DO YOU LOVE ME 05
ACCEPT THE REALITY
Ugumu wa maisha ulianza hapa maana hatukuwa na chaguzi tena, kutoka kumsaidia mtu hadi anarudi katika afya yake hadi anakuja kukufukuza kama mtumwa, mwizi ama mtu mwingine mtenda mabaya. This was pain to us lakini hatukuwa na jinsi, tulikubali kuuchukua ukweli ule na kuondoka nyumbani kwake.
Safari yetu ilienda kutua hadi Dar es salaam ambako nilifikia nyumbani kwa Mama. Maisha ya Rola yalikuwa chini ya Hussein ambaye alimwamini kwa kila kitu, mipango yake ilianzia kwa huyu mwanaume. Hussein akawa kama Baba na Mama kwake, alimwamini na Husseina akupokea uaminifu kutoka kwa kigoli huyu.
Maisha ya Dar es salaam hayakuwa mabaya sababu nilirudi tena katika biashara yangu ya kuuza Ice cream kama ilivyokuwa kawaida. Kwahiyo ikawa nashirikiana na Rely katika biashara hii huku siku zingine akabakia nyumbani kwa ajili ya kumtazama Mama yake ambaye kadri siku zilivyozidi kwenda, ndivyo alivyokuwa akizidi kurenduka.
Siku za mwanzoni Mama yangu alikuwa yupo sawa lakini kadri siku ambavyo zilivyozidi kwenda ndivyo Mama alianza kuchoshwa na uwepo wetu pale nyumbani hasa Mama Rely. Nilianza kuyasikia maneno kwa majirani kuwa Mama yangu anamnyanyasa Rely na familia yake huku akisema kwamba wapo pale kama misukule na siku yoyote anaweza kuwafukuza. Mwishowe nikaja kujionea mwenyewe waziwazi.
Siku moja asubuhi kabla ya kuingia katika mihanjo yangu, Mama aliniita na kunikalisha kitako. Nikajua kwamba Mama angekuwa na jambo la maana la kunieleza lakini haikuwa hivyo.
“Hii hali inayoendelea ndani unaielewa?”
“Ipi tea Mama?”
“Baba wewe, huyu mtu atakuwa hapa kila siku au wanapanga kuondoka? Maana nimechoshwa kwakweli, nyumba kila sehemu unayokaa kuna mate”
“Mama, kwani nilikueleza nini? Hawa watu hawana pa kwenda zaidi ya mimi kuishi nao hapa”
“Weee! Hapana kwakweli, nimechoka kufuga huyu mgonjwa. Kwani mie ndio nilimwambia aroge sasa?”
“Mama, kwanini unafika mbali hivyo?”
“Rahim, kiukweli nimechoka kuishi na huyu mwanamke hapa ndani. Ikiwezekana ondoka naye, sitaki kabisa. Tafuta eneo lingine la kuishi. Tazama, wamekaa hapa ndani ya mwezi mmoja tu lakini sina amani katika maisha yangu. Nyumba inanuka mate kila sehemu. Sasa jifanye mbishi, haki ipo siku nitamtupa huyu mtu” Mama alifoka huku akiwa hataki kabisa kusikia lolote lile ambalo ningemweleza
Huu ukawa ni wakati mwingine mgumu kwangu kwani sikuwa na sehemu ya kwenda kuishi nje ya pale nyumbani. Niliumiza kichwa mno, nikatamani nimwambia Rely juu ya kile ambacho nilikuwa napitia lakini nilishindwa. Nikabaki kuwa mpweke na mwenye mawazo sana.
Afya ya Mama Rely ikazidi kuwa mbaya, alikuwa anaweza kuamka saa tisa usiku akaanza kupiga kelele mithili ya kuku aliyeona mwewe. Bila kumfunga kamba ama kumwekea dawa za kumlaza asingeweza kulala.
Maumivu yakamwandama Mama Rely, huu ndio ukawa upande wa pili wa mwanamke huyu, ile roho mbaya ambayo nilikuwa nayo ya kumtaka ateseke iliniisha kabisa. Nilianza kumuonea huruma kwakweli.
“Natamani Mungu angemchukua Mama yangu, hii ni zaidi ya adhabu anapitia” Rely alizungumza kwa uchungu sana akiwa anamtazama Mama yake ambaye aliendelea kutema mate.
“Kesho kuna sehemu nitakupeleka ili tuone inakuaje?”
“Wapi huko mume wangu?”
“Kule ambako Rola alipona, huenda atapona pia” Nilimuahidi huku nikiwa tayari kumpeleka kwa mganga ili aweze kupona.
Nakumbuka tulilala vizuri na asubuhi ilipopambazuka tu, jambo la kwanza lilikuwa ni kwenda katika chumba ambacho Mama Rely alikuwa akilala. Maskini! Sikumkuta. Nikapatwa na mashaka huenda Mama yangu atakuwa amemtoa, nilienda kumuuliza.
“Mama Rola yupo wapi?”
“Khe! Nimemtupa bwana, haiwezekani awe ananipigia kelele usiku kucha nashindwa kulala. Nimemfungulia mlango katoka”
“Mama, unafanya nini lakini?”
“Bwana usinipangie namna ya kuishi sijui kama unanisikia? Yumba ya kwangu, maji ya kwangu na kila kitu cha kwangu humu ndani. Nimeshakuambia ondoka na huyu chizi wenu hukunisikia. Ulitaka nifanyaje sasa?” Mama aligomba
Dah! Sikutaka kugombana naye, kwa bahati mbaya Rely alisikia kile ambacho kilikuwa kimeongelewa na Mama. Nilipoingia chumbani nilimkuta akiwa analia mno, alihisi kunyanyasika.
“Kumbe Mama yako hana mapenzi na Mama yangu halafu hujaniambia? Leo hii amemterekeza. Wapi nitampata Mama yangu sasa?”
“Baby, mimi sikujua kama Mama angefanya hivi. Lakini hili la kumtafuta, naomba uniachie mimi.... .