata jicho la hasira , mpaka nikajisemea he huyu afande vipi mbona kama amechukia gafra ,
Nini kitaendelea, je afande atamwambia ukweli mke wa jamaa au atauchuna tu awaache na maisha yao ,?
Usikose uhondo huu , kumbuka koment zikiwa nyingi basi haichelew kuja ,
ITAENDELEA
NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3
SEHEMU YA 8
Yule afande akanikata jicho la hasira mpaka nikajisemea he huyu afande vipi mbona kama amenikasirikia gafra ,
Akamgeukia mke wangu na kumwambia wewe nimpuuzi sana ,yaani unayotafanya hata shetani hafanyi hivyo , mke wangu akasema kwani nimefanya nini ,? Yule afande akamjibu inamaana hujui ulichokifanya ,,? Umeingiza mwanaume kwenye nyumba ya mumeo tena mnafanya na mapenzi wewe ni Bure kabisa ,hebu mtoe huyo mwanaume huko ndani la sivyo ntachukua Sheria mkonon, nikamuona mke wangu amenywea lakini moyoni nikawa nawaza asije akachukia akaondoka ,
Mtoe bas mi nnaharaka zangu ," yule afande aliongea kwa hasira utazani ni yeye aliefumania , nikamuona mke wangu anaingia chumbani na kabla hata hajafunga mlango nikajikuta nimezama ndani , nikamuona yule jamaa amejibana nyuma ya mlango , nikamkunja , akanisukuma nikadondoka chini , kabla sijaamka akafungua mlango kwa spidi akachomoka , lakini akadakwa na yule afande pale mlangoni , nilipotoka sijauliza nikaanza kumpa kipigo yule jamaa ,yule afande akawa anacheka huku ananiambia unampigaje mtu kama mwanamke wewe kaza mikono hiyo, nikajitahidi kukaza mikono maana hata mimi nilijistukia kuwa siwez kupigana kabisa ,na ningekuwa mwenyewe nisingeweza hata kumgusa huyu jamaa ,
Yule jamaa akanisukuma tena kwa mala nyingine na kutoka zake nje mbio , yule afande akawa ananiangalia huku anatabasam sikujua alimaanisha nini , ila mi nikajifanya najitutumua nakusema aisee anabahati sana ningemuumiza , yule afande akawa ananiangalia tu , mke wangu alijifungia ndani hakutaka hata kutoka , nikamgongea huku nikijifanya nnahasira sana mbele ya yule afande , lakini mke wangu hakutoka mpaka yule afande akagonga mlango kwa nguvu na kumtishia kuwa atauvunja mlango ndo akafungua ,
Cha ajabu alipofungua tu hasira zote zikaisha nikamkumbatia huku nikimpa pole , yule afande akachukia akaniambia hebu nyanyuka twende kituon , nikashangaa nikamuuliza kufanya nini tena ,? Akaniambia twende tukafute kesi , nilinyanyuka huku nikimuacha mke wangu akiwa bado analia mpaka nikawa namuonea huruma ,
Tuliingia kwenye gar huku yule afande akiwa na hasira akaniuliza sasa wewe ulikuwa unamuomba samahi ya nini mkeo ,? Nikawa sina jibu maana hata mimi mwenyewe nilishangaa tu namuomba samahan ,
Mkeo ndo alitakiwa aombe samahani na sio wewe , na ulitakiwa uonyeshe ujasiri wa mwanaume , yule afande alisema nilimuona kama amechukia sana , hebu nipe namba zako , aliongea tena yule afande nikajiuliza hizo namba ni zanini , nipe namba zako nitakuonesha jinsi mwanamke anavyoomba msamaha , aliongea tena , nikajisachi nikakumbuka simu nimeacha ndani nikamwambia basi anisubilie nikachukue simu ,nikaingia ndani nikamkuta mke wangu kanyamaza hata halii tena macho makavu akaniuliza kwa hasira , hivi ukiulizwa yule mwanaume umempigia nini utajibu nini ,? Nikashangaa maana sikutegemea swali kutoka kwake ,nikamjibu kuwa kwa vile alikuwa anafanya mapenzi nawewe , mke wangu akaamka na kunishikia kiuno huku anasema kwa taarifa yako yule alikuwa hafanyi mapenzi na mimi bali tulikuwa tunapiga mahesabu tu ya vipodozi vyangu humo ndani , sasa unampiga mkaka wawatu amekukosea nini na kwanini hujauliza kwanza ,? Nikabaki nimeganda tu , akaendelea kusema mimi naomba tuachane tu na kila mtu abaki na maisha yake nishachoka mimi kuishi kwa manyanyaso ,mke wangu akaingia ndani na kuanza kufunga vitu vyake,
Nikarudi kule kwa afande nakumpa ile simu yangu huku nikimweleza kuwa mke wangu anaondoka ameamua tuachane , niliongea huku machozi yakinilenga lenga ,yule afande akasema hawezi kuondoka huyo anatingisha kiberiti na akiondoka nipigie namba yangu hiyo , akanirudiahia simu , nikamuuliza kuhusu kesi akaniambia haina haja ataifuta tu kwan ameshaona mwenye kosa ni nani,
Nikashuka kwenye gari nakuingia zangu ndani, nikamkuta mke wangu kajifungia chumbani huku anaimba wala hana hata wasi wasi ,ilifika jion nikaenda kumchukua mtoto niliporudi sikumkuta , nikampigia simu ila hakupokea , nikaona ngoja niuchune tu ila kiukweli nilikuwa na mawazo sana nilitamani tuishi kama zamani na mke wangu ila nikama haiwezekani ,
Wakati nnamawazo simu yangu ikaita , alikuwa ni yule afande akaniuliza vipi mbona kama unaongea kiunyonge ,nikamjibu hapana ila mke wangu hayupo hajarudi mpaka sasa , akaniambia basi ngoja nije ,
Nakweli muda kama wa saa tatu tatu hivi usiku nikaona kagari keupe kazuri zuri kamepaki nje ,huku dereva anapiga honi mwanzo nikazani ni mke wangu maana nishazoea huwa analetwa na gari ,lakini nilipotoka tu nikamuona yule afande ndo yupo ndani ya kigari hicho ,alivaa nguo zake za nyumbani yaani alionekana ni Binti mrembo sana ,akaniuliza vipi mbona unawasiwasi na maisha yako wewe ,""? Nikamjibu hapana sina wasi wasi , akashuka kwenye gari tukasimama huku tumeegemea kigari chake , gafra tuliona gari linakuja upande wetu na likafika karibu kabisa na gari la yule afande , likasimama , akashuka mke wangu na pia akashuka jamaa mmoja hivi sio yule wa mchana , wakakumbatiana inavyoonekana ni kama hawajatuona , nikapandwa na hasira nikataka niende lakini yule afande akanidaka na kunikumbatia ,wakati namshangaa yule afande nikamuona mke wangu kama amestuka kitu akawa anakuja upande wetu si akatuona , nikamwambia afande niachie mke wangu atatuona , ye akanijibu onyesha uwanaume wako hapa sawa ,,? Aliongea hivyo huku akileta mdomo wake ukagusana na mdomo wangu sasa mke wangu akatukuta tukiwa kwenye hali ile ,
Ooohooo nini kitaendelea hapo koment zikiwa nyingi leo leo INAKUJA ,
ITAENDELEA,....FULL.