VYOTE NDANI GONGA94
NISAMEHE MAMA SEHEMU YA: 21
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SONGA NAYO.........
Kaka Julius akanisogelea Tena karibu zaidi akaniuliza
"Ni Nini hiki .....??"
"Utanipa nafasi nizungumze au utaendelea kunitunishia kifua, kwanza kwanini nitumie nguvu zangu kukuelezea ikiwa video tu ujaielewa maneno yangu utayaelewa "
Nikamsukuma kaka Julius na kumfuata wifi kwanza nilimchapa kibao kimoja Cha mwana ukome Kaka akataka kusogea karibu yangu lakini toby akamshika na kumkaba vilivyo
"Hivi unakumbuka nilikuuliza una uhakika huyu mtoto Ni wetu ??"
Nilikuwa nakuvumilia kwaajili ya precious tu, lakini nilipokuja kugundua hata precious pia sio damu yetu nikaona hauna faida kwetu, na unaongelea kuhusu Jana kukusukuma, wewe kwanini ulinivuta nywele?? Kwamba mimba yako ndo ilikutuma? Nimejisikia vibaya wewe kupoteza mtoto wako lakini hii skendo unayoonesha kwa Kaka yangu ndo inanifanya nioneshe mabaya yako, najua Julius ataumia Sana kujua ukweli lakini ndo ukweli huo "
Niliongea uku nalia nikawatumia video zote kila mtu akazidi kupigwa na butwaa yule mama akaona Mambo yashaharibika akataka kukimbia, lakini Toby alikuwa vizuri akamuachia Julius na kuwai kifunga mlango, kitendo Cha yule mama kutaka kukimbia kilimfanya Kaka Julius kunielewa lakini siku hiyo nilikuwa na maumivu makubwa nikaamua kuongea
"Kaka Julius ulikuwa uko sahihi kuwa sijabadilika maana leo naihatibu ndoa yako kwa ushahidi wenye kishondo kabisa, nakumbuka tulisema kuwa tusahau kila kitu lakini leo umenikumbusha kila kitu najuwa Mimi Ni mkosaji mno"
Kaka Julius hakutaka niendelee kuongea akaja karibu yangu na kusema
"Am sorry"
Kisha akanyoosha kwa Irene jamani alimpiga bao moja la kwenda bao la mama wa kambo, kila mtu alistuka, nilimzuia Kaka Julius kwasababu irene alikuwa bado mgonjwa yaani kwa kawaida tunasema yeye Ni mzazi tu atakama mtoto hayupo nilimtuliza Kaka angu akatulia
"Kabla sijafanya kitu kibaya irene beba mtoto wako uzuri ulikuwa umeshapaki kila kitu toka sitaki kukuona wewe na Hawa wenzio, Dickson changanya miguu mchukue mkeo na muondoke "
Aliongea Kaka kisha akaondoka juu akaja kutoka akiwa amembeba precious na bellah, nikaona Sasa Kaka kachanganyikiwa nikamchukua bellah kumuweka pembeni nilipotaka kumchukua precious wifi aliwai na kusema
"Tutakutana mahakamani"
Nikasema
"Una kichaa wewe eeeh "
Basi taratibu wakabeba mizigo yao na kuondoka precious alikuwa anajionea kila kitu sawa tu maana aelewi hili Wala lile
Niliingia ndani nililia Sana nilijua tu Kaka angu anapitia wakati mgumu, siku hiyo Julius alilewa Sana mpaka akaanza kukumbushia Mambo ya nyuma kabisa nikaogopa nikamuomba Toby aondoke na Bella watarudi nikiwaita, toby hakuwa mkaidi fasta wakachukua gari na kuondoka
"Hivi Mimi Nina mkosi gani kwenye mahusiano nilipokuwa na wewe ulikuwa unanilia pesa zangu tu , bado nikaja kujua wewe ni dada yangu, haya mwanamke mwingine manidhurumu kabisa mtoto wangu, niliyemuoa ndo kanisaliti mpaka kanisaliti Tena "
Alikuwa akiniuliza Kaka Julius niliona aibu eti kati ya watu ambao ametembea nao na Mimi nimo, nilitumia muda mwingi kumtuliza mwisho akalala, nikaomba mlinzi ampeleke chumbani kwake.
Asubuhi na mapema mtu wa kwanza kutuamsha alikuwa Ni mwanasheria wa kaka Julius alikuja akiwa na karatasi za taraka lakini pia mgawanyo wa Mali ambao utafanyika mahakamani
"Huyu mwanamke mpuuzi kweli Mali gani na kila kitu alikikuta hapa amekuja na Dera lake tu umu ndani alikuja Kama house girl kumpenda ndo imekuwa kosa "
Alilalamika kaka.
Siku iliyofuata kesi yetu ilikuwa inaanza saa 7 mchana basi mapema Sana tulikuwa tumeshafika pale mahakamani, taratibu zikafuatwa na kuonekana kuwa mali ni za kaka lakini pia kwakuwa wanataka kuachana inabidi wagawane kwaajili ya malezi ya mtoto ambaye Ni precious
"Lakini precious sio mwanangu muheshimiwa hakimu "
"Tutaaminije bila vipimo ??"
"Well Sasa hivi sayansi na teknologia imekuwa sana majibu ya DNA yanatoka baada ya nusu saa tu nahisi tupime hapa hapa "
Alizungumza Kaka lakini mama precious akadakia
"Nimeshapima na haya Ni majibu "
Basi majibu alipatiwa hakimu na muda na ilionekana kuwa precious ni mtoto wa Kaka Julius kwa asilimia 97 nikasema hapa Kuna kitu , kabla sijaomba nafasi ya kuzungumza Kaka akasema
" Sikuwepo wakati wanapima nafikili tupime hapa , mahakama kubwa Kama hi huwa na dokta wao , lakini pia naomba aje dokta ambaye mama precious alipima mwanzo ili tupate ukweli.
Na uzuri dokta alikuwepo kabla mambo hayajawa mengi dokta akatoka mbele na kuomba radhi kwa udanganyifu kwani alilipwa na Irene kuandika report ya uongo basi tukatoka pale tukiwa na ushindi wetu ingaww nilikuwa nikitamani Sana precious awe wetu na tupewe Haki ya kumlea. Nilipokuwa nataka kuingia kwenye gari irene aka.............
ITAENDELEA........
Kaka Julius akanisogelea Tena karibu zaidi akaniuliza
"Ni Nini hiki .....??"
"Utanipa nafasi nizungumze au utaendelea kunitunishia kifua, kwanza kwanini nitumie nguvu zangu kukuelezea ikiwa video tu ujaielewa maneno yangu utayaelewa "
Nikamsukuma kaka Julius na kumfuata wifi kwanza nilimchapa kibao kimoja Cha mwana ukome Kaka akataka kusogea karibu yangu lakini toby akamshika na kumkaba vilivyo
"Hivi unakumbuka nilikuuliza una uhakika huyu mtoto Ni wetu ??"
Nilikuwa nakuvumilia kwaajili ya precious tu, lakini nilipokuja kugundua hata precious pia sio damu yetu nikaona hauna faida kwetu, na unaongelea kuhusu Jana kukusukuma, wewe kwanini ulinivuta nywele?? Kwamba mimba yako ndo ilikutuma? Nimejisikia vibaya wewe kupoteza mtoto wako lakini hii skendo unayoonesha kwa Kaka yangu ndo inanifanya nioneshe mabaya yako, najua Julius ataumia Sana kujua ukweli lakini ndo ukweli huo "
Niliongea uku nalia nikawatumia video zote kila mtu akazidi kupigwa na butwaa yule mama akaona Mambo yashaharibika akataka kukimbia, lakini Toby alikuwa vizuri akamuachia Julius na kuwai kifunga mlango, kitendo Cha yule mama kutaka kukimbia kilimfanya Kaka Julius kunielewa lakini siku hiyo nilikuwa na maumivu makubwa nikaamua kuongea
"Kaka Julius ulikuwa uko sahihi kuwa sijabadilika maana leo naihatibu ndoa yako kwa ushahidi wenye kishondo kabisa, nakumbuka tulisema kuwa tusahau kila kitu lakini leo umenikumbusha kila kitu najuwa Mimi Ni mkosaji mno"
Kaka Julius hakutaka niendelee kuongea akaja karibu yangu na kusema
"Am sorry"
Kisha akanyoosha kwa Irene jamani alimpiga bao moja la kwenda bao la mama wa kambo, kila mtu alistuka, nilimzuia Kaka Julius kwasababu irene alikuwa bado mgonjwa yaani kwa kawaida tunasema yeye Ni mzazi tu atakama mtoto hayupo nilimtuliza Kaka angu akatulia
"Kabla sijafanya kitu kibaya irene beba mtoto wako uzuri ulikuwa umeshapaki kila kitu toka sitaki kukuona wewe na Hawa wenzio, Dickson changanya miguu mchukue mkeo na muondoke "
Aliongea Kaka kisha akaondoka juu akaja kutoka akiwa amembeba precious na bellah, nikaona Sasa Kaka kachanganyikiwa nikamchukua bellah kumuweka pembeni nilipotaka kumchukua precious wifi aliwai na kusema
"Tutakutana mahakamani"
Nikasema
"Una kichaa wewe eeeh "
Basi taratibu wakabeba mizigo yao na kuondoka precious alikuwa anajionea kila kitu sawa tu maana aelewi hili Wala lile
Niliingia ndani nililia Sana nilijua tu Kaka angu anapitia wakati mgumu, siku hiyo Julius alilewa Sana mpaka akaanza kukumbushia Mambo ya nyuma kabisa nikaogopa nikamuomba Toby aondoke na Bella watarudi nikiwaita, toby hakuwa mkaidi fasta wakachukua gari na kuondoka
"Hivi Mimi Nina mkosi gani kwenye mahusiano nilipokuwa na wewe ulikuwa unanilia pesa zangu tu , bado nikaja kujua wewe ni dada yangu, haya mwanamke mwingine manidhurumu kabisa mtoto wangu, niliyemuoa ndo kanisaliti mpaka kanisaliti Tena "
Alikuwa akiniuliza Kaka Julius niliona aibu eti kati ya watu ambao ametembea nao na Mimi nimo, nilitumia muda mwingi kumtuliza mwisho akalala, nikaomba mlinzi ampeleke chumbani kwake.
Asubuhi na mapema mtu wa kwanza kutuamsha alikuwa Ni mwanasheria wa kaka Julius alikuja akiwa na karatasi za taraka lakini pia mgawanyo wa Mali ambao utafanyika mahakamani
"Huyu mwanamke mpuuzi kweli Mali gani na kila kitu alikikuta hapa amekuja na Dera lake tu umu ndani alikuja Kama house girl kumpenda ndo imekuwa kosa "
Alilalamika kaka.
Siku iliyofuata kesi yetu ilikuwa inaanza saa 7 mchana basi mapema Sana tulikuwa tumeshafika pale mahakamani, taratibu zikafuatwa na kuonekana kuwa mali ni za kaka lakini pia kwakuwa wanataka kuachana inabidi wagawane kwaajili ya malezi ya mtoto ambaye Ni precious
"Lakini precious sio mwanangu muheshimiwa hakimu "
"Tutaaminije bila vipimo ??"
"Well Sasa hivi sayansi na teknologia imekuwa sana majibu ya DNA yanatoka baada ya nusu saa tu nahisi tupime hapa hapa "
Alizungumza Kaka lakini mama precious akadakia
"Nimeshapima na haya Ni majibu "
Basi majibu alipatiwa hakimu na muda na ilionekana kuwa precious ni mtoto wa Kaka Julius kwa asilimia 97 nikasema hapa Kuna kitu , kabla sijaomba nafasi ya kuzungumza Kaka akasema
" Sikuwepo wakati wanapima nafikili tupime hapa , mahakama kubwa Kama hi huwa na dokta wao , lakini pia naomba aje dokta ambaye mama precious alipima mwanzo ili tupate ukweli.
Na uzuri dokta alikuwepo kabla mambo hayajawa mengi dokta akatoka mbele na kuomba radhi kwa udanganyifu kwani alilipwa na Irene kuandika report ya uongo basi tukatoka pale tukiwa na ushindi wetu ingaww nilikuwa nikitamani Sana precious awe wetu na tupewe Haki ya kumlea. Nilipokuwa nataka kuingia kwenye gari irene aka.............
ITAENDELEA........
Umesoma kwa utulivu Β· dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi nisamehe-mama-sehemu-ya
