Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........18
Whatsapp..............0613083801
ilipoishia......
damu ni nzito kuliko maji mwanamama katalina alishika mkono wa mwanae nakufuta damu zilizokuwa zikimtoka kwa kutumia nguo yake aliyokuwa amevaa.....
ENDELEA NAYO....
Mwanamama Katalina aliamua kumchukua mwanae nakwenda nae nyumbani ila Albert alipanga kuja kufanya kitu kibaya kwa mwanadada Mary.
Ndani ya mda mfupi tu waliweza kufika nyumbani na Albert alikumbuka mazingira aliyomwa nayo mwanadada Diana,
"Mama ngoja niende kwa Diana kwanza nahitaji kuwa nae karibu kwa sasa",Albert alikuwa amependa kwelikweli ulikuwa humwambii kitu kwa mrembo Diana na upendo wake ulikuwa wa kitofauti kwa mwanadada huyo licha ya ulemavu aliokuwa nao Diana bado haikumufanya apunguze upendo wake kwa Diana.
"Mwanangu wewe umeshafikia umri wa kuoa sasa ivi ni vyema ukatafuta mwanamke mwingine wa kuwa nae ila nisingependa kukuona ukiwa Karibu na Diana naomba ufanye ivi kwa ajili yangu"Mwanamama katalina bado alishikilia msimamo wake wa kutokumpenda Diana.
"Mpaka pale utakapo niambia sababu ya wewe kumchukia Diana ndiyo nitaweza kuacha kumpenda huenda utakuwa na sababu yenye mashiko mama itakayonifanya nifate uamuzi wako",Albert aliongea.
Aliamua kutoka pale nyumbani na kuelekea kwa Diana pia alikuwa na uhakika kuwa Mary hawezi kurudi tena kumchukua mama yake mzazi kwa wakati huo.
Alifika mpaka kwa Mr.James nyumbani kwao Diana na kupaki gari yake nje alishuka na mlinzi akamfungulia kisha yeye kuingia ndani ya get la nyumba hiyo, ila kabra hajafungua mlango ili aingie ndani alisikia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea mle ndani na hii ilimfanya asite kidogo kuingia ndani.
"Baba ulisema Kuna sababu iliyokuwa inakufanya umchukie mama yake na Albert?", Diana akiwa amekaa na baba yake aliamua kumuuliza.
"Ndio ipo sababu na yeye ndiye aliyesababisha mimi niharibu maisha ya mtu mwingine asiye kuwa na hatia ndiyo mana nilitokea kumchukia",Mr.James aliongea.
"Sababu gani iyo baba naomba usinifiche na uniambie kile kitu?".
Mr.James alifikilia kama ndiyo mda sahihi wa yeye kumwambia binti yake ukweli wote ila hakuona sababu ya kuendelea kumficha tena kwani ata kama angeficha lazima kuna siku ukweli wote ungefahamika tu.
Mr.James alianza kumsimulia kila kitu Diana tangu walipokuwa na mahusiano kipindi cha ujanani na Katalina na kutengeneza ugomvi kutokana na kukosana kwao pia alimpa sababu iliyomfanya amchukie na awe na ugomvi nae mpaka leo,
"Binti yangu bira katalina kunifanyia vile na kutengeneza mazoea na mwanaume mwingine mimi nisingetembea na rafiki yake aliyekuwa akiitwa Beatrice nilifanya vile makusudi kama sehemu ya kumuumizi katalina ili na yeye ajue kuwa kuna uchungu wa kusalitiwa,
Tazama nilikatisha ndoto za mama yako mana nilivyotembea nae alipata mimba na hakuweza kuendelea na shule tena na nyumbani kwao alifukuzwa japo aliamua kukuleta wewe nyumbani na mimi nilichukua jukumu la kukulea wewe,
Asingekuwa katalina basi huenda wewe mwanangu ungekuwa Karibu na mama yako mzazi", Mr.James aliongea.
"Lakini baba mbona haina haja ya sisi watoto kutuingiza kwenye ugomvi wenu yani leo hii mimi nasumbuliwa na miguu na nahisi katalina alininyima kula ile siku ya mashindano na ndiyo iliyonifanya nikose nafasi ya kuwa Miss Tanzania na yote ni sababu ya ugomvi wenu,na mpaka leo hii sijui mama yangu alipo toka alipokuja kunikabithi kwako..
"Mimi na jua ni wapi mama yako alipo",alikuwa ni kijana Albert aliyesikiliza mazungumzo yao mwanzo mpaka mwisho na hii kumfanya aingie ndani na kuongea.
"Unamaana gani wewe kijana kusema unajua alipo?",Mr.James aliongea.
Albert ilibidi aanze kuwaelezea jinsi anavyojua yeye sababu mama yake alishawahi kumwambia juu rafiki yake wa enzi hizo ambae ni Beatrice mama mzazi wa Angelina, alimwambia Diana huenda atakuwa ana undugu na Angelina kitendo ambacho Diana alipinga kabisa kwani hakuamini kama atakuwa na undugu na mtu anayemchukia kiasi hicho na yeye aliamini bira Angelina asingekuwa kwenye ulemavu kwa kukoswa uMiss Tanzania na huenda ungekuwa upande wake.
Mr.James na Albert walikubaliana kwenda kwao Angelina ili Mr.James ajihakikishie kama ndiye Beatrice mwenyewe wa enzi hizo.
Ndani ya kampuni kubwa la uigizaji manager sasa alianza kutengeneza ukaribu na mwanadada Angelina na Manka aliliona hilo,
"Ndugu yangu huyu manager wako mbona simuelewi yani tangu uje hapa mda wote anataka kuwa Karibu na wewe au tayali mnamahusiano nini Angelina",Manka alimuuliza rafiki yake.
"Ni mambo ya kikazi tu wala hakuna kitu kingine, unafikilia kitu ambacho hakipo Manka"
"Big Don!!!,Big Don!!! huyooo", ni sauti zilizokuwa zikisikika kutoka nje katika kampuni hilo na ata Angelina na Manka nao waliweza kuzisikia.
Alikuwa ni yuleyuke msanii mkubwa maarufu leo pia aliamua aje katika kampuni hilo kubwa la uigizaji na kama ilivyo kawaida uwepo wake lazima usababishe watu kujazana upande wa nje.
Aliingia mpaka ndani katika kampuni hilo na watu waliokuwa wakimfata kwa nje wazuiliwe kuingia ndani, safari ya msanii huyo maarufu mwimba mziki ilimpeleka mpaka kwa manager mwenyewe wa hiyo kampuni,
"Ni mda mrefu sana ndugu yangu leo mbona umekuja bira kutoa tarifa?,na sio kawaida yako kabisa"manager aliongea.
"ilikuwa lazima nifike hapa umesahau kama wewe ndio una mmiliki Miss Tanzania na yupo kwenye kampuni yako hii",Big Don aliongea.
"Hahahahahahahaha, huu mwaka kweli na kazi usitake kuniambia na wewe unamtaka?"
"Ndiyo mana niko hapa Mr.... yule kwangu ni pesa nipe yule mtu nikuonyeshe namna ya kumtumia mimi nitengeneze nae pesa"
"Siwezi kukupa temu hii Big Don",manager aliongea tena akiwa amethamilia kabisa kupinga kile anachokitaka msanii huyo.
"Basi sawa",Big Don alijibu na mkono wake aliupeleka ulipo mfuko wa koti lake alilokuwa amevaa.
Big Don alichomoa simu yake na kufungua sehemu yenye picha Kisha kumuonyesha Manager huyo,
"Unaiona hii picha ya kwanza ni tarifa zako za wewe kuwa mwathilika na usijiulize nilizipataje, hii picha ya pili upo na huyu mdada tena mkiwa uchi kabisa, na hii ya tatu upo na mwanafunzi na unajua kabisa sheria zetu haziruhusu mtu kutembea na mwanafunzi", Big Don alimaliza kuongea.
"Nani kakupa izo picha"manager aliongea huku kijasho kikianza kumtoka.
"Sio mda wa kukwambia ni nani aliyenipa izi picha ila nasubiri kauli yako ya mwisho manager kabra sijafanya maamuzi unanipa Miss Tanzania au hunipi?"
Ulikuwa ni mtihani mgumu kwa manager ila hakuwa na kingine cha kufanya zaidi ya kukubali kumpa Miss Tanzania msanii huyu maarufu anayejulikana kama Big Don, na walipanga kufanya yale mabadilishano bira kumshirikisha mhusika mwenyewe ambaye ni Anjelina.
Albert na Mr.James waliamua kwenda mpaka kwa Mwanamama Beatrice ili Mr.James akajihakikishie kama ni mama yake na Diana, kwakuwa wote walikuwa hawapafamu walijaribu kuulizia mpaka walipofanyikiwa kupapata na hii ni kutokana na ukubwa wa jina alilonalo mwanadada Angelina kwa wakati huo.
Mwanamama Beatrice akiwa ametulia ndani akitazama runinga alisikia mtu akibisha hodi hali iliyomfanya anyenyuke na kwenda kufungua mlango,alikutana na sura ya kijana Albert japo ilikuwa ngeni machoni mwake lakini kwa pembeni yake alimuona Mr.James ila sura yake hakuikumbuka vizuri kutokana na miaka mingi kupita bira wao kuonana,
"Karibuni mpaka ndani,",Mwanamama Beatrice aliwakalibisha kiunyenyekevu ila sauti ile ilimfanya Mr.James aweze kuikumbuka vizuri licha ya miaka mingi kupita lakini sauti ya mwanamama Beatrice haikubadilika sana.
Mr.James aliingia ndani na kukaa na mda wote alikuwa akimtazama Mwanamama Beatrice hali iliyomfanya ata yeye aweze kushituka kwa jinsi alivyokuwa akiangaliwa na Mr.James.
Aliamua kuvunja ukimya Mwanamama Beatrice baada ya kuona wageni wake hawaongei kipi kilichowafanya wawe pale,
"Niwasaidie nini?",Mwanamama Beatrice aliongea.
"Beatrice", ni Neno lililotoka mdomoni mwa Mr.James na kumfanya Mwanamama Beatrice ashangae kidogo kwa jina lake kutamkwa.
"Ndio ni jina langu kwani wewe nani na umelijuaje jina langu?"
"Mimi ni James", Mr.James aliongea na Mwanamama Beatrice hakuhitaji maelezo mengine tena ya kuelezewa tayali alikuwa ameshamfahamu Mr.James na sasa alitaka kujua ni kipi kilichowaleta pale nyumbani.
Mr.James alimweleza Beatrice hali ya mwanae Diana ya ulemavu alionao na hii kumfanya Mwanamama aumie sana ndani ya moyo wake baada ya kupokea tarifa hizo na aliamua mda huohuo waongozane ili akamuone mtoto wake Diana.....ITAENDELEA.
Diana atachukua hatua gani akigundua mtu anayemchukia ni ndugu yake..?
NB: Story hii NIYAKUTUNGA na haina ukweli wowote ule unaoendana na taratibu za nchi yetu????.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k?????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..