Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........17
Whatsapp..............0613083801
ilipoishia..........
"Fanya unachojua uende nyumbani mama yako hayupo salama", alianza kumwelezea jinsi alivyokuwa.
"Diana nakuja sasa ivi tu",Albert aliondoka upesi akimuacha Diana kwenye maswali mengi.........
ENDELEA NAYO......
Albert alifika nyumbani kwao na kweli alikuta get lipo wazi na mlinzi akiwa amelala chini aliingia mpaka ndani na kuanza kumuita mama yake lakini hakuambulia chochote zaidi ya ukimya kutawala katika nyumba yao,
"Huyo atakuwa Mary ndiye aliyefanya kitendo cha kumchukua mama yangu", alichukua simu yake na kumpiga Mary na mda huohuo Mary alipokea simu,
"Mr.Albert",Mary aliongea kwa mapozi.
"Mary naomba usimguse mama yangu nitakufanya kitu kibaya sana",Albert aliongea na kutoa vitisho kwa Mary, lakini mwenzake ndio kwanza alianza kumcheka na kuendelea kuongea,
"Umevunja makubaliano yetu Albert na mimi natekeleza kile nilichokwambia kosa lako ni moja tu la kushindwa kunifanya niwe Miss Tanzania", sauti ya Mary ilibadilika na hakuonyesha utani ata kidogo na ata Albert alilitambua hilo.
"Chochote kile nitakupa ila naomba usimguse mama yangu Mary mwache kama alivyo",Albert aliongea.
"Vizuri kijana mwelewa sana basi nisikilize kwa umakini kile nitacho kwambia na temu hii ukifanya kinyume na makubaliano yetu nakuahidi Albert utamkuta mama yako ameshakufa",
Mary aliongea na kumfanya Albert atege sikio lake vizuri kumsikiliza.
Mary aliendelea kuongea na kuna mpango aliokuwa nao,
"Nilipoteza pesa nyingi sana nilizotumia kama maandalizi kwenye mashindano ya Miss Tanzania, kwa kukuhurumia njoo na Tsh 100million mama yako nitamuachia na baada ya hapo nitaenda kuzitumia nikimaliza nitakuja kuchukua tena pesa zingine mpaka nitakapo tosheka", mwanadada Mary alimaliza kuongea akisubiri jibu kutoka kwa Albert.
"Mary mbona unanifanyia ivyo,kama shida ni pesa nitakuja nazo izo pesa ili umuachie mama yangu", Albert alijibu kumaanisha amekubali kwenda na zile pesa ili mwanamama katalina aweze kuachiwa.
Albert hakuwa na njia nyingine zaidi ya kwenda kutoa kiasi hicho cha pesa na alikitoa kwenye akaunti ya familia yao ili mama yake aweze kuachiwa.
Ndani ya gari la kifahari anaoenakana mwanadada Angelina akiwa na rafiki yake Manka aliyeamua kuacha kazi ya kwenye mgahawa na kazi aliyokuwa nayo kwa wakati huo nikutembea na Angelina karibu kila sehemu anayoenda na
safari yao iliwapeleka mpaka sehemu lilipo jengo la kampuni kubwa tu aliloingia nalo mkataba mwanadada Angelina,
"Angelina utaweza kweli kuigiza rafiki yangu?",Manka alimuuliza mwanadada Angelina.
"Sijui lakini nitajitahidi mpaka niweze japo haitakuwa kazi rahisi", Angelina aliona kazi ya kuigiza itamfaa na atazidi kujizolea umaarufu zaidi ndiyo mana aliingia mkataba na kampuni la uigizaji.
Kwenye kampuni hilohilo la uigizaji leo Stewart aliamua kuja ndani ya kampuni hilo na aliitaji kuonana na kiongozi kwa ajili ya mazungumzo japo ilikuwa ngumu kwake kupewa nafasi ya kuonana na kiongozi huyo ila siku zote pesa inaongea ndicho alichokifanya kijana Stewart, kiongozi alikuja kumsikiliza ni kipi kilichomfanya awe pale,
"Kipi ulichoniitia kijana na unashida gani na mimi?", manager wa kampuni hilo maarufu la uigizaji aliongea.
"Nina dili nahitaji tuweke makubaliano ya mimi na wewe",Stewart alikuwa na malengo yaliyomfanya aje kwenye kampuni ndiyo mana alihitaji kumuona manager.
"Makubaliano yapi hayo?"
"Nitakulipa kiasi cha pesa kitakacho kutosha ila nitafutie nafasi ya mimi kuwa karibu na Miss Tanzania nahitaji kuwa karibu nae, na ata ikiwezekana nipangie kipande cha uigizaji kitakacho tuweka karibu mimi na yeye", Stewart aliongea tena alionyesha kabisa anamaanisha kile alichokizungumza.
"Hahahahahahaha,unazani unaweza kunishawishi nikubali ilichokisema?, nisikilize kwa umakini mimi mwenyewe sina shida na pesa ninazo za kutosha tu ila nilimchukua Angelina kwa mipango yangu mwenyewe ujiulizi kwanini karibu Miss Tanzania wote sisi ndiyo tunakuwa wa kwanza kuwapa mikataba kwenye kampuni yetu?",Manager aliongea na kumfanya Stewart akili ndani ya moyo wake kuwa anakazi kubwa ya kufanya.
"Kiasi chochote kile kilicho ndani ya uwezo wangu nitatoa ila naomba unifanyie kile ninacho kwambia",Stewart aliongea kwa mara nyingine lakini hata hakujibiwa zaidi ya manager yule kunyenyuka nakuondoka.
Alivyoondoka tu manager yule alikuja kijana mmoja na kumsogelea Stewart akimwambia kwa sauti ya chini ili watu wengine wasiwasikie,
"Nisikilize huyu manager ameshajikatia tamaa ya kuishi hapo unapomuona ana magonjwa kama yote likiwemo na gonjwa la virusi vya UKIMWI ndiyo mana ata pesa zako amekataa, fanya unachoweza wewe umsaidie yule binti na amefanya kosa kuingia makubaliano na hili kampuni bira yeye kujua", kijana yule aliongea na kuondoka akimuacha Stewart njia panda akiwa hajui kitu gani afanye aweze kumsaidia Angelina ndiyo mambo mengine yafate aliamua kutoka ndani ya lile kampuni,
Huku upande wa nje Angelina na Manka walikuwa wakiwasili ndani ya kampuni hilo na walipotelemka tu kwenye gari Stewart aliweza kuwaona,
"Huu ndio mda mwafaka wa kumwambia huyu mrembo lasivyo atapotea kama nilivyoambiwa na yule jamaa", Stewart aliongea na kuamua kuwasogelea mpaka walipokuwa.
"Hapa sio sehemu salama kwako Angelina inakupasa uvunje mkataba wako na hili kampuni lasivyo utaingia matatizoni mda sio mrefu", Stewart alifika nakuongea pasipo ata kutoa salamu.
"Heeeh makubwa unamjua huyu?",Manka aliongea kama kawaida maneno kwake huwa hayaishi aliamua kumuuliza Stewart.
"Namjua na nipo hapa kwa ajili ya kukusaidia Angelina niamini mimi"
"Nikuamini mtu ambae ata sikujui wewe mtu wa ajabu sana, Manka twende ni mda wa kazi huu hatuwezi kupoteza mda kuongea na mtu asiyeeleweka hapa",Angelina aliamua kuondoka akiwa na Manka.
Lakini Stewart alihapa kufanya juu chini ili amsaidie Angelina alafu badae aeleze kile kilicho ndani ya moyo wake na wakati huo alishamsahau kabisa mwanamke anayeitwa Diana.
Upande wa Albert aliweza kufika sehemu aliyoelekezwa na Mary kwenye mkono wake akiwa na begi lenye pesa,simu ya mkononi iliita na kumfanya apokee,
"Simama hapohapo nimeshakuona hutakiwi kupiga hatua yoyote ile",ilikuwa ni sauti ya Mary iliyomwamulisha Albert.
Ndani ya mda huo alitokea Mary akiwa na vijana wake waliokuwa wamemshika mwanamama katalina.
"Mama!!", Albert aliita baada ya kumuona mama yake kafungwa kamba kama mtu aliyekamatwa kwa kosa la wizi.
"Tulia kijana mbona unataka kuwa kama mtoto,mama yako ni mzima nipatie pesa zangu na ole wake nikienda kuzihesabu nikute zimepungua utajuta kunifahamu Albert", Mary aliongea.
"Aya mwachieni huyo mwanamke".
Vijana walimwachia mwanamama katalina na Albert alimuwahi mama yake akienda kumshika na kumtazama kama kutakuwa na sehemu yoyote ile aliyodhulika
"Mwanangu hukutakiwa kutoa kiasi kikubwa cha pesa kiasi hicho",mwanamama aliongea mana milion 100 ni nyingi sana alizompatia Mary.
"Sio pesa hizi tu siku nyingine nitakuja tena kuchukua ngoja nikatumie kwanza hizi zikiisha nitarudi",Mary aliongea nakuondoka maeneo hayo akiwa na vijana wake.
Walipoondoka tu Albert alikunja mkono wake kwa hasira na kupiga ngumi chini na kufanya mkono wake utoke damu,
"Nini unachofanya Albert mwanangu ona mpaka umejiumiza", damu ni nzito kuliko maji mwanamama katalina alishika mkono wa mwanae nakufuta damu zilizokuwa zikimtoka kwa kutumia nguo yake aliyokuwa amevaa... ITAENDELEA
Mary kaahidi kurudi kwa mara nyingine akimaliza kutumia pesa walizompatia,karibu katika sehemu ijayo tuone kama atarudi tena.
NB: Story hii NIYAKUTUNGA na haina ukweli wowote ule unaoendana na taratibu za nchi yetu????????????????.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k???????????????????????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..