PART 10
JINSI UTULIVU ULIVYOPONYA NDOA YANGU
Pastor aliniambia hakikisha hauwapi adui zako kile wanachotaka au kutarajia. Akasema Mumeo anajua kabisa utakasirika, utauwasha Moto, utalia, sasa wewe fanya tofauti, badili gia angani. Tulia, relax kama hakuna kitu.
Sio siri sikuendelea kufungua zile picha nilitulia nikaachana nazo, japo moyo ulikuwa na maumivu sana ikabidi niingie kwenye maombi kumsihi Roho Mtakatifu anipe amani. Unajua unajiuliza hivi huyu mwanaume kweli Mume wa Ndoa anakuacha anaenda nje na anatumika haswaa, kuna muda nilikuwa nasikia sauti inasema MPASUE KICHWA HUYU, AU NASIKIA VUNJA VIOO VYA GARI, lakini najizuia. Hasira ilikuwa kali sana sana. Nikamwambia Mungu nipe utulivu.
Nilianza maombi, Mume wangu sikumwambia chochote, nilikuwa kimya sana mule ndani, japo yeye alitarajia vurugu na akatarajia labda nitafanya kitu chochote ila sikufanya, japo ukimya wangu uliongezeka zaidi, nikawa kuongea tena siwezi. Anaenda kazini anarudi Mimi kimyaa.
Baada ya wiki nakumbuka kulikuwa na Birthday ya rafiki yangu tuko nae kwenye kikoba aliamua kufanya Party, nikasema hapa natoka na siagi mtu ntarudi usiku acha nikatoe stress. Siku hiyo Mr alitoka alienda kazini, jumamosi huwa saa kumi na mbili anarudi, Mimi saa kumi na moja nikatoka. Nilivaa kagauni keusi kafupi, kiatu changu kizuri cha juu na kapochi, nilikuwa simple but classic. Basi bwana Mr Akarudi akakuta watoto na Dada wa kazi akauliza Mama yuko wapi, wakasema hayupo katoka, na sikutoka na gari niliita Bolt sikutaka hekaheka, basi akauliza mbona katoka bila Gari wakamwambia hatujui ila katoka.
Na Simu niliweka silence sikutaka kelele, nilitaka nirelax nitafute amani yangu ya moyo. Nikawa busy na wenzangu tunakula tunacheza yani raha tupu.
Kumbe bwana huku Jamaa kapiga simu mara kumi, katuma mamessage kibao, Mke wa Mtu sahizi uko wapi, pokea simu tafadhali, nakwambia nikijua ulipo nikakufwata utanijua, pokea simu 😀😀 vitisho haswa.
Akampigia Dada yangu Dada akasema hata Mimi nampigia hapokei, akampigia Mama yangu, Mama nae akasema hata Mimi nampigia simpati sijui atakuwa wapi, akaanza kuhangaika. Akatoka nyumbani kunitafuta.
Akawapigia wazazi wake kawaomba waje nyumbani kuna matatizo, na akaita hadi wasimamizi wa harusi waje.
Sasa imefika saa nne nikawa nimeshawakumbuka wanangu, ndio nachukua simu niite bolt nakuta missed call kibao, na Yeye akaanza kupiga tena. Nikapokea Hallow uko wapi, nikamwambia niko sehemu fulani, akasema nisubiri hapo hapo nakuja, nisubiri hapo hapo, nikasema sawa. Yani alikuwa kama Mtu mwenye pressure hivi.
Basi nikatulia, nikamsubiri akaja. Alivyokuja nikatoka kwenye sherehe namfwata, nilikuwa nimependeza mnoo yani mnoo, aliponiona akashuka faster, akaanza ulikuwa wapi, nani kakutoa outing, nani huyo, akasema aisee nitakunyonga niambie ulikuwa wapi kwa hasira, Nikamwambia hapana nilikuwa kwenye Birthday ya rafiki yangu, twende ukaone, ikabidi nimpeleke kwenye birthday ndio kuingia akawaona wenzangu wengi akasalimia tukatoka. Ila tunatoka pale akaanza kwanini hujaniambia kama unatoka, kwanini hujaniaga, kwanini umeacha gari, nani kakuleta. Nikamwambia nilipanda Bolt gari haina mafuta. Basi tukaanza safari ya kurudi, mara naona katafuta hospital akapaki, nikamwambia hospital sahizi kweli, akasema ulisema tukapime naomba tukapime, nikamwambia sawa. Basi tukashuka, imagine hiyo ni saa tano, tukaingia hospital, tukamuona Doctor, tukamuomba atusaidie. Basi tukapima, tukawa tumekaa tunasubiri majibu. Hapo nimekaa simu zinaita Mama, Dada wananiambia unatafutwa, nikawaambia niko nae nilienda kwenye sherehe, wakasema sawa kama amekupata.
Basi tulipokea majibu, tuko sawa kiafya, tukaanza safari ya kurudi nyumbani. Njia nzima analalamika, kweli Mke wangu umevaa nguo fupi namna hii kweli, halafu hujaniaga kweli, Mimi nikanyamaza tu kimya. Tumefika nyumbani nikaingia bafuni kuoga, natoka namkuta yuko na simu yangu, anapekua message, Whatsapp yani kila mahali wala sikumsemesha nikaenda kulala. Baadae akaja kitandani akanifunua shuka, akaanza kwanini hukupokea simu zangu nakupigia masaa matatu hupokei, inaonekana ulikuwa na Mtu mahali ndio baadae ukienda kwenye party, kwanini usiage, niambie ukweli ulikuwa na nani. Kwanini unatoka unaacha watoto peke yao? Nyie ugomvi ukaanza huo usiku, akaniamsha niambie ulikuwa wapi, ulikuwa na nani? Akaanza hata kama nimekukosea sistahili hii adhabu, husemi kitu, hujibu chochote na wala hunijali, yani huonyeshi kuumia kwa chochote kuhusu Mimi, inaonyesha hunipendi tena na kuna Mtu unampenda. Wewe zamani ulikuwa hadi unanililia kweli Jane umekuwa hivi sasahv kweli?
Naomba niambie huyo mwanaume ni nani, anaekupa kiburi, naomba niambie nimfwate Mimi nimerudi kwenye familia yangu na siko tayari kuipoteza Ndoa yangu. Sitakubali nitakuua na Mimi nife, sema ukweli kabla sijakuumiza, Daaaah niliishiwa nguvu jamani.
Niwe mkweli sikuwa na jibu nikabaki nashangaa imekuwaje jamani, hivi kweli mambo yote aliyonifanyia Leo Mimi kwenda tu kwenye Birthday imekuwa kesi kweli. Akanikaba nakwambia niambie nani anakupa kiburi, mbona hujali kuhusu Mimi kabisaaa, ikabidi nianze kulia nilipiga kelele niuwe, niuwee kama uniamini basi niuwe, hivi kweli Mimi na akili zangu nichepuke ya nini? Labda kama wewe hunipendi, unataka sababu ya kuondoka tena. Alivyoona nalia sana akawa mpole, akaanza Basi Mama basi Mke wangu nisamehe, unajua nina wivu, lakini pia You have been acting so strange now days, umebadilika sana Mke wangu nisamehe basi nisamehe
Nikaanza kulia, nikakumbuka kila uchungu wacha nimwage machozi
ITAENDELEA.