DO YOU LOVE ME 07 (S2)
CHEATING MESSAGE
Baada ya Rely kuwa amepoteza faham ilibdi wamchukue na kwenda kumpa huduma ya kwanza ambayo haikumchukua mda mrefu akawa ameamka lakin alikua na majeraha madogo sehem ya paji la uso.
Baada tu ya kuamka alianza kulia huku akilalamika kwanin Mungu kamchukua mama yake ingali yeye bado anamhitaji.
Hakukuwa na namna zaidi ya kuchukua mwili wa Mama Rely na kwenda kuupumzisha kwenye nyumba yake ya milele. Ulikuwa ni wakati mgumu kwa Rely kwani hakuwa wa kula wala kunywa. Aliona dunia nzima ni kama imemsaliti na kumuacha peke yake. Nilijitahidi sana kumtia moyo na kumfariji hatimaye alianza kuwa sawa japo nilichukua mda mrefu sana kumuweka sawa.
Rely aliweka chuki kubwa sana ndani ya moyo wake juu ya Mama yangu mzazi. Akiamini kwamba mama yangu ndio chanzo cha kifo cha mama yake. Suala hili likapelekea Rely kukataa kabisa kubaki pale nyumbani. Kwakuwa nilikua tayari nilishaongea na rafiki yangu kuhusu kunitafutia chumba cha kupanga, sikua na shida tena kwasababu chumba kilipatikana na kisha tukahamia huko na kuyaanza maisha mapya ambayo hayakua mazuri sanaa japo niliendelea kupambana kuhakikisha tunaishi.
Siku zikasogea huku nikiendelea kupambana zaidi kutafuta kazi ya kufanya, maana mjini bila kazi hakuna utakachofanikiwa sababu kila kitu kufanikiwa ni lazima pesa iwepo. Kwahiyo nililazimika kuingia mtaani kutafta kazi. Rely pia alianza kutafta kazi ambapo yeye alipata katika mgahawa mmoja ambao kwa namna yake ulikua na hadhi kidogo. Mimi niliendelea kutafta kazi bila mafanikio lakini sikukata tamaa na safari hii nikaona nifungue kibanda cha chips na kuanza kuuza chips pale mtaani.
Maisha yaliendelea kuchanja mbuga japo kwa tabu lakini ikawa ni bora kuliko kukaa tu kujibweteka bila kazi. Nashkuru Mungu kwa kipindi hiki kidogo tuliweza kupiga hatua kwa kiasi fulani kwani pesa aliyokua akipata Rely tulikua tunaunganisha na ile nnayopata Mimi kisha tunaweka mikakati ipi ambayo tutaifanya ili kujiinua zaidi ya pale tulipo.
Wakati Sisi tukiendelea na maisha yetu ya kawaidaa, upande wa pili ambapo alikuwepo Rola pamoja na mpenzi wake Hussein, mambo yalikua safi kabisa kwasababu wao hawakua na shida kama tulivyokua Mimi na Rely. Waliishi kama wafalme kwasababu kila kitu walikua nacho na kikubwa zaidi ata baadhi ya kampuni alizokua nazo Rola aliandika jina la Hussein kitu ambacho kilimfanya Hussein kufurahi zaidi.
Kitendo cha Hussein kupewa umiliki wa baadhi ya mali za Rola kilimfanya kuwa na kiburi sanaa kwasababu alianza kutumia pesa zile kwa maslahi yake binafsi. Mwanzo Rola aliona sio mbaya kwasababu ni mume wakd labda kuna vitu anafanya lakin ukweli haukua hivyo badala yake Hussein alikua akitumia pesa pamoja na wanawake wengine na cha kuumiza zaidi ni kwamba alikua na mwanamke wake ambae anampenda sana kuliko ata anavompendaa Rola na huyo mwanamke ndio ameitawala zaidi akili ya Hussein japo akiwa na Rola atapretend tuu. Kwahiyo hapa tunaweza kuona kwamba Hussein alikua kwa Rola sio kwa mapenzi bali ni kwa manufaa yake binafsi.
Japokuwa nilikuwa naishi na Rely kama mume na mke lakini utashangaa sana nikikwambia kwamba bado nilikua nampenda Rola na niliimani kwamba siku moja atarudi tu kuwa wangu. Hii hali sikutaka kumuonesha Rely ambaye najua kwa namna moja au nyingine ingeweza kumletea majeraha na kumsababishia shida. Lakini mawazo yangu kumbe yalikuwa ni tofauti na ya mwenzangu kwasababu wakati Mimi nawaza nisiomuoneshe kwamba bado nampenda Rola, yeye pia aliwaza kuniacha na kwenda kuishi maisha yake. Rely aliona hawezi kuishi na mtu ambae Mama yake mzazi hana utu, akasahau kwamba Mimi ndio niliyemuoa na sio Mama yangu.
Siku moja nilikua nimekaa nae seburen kwetu tukipanga namna ya kuongeza mtaji katika kibanda changu cha chips..
"Rely unajua nataka nitanue hii biashara yangu maana naona kama imekua sasa. Kwahiyo nataka nifungue kibanda mtaa wa pili apo lakini nitaweka mtu mwingine.."
"Ni sawa sio mbaya hata hivo najua pesa itabaki nyingine, ningeomba hiyo itakayobaki basi nifungue walau hata duka nianze kuuza.."
"Unamaanisha utaacha kazi kule mgahawani??" Niliuliza kwa shauku kwasababu sikutaka kusikia kwamba Rely anaacha kazi kule mgahawani ukiangalia ni sehemu ambayo anatusaidia sana.
"No, siwezi acha lakini nitaweka mtu piaa dukani.."
"Apo sawa.." Nilimjibu hivyo huku nikiwa naendelea kuhesabu pesa ambazo nilikua nazo mkononi.
Siku moja wakati nipo chumbani nikijiandaa kwa ajili ya kwenda kutafuta site ambayo itakua nzuri kwa kuweka kibanda changu cha chips. Simu ya Rely iliita sanaa lakini Rely hakuwemo chumbani nikaona wacha niipokee si ni sim ya mke wangu bana. Wakati nasogea kuipokea ikakata, basi nikaachana nayo lakin mda huo huo iliingia meseji kwenye simu yake iliyosomeka hivi... "Naomba kama hutojali leo uje hapa restaurant nina maongezi na wewe mpenzi wangu juu ya lile swala lako la kufungua duka.."
Niseme ukweli tu kwamba hii meseji ilinifanya nijiulize mara mbili mbili. Je Rely ananicheat au ni nini kinaendelea ambacho Mimi sikifaham...???
Japokua kweli nilikua nampenda ndugu yake lakin yeye hakupaswa kunifanyia hivi mim kwasababu mim ni mume wake, inamaana swala la kufungua duka kuna mwanaume mwingine anajua tena tofauti na mim..?? Nilichanganyikiwa.. ITAENDELEA
.