MWARABU HUKO MI SIJAZOEA 34
Yale maneno ya mke mwenzangu yalinifanya nitafakari anayosema ni kweli au ameamua kugombanisha sababu kapewa taraka? Nikazidi kuchanganyikiwa mbona kama asemacho ni kweli mbona adui zangu wanazidi kuongezeka Mamujee mm? Nilibaki na bumbuwazi sijui nifanye nn? Nimuamini mke mdogo wa Mahamod? Au nimuamini Mahamod kwa kumleta mkewe nyumbani kwangu anisaidie kazi? Nilipooza nikawa mnyonge sana huku shangazi na mwanae sijui wanapanga nn juu yangu? Huku nako naambiwa haya?
Sikuongea chochote maana Roby alikuwa ananiangalia kama anataka kujua nimeongea na nani na nimeongea nn
Nikaanza kupata wasiwasi cjui ulitokea wapi ila nilipata hofu sana
Roby alikaa kwangu kama siku tatu iv akaniaga anaondoka nikamwambia sawa wasalimie sikumpa hata mia
Aliondoka zake nikabaki napambana na maisha yangu,, bi mkubwa sikumwambia chochote kuhusu ile cm ya mke mwenzetu nilikaa kimya
Maisha yakaendelea hatimae mimba ilifika miez tisa na ujifunguaji wangu ni Opp nikaandikiwa cku ya kufanyiwa opp bc nilikaa kujiandaa ila nipo nimechanganyikiwa nafikilia maneno ya bi mdogo bado yapo kichwani hata nijisaulishe vp ila hayatoki,,,, mume wangu ananipigia cm kunitia moyo maana presha ndio lilikuwa tatizo kwangu inapanda mara kwa mara nilitamani nipate mtu wa kumuhadisia yale maneno ila sikumpata nimwambie nani? Kaka yangu? Hapana sina uhakika nayo kama sio ya kweli huoni nitakuwa nimeweka doa kwa kaka yangu juu ya Mahamod?? Cjui nimwambie nani matatizo yangu sina Wazazi hata shangazi yangu simuamini yeye ndio yupo tayari kufurahia kifo changu
Nikapata wazo ngoja nimuhadisie Dada yangu wa kazi yeye nipo nae kwa mda mrefu ananifahamu vzr na anawafahamu vzr wakina Mahamod nilishaenda nae Dubai
Zilibaki kama wiki mbili ndio tarehe yangu ya Opp nilimuaga bi mkubwa kama nanyoosha miguu kidogo nafanya mazoezi, huwezi kufanya mazoezi kipindi hiki huoni unajitafutia matatizo Mamujee?? Bi mkubwa alikuwa ana wasiwasi na hali yangu, nikamwambia siendi mbali nanyoosha miguu tu pia sitakuwa peke yangu naenda na Dada, bc aliruhusu ila kishingo upande nikamwita Dada nikamwambia twende tukafanye mazoezi
Tukiwa njiani na Dada nikaanza kumsimulia yale maneno niliyoambiwa na bi mdogo, Dada akaniambia Dada Mamujee usikatae wala simuamini Mwanadamu yule unaemuamini ndio huyo ana kuhumiza? Aisee Dada wa kazi alinipa kauli ambayo ilinifanya niamini kuwa inawezekana bi mkubwa na mumewe hawana nia nzuri na mm na hivi Mahamod ni mganga na chumba chake cha Uganga haruhusiwi kuingia mtu yeyote zaidi ya Mahamod mwenyewe na bi mkubwa tu
Nikamuuliza Dada sasa mm nifanyaje? Akaniambia nenda kwenu kama ulivyoambiwa,, mhh kwetu wapi? Inamaana niende Musoma? Kwa nani yule Baba mdogo aliyeshirikiana na mkewe kunipiga hadi kunusurika kifo?? Nilijiuliza mwenyewe baada ya Dada yangu wa kazi kunambia niende kwetu,, nikawaza au niende tena kwa Kaka Arusha nikajifungue huko kama hawa mapacha?? Lkn kaka namwambia nn? Hata ivo kaka mwenyewe hata mke hana kila cku kunibadirishia wanawake tu mara waje wanipe makesi yao niwasuruhishe yaan ni shida tu
Bc nikasema liwalo na liwe nitakaa hapa hapa nione
Nilirudi nyumbani na Dada nikamkuta bi mkubwa ana wasiwasi kweli vp mbona mmechelewa nilijua umepata shida bado kidogo nikupigie cm kumbe cm hukubeba? Nikamwambia Dada ondoka shaka nipo sawa
Cku zilikimbia hatimae cku ya kujifungua ilifika nikapelekwa hospital nikalazwa ili kesho yake nifanyiwe opp nikiwa pale hospital nikaanza kuota mandoto ya ajabu ajabu mara nimejifungua mtoto kafa mara mtoto wangu kaibiwa
Usiku presha ikapanda sana nikapewa vidonge Dactar akaniambia Mamujee acha kupaniki relax, nikamwambia docta mbona najiona nipo sawa? Akaniambia presha ipo juu sana so jitahidi kutoa mawazo, bc asbh palikucha kabla sijaingia kwenye chumba cha Opp nimeingia kwenye vipimo mapigo ya mtoto hayaonekani nikawaisha kwenye operation presha bado ipo juu ikabidi nipewe vidonge kwanza operation isubiri presha ishuke, badala ya saa 4 asbh nimekuja kufanyiwa opp saa kumi jioni,,, nimekuja kupata fahamu nipo wodini kitu cha kwanza nikaomba mtoto nikaambiwa subiri upate nguvu nimekaa mtoto sipewi jmn mwisho nikaamua kuuliza mtoto wangu yuko wapi? Nimekuja kupewa jibu usiku kwamba mtoto wangu amefariki
OH My God njooni msome yote mpaka mwisho kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni