VYOTE NDANI GONGA94
NISAMEHE MAMA SEHEMU YA: 18
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SONGA NAYO.....
Julius akatoka mbio mpaka kwenye gari Safari ikaanza kuja muhimbili.
Kwa upande wangu nilifikishwa muhimbili nikiwa sijitambui Wala sijielewi kabisa, na kwakuwa simu ilikuwa imeshapigwa kwaajili ya ujio wangu kila kitu kwaajili ya upasuaji kiliandaliwa na Moja kwa moja niliingizwa kwenye chumba Cha upasuaji na huduma ikaanza yaani ilikuwa haraka haraka maana Hali yangu ilikuwa mbaya sana, dokta Kim akiruhusiwa kuingia kwasababu sio dokta wa hospital hiyo hivyo alikaa nje ya chumba nilichokuwa nafanyiwa upasuaji alizunguka huku na huku, baada ya muda alifika Julius alichanganyikiwa Sana jinsi alivyokuwa akitembea na kuongea peke yake kwa watu wengi walizani ameanza kupatwa na uchizi Nyie ndugu Ni ndugu, mimi niliikosea Sana familia yangu lakini wananipenda mno.
Baada ya kuuliza alielekezwa nilipo alikuja mbio na kukutana na dokta Kim nje.
"Dokta afadhali nimekuona saada Yuko wapi....??"
" Tulia kwanza, kqa chini nakuomba "
"Saada Yuko wapi bwana "
Julius alipandisha sauti.
"Kaa chini Julius ulikuwa unaendesha gari lakini unavyoema Ni Kama ulikuwa ukikimbia vile hi Ni hatari kwa afya yako sawa kaa chini tuongee"
Julius akaona huyu ananiletea ujinga akaanza kufungua vyumba vilivyopo eneo lile na kuangalia, lakini kama dokta alivyosema Julius akuchukua muda akaanguka chini na kupoteza fahamu ,dokta kimu akajikuta akipata mgonjwa mwingine akiwa kwenye hospital ya watu, haraka akapelekwa wodini na kutundukiwa dripu la nguvu.
Baada ya masaa kadhaa dokta aliyekuwa akinihudumia na jopo lake walitoka kuashiria kuwa wamemaliza nje wakakutana na dokta kimu.
"Saada anaendeleaje..??"
"Nifuate ofisini"
Haraka wakaongozana Hadi ofisini kwaajili ya maongezi.
"Aaaah tunashukuru Mungu tumefanikisha yaani , ulituambia utumbo umejikunja tu, kiukweli ulijikunja na kuanza kukatika, ndio maana Hali yake ilikuwa mbaya kiasi hiki, tumuombee apone maana uwezekano ni mdogo sana, na wewe Ni dokta me uwa sipendi kukatisha tamaa familia ya mgonjwa nakuambia kwasababu wewe uhusiki nae huyu mgonjwa ana hali mbaya mno "
Dokta Kimu akaishia kushusha pumzi tu maana aliona Mambo Ni magumu Sana akifikilia muda huo Kaka angu Yuko kitandani akiamka atamwambia Nini ndo alichoka zaidi
" Mpaka Sasa natakiwa kuondoka hapa hospital nashindwa sijui kwanini moyo wangu umekuwa mgumu kuiacha hi familia yaani daaah Niko nje dokta "
Alizungumza dokta Kimu na kutoka nje akiwa anafuta machozi.
Usiku Sana Kaka Julius aliamka na kujishangaa akiwa na dripu la maji na yupo kitandani hakuwa hakikumbuka Nini kilitokea Zaidi alikuwa akiitaji jina langu.
Baada ya siku tatu ndio napata fahamu nikiwa ICU Nina mipira ya gesi na ya chakula lakini pia sikuweza kuinuka Wala kufanya chochote kwani sikupona vizuri na ndio kwanza nimeamka kwa Mara ya kwanza tangu nilipofanyiwa upasuaji.
Madaktari walikuja na kunitoa ile mipira na kuniamisha wodi na kunipeleka wodi ya kawaida hapo hata ndugu zangu walikuwa na uwezo was kuja kuniona na wa kwanza alikuwa bellah na Kaka Julius, nilitabasamu nilipomuona Bella yaani Bella alikuwa na sura ya Benny kabisa nilipomuangalia tu machozi yakaanza kunitoka, Bella mwanangu akanikumbatia
" Mama usiumwe Tena bwana Mimi hata shule siendi ukiumwa "
Nikacheka Kaka Julius alikuwa akiniangalia akanisogelea na kupiga magoti pembeni yangu
"Unajisikiaje??"
"Vizuri namshukuru Mungu kwakweli "
"Utakuwa sawa mpenzi sawa utakuwa sawa pacha sawa dada "
Nikatabasamu kutoka ana maneno mazuri niliyokuwa nikipewa na kaka yangu, nilikaa hospital takribani mwezi mzima, ndipo niliporuhusiwa, nilipofika nyumbani Moja kwa Moja chumbani kwangu wifi yangu akaja na kumuita bellah
" Precious anakusubili mkale sawa "
"Mimi nakula na mama "
"Jamani bellah nenda kale na dada p sawa anakusubili wewe "
Niliongea ili kumfanya bellah akubali lakini alikataa nikaomba Toby alete chakula ili niweze kula nae
"Mama huyu shangazi ananivutaga mashavu "
"Unasemaje.....??"
"Niliuliza kwa hasira Sana na nilijua Ni kweli kwanini amtaje yeye ajawai mtaja Toby na Mara nyingi Toby ndo uwa anakaa na bellah lakini sijawai kupokea malalamiko
"Kwanini anakuvuta mashavu "
"Anasema nakula Sana naleta hasara, halafu mama eti ukifa ndio aurudi Tena....??"
Aliuliza Bella nilistuka muda huo huo akaingia toby
"Bellah nilisemaje eeh usiwe unaongea hivyo "
"Kwani anaongeaga hivi ??"
"Ndio dada angu yaangu tangu uko hospital ananiuliza hivyo ukimuuliza anasema wifi yako ndo kasema wewe unakufa aurudi, nachanganyikiwa sijui kitu kinachoendelea "
"Aaaah toby huyu mtoto tu aelewi unajua wifi yangu amezoea kumwambiaga mama ake utakufa ukikataa chakula na dawa Sasa huyu amekalili "
Niliamua kupotezea tu ingawa nilishajua ukweli kuhusu wifi yangu.
Nilikaa sawa kabisa na kurudi dukani kwangu Kaka Julius alikuwa makini Sana na Mimi Chakula kwa wakati, nilianza clinic ya waathirika wa ukimwi na nilianza kutumia dawa zangu, ukiangalia na misosi ninayokula yaani nilikuwa nanenepa tu napendeza mtu akiniona lazima anitamani yaani lazima atamani niwe mke wake bila kujua kuwa naumwa.
Siku ya jumapili kama kawaida yangu sikufungua duka na siku hiyo familia nzima tulikuwa nyumbani, nikawa nimekaa chumbani naperuzi mitandaoni Mara wifi yangu akaingia
"Mmmmh yaani Kama kwako unachati tu wenzio wote tumekaa sebleni wewe Ni Nani ujikalishe uku peke yako ??"
"Wifi Sina mood nzuri kabisa kabisa ndio maana unaona nimekuja kukaa mwenyewe uku naomba uniache tu na utoke nje "
"Yaani unanifukuza kwenye nyumba yangu we una upungufu wa akili au??"
"Kwani shida ako Nini "
"Shida yangu unanibana kwenye nyumba yangu Sina uhuru beba kifaranga chako uchafu wako huu, na lile beberu lako ondokeni kwani mpaka mkae hapa "
"We unijui vizuri Tena ukiendelea kuhusu Bella nitakuoneesha show kamuulize kwanza mumeo kuhusu Mimi usikurupuke "
Nikainuka na kutoka nje akasonya na kunifuata nyuma na kujiongelesha kwa sauti
" Si hivyo umetoka nje kila mda ndani ndani tunakumisi bwana kila siku dukani asubuhi ukirudi usiku hatupati muda wa kuzungumza na kuinjoy pamoja"
Alizungumza wifi yangu Kaka akawa anacheka tu nilimkata jicho Hilo na kujisemea kimoyo moyo
"Wewe cheza ukouko kweye vumbi ukiingia Rami wewe utajuta kwanini ulikuja mjini"
Kwakuwa nilitaka kumjua vizuri wifi yangu na familia yake nilimuomba toby akakae dukani kwangu kwa wiki Moja tu.
Nikawa natoka asubuhi saa sita nimerudi , siku hiyo nilishaoanga liwalo na liwe lazima nimnyooshe huyu wifi yangu ili aniheshimu, nikawa namfata chumbani kwake nilipofika mlangoni Nika...............
ITAENDELEA..........
FORGIVE ME, MOM ππ
Umesoma kwa utulivu Β· dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi nisamehe-mama-sehemu-ya
