Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........02
Whatsapp.............0613083801
ilipoishia.........
"Unaakili wewe, unashindwaje kuwa makini mpaka unachafua watu?",aliongea kwa sauti ya juu iliyomfanya ata boss wa mgahawa ule asogee kuangalia tatizo Nini?.........
ENDELEA NAYO.....
Baada ya kupigwa Kofi na Diana,Angelina nae hakutaka kuwa mnyonge alimpiga kofi Diana lililomuangusha mpaka chini, Albert alisogea alipokuwa ameanguka Diana na kumnyenyua kisha akamtazama usoni alipopigwa na Angelina nakumwambia Diana,
"Diana,haina haja ya kuendelea kupigana na watu waliojaa shida naomba tuondoke eneo hili usije ukapoteza sifa yako bure na ukumbuke wewe upo kwenye kinyanganyilo cha kuwa Miss Tanzania, emu tuondoke", Albert alimchukua Diana na kuondoka nae lakini alimkata jicho Angelina lisilo la kawaida na alipomfikisha Diana kwenye gari alirudi alipokuwa Angelina na kumwambia,
"Kwa ulichokifanya utalipa nakwambia wewe mwanamke haiwezekani umchafue mwanamke wa ndoto zangu na bado umpige kofi", baada ya kuongea vile aliondoka na kumuacha Angelina akiwatazama tu huku na yeye akiwa na hasira na mwanadada Diana .
kipindi ugomvi huo unandelea boss wa mgahawa huo hakuongea chochote kile ila walipoondoka tu Albert na Diana alimugeukia Angelina,
"Angelina kila siku wewe niwakufanya makosa na leo kwa mara nyingine tena umerudia makosa yaleyale yani unampiga mteja?, your fired Angelina", boss aliongea.
"Lakini boss ni bahati mbaya nilijikwa na sikuthamilia kufanya kile kitendo lakini yeye akanipiga na mimi ikabidi nimrudishie", Angelina alijaribu kujitetea mbele ya boss wake huyo.
"Naomba nisikuone hapa kuanzia sasa ivi Angelina utanipotezea wateja,kuna watu wengi wanaohitaji hii kazi naona uzuri wako unakufanya mpaka usahau majukumu yako, sitaki kukuona kwenye huu mgahawa tena haijalishi utakuja kufanya nini hapa kuanzia leo", boss aliongea nakuondoka akimuacha Angelina asijue kitu cha kufanya.
Lakini mda huohuo rafiki yake alifika ambae ni Manka,
"Pole Angelina,ila nilijua tu boss lazima siku moja atatafuta sababu ya kukufukuza mana tangu ukatae kumpa anachokitaka amekuwa ni mwenye hasira sana na wewe, ata kama ni mimi mtu hawezi kunipiga kofi alafu nikamwangalia tu",Manka aliongea.
"Haina shida Manka ngoja kwanza niende nyumbani nikapumzike", Angelina aliongea kiunyoge na kumuaga rafiki yake kisha kuondoka.
Historia fupi ya Angelina.....
Angelina ni Binti anayeishi na mama yake na alibahatika kusoma mpaka elimu ya juu lakini kutoka na ufinyu wa ajira ilimlazimu atafute kazi ndogondogo za kuyafanya maisha yao yaende na yeye ndiye mtu aliyekuwa akitegemewa na mama yake kwa wakati huo.
Tuendelee na stori yetu.....
Upande wa Albert pamoja na Diana wakiwa ndani ya gari Diana alionekana ni mtu mwenye hasira kwa kile kilichotokea hali iliyomfanya Albert awe na kazi ya kumtuliza,
"Nilitaka leo niende kujisajili moja kwa moja yule mjinga kavuluga ratiba yangu na mbaya zaidi kanipiga mbele za watu"
"Pole sana Diana kwa kilichotokea, ata kesho sio mbaya Diana yakupaswa utulize hasira zako, ninachojua mimi ni kuwa Miss Tanzania huwa hana hasira ivyo tabasamu halitakiwi kupotea kwenye uso wako", baada ya Albert kutamka Neno Miss Tanzania lilimfanya Diana atabasamu.
Moja ya ndoto aliyokuwa nayo Diana ni kuwa Miss Tanzania na sio kwa sababu ya pesa anayopewa mshindi bali atambulike kama mrembo wa taifa na jina lake liwe kwenye record ya washindi.
"Albert naomba unipeleke nyumbani najua baba yangu atakuwa ananisubiri Sasa ivi", Diana alisema na Albert hakujibu kitu zaidi ya kuendesha gari na kumpeleka mwanadada huyo nyumbani kwao.
Nje ya nyumba ya kafahari iliyooneka mbele ya macho yao na Albert anasimamisha gari na kupiga honi mbele ya get la nyumba hiyo na haikuchukua mda mlinzi alikuja kufungua get na gari ikaingia ndani,
Baada ya gari kuingia ndani tu anaonekana mbaba anayetoka ndani ya nyumba hiyo nakushuhudia ugeni wa siku hiyo katika nyumba yake,
"Dady I miss you",Diana alitelemka na kwenda kumkubatia baba yake mzazi ambaye nae alipokea kumbatio la binti yake huyo.
Wakiwa Bado wamekumbatia kati ya baba na binti yake Albert nae alitoka kwenye gari na kunza kutoa mabegi ya Diana ila baba Diana alimuona na kuamua kumfata,
"Mara ngapi kijana nimekuambia ukae mbali na binti yangu ila hutaki kunielewa, mama yako hajakwambia kwamba unatakiwa uwe mbali na binti yangu?", baba wa Diana anayefahamika kwa jina la Mr.James aliongea.
"Hapana sio ivyo mzee nilikutana na Diana airport ikabidi nimlete mpaka nyumbani hapa", Albert alijaribu kujitetea mbele ya Mr.James.
Diana mazungumzo yale alikuwa anayasikia akaamua kusogea mahali pale,
"Dady nini unafanya lakini?, Albert kanisaidia kunileta mpaka hapa nyumbani yani toka nimeenda masomoni na kukaa huko miaka mitatu nikajua hautakuwa na hasira na Albert ila mpaka leo bado unamchukia, nini kakukosea mpaka uwe na chuki nae?",Diana aliongea na hakupendezwa na kile baba yake alichozungumza mbele ya Albert.
"Naomba uingie ndani nitadili na wewe badae, aya wewe kijana washa kigari chako utoke nyumbani kwangu haraka sana", Mzee james aliongea akiwa hana utani ata kidogo.
Albert aliingia kwenye gari na kuondoka huku akiwa na maswali mengi kwa nini Mr.James anamchukia na ata upande wa mama yake mzazi nae anamchukia Diana.
Baada ya Albert kuondoka Diana alimtazama baba yake na hakufurahishwa na kile alichokifanya.
"Baba haiwezekani uzikatishe ndoto zangu za miaka na miaka na endapo ikitokea nikakosa kitu ninachokitaka cha kuwa Miss Tanzania nitakuchukia maisha yangu yote",, Diana aliongea nakuingia ndani akiwa na hasira na kumuacha baba yake akimtazama tu.
"Nisamehe binti yangu hujui ni kipi kilichotokea kati yangu mimi na katalina ndiyo mana sitaki kukuona ukiwa karibu na mtoto wake bora uwe na kijana mwingine ila sio Albert", Mr. James aliongea baada ya Diana kuingia ndani.
Turudi kwenye kampuni ya FNF wanadada walikuwa wakiendelea na usajili huku baadhi wakipatiwa utaratibu na Mwanamama katalina, na moja ya wadada waliokuwepo pale ni mwanadada anayefahamika kwa jina la Faith aliyekuwa akiongea na moja ya mwanadada mwenzake alikuwa pale,
"Sikutegemea kama mashindano ya mwaka huu yatakuwa na watu wengi kiasi hiki na kila mtu ukimuangalia anasifa zote za kuwa Miss Tanzania"
"Don't afraid Faith, you need to believe (usiogope Faith unapaswa ujiamini),"
"Mary kuongea ni vyepesi ila sio rahisi kama unavyofikilia kila mtu anataka kushinda hapa na ushindani utakuwa mkubwa mimi naona bora turudi tu tukaendelee na mambo yetu mengine, naona kabisa hapa hatuna chetu",Faith aliongea na kumfanya Mary akasilike.
"Ivi una matatizo gani, kisa umeona visula vya hao mabinti tayali umeshaanza kuogopa ndio mana huwa sipendi kukuweka kwenye mipango yangu na hapa tayali Kuna mpango nilikuwa nimeshaupata kwenye kichwa changu ila sikushirikishi ng'o"Mary aliongea na alichukizwa na kitendo cha Faith kuanza kukata tamaa mapema akimuimiza waache kushiriki.
"Niambie basi rafiki yangu mpango Gani huo ulionao, Mimi na wewe tumetoka mbali nakukubali kwenye mipango Mary",Faith aliona ajirudi mbele ya rafiki yake huyo.
"Tega sikio lako nikuambie vizuri",Mary alimwambia Faith.
"Sasa sikia wewe siunaona msimamizi wetu anakijana handsome, yule ndio mpango mzima inatakiwa nifanye juu chini niwe nae ili mambo yaende vizuri, hapa nikufunga goal la mkono tu bira ivyo sitaupata uMiss Tanzania na wewe utakuwa mshindi wa pili Mimi wa kwanza",Mary aliongea.
"Waoooooooh Mary unamipango",Faith alijisahau na kuongea kwa sauti ya juu.
"Hey discipline is very important (heshima kwenu ni kitu mhimu)", Mwanamama katalina alifika pale nakuongea na hii ni baada ya Faith kujisahau nakuongea kwa sauti ya juu iliyosikika Karibu kila pande ndani ya kampuni hilo la FNF na kusababisha Mwanamama katalina kufika pale.
Na pia aliwapa maelezo mengine warembo hao ni kipi wanachotakiwa kufanya na kisha baada ya hapo aliamua kundoka katika kampuni hilo na kwenda kupanda kwenye gari lake na moja kwa moja akielekea nyumbani kwake,
Upande wa Angelina baada ya kufukuzwa kazi mda huo alikuwa akielekea nyumbani kwao na mawazo mengi yakitawala kichwa chake hali iliyomfanya apoteze umakini na kusahau kama yupo barabarani, akiwa bado anatembea alishanga kusikia honi ya gari ikipigwa kwa sauti ya juu hali iliyomfanya ageuka kutazama ni wapi inapotokea, ila alipogeuka tu hakuwa na bahati kwani aligongwa na gari,
"Mamaaaaaaaa",ni sauti iliyotoka mdomoni mwa Angelina.
"Nimeua,nimeua mimi....",aliongea baada ya kuona kasababisha ajali.
Alishuka ndani ya gari lake na kumwagalia mtu aliyemgonga yupo katika hali gani, baadhi ya watu waliokuwa pale walisogea ili kuangalia tukio la ajali hiyo,
"Wewe mama unashangaa nini?, umegonga mtu alafu bado unamwangalia tu njooni tumebebe na kumbakiza kwenye gari lake ili apeleke hospital", moja ya kijana aliongea na watu wakasaidizana kumbeba Angelina na kumuweka kwenye gari la mhusika aliyefanya tukio lile.
"Wewe mama washa gari tuondoke mbona umezuba na wewe ndio mhusika",moja ya kijana aliyejitolea kupanda kwenye gari hilo kwa ajiri ya kuhakikisha Angelina anafikishwa hospital moja kwa moja aliongea baada ya kumuona mhusika akiwa bado anatetemeka na akishindwa ata kuendesha gari kutokana na woga.
Mtu akiyefanya tukio lile la kumgonga Angelina hakuwa mwingine bali ni Mwanamama Katalina ambaye mpaka mda huo alikuwa na wasiwasi wa hali ya juu kwa kilichotokea, aliamua kuwasha gari na kuelekea moja kwa moja hospital kwa ajili ya Angelina kupatiwa matibabu na ndani ya mda mfupi tu waliweza kuwasili na kumpeleka mgonjwa wao mahali husika, na baada ya taratibu zote kufanyika kilichokuwa kikisubiliwa na Mwanamama katalina ni majibu ya doctor tu.
Katalina alichukua simu yake na kumpigia mwanae Albert,
"griiiiiiiigriiiiiiigriiiiii!!!!",simu iliita upande wa Albert.
"Mama nae anataka nini huyu?, hajui mimi nimevulugwa hapa",Albert aliongea kwa kulalamika alipokuwa akiendesha gari na hii ni baada ya yeye kufukuzwa nyumbani kwao Diana ila ilimbidi aipokee simu ya mama yake,
"Hello mom"
"Albert nimeua mama yako..", katalina aliongea huku akilia.
"Unamaanisha nini mama?"
"Njoo katika hospital ya... utanikuta hapa",aliongea na kukata simu.
Albert bira kujali kama yupo barabarani na barabara sio yake peke yake aligeuza gari pasipo kutazama vizuri ili...ITAENDELEA.
Hali ya Angelina itakuwaje na vipi kuhusu mpango wa Mary wa kumpata Albert ili iwe vyepesi kwake kuupata uMiss Tanzania kama anavyoamini. karibu katika sehemu inayofyata.
NB: Story hii NIYAKUTUNGA na haina ukweli wowote ule unaoendana na taratibu za nchi yetu??.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k?????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba.
.