DO YOU LOVE ME..... 01 (S2) ????????????????????
LAST FOREVER
Maamuzi yake yalikuwa yamesimama hivyo na hakutaka kusikia upande wangu wa pili ambao umebeba hisia nzito dhidi yake. Rola akaniua mbele ya macho, akaniua nyuma ya macho yake. Hakutaka kupokea hisia zangu huku akisisitiza kwamba, nimeshamuoa Rely basi nibakie kwa huyo mtu.
"Ulishafanya maamuzi ya kumpenda na kumuoa mwanamke mwingine, kwanini unataka uishi na mimi? Unadhani watanichukuliaje huko nje? Sidhani kama ni sahihi. Hivyo basi, njia rahisi ya mimi na wewe kuishi kwa amani ni kuwa marafiki tu"
"Lakini kumbuka upendo wangu kwa Rely ulikuwa wa kulazimishwa. Sikupanga wala sikuwa tayari kuingia katika mahusiano na huyu mtu. Ningefanyaje ikiwa tayari wazazi walishaona nafaa kuoana naye? Lakini kwa sasa nipo tayari kuachana naye ili nikuoe Rola. Please pokea upendo wangu. Kwanini unataka niwe nateseka kila napokuona? Natesekaa kila ninaposikia jina lako? Mimi ni binadamu, nina moyo mmoja ambao unafanya maamuzi sahihi. Sidhani kama kukuchagua wewe uwe sehemu ya maisha yangu ni maamuzi mabaya"
"Sitaki kusikia hizi habari Rahim, tena usitake nikuchukie sababu sioni umuhimu wa neno nakupenda ikiwa ulioa mtu mwingine. Ok, ulipambana kwa ajili yangu na nashkuru kwa hilo. That's ili nisifute alama ya msaada wako katika maisha yangu basi naomba tubakie kuwa marafiki. Hakuna kingine naweza sema. Samahani kama nitakuwa nakukosea. Kuwa marafiki ni bora zaidi na utalinda msaada wako kwangu kuliko kuwa wapenzi. Binafsi, sina hisia na wewe hata chembe" Rola alinipiga misumali mingi yenye kuumiza ndani ya moyo wangu.
Nikakosa furaha tukiwa Dar es salaam, nikakosa furaha tukiwa airport wakati tukijiandaa kwenda Zanzibar na hata tulipofika huko nilipoteza kabisa amani ndani ya moyo wangu.
"Rely anaendelea kumtafuta Mama yake. Mama Rely ametoweka nyumbani tangu wiki moja nyuma. Hajulikani wapi yupo?" Lilikuwa ni sauti la Thelesia ambaye alitupokea Airport.
"Wapi ameelekea sasa?" Niliuliza
"Mama kageuka kuwa chizi pamoja na Baba pia ambaye amelazwa hivi sasa. Kwa kifupi familia imeingia katika wakati mgumu"
"Wameyataka, waliona raha kunitesa si ndio" Rola alipayuka kwa hasira, moyoni nilijua nini kilikuwa kinaendelea. Nikafahamu yale ndio yalikuwa yaliyotabiriwa na mganga. Tayari watu wabaya wamejulikana na hali ya uchizi imewaingia.
Basi, tuliondoka hadi nyumbani ambako tulikaa hadi jioni, Rely alikuja akiwa hoi bin taabani.
"Mama amepotea Rola" Rely alitujuza akiwa anakaa katika sofa.
"Hakuna unayemwambia asiyejua nini shida? Mama yako aliniroga akadhani kwamba kila kitu hakina mwisho"
"Basi, naombeni mkanisaidize kumtafuta"
"Hakuna wa kufanya hivyo kwa hivi sasa. Kwanza nataka kujua wapi Hussein yupo?"
"Hussein yupo hapa hapa Zanzibar"
"Sawa, kesho mtanipeleka. Nataka kuonana na barafu wa moyo wangu"
"Unadhani atakuwa na mapenzi ya dhati kwako? Halafu Mama hakukuroga"
"Huna hunalolijua, vyema ukapiga kimya" Rola alijibu na aliondoka nami nilibaki na Rely pale sebureni.
Rely alinisimulia vitu vingi sana kuhusu maisha yao pale nyumbani mara baada ya Mimi kuondoka.
"Kulikuwa na vitu vinakuja usiku na kutua juu ya bati au dirishani katika chumba cha Wazazi wangu. Vinakonga na kuwaita, sijui ni vitu gani?"
"Mh! Pole sana"
"Ahsante, usiniambie kwamba wewe ndio umefanya kazi ya kumtibia Rola?"
"Ndio, nimemtibia"
"Yaani wakati mimi nateseka na familia yangu, wewe upo busy kumtibia Rola. Ulitumwa kwani?"
"Hakuna kunilaumu katika hili sababu ilikuwa ni lazima Rola apone"
"Ok, kapona. Unadhani hizi mali zitakuwa za kwangu tena? Kwanini unafanya mambo bila kunishirikisha Rahim? Unataka nikupende vipi ili uamini kwamba nakupenda? Sijui hata umepatwa na nini kha?"
"Hata hajapatwa na kitu Rely. Yah! Baba na Mama yako waliniroga na sasa mwenye mali nimerudi tena mjini kumiliki mali walizoacha wazazi wangu. Mwanasheria aliyekaachiwa hizi mali ili aziongoze namjua vizuri. Najua kila kitu sababu kumbukumbu za miaka yangu niliyoishi bado zipi kichwani. Nataka ujue kwamba, kuanzia sasa wewe ni mtumwa katika hii nyumba na nisisikie unajaribu kumtafuta Baba yako kwa kutumia mali zangu. Simamisha kabisa hilo zoezi. Wazazi wako wakajua kwamba nitaumwa milele, nothing last forever. Kuna muda maumivu yanaisha na maisha ya kawaida hurudi. Wao si walimaliza vita, mimi ndio nimeanza sasa" Rola ambaye alikuwa amesimama katika ngazi ya kupanda juu alizungumza.
Nilijikuta namtazama Rola sio chini ya mara moja wala mbili, moyoni nikajiuliza kama ni yeye ama sio yeye? Sikutegemea kuwa siku moja Rola kama akiwa mzima basi anaweza kuzungumza maneno kama haya? Lakini huyu ndio Rola, aliyekuwa chizi hapo kabla na sasa ni binadam mwenye akili zake timamu.
Nunua season two kwa 1000Tsh! Kumbuka hii ndio Season ya Mwisho Kwa simulizi huu.
Nifollow Instagram, natumia .