Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

MISS TANZANIA Mtunzi...................Zooper Sehemu..ya...........28

1st Jun, 2025 Views 41

Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........28
Whatsapp..............0613083801

ilipoishia.......
hasira zilimshika na kuwasha gari lake aliliondoa kwa kasi akiwafata wao walipo tena wakiwa hawana habari kama kuna gari nyuma yao inayokuja kwa kasi............

ENDELEA NAYO......
Gari ilikuwa ikija kwa kasi na bahati nzuri Doctor Tayler aliweza kusikia sauti ya gari hilo aligeuka nyuma na kuona gari ikiwafata haraka alimvuta Diana pembeni na yeye kusogea pembeni huku gari ikiwakosa kidogo tu kuwagonga.

Gari ilienda mpaka mbele na kusimama kisha alishuka mwanadada Naisha tena akiwa kwenye hasira isiyo ya kawaida nakuwafata,
"Huyu ndiyo mgonjwa uliyekuwa unaniambia Tayler?, nimewafatilia toka mda mrefu sana na dalili zote nimeziona kuwa nyinyi ni wapenzi",Naisha aliongea akiwa na hasira sana.
"Tayler,who is she?"Diana alimuuliza Doctor Tayler aliyekuwa kimya na kukoswa cha kumjibu.

Doctor Tayler alishindwa afanye maamuzi gani kwa kuwagonganisha warembo wale wawili na kila mmoja alikuwa na umhimu kwake.

Naisha aliamua kufanya maamuzi aliyoona ni sahihi kwa upande wake,
"Tayler inakubidi uchague kati ya mimi na huyu mwanamke nani unayempenda na unataka kuwa nae?",Naisha aliongea.

Ata Diana nae aliamua kukaa kimya aone Doctor Tayler atafanya maamuzi gani kwa kile alichokisema mwanadada Naisha,
Tayler alikaa kimya na hili likawa jibu tosha kwa wote kuwa hana uwezo wa kumchagua mmoja kati yao,Naisha aliamua kuondoka na kuwaacha wawili wale wakiwa wamesimama na ata hamu ya wao kuelekea sehemu waliyokuwa wakienda nayo iliisha kabisa huku Diana akiondoka kwa hasira na kurudi walipokuwa wakiishi, Doctor Tayler aliamua kumfata mwanadada Diana.

Walifika mpaka ndani huku Diana akiwa hataki kumsikiliza Doctor Tayler, na akiwa kama mwanaume aliamua kujitetea na hii ilimfanya Diana aweze kumpa nafasi ya kumsikiliza,
"Diana kumbuka ni mazingira gani tuliyokutana mimi na wewe niukweli usiopingika kuwa Naisha alikuwa mtu wangu zamani lakini sasa ivi wewe ndiyo upo katika moyo wangu",Doctor Tayler aliongea .

Diana pia alifikilia na kukubaliana na maneno ya mwanaume huyo na tofauti zao zikawa zimeisha huku maisha mengine yakiendelea kati ya Diana na Doctor Tayler.

Nchini Tanzania, ukaribu uliozidi kujengeka kati ya Albert na Angelina ulimfanya Albert ampende mwanadada huyo na sasa kilichokuwa kimebaki nikumweleza tu kile kilichokuwa ndani ya moyo wake na temu hii aliamua kumshirikisha Mwanamama katalina ili mambo yawe raisi kwa upande wake.

Angelina yeye alikuwa anaendelea na maisha yake kama ilivyokawaida lakini alishangaa kuona Albert amezidisha ukaribu kwake yani saa moja lilikuwa haliwezi kupita bira kutafutwa na Albert asipopiga simu atatuma ujumbe, kitu pekee ambacho hakuambiwa na mwanaume huyo ni neno nakupenda.

Taratibu siku zilizidi kusogea na Albert aliamua kuweka wazi hisia zake kwa mwanadada Angelina alimweleza ni jinsi gani anavyotamani kuwa na yeye kwenye maisha yake japo kwa Angelina ilikuwa ngumu kukubali kwa wakati huo lakini pia Mwanamama Katalina alienda kukaa na rafiki yake au Mwanamama Beatrice nakumuomba wawaunganishe watoto wao waweze kuoana, Beatrice aliona ni jambo la kheri na hakuwa na kipingamizi kwenye hilo alishauliana na mmewe Mr.Gerald na wote walikubaliana kumuozesha Angelina kwa Albert, kazi ilibaki kwenye kumshawishi Angelina aweze kukubali kuolewa na Albert.

Angelina alikuwa mgumu kukubali lakini mbele ya mama yake mzazi na Mwanamama katalina hakuwa na pingamizi lolote lile alikubali na bira kupoteza mda ndoa ilipangwa kati ya Angelina na Albert.

Manka alizipata tarifa zile za Angelina kuolewa na Albert, haraka alimpelekea Stewart tarifa zile ambae nae hakuamini kusikia mwanamke aliyekuwa akimpenda anaenda kuolewa na mwanaume mwingine alichukua simu yake na kumpigia Angelina aliyepokea huku akiwa na wasiwasi kidogo mana alijua ni jinsi gani Stewart alivyokuwa anajisikia kwa wakati hu baada ya kusikia yeye anaolewa,
"Angelina mbona umekubali kuolewa mapema sana na mimi uliniambia haupo tayali kuingia kwenye mahusiano kwa sasa, kwanini Angelina?",Stewart aliongea maneno ya kulalamika yaliyokuwa yakimfikia mwanadada Angelina kupitia simu.
"I'm sorry Stewart sikuwa na njia nyingine tofauti na hii naomba unisahau na umtafute mwanake mwingine atakaye kufaa mimi sifai kuwa mke wako nisamahe sana", Angelina aliongea nakukata simu huku upande wa pili Stewart akijihisi kuchanganyikiwa maumivu ya moyo yalikuwa ni makali isivyo kawaida alijaribu kumpigia  simu Angelina kwa mara nyingine ila simu iliita bira kupokelewa na badae ikawa haipatikani kabisa.

Tarehe ya ndoa ilipangwa na zilikuwa zimebaki siku chache tu waweze kufunga ndoa.

Nchini Canada Diana hakuwa na hamu ya kurudi Tanzania na ata Mr.James alivyokuwa akimhimiza alidai bado kwanza hali yake haijakaa sawa na akiwa sawa atarudi tu na yote ni kwa sababu ya mahusiano aliyokuwa nayo kwa wakati huo na Doctor Tayler.

Siku hii ilikuwa mbaya kwa mwanadada Diana kwani alitoka na kumuacha Doctor Tayler akiwa nyumbani lakini alivyorudi alishangaa kukutana na hali ya kitofoauti.
Kwanza alikuta nguo zote za Doctor Tayler hazipo na alipojaribu kuzunguka kumuangalia hakufanyikiwa kumuona, aliamua kurudi ndani na kukaa kwenye kochi akitafakari ni wapi Doctor Tayler atakuwa kaenda.

Alipotazama juu ya meza aliona barua iliyoandikwa na Doctor Tayler aliichukua na kuisoma barua ile iliyokuwa na maneno ya kuumiza,
"Nisamehe Diana kwa kukupotezea mda wako nikweli nakupenda lakini Naisha niwa mhimu zaidi kwangu pia siwezi kuwa mbali na Naisha Diana kwasababu nyumbani kwao wanamali nyingi na za kutosha,I'm sorry" ni barua iliyokuwa na maneno machache ila yenye kueleweka yaliyomfanya Diana alie kama mtoto mdogo kwa kuachwa na Doctor Tayler.

Mawazo yalitawala kichwa cha Diana tangu alipoondoka Doctor Tayler hali iliyomfanya apatwe na ugonjwa uliowafanya madoctor washindwe kuelewa ni kipi kinachomsumbua mana kama kumpima walimpima ila hawakugundua chochote kilichokuwa kikimsumbua.

Diana hakutaka tena kubaki Canada alijiandaa kwa ajili ya kurejea Tanzania.

Nchini Tanzania siku iliyokuwa inasubiliwa kwa hamu ilifika watu mashuhuli walihuzulia katika harusi hiyo ya Albert na Mwanadada Angelina, na ilizungumzwa karibu nchi nzima, ukubwa aliokuwa nao mwanadada Angelina ambae bado alikuwa akishikilia taji la Miss Tanzania .
Ata Mary mwanamke aliyetaka kuifilisi familia ya Albert nae alikuwepo na sasa walikuwa ni marafiki wakubwa na Albert.

Maumivu yalikuwa kwa kijana Stewart ila hakuwa na njia nyingine zaidi ya kukubaliana na hali halisi japo yeye hakutaka kwenda kwenye ndoa hiyo mana ingekuwa ni zaidi ya maumivu kumuona mwanamke aliyekuwa akimpenda akiolewa tena mbele ya macho yake.

Ndoa ilifungwa kati ya Albert na Angelina na karibu kila mtu aliisifia ndoa hiyo ikipambwa na vyombo mbalimbali vya Tanzania.

Nchini Canada tunamwona mwanadada Diana akiwa airport na akijiandaa kwa ajili ya kurejea Tanzania......ITANDELEA 

Diana anarejea na tayali Albert ameshafunga ndoa na mdogo wake Angelina, majibu zaidi yapo sehemu ya 29.
   

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

ANIPHA 6--7.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 05

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

side chick episode 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

SIDE CHICK EPisode 2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY???15

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 18

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 17

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 8

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA Sehemu ya 32

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA? Sehemu 13.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY ???11

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

BOYCHILD PART 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 4.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 29

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

LOVE Part 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 28

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NAWASHWAA Sehemu nne.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NJERI part 26

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest