MWARABU HUKO MI SIJAZOEA 14
Tusameheane bize kupambana na life....
Bc nilivyopokea zile taarifa za kifo cha kaka Denis nikajikuta naishiwa nguvu na kulala hapo hapo , nilikuja kushtuka baadae sana nimechoka kichwa kizito, nikatafakari sana maisha yangu nikasema hapa nijikomboe tu mwenyewe maana sina yeyote wa kumkimbilia, nilikuwa na namba ya yule Dada jirani ya Kaka Denis, nikampiga lkn haikupatikana, nikajinyanyua zangu pale nikaingia bafuni kuoga, nimekaa zangu huku nina mawazo lukuki, Mahamood akanipigia cm akaniambia atakuja kulala, bc nilimuuliza niandae chakula gn?, akaniambia chakula atakuja nacho yeye, bc niliandaa chumba vzr nikapuliza udi, Mahamood aliniletea huo udi kutoka Dubai,, nikakaa zangu sebleni nimevaa kinguo cha kulalia namsubiri Mahamood,, kiukweli nilianza kumzoea na kumuona mtu wangu wa karibu,,,,
Mahamood alifika tukakumbatiana nilianza kumpenda na kumuona wa kawaida tu,, akaniambia Mamujee ngoja nikaoge kwanza nimechoka sana,, aliingia bafuni nikawa naandaa chakula ili tule,,, CM ya Mahamood ikawa inaita sn,, wala sikujihusisha nayo, alivyotoka mwenyewe ndio akaichukua, alikuwa mke wake mdogo wa Uingereza, wakaanza kuongea kiarabu wenyewe huku wanachanganya na kingereza,, yaan kama vile Mahamood alikuwa anajitetea flani iv,, waliongea mda mrefu sana,,, mm nipo kimya naangalia tv tu,, cm ilivyokata ndio akaanza kuniambia, huyu mke wangu wa pili mkorofi sana, yaan anataka kila wakati niwe nae tu? Ukiwa nae mbali hata miezi miwili tu anaanza kelele? Kila kitu anacho na yeye anasimamia kampuni yetu kubwa huko ila mkorofi tu, mwenzake mke mkubwa hana shida ata ukikaa miezi sita hujamuona wala hajali,,, nikasema mhhhh sasa hapa nitapaweza kweli mkurya mie bc nikazidi kuwa mpole,, tulikula chakula vzr huku tukipiga story tofauti tofauti,, akazidi kunisisitiza kuwa anataka kunioa na nimzalie watoto wawili tu,, bc tulilala na tukafanya mchezo ila kwa njia ya kawaida,, asbh tuliamka akajiandaa ili aende kazini kwake
Tulikaa na Mahamood pale hakwenda Hotelini tena alikuwa anakaa kwangu,, kweli nilimzoea nikimuona kama ndugu, rafiki, yaan nilimuona kila kitu,, safari yake ya kuondoka ilikaribia akaniambia hataki tena nifanye biashara zangu za kuzunguka zunguka, akaniahidi akirudi atakuja kunifungulia biashara,, bc aliniingizia hela ya kutosha kwenye akaunti yangu na kuondoka zake,, kiukweli nilikuwa na hela ya kutosha,, nikaanza maisha yangu huku nikimiss Mahamood,,,
Sikutaka kumsikiliza sanaa Mahamood nikaanza biashara zangu upya, yaan hela ya benki nilikuwa siitoi hata mia natumia hela za biashara zangu tu,, ilipita kama wiki bila ya mawasiliano na Mahamood, ila nikawa mvumilivu coz kama cm bc lzm anipigie yeye,,, niliendelea na mishe zangu huku nakaa mwenyewe nyumba kubwa ila nikazoea
Asbh moja nimeamka nikaanza kujisikia vbya kizunguzungu, hadi nashindwa kutoka kitandani,, nikahisi ni maleria maana sijaumwa mda mrefu,, nilivyopiga mswaki ndio nikatapika haswa yaan njano tupu, nikasema ngoja niende hospital, nikajiandaa kwenda hospital, nikachukua bajaji hadi hospital, ni hospital ya kulipia, nimefika hospital tu naanza kujiandikisha mapokezi nikashangaa mtu amenigusa bega,, kugeuka namuona shangazi huyu hapa nikamsalimia vzr, akaanza kuniambia vp unaumwa? Nikamwambia ndio,, bc akaniambia nenda kwa Dactari then nakusubiri palee,,, mhhhh nikasema sawa,, bc nikaingia zangu kwa doctor nikaandikiwa vipimo vzr, nikaingia kupima,, majibu yalivyotoka mhhhhh
Soma muendelezo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005.