Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........12
Whatsapp..............0613083801
ilipoishia sehemu iliyopita........
Alivyotokeza mbele ya umati karibu kila mtu alishangaa kuona tabasamu la mwanadada Angelina na utembeaji wake wa kitofauti uliwafanya wote ukumbini kukaa kimya......
ENDELEA NAYO.....
Tabasamu la mwanadada Angelina na utembeaji wake wa kitofauti uliwafanya watu wote ukumbini kukaa kimya.
Stewart alimtazama mwanadada Angelina na kujikuta akibaki mdomo wazi na kusahau kama amekaa na wazazi wake karibu,
"Wewe mtoto mbona mpaka unatuchaganya sisi tupo hapa kumshangilia Diana na sio hawa wengine?",Mama yake aliongea baada ya kumuona mwanae akimtazama Angelina, akili za stewart zilikuwa kwa Angelina aliyevutiwa na tabasamu lake na kile alichokuwa akikifanya kwenye jukwaa lile.
Siku hiyo Angelina alikuwa tofauti kwani alivutia isivyo kawaida na ata Albert nae alikili ndani ya moyo wake kuwa Angelina siku hiyo alikuwa yupo tofauti na alitembea kwa mwondoko uliomvutia karibu kila mtu aliyekuwa kwenye huo ukumbi na ata kuongea aliyapangilia maneno yake yaliyomfurahisha karibu kila mtu.
"Aya mshiriki mwingine huyo hapo mnamuonaje majaji", Mwanamama katalina aliamua kuwauliza ili watoe mawazo yao.
"Sina cha kusema kwa huyu zaidi ya kumpa alama za juu tu", moja ya jaji aliongea na hii kumfanya mwanamama katalina kutabasamu.
Angelina alimaliza zamu yake nakuondoka huku watu wakimpongeza zaidi ya walivyompongeza Diana kuonyesha kuwa amefanya vizuri zaidi.
Washiriki wengine walipita mpaka walipomaliza na sasa ulifata mzunguko wa pili napo walifanya ivyoivyo na watu waliofanya vizuri zaidi ni Diana pamoja na Angelina, mwanadada Mary yeye hakuwa na wasiwasi mana aliamini kwa ujanja alioufanya wa kumtisha Albert lazima ushindi uwe upande wake tu.
Baada ya mzunguko wa pili kuisha sasa walikuwa wanaenda mzunguko wa tatu ambao ni lala salama na kila mshiriki katika mzunguko huo alijitahidi kufanya vizuri zaidi kuliko mizunguko iliyopita.
Kama ilivyokuwa kwenye mzunguko wa kwanza na wa pili na ata watatu mwanadada Diana alifanya vizuri sana na pia ata mwanadada Angelina nae alifanya vizuri sana hali iliyoanza kuwaumiza majaji vichwa yupi anayefaa kuwa mshindi kati ya wale watu wawili.
Kila jaji aliandika marks kwa alivyoona yeye na ata upande wa mwanamama katalina nae pia akifanya ivyoivyo,
Mda ulifika wa washiriki wote kuitwa ili mshindi atangazwe, Mary alimtazama Faith na kumkonyeza kuwa ajiandae kwenda kuchukua taji la mshindi wa pili.
Miss Tanzania wa mwaka uliopita nae pia alikuwa kwenye shuhuli hiyo kwa ajili ya kumkabizi taji mshindi wa mwaka huo.
Mhusika aliyekuwa akitangaza washindi alisimama nakuanza kutaja majina ya washindi huku karibu kila mshiriki akiwa na hofu na wengine make up kuanza kufutika kwenye nyusi zao kutokana na kutokwa na jasho.
Majina yalianza kusomwa ya washiriki waliofanya vizuri na temu hii utaratibu ulikuwa ni kuanzia kusoma mshiriki aliyeshika nafasi ya kumi(10) mpaka nafasi ya kwanza (1),
Mshiriki aliyeshika nafasi ya kumi(10) alitajwa, badae akafata wa tisa mpaka wa tano(5),na kwenye majina yaliyotajwa jina la mwanadada Mary halikuwemo na hii kumfanya aamini kuwa yeye ndio mshindi sasa kilichokuwa kikisubiliwa ni kuanzia namba tano mpaka namba moja.
Mshiriki aliyeshika nafasi ya tano alisomwa na hakuwa mwingine bali alikuwa Faith na hii ilimfanya Mary kushituka baada ya kuona rafiki yake amekuwa wa tano badala ya kuwa mshindi wa pili baada ya yeye kuwa wa kwanza.
Mshiriki wa nne alisomwa na kujumuika na washiriki wenzake sita waliokuwa wametajwa na sasa walibaki washiriki watatu na hii ndio iliongeza hofu kwa wengine waliokuwa wamebaki mana kila mtu aliamini anafaa kuwa mshindi siku hiyo.
Mshiriki namba tatu alisomwa nakusogea mbele,
Mc wa kushuli aliongea kabra hajamtaka mshindi wa pili na mshindi wa kwanza....
"Huu mwaka umekuwa na ushindani wa kipekee mshindi wa kwanza kamzidi alama mbili tu mshindi wa pili,kwangu mimi kungekuwa na uwezekano basi ningebadilisha utaratibu na kuifanya tanzania iwe na Miss Tanzania wawili na sio mmoja tena kwani wote wanasifa za kuitwa Miss Tanzania...
Aliyeshika nafasi ya pili katika mashindano yetu haya ni....Diana...", jina la Diana lilitajwa kama mshindi wa pili na hii ilimfanya Diana masikio yake yasiamini kama ndoto zake zimeshindwa kutimia ila hakuwa na kingine zaidi ya kusogea sehemu husika.
Albert aliumia kuona ndoto za Diana zimeshindwa kutimia lakini kwa wakati huo akili zote zilikuwa kwa mama yake mzazi juu ya usalama wake,
Upande wa Stewart nae hakutalajia kama Diana atakuwa mshindi wa pili ila alipiga makofi kumpongeza kwa nafasi aliyoipata.
Ni mtu mmoja tu aliyekuwa amesalia ambae ni mshindi wa mashindano na kila mtu alikuwa na hamu ya kusikia ni nani aliyeibuka msindi na kuwa Miss Tanzania.
Kama ilivyokawaida Mshereheshaji alijiandaa kwa ajili ya kumtaja msindi wa mwaka huo husika,
"Na mshindi wa mashindano yetu ya mwaka huu..... na ndiye atakaye kuwa Miss Tanzania jina lake ni Angelina....",
Jina la Angelina lilisikika na kuwafanya watu wapige makofi kumpongeza mshindi wa shindano hilo.
Angelina alitokwa na machozi ya furaha baada ya kutangazwa kama mshindi na baadhi ya washiriki walisogea na kuanza kumkumbatia kama ishara ya kumpongeza, ni mtu mmoja tu kati ya wale washiriki ambae hakwenda kumpongeza Angelina ambae ni Diana aliyeumizwa sana na kuona Angelina ameshinda na kumfanya asitimize ndoto aliyokuwa akiitamani kwa mda mrefu.
Mwanamama katalina alisogea mpaka alipo Angelina na kumkumbatia kwa furaha bira kujali kama kulikuwa na wanahabari waliokuwa wakipiga picha na wengine kuchukia video kwa kile kilichokuwa kikiendelea.
Mda wa zawadi ulifika mshindi wa tatu alipatiwa milion 15 huku mshindi wa pili akipatiwa milion 30 na mshindi wa kwanza ambae ni Angelina akijishindia milion 60 pamoja na gari alilozawadiwa hapohapo nakupatiwa funguo zake.
Kiti cha heshima kililetwa na Angelina alienda kukaa kwenye kile kiti huku upande wake wa mkono wa kulia akisimama Diana kama mshindi wa pili na upande wake wa mkono wa kushoto akisimama mshindi wa tatu na mataji yaliletwa ya washindi wote watatu pamoja na kofia ya kimalikia kwa ajili ya mshindi, na jukumu alilopewa la kuwavalisha washindi hao ni Miss Tanzania wa mwaka uliopita aliyemvalisha Angelina na kumpongeza kwa ushindi pia aliwavalisha mataji mshindi wa pili na mshindi wa tatu.
Upande wa Mary baada ya kuona mshindi mwingine katangazwa tofauti na alivyotarajia yeye alikasilika hali iliyomfanya aondoke maeneo yale kwa hasira na Albert alikuwa akimtazama,
Albert alivyoona Mary kaondoka alimfata mama yake bira kujali kama bado yupo kwenye majukumu yake,
"Mama naomba unyenyuke tuondoke",Albert alivyofika alimwambia mama yake.
"Unakichaa siku hizi mwanangu huoni kama bado nipo kwenye shuhuli maalumu hapa"
"Mama hii ni lazima naomba tuondoke lasivyo nitakupoteza mama yangu naombe uelewe hiki ninachokwambia"
"Utanipoteza kivipi Albert", Mwanamama katalina alimuuliza mwanae...ITAENDELEA.
Nyie Miss Tanzania kaishapatikana lakini huko mbele kuna mambo huko subirini mtaona tu ????????????
NB: Story hii NIYAKUTUNGA na haina ukweli wowote ule unaoendana na taratibu za nchi yetu????????????????.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k???????????????????????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..