NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3
SEHEMU YA 13
SHUUUKA CHINIII,,,!
nikamuona bado anasua sua nikamwambia utaniuzi shuka chini unanichafulia gari langu , mke wangu akasema lakini nimekuja na mtoto , nikashangaa nikamwambia yuko wapi akanioneshea na kidole ,kweli nilimuona mwanangu akiwa kando ya nyumba nyingine iliyoko pembeni ya ile nyumba ninayojenga ,
Nilishuka nikatembea nikam beba mwanangu huku nikimuuliza kwanini umekuja na mama huku,? Akaniambia mama aliniuliza baba yako anaendaga wapi nikamwambia kuna nyumba anajenga tulishawahi kuja akaniambia tuje tuione ndo tukaja ,
Sikumlaumu sana mwanangu , nikam beba na kumuingiza kwenye gari ,
Sasa nikashindwa kumtoa tena mke wangu kwenye ile gari kwa kuwa mtoto nae alikuwepo lazima angejisikia vibaya ,nikawasha gari na kuondoka ,
Wakati tuko njiani mke wangu akaanzisha maongezi, kwa kuniambia mume wangu umenifundisha kitu naomba unisamehe kwa kila jambo nililokufanyia ,nakuahidi sitorudia tena ,sikumjibu niliendelea kuendesha gari maana sikutaka mtoto ajue kama tunaugomvi mimi na mama yake ,aliendelea kujiongeleaha wala sikumjibu , mpaka tunafika nyumbani , tuliingia ndani na mimi nikaingia zangu jikoni kwa ajili ya kuandaa chakula changu na mwanangu , akaja kule jikoni na kuniambia eti usijali leo ntakupikia chakula kitamu sana , nikamwambia unanipikia mimi au yule bwana ako wa asubuhi ,? Hakunijibu nahisi kama aliona aibu , nikamwambia kama hunijibu ondoka humu jikoni nikimaliza kupika uje upike chakula chako , nikamuona haondoki ndo kwanza ana andaa andaa sufuria ya wali, nilimwambia tena ondoka humu jikoni , akaniambia lakini si nilishakuomba msamah,,,,, kabla hata hajamaliza nilijikuta nimechukua prampein ile ya kupikia chapati nikampiga nayo ya kichwa TOKA NIMEKWAMBIA ,,, yaani sijui hata hasira zilitokea wapi ,
Mke wangu alitoka huku ameshika kichwa ile sehemu niliyompiga huku analia , aliingia mpaka chumbani kule kwa mtoto nikamsikia analia , kwa upande fulani huruma iliniingia nikatamani kwenda kumuomba msamaha ,lakini miguu iligoma kabisa , nikapika wali njegere kwa Nazi weee kitu kilinukia mpaka mtaa wapili ,
Nikala na mwanangu tukashiba nikampeleka kulala na mimi nikaenda kulala kwenye V8 langu si unajua kipya kinyemi ,
Wakati nimejipunzisha zangu nasikiliza mziki taratibu sms ikaingia alikuwa ni mke wangu eti anaomba nimsameha anajua nnahasira lakini anaomba tu msamaha tuish kama zamani ,
Sikuweza kumaliza sms hiyo nikazima simu nikajipunzisha ,
Asubuhi nikawasha simu yangu nikakutana na mesegi kibao zote za mke wangu hata sikuhangaika kuzisoma nikazifuta , nikamuona anamuandaa mtoto kwa ajili ya shule ,nikampita tu ye ndo akanisalimia za asubuhi nikamjibu salama nikaingia zangu kuoga ,
Nilitoka kuoga nikaingia zangu chumbani nikauchapa usingizi ,nilipoamka nikakuta amepika maziwa na chapati na supu et ameniwekea halafu yeye akaandika kikaratasi eti kula mume wangu ushibe,
Mi hata sikula ,
Nikapika vyangu nikala , ilifika saa 8 hivi au 9 kwenye kumi kumi kasoro Nakumbuka , nikapigiwa simu namba ngeni ,nikapokea kumbe alikuwa afande , akaniambia njoo kituoni kuna jambo , mkeo kakamatwa ameleta fujo kwenye duka la watu la vipodozi, nikashangaa nikamwambia nakuja , niliwasha V8 langu nikaenda mpaka kituon nikashangaa mpaka polisi wananiangalia , maana ile gari ni kama ya mkuu wa wilaya au m bunge kama sio waziri fulani , nikasikia polis mmoja akimwambia mwenzake unamkumbuka huyu jamaa si tulimuweka ndani juzi juzi kumbe ni mtu mwenye pesa zake aisee ,
Siku jali nikapita mpaka kwa mkuu wa kituo ,nikamkuta mke wangu kakalishwa chini aliponiona akaanza kusema eti mume wangu lile duka letu kuna mtu anasema la kwakee , mlango ukafungwa huku ndani tukiwa mimi yule afande na mke wangu , sikuyajali sana maneno ya mke wangu nikamsalimia afande kwa kumkumbatia ( kumbuka huyu afande ni yule alienisaidia kipindi kile ,)naye akanikumbatia sasa mi si nikaongeza manjonjo nikam busu afande mdomoni yule afande akaniwahi kwa kunishika nyuma ya kichwa na kunikandamizia mdomoni kwake tukawa tunanyonyana mate ,
Nikamuona mke wangu anatoa macho kama kaona muvi ya kutisha ,
Tuliachiana huku yule afande akisema I love you , nami nikajibu I love you too, tukakaa kwenye viti huku mke wangu akiwa haamini kila kitu anachokiona ,
Afande alimwita afande mwingine akamwambia amchukue mke wangu ampeleke mahabusu kwa sababu muda ule anamaongezi na mimi , mke wangu akanyanyuliwa kama mwizi huku akiniambia nisaidie mume wangu , mi nikamwambia kwanza sijaja kwenye kesi yako mi nimekuja nnamaongezi na huyu mke wangu ,nikamuoneshea kidole afande , mke wangu akaanza kulia akapelekwa mahabusu huku akilia kwa sauti ,Akisema jamaanii naombeni mwambieni mume wangu anisamehe nimekoma mieeee ,,!!!
Nini kitaendelea. Usikose uhondo huu ????????
Koment ziwe nyingi
ITAENDELEA .