MWARABU HUKO MI SIJAZOEA 39
"Mahamood" nilisema kwa mshangao huku nikijaribu kumsogelea anazidi kujibaranguza kule na huku, ghafla kelele zikaanza analia kwa nguvu
"Niache.....Ya Allaaaaaaah aaaaii" alikuwa anasema hivyo Mahamood nikaanza kuogopa na kuita kwa nguvu
"Happy" hilo ni jina la dada wa kazi ambaye alikuwa anaishi pale, kweli haikuchukua muda akatoka chumbani kwake akamshangaa "eh eh"
Ubaya mmoja alikuwa kama vile ana mapepo mwanaume yule, Happy akaniuliza "Amekuwaje tena?"
Nikasema huku nikilia "mi sijui, sijui ana mapepo?" Mara happy akaanza kumuombea shindwa, shindwa.....kwa muda mrefu mpaka pale Mahamood alipotulia na kuwa sawa kabisa
Nikamuuliza "mume wangu vipi umepatwa na nini?" Akatikisa kichwa na kusema "hapana ni kawaida"
Nikamuuliza kawaida vipi mbona sijawahi kukuona na hii hali? Niambie ukweli una tatizo gani? Akaniambia tukaongelee chumbani tukiwa peke yetu.
Mi nilianza kuogopa hata chumbani naendaje naye lakini sikuwa na kipigamizi ilinibidi niende naye chumbani tukakaa na kuongea akaniambia kwamba hiyo ni adhabu anayoipata baada ya kumpa mimba yule mwanamke ambaye alikuwa haruhusiwi kuzaa naye
Nikamuuliza mbona mimi nilipopataga mimba ya mapacha na mtoto wa pili haikuwa hivyo? Akasema eti nyota yangu mimi inang'aa ndiyo maana
Niliwaza sana, kwa hiyo anatumia nyota yangu ili mambo yaende? Lakini sikuweza kumuambia kabisa, nilimuuliza tu sasa utafanyeje? Akasema anajua jambo la kufanya
Tuliendelea kulala japo sikusinzia tena mpaka asubuhi, maisha yakaendelea Mahamood akaogopa kurudi tena Dubai kwa kuhisi mizimu itaenda kumtesa.
Biashara za Mahamood zilianza kuwa ngumu ghafla, kule kwenye biashara ya magari wateja wakawa hawaji tena, afya yake naye ikazidi kudorora, mara kwa mara ile hali ya kuzimia ikawa inamtokea na kuwa kama vile ana mapepo.
Siku moja akajifungia chumbani mwenyewe akawa anaomba dua ili mambo yake yakawa sawa, mimi nikiwa sebleni na watoto pamoja na Happy tulisikia kama kishindo ndani, halafu ghafla akaanza kupiga kelele kwa nguvu chumbani
Nikaenda haraka nikajaribu kufungua mlango umebanwa kwa ndani, nagonga lakini yeye anazidi kulalamika kama vile anapata maumivu makali sana
Fungua mahamood, fungua tafadhali, lakini wapi hakunifungulia ikabidi happy aje anisaidie tukavunja mlango na kuingia ndani, nilimkuta amelala hoi anatoka damu puani na mdomoni halafu amepoteza fahamu.
Nikawaza mambo mengi, mimi naye nikajikuta nalia sana, tukajitahidi kumbeba tukashindwa hivyo tukatoka nje na kuomba msaada na kumtoa nikampakiza gari na kumuwahisha hospitalini haraka sana.
Tulipofika hospitali alifanyiwa matibabu, saa 10 usiku alishtuka mimi bado sijalala namtazama tu aliponitazama nikashtuka na kumshika mashavuni "umeamka?"
Hakunijibu nikasema Mahamood unajisikiaje? Una tatizo gani niambie ukweli? Akasema mke wangu wanataka kunichukua, wanataka kunichukua alisema huku akitokwa na machozi
Kina nani hao? Nilimuuliza akaendelea tu kulia huku akisema wanataka kuniua mimi, kiukweli nilichanganyikiwa
Maliza kwa sh 1000
Wahi WhatsApp 0743433005.