DO YOU LOVE ME 03 (S2)
PAINT PAINTER
Niliingia ndani na kumkura Rely ambaye alikuwa akidondosha machozi sio kawaida. Alikuwa hana furaha wala amani ndani ya moyo wake na alionekana kama kuna jambo kubwa limemkuta. Nikashikwa na wasiwasi, nilienda kumuuliza nini ambacho kinamliza? Jibu lake liliniumiza moyo ijapokuwa nilitarajia hili.
"Baba amefariki Rahim" vuta picha kauli kama hii inamtoka mwanamke ambaye alikuwa akimpenda na kumchukulia Baba yake kama ndio kila kitu. Yale maumivu yote yahamishe kwa Rely. She was crying like a child akilalamika kwanini Mungu amemtwaa Baba yake mapema vile.
Kazi kubwa ilikuwa upande wangu ni kumweka sawa, nilianza kumbembeleza ili akae sawa. Alipoingia Rola, hakuwa na muda wa kusubiri jambo, alisema.
"Najua tayari kuna mchawi kafa, kumbe kuna muda hata nyie mnaona maumivu. Haya niambie nani kafa? Yule wa hospital ama yule mwingine chizi aliyekimbia mji?"
"Rola, maneno gani unaongea haya? Sawa una haki ya kumchukia aliyekuumiza lakini ni hadi siku aliyekufa kweli? Jaribu kubadilika basi" Nilimsihi na kumkataza
"Khe! Naona unataka kunifundisha namna ya kumpenda na kumchukia mtu si ndio? Hivi nani ana sauti humu ndani? Mbona mnajisahau kama mko hapa kutumikishwa na kufanya kile nachokitaka? Au mnategemea uchawi wenu? Si ndio? Halafu wewe Rely, huna linalokuliza la maana hapo. Baba yako alikuwa mchawi, ko furahia maana mchawi kafa hata kizazi saivi utakiona"
"Rola, unafika mbali. Kumbuka maneno unayoyaongea unamuumiza mwenzako. Ok, hakuna wa kukufundisha sababu hayo ni maisha yako na umeyachagua kuishi hivyo lakini kumchukia marehem ni kujichosha. Hukupaswa kufanya hivyo"
"Haha! Nitamchukia leo, kesho na kesho kutwa hadi Kiama. Aliwauwa wazazi wangu unadhani napenda? Nimebaki Yatima hapa, wakanipiga na uchizi, nilipenda unadhani? Hata hivyo, Hussein ameniambia vitu vingi sana kuhusu ninyi watu na wewe ukiwemo, sasa navifuatilia. Nikijua ukweli tu, mtakuja kusaga meno na kila mmoja atalia zaidi ya leo" Rola alituchimba mkwara kisha huyo aliondoka zake.
Nilibaki na Rely pale sebureni hadi muda wa kuondoka kuelekea hospital ulipofika. Tulienda kuubeba mwili wa marehemu huku Rely akiwa ni mwenye maumivu makali sana moyoni mwake. Macho yake hayakuacha kudondosha machozi katika kila sekunde ambayo ilikuwa ikiyoyoma ama kwa hakikia 'msiba ukiwa wako lazima chozi likutoke' Rely alilia haswa.
Asubuhi baada ya msiba kufika pale nyumbani tulianza kufanya taratibu za mazishi lakini Rola hakuonesha ushirikiano. Muda wote akawa na simu ambayo alikwisha inunua.
"Kuna muda hadi najutia sekunde zangu za ushauri juu ya huyu binti" alinieleza Thelesia tukiwa tumesimama tukitazama wafiwa wengine ambao walikuwa wanaingizana pale nyumbani.
"Binafsi sikujua kama angekuja kuwa hivi hadi nashindwa la kusema"
"Karembo sawa ila sasa tabia zake hapana, watu wanabadilika lakini huyu amebadilika zaidi"
"Tuachane naye. Vipi umesikia lolote kuhusu kupatikana kwa Mama Rely?"
"Mh! Hapana ingawa Lukman alisema kwamba alionekana maeneo ya Kizimkazi lakini sina hakika maana ni taarifa ya juu juu tu" Thelesia alieleza huku akisema kile ambacho ameambiwa na Lukman.
Lukman alikuwa ni miongoni mwa wafanyakazi wa mle ndani ambao walijishuhulisha na umwagiliaji maua. Nikiwa naendelea na maongezi na Thelesia, alikuja Rola na kusimama kando yangu. Akamwamuru Thelesia kuondoka, alikuwa na maongezi binafsi ambayo alitaka tuzungumze. Nami nilimpa uwanja huo.
"Ngumu sana kuishi na mtu ambaye amenisaidia katika maoshi yangu sababu inanilazimu nisifanye vitu vibaya ili asichukie pale nitakapomkera"
"Sijaelewa"
"Namaanisha hivi, nimewaandalia mazingira ya kuishi huko Dar es salaam yaani wewe na Rely mtaishi huko. Hapa Zanzibar natakiwa kuishi na Hussein wangu" Rola alinitaarifu akiwa mkavu usoni.
"Sio uamuzi mbaya lakini kwanini tusiishi pamoja? Yaani mimi, wewe na Rely hapa kama familia?"
"Hussein hajataka ninyi muwe hapa na yule ni mume wangu, kipenzi cha moyo wangu. Mwanaume ambaye akisema 'we toka hapo' natoka haraka sana. Namskiliza na ndio ametaka ninyi mhame katika hii nyumba"
"Ok, mwambie Hussein kwamba, hakuna wa kutoka katika hii nyumba" Nilimwambia na kuweka msimamo wangu kama mwanaume kisha niliondoka na kuelekea eneo lingine ambako kulikuwa na watu wengine waliokuja katika msiba.
.