UTAMU WA MABOSS??? 6~7
Linda alipakiwa kwenye gari akaketi pembeni ya Alex aliwaelekeza anakoshukia wakampeleka mpaka huko..
Walimshusha wao wakaondoka zao..wakati Alex na sam wanaendelea na safari yao Alex alimwambia Sam "Yule binti ana wazimu sana"
ALEx alisema na kumtazama Sam huku Sam akiwa anamtazama kwenye kioo.
"Bwana, unatabasamu," alisema Sam
"Unamaanisha nini kuwa natabasamu, Kwan umeniona nikitabasamu ?," Alex aliuliza
"Ndio ulikuwa unatabasamu Mr au msaidizi wako kakuvutia" ??
“fatilia mambo yako” Alex alisema kwa ukali na Sam akanyamaza mara moja.
Walifika nyumbani na Sam akaegesha gari kati ya magari mengine kwenye gereji. Alex alishuka na kuliona gari jeupe ambalo lilikuwa packing na kushangaa sana..
"Sam ili gari la nani Mimi Sina gari nyeupe,..Sam naye alitulia..
Alex alimwambia Sam nahisi Kuna mtu ndani ya nyumba yangu" Aliongea kwa sauti ya wasiwasi.
"Ndio, nilisahau kukuambia kuwa wazazi wako walikuja mchana," alisema Sam na Alex akapumua.
"Ohh kumbe wanandoa hao wa zamani wamerudi Chicago,..
Alex aliingia ndani na kukaribishwa na kumbato la mama yake.
"Angalia mwanangu, mbona umekonda hivi ," alisema mama yake Alex huku akimgeuza Alex kana kwamba alikuwa anataka kumkagua zaidi.
.
"Mama acha.ulikuwa haupo kwa miezi 6 ni lazima nibadilike" Alex akasema huku akiwa anaelekea CHUMBAN kwake akiwa kana kwamba anampuza mama yake.
"Hiyo ndio njia sahihi ya kumkaribisha mama yako" akasema mama yake alex
"Samahani mama. Umekula na baba yuko wapi" Alex aliuliza na mama yake akatabasamu.
"Ndio nimekula na baba yako yuko kwenye chumba tulichojiwekea" alisema na Alex akaitikia kwa kichwa.
" SAWA. Naelekea chumbani kwangu sasa"akasema Alex..
"Hutakula" akauliza mama yake Alex
"No, I'm good. Goodnight mama" Alex alimwambia mama yake na kumshika shavu kabla ya kwenda chumbani kwake.
Alex alianguka kitandani kwake na hakutaka kula wala kunywa. Hakuoga hata kubadili nguo.
Asubuhi iliyofuata aliamka na kuvaa kwa ajili ya kazi. Alijiandaa na kushuka ukumbini ambapo alimkuta baba yake anasoma gazeti la habari.
"Habari za asubuhi baba" alimsalimia na baba yake akamtazama.
"Habari za asubuhi Alex, naona unaenda kazini" akasema baba yake Alex.
"Ndio naenda" akajibu
"Hakikisha unakuja kula usiku wa leo kwa sababu mama yako alisema haujakula chochote kabla ya kulala, zaidi ya hayo tuna mambo ya kujadili," alisema baba yake Alex na Alex akaitikia kwa kichwa kabla ya kuondoka.
Alifika ofisini dakika 10 kabla ya saa mbili na aliwah ili Linda amkute kazin so Linda ana dakika 10 tu za kufika kazini.
****************************
Linda tayari ameingia barabarani saa 7:30 asubuhi. Alishuka kwenye teksi na kwenda moja kwa moja hadi ofisini kwake lakini alikutana na Ella akiwa njiani.
"Habari za asubuhi linda" alisalimia na Linda akamtazama akiwa na mshangao.
Ella ni nini"akauliza Linda
"Je, huna marafiki wengine" Linda aliuliza kwa sababu haelewi ni kwanini Ella anamganda kama mpnz wake tangu walipokutana siku 2 zilizopita na Wala hawajazoeana sana.
"Jambo ni kwamba, sina rafiki. Wewe ndiye rafiki pekee niliye naye sasa" akasema ella
"Kwanini" akauliza Linda
" mimi ni mtu mwenye shughuli nyingi na sichangamani na watu lakini nimetokea TU kukupenda wewe " akasema ella.
"Awwn, unanifanya nione aibu sasa" Linda alizungumza huku akijifunika uso wake na ella akacheka jambo ambalo lilimfanya Linda nae aungana naye.
"Hata hivyo samahani MAANA SIKUJUA KAMA huna marafiki" akasema Linda
"Usijal ila nitakuja ofisini kwako baadaye” Alisema na Linda akaitikia kwa kichwa kisha kila Mmoja akaenda kuendelea na majukum yake.
Linda Aliweka pochi yake kwenye meza yake na kukimbilia ilipo kahawa,
" nina uhakika huyu boss mpzi yuko ofisini kwake,sasa hii kawaha Natakiwa kuiandaa vipi maana Niliifanya kahawa ipate joto akanifokea sana, inaonekana hapendi iwe baridi au moto, so Natakiwa kutengeneza kahawa ya uvuguvugu, akawaza linda.
"Na leo lazima nimkomeshe nitamuwekea vidnge vya usingizi kwenye kahawa yake kisha nimvuruge kama alivyonivuruga Mimi nywele ZANGU,..
"Yani leo ataamini mimi ni genius, nina akili kuliko yeye, alijisemea Linda Kisha akaweka daw za usngz kwenye kahawa ya Alex na kuikoroga huku dawa zikiyeyuka Kisha akampelekea.
"Habari za asubuhi bwana" Linda alisalimia,
"Kahawa yangu" Alex aliuliza na Linda akampa.
"Ewaaa! Sasa Leo umefanya kama bosi anavopaswa kufanyiwa, akasema Alex.
"Ratiba yangu ya leo ipoje " akauliza Alex
"Hakuna chochote Leo bwana ila nitakujulisha kama kuna lolote litakalotokea" akasema Linda.
"Sawa na usisahau kuangalia email na kuzijibu, tumia ubongo wako wakati wa kufanya kazi umenisikia, alisema Alex na kutabasamu, ingawa lilikuwa tabasamu la dhihaka lakini na Linda alitabasamu pia..
Wakat Linda anatoka kwenye ofisi ya Alex alimtizama kisha akawaza "Alex ngoja tuone mimi na wewe nani atadhihakiwa, alisema kimoyomoyo kutoka ofisin.
:
Linda alitoka nje ya ofisi na kwenda kuangalia emails ambazo Huwa zinatumwa kwenye kampuni.
Alimaliza kuangalia kwa takriban masaa 2, "ndio inachukua muda mrefu hivi Linda aliwaza maana aliamin kazi ya kukagua emails ni yadakika chache,lakin ilikuwa tofauti na alivyofikiria.
Alipiga miayo kwa uchovu na kwenda ofisini kwa Alex akiwa amebeba makeup kit.
Alianza kumremba Alex ambae alikuwa tayar amelala kutokana na kunywa kahawa yenye dawa ya usingizi.
Alichukua wanja na kutengeneza nyusi zake, kisha akamremba chini ya macho kwa kutumia rangi ya bluu, alichukua lipstick yake nyekundu na ya zambarau na kumpaka Alex rangi ya zambarau kwenye mdomo wa juu na nyekundu kwenye mdomo wa chini.
Alafu sehemu ya chini ya mdomo akampaka rangi nyeusi.
"fikiria jinsi atakavyoonekana akiamka??? Linda alijiambia
" Nashukuru Mungu hakusogeza hata mkono nilipokuwa nafanya make-up coz niliifanya kwa umakini na dawa za usingizi zimenisaidia sana, Linda akawa anajiambia.
"Anafanana na shetani " alisema linda na kuanza kucheka kimya kimya.
********************************
Alex Aliamka karibu saa kumi na Moja jion na akatizama saa yake akashangaa jioni imefikaje haraka hivo.?
Inamaana nimelala masaa yote hayo??Ilikuwaje mpaka nimelala muda wote huu? Mwisho alikumbuka kuwa alikunywa kahawa baada ya hapo hakumbuki kitu kingine chochote , au ile kahawa ilikuwa na dawa? Akawa anajiuliza Alex.
"Na nani anaweza kuniwekea dawa kwenye kahawa? Alex akawa anajiuliza.
" Inaweza kuwa Linda? Hapana, asingefikia kiwango cha kunitia dawa kwenye kahawa hata kama ananichukia kiasi gani, labda nililala tu, akawaza Alex.
Aliangalia wakati na akakumbuka bado ana chakula cha jioni cha kuhudhuria, ambacho alitakiwa akale pamoja na wazaz wake.
Alex alisimama na kutoka nje ya ofisi yake huku akiwa ameshika simu yake na kuweka kwenye sikio lake.
Alikutana na Linda ambaye alikuwa anakuja ofisini kwa Alex .
"Bwana umeamka," akasema Linda
"Potea" Alex alisema na kuendelea kutembea huku Linda akiwa nyuma yake huku akimcheka tu?
Alex hakujali kwa kuwa anamjua Linda ni chizi aliamini huenda uchizi wake umemkolea ndo maana anacheka cheka ovyoo
Alex aliona kitu cha ajabu alipofika mapokezi na wafanyakazi wake wote walianza kunung'unika na kunong'onezana kitu??
Wengine walikuwa wanacheka na kumwangalia zaidi usoni Alex alishangaa alitoa simu yake na kujitizama kwenye camera asalaaaaale??
Itaendeleaaaaaaa
Full 1000
WhatsApp 0742133100.