Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

MPANGAJI 02 ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ

23rd Jun, 2025 Views 16

MPANGAJI 02

๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ

Ilipita wiki moja na hali ikawa shwari kabisa kwa wapangaji wa mzee Mhina, siku hiyo usiku Sele alikua anarudi zake na kwa bahati mbaya siku hiyo alikua amechelewa kupita siku zote na hivyo ilibidi agonge geti na kusubiri kidogo, alikua amevaa begi lake kama kawaida na mkononi akiwa na mfuko wa chipsi na soda yake tayari kabisa kuingia ndani, mara nyingi alikua akichelewa alifunguliwa mlango na kaka Ephraim au mzee Ngoda,

siku hiyo ilikua tofauti sana kwani wakati geti linafunguliwa Aliona sura ngeni kabisa machoni pake ya msichana mrembo umri wa miaka 25-28 hivi, Sele alijikuta akishikwa na kigugumizi na akili yake ikasimama kidogo akiwa ameduwaa pale getini.

โ€œingia ndani kaka Sele!โ€ alisema Yule msichana nae akiduwaa

โ€œah ah, bila Shaka wewe ni Ester?โ€ alisema Sele sasa akiingia ndani

โ€œumejuaje?โ€ aliuliza Ester akimalizia kufunga geti.

โ€œah mama yake alisema utakuja wiki iliyopita kwahiyo nimeona wewe ndio mgeni tu hapa vipi mbona hujalala mpaka sasa hivi!โ€ aliuliza Sele akieleka mlangoni kwake.

โ€œah kuna tamthilia naangalia kwahiyo niliposikia unagonga nikaona nikufungulie na nikuone maana nasikia tu sele! Sele!โ€ alisema akitabasamu

โ€œohoo ushasikia umbeya tayari!โ€ alisema sele sasa akiingia chumbani kwake,
Sele aliingia ndani kwake huku mawazo yake yakiwa kwa Ester ni kweli alikua anakutana na wasichana wengi kila siku, na hata hapo walikuja wapangaji wengi tu wa kike na kuondoka lakini haijawahi kutokea msichana aliyeubamba moyo wake kama ilivyokuwa kwa Ester,

โ€œsiamini kama nimekamatika hivi!โ€ alijisemea Sele akifungua soda yake na kunywa,
Pamoja na kuwa ilikua ni mara ya kwanza wanaonana na binti Yule Sele alijiapiza kabisa Yule binti ameushika moyo wake.

Ester nae kwa upande wake aliona kitu cha tofauti kwa sele, kwanza zile hadithi alizokuwa amesikia kwa mama yake pamoja na wapangaji wengine kuhusu sele alitaka kuthibitisha kwa macho yake, na hivyo baada ya kusoma ratiba ya sele na kukosa kumuona mara kadhaa ndipo sasa siku hii akaamua kujitahidi kuwahi nafasi ya kufungua mlango ili amuone sele.

Haikua sababu ya mapenzi wala nini Ester alitaka tu kuona huyo Sele ni mtu wa namna gani, ni jini kweli? Au ni mtu wa namna gani! Na pengine akirudi kazini kwake Lindi basi angekuwa na kitu cha kusimulia walimu wenzake au pengine hata wanafunzi wake.

Ester alikua mwalimu wa sekondari ya kata ya kibaoni akifundisha Kiswahili na Historia, ni mwaka mmoja tu ulikua umepita toka aajiriwe katika shule hiyo baada ya kumaliza chuo cha aualimu huko Butimba Mwanza , kulikua na tetesi kuwa mama Mwajuma alikua amemficha mtoto wake huyo kwa mume wake baada ya yeye kuja Dar, na ndio maana hakuwahi kufika hapo nyumbani, na baada ya kukusumbuliwa sana na Ester mwenyewe ndipo sasa hakuwa na jinsi isipokuwa kumleta Ester amuone mama yake na baba yake wa Kambo,
Hivyo ester alitumia likizo ile ya pasaka kuja kumtembelea mama yake na ndipo sasa akasikia kuhusu Sele,
โ€œkwakweli huyo Sele ni kama jini mwanangu yaani hapa pengine anatusikia!โ€ ester alikumbuka maneno ya mama yake mchana huo na kisha akatabasamu tu akivuta shuka kulala katika chumba cha mwajuma,

Siku hiyo sele Alijikuta anachelewa makusudi kutoka ili tu amuone Ester ni kweli alimaliza kujiandandaa kabisa na kisha akawa anasikiliza huko nje kama atasikia sauti ya wanawake na ester akiwemo ndipo akatoka na begi lake na kuangaza huko na huko.

โ€œza asubuhi shemeji!โ€™ alikuwa aisha akimsalimia Sele

โ€œah poa tu vipi hajambo kaka!โ€ alisema sele akiangaza macho huko na huko na hatimaye akamuona Ester akitoka.

โ€œkaka Sele za asubuhi! Nataka leo twende huko mjini na mimi niangaze macho jamani, si unajua nimetokea kijijini jamani!โ€ alisema Ester huku akiongeza mwendo kuelekea kule Sele aliko.

โ€œdah Litakufa jitu leoโ€ aliwaza Sele.

โ€œooh twende basi nikutembezeโ€ alisema sele nae akiwa siriasi

Wapangaji wengine walitoka kuchungulia kwani hakuna aliyewahi kuongozana na Sele hata siku moja!

โ€œkweli mtu na mtuwe!โ€™ alisema mama Mwajuma akiwa ameshika mdomo

โ€˜mama baadae jamani natoka na kaka Sele!โ€ ester alisema kwa sauti..

โ€œsele unafanya nini ?โ€ alisikia sauti ikimwambia kwenye hisia zake.

โ€˜unafanya makosa Seleโ€™.

โ€œACHA UF..LA SELE wewe ni mwanaume!โ€ sauti nyingine ilimwambia.

Hakujali aliendelea kupiga hatua akiwa sambamba na Ester ambaye alikua na mkoba wake na simu yake ya Samsung galaxy.

โ€œmh kwahiyo tunaanzia wapi? Kazini kwako au mtaani kwanza?โ€ aliuliza ester!

โ€œwewe umesemaje kwani?โ€ Sele nae aliuliza

โ€œnilisema tukaangalie mjiโ€ alisema ester

โ€œBasi sasa leo nitakutembeza mpaka miguu iume!โ€ alisema Sele

โ€œkwahiyo kazini kwako hatufiki?โ€ aliuliza Ester

โ€œhapana mama, leo utembee uone mji kama ulivyotaka!โ€ alisema Sele kwa upole

โ€œkwahiyo kaka Sele nimesababisha wewe usiende kazini jamani!โ€ aliuliza Ester

โ€œmh mbona umekazania kazi! Kaz! Kwani umeambiwa nafanya kazi gani! Hahaha?โ€ Sele aliulizahuku akimtazama Ester.

โ€œhamna Bwana, si unajua tu mjini hapa kazi ni muhimu sana!โ€ alisema Ester.

โ€œbasi kama ulivyosema hapa ni mjini sio kila kazi lazima uendeโ€ alisema Sele na sasa walikaribia kufika Stendi
โ€œkariakoo, posta, kivukoni!โ€ ilikua sauti ya konda akinadi dala dala.

โ€œtwende zetuโ€ alisema Sele kisha wakaingia kwenye gari
Njiani walipiga hadithi za hapa na pale na Sele alijisikia vizuri sana na wakati mwingine alicheka hadi abiria wengine waligeuza shingo zao kuwatazama, kwa yoyote aliyewaona hakika alijua tu hawa ni wapenzi wapya ama wanandoa ambao wanakwenda kula fungate, kwani wakati mwingine Ester alimlalia mabegani sele,

Ester alimkumbuka mpenzi wake Ima, ambaye alianza nae mahusiano akiwa chuo cha ualimu , walikua na ndoto nyingi za kuishi pamoja bila kujua ima alikua na mpenzi wake mwingine aliyekuwa nae, siku ya mahafali yao Msichana huyo alikuja chuoni na kisha Ima Akamtambulisha mbele yake kuwa ni mchumba wake, ni bahati tu rafiki zake Ester waliwahi kumuweka โ€œchini ya ulinziโ€ vinginevyo siku ile ingekuwa ya mwisho kwa ester,
Na kutoka pale Ester alijiapiza hatakuja kupenda tena mwanaume katika maisha yake, na ndio maana walimu wenzake pamoja na maafisa elimu aliwatolea nje mchana kweupe na hakutaka mazoea na yeyote, sasa alipopata habari za Sele kidogo zilimstaajabisha hususani aliposikia hajawahi kutembelewa na mwanamke yoyote,

Ester alikuwa anakumbuka hayo yote sasa wakiwa karibu kabisa kufika kariakoo

Walifika na kushuka na kuanza kutembea huko na huko, na kununua vitu vidogo vidogo,

Baadae walifika kwenye mgahawa na kuagiza supu, walimaliza kisha wakaedelea na mizunguuko kutoka kariakoo hadi posta na kuendelea na mizunguuko mpaka kufika saa 7 mchana Ester alikuwa hoi taabani wenyewe wanasema aliomba poo.

โ€œhahaha hapa ujue nataka tuunge mpaka Temeke tushuke taifa tukaangalie mechi ya taifa starzโ€ alisema sele
โ€œno no no Sele nimechokaโ€ alisema Ester.

โ€œokay tumchukulie mama Mwajuma zawadi basi tugeuke ila mimi nitakuacha home siwezi kubaki nyumbani sasa hivi! Ujueโ€ alisema Sele

โ€œhaya bhana turudi tuuโ€ alisema Ester kisha wakarudi kituoni na kupanda dala dala,
โ€œkweli leo nimetembea mjini, ila Dar ni nzuri kwakweli!โ€™ alisema Ester huku akishushia na fanta yake
โ€œyeah mzee baba Kajitahidi kuweka mji vizuriโ€ alisema Sele

โ€œhivi una mishe gani Lindi!โ€™ aliuliza Sele

โ€œmimi ni mwalimu jamani Sele si nilikuambia!โ€ alisema Ester

โ€œ ah kweli asee nakumbuka, kwahiyo unakula likizo sio!โ€

โ€œyeah, wewe ndio umegoma kabisa kuniapeleka kazini kwako!โ€ alisema ester

โ€œhahaha si upo bhana tutaenda siku moja!โ€™ alisema Sele sasa akichukua mizigo na kushuka!..

.. ๐Ÿ itaendelea

FULL TSH 1000
NAMBA YA MALIPO NI 0657774735
JINA MKEGANI MPONDA MTANDAO NI TIGO.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

MPANGAJI 02 ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ๐Ÿ  >>> https://gonga94.com/semajambo/mpangaji-02
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 34

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA 33

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA_32

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA_31

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA _26 & 27

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA_25

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA_24

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA_23

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA_22

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA _20 & 21

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA_18 & 19

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA _16 & 17

majario rewards 100 Comments 0
 

SAKINA 14 & 15

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 13

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 12

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 11

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 10

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 9

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 8

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 07.

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 06.

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 05.

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 04.

majario rewards 100 Comments 0
 

TAMU YA SAKINA 03.

majario rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY 38

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY 34

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

TUWASHUKURU KINA BABA

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MARIA Sehemu 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MARIA Sehemu ya 10

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MARIA Sehemu ya 7

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA sehemu ya 37

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA sehemu ya 36

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest