Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........24
Whatsapp..............0613083801
Ilipoishia.........
Angelina hakuamini kusikia yale maneno kutoka kwa kijana Stewart na alipomtazama usoni macho ya stewart yalimaanisha kile alicho kizungumza kina ukweli, Angelina alifungua kichwa chake na kuongea......
ENDELEA NAYO......
"Stewart nashukuru sana kwa kunipa nafasi katika moyo wako nikupongeze kwa kushindwa kuficha hisia zako kiukweli nakupa hongera kwa hilo, lakini kwa sasa sipo tayali kuingia kwenye mahusiano ya aina yoyote ile na wala kuufungua moyo wangu kwa mwanaume yoyote yule ni ngumu kwa sasa, nivyema ukanisahau na kumtafuta mtu ambae atajali hisia zako na kukupenda kwa dhati", Angelina baada ya kuongea hayo maneno hakutaka kukaa tena pale mana angekuwa anaendelea kumuumiza kijana wa watu.
Angelina alienda mpaka lilipo gari lake na kupanda kisha kuondoka maeneo hayo akimuacha Stewart kwenye mawazo baada ya ombi lake kukataliwa na mwanadada Angelina.
"Diana nilimpenda sawa lakini wewe Angelina nimekupenda zaidi ata kama umenikataa lakini mimi siwezi kukata tamaa lazima nipambane na nitahakikisha unakuwa wangu",Stewart alikula kiapo cha kumpata mwanamke anayempenda ambae ni Angelina.
Stewart aliishia kutazama gari la mwanadada Angelina likitokomea.
Upande wa mwanamama katalina siku huo nyumba ilikuwa haikaliki palepale alikumbuka kumpigia mme wake aliye nchi za nje,alimtafuta na bahati nzuri alifanyikiwa kumpata,
"Albert amekamwatwa na polisi",ndio neno la kwanza aliloongea na hakukumbuka ata kutoa salamu kwa mme wake kwa wakati huo.
"Amekamatwa!!",Mmewe aliuliza kwa mshangao baada ya kupewa tarifa zile mpya.
Mwanamama katalina alianza kumsimuliza kila kitu mme ya kilichokuwa kikiendelea hasa kitendo cha Mary kuhitaji pesa kutoka kwenye familia yao,
"Nisikilizie kwa umakini katalina huyo binti hawezi kuicheza familia yangu kiasi hicho naomba usifanye kitu chochote atakachokwambia kufanya nakuja mda sio mrefu ni muonyeshe sasa kwamba pesa zinatafutwaje",mwanamama katalina kidogo alipunguza plesha na haichukuwa mda alikata simu baada ya kuongea na mme wake,
Lakini palepale simu nyingine iliita namba ikiwa ngeni iliyomlazimu kuipokea,
"Oooooh pole sana mama yake na Albert nazani sauti yangu umeshaifahamu tayali haina haja ya kuanza kujielezea kwako",ilikuwa ni sauti ya mwanadada Mary aliyeamua kumpigia Mwanamama Katalina ili apate kile anachokitaka.
"Shariti langu ni dogo tu kama unataka mwanao aachiwe huru na mimi niwaache muendelee na maisha yenu",mwanadada Mary alizidi kuongea kwa mapozi.
"Sharit gani unataka nifanye?"
"Nahitaji nusu ya mali zenu tugawane pasu kwa pasu hicho ndicho kitu ninachokihitaji",mwanadada Mary aliongea na kumtakia mwanamama katalina kufanya vile anavyotaka yeye.
Mwanamama katalina alikumbuka maneno aliyoambiwa na mme wake mda sio mrefu alikata simu bira kujali kama Mary mwenyewe ndiyo aliyepiga,
"Utanisamehe mwanangu Albert wewe ni mwanaume naomba uvumilie tu mda sio mrefu tutakuja kukutoa ila siwezi kukagawana mali na mtu kama Mary hata siku moja.
Upande wa mwanadada Mary baada ya kukatiwa simu na mwanamama katalina alichukia sana na alitamani ata Albert angekuwa mikononi mwake basi angempa ng'eo ila hakuwa na namna zaidi ya kukubaliana na hali halisi.
Asubuhi ya siku hiyo mke wa Mr.John alishangaa kuona mwanae Stewart amechelewa kuamka na haikuwa kawaida yake ilimbidi amuulize tatizo nini ila kijana hajutaka kumwambia mama yake kipi kinachomsumbua zaidi ya kumtoa hofu tu kuwa hana shida yoyote ile.
Kama ni kupenda temu hii Stewart alikili mwenyewe kuwa anampenda sana Angelina na aliapa ikitokea amempata basi ata mtunza mrembo huyo kama mboni za macho yake
Upande wa mwanadada Angelina aliletewa tarifa na Manka zilimfanya ashangae kile alichokisikia,
"Unauhakika na unachoongea Manka au umetunga maneno yako kama ilivyokawaida?"
"Angelina nauhakika na ninachokuambia Albert yupo kituo cha polisi amekamatwa na kesi tayali imeshafunguliwa japo sijui ni kitu gani kinachoendelea kwenye kesi aliyonayo Albert", Manka alimaliza kuongea ila mda huo Angelina alinyenyuka na kuondoka akielekea polisi moja kwa moja kwenda kujihakikishia na macho yake.
Angelina alifika na kuruhusiwa kuonana na kijana Albert japo aliangaika kupatiwa nafasi ya kuonana naye,
"Albert tatizo nini mpaka uko hapa ?",Angelina alimuuliza huku akimtazama kwa jicho la huruma mwanaume huyo.
"Ni wanadamu tu sio kila aliye jera ana makosa Angelina wengine wanafungwa kwa kusingiziwa"
"Nikweli usemalo lakini ningetamani kujua ni kipi kilichotokea na kukufanya uwe hapa".
Albert alianza kumwelezea Angelina kuanzia mwanzo mpaka mwisho na hakuacha kumwambia kuwa chanzo cha yeye kuwa hapo ni Mary kushindwa kwenye mashindano ya Miss Tanzania.
Angelina aliondoka maeneo hayo akiwa ana mengi kichwani alimuona Mary ni mwanamke wa ajabu sana na anayethamini pesa kuliko kitu chochote kile,
"Hapa lazima nitafute njie ya kumsaidia Albert aweze kuachiwa",Angelina alitafakari na aliamua kwenda kwao Albert ili ajue mwanamama Katalina amechukua maamuzi gani.
Na alipokuwa njiani mwanadada Angelina kidogo tu apate ajari na hii ni kutokana na kutokuwa makini ila mungu alikuwa upande, ndani ya dekika kadhaa tu aliweza kuwasili nyumbani kwa mwanamama katalina na kumkuta akiwa ni mwenye mawazo,
"Nimetoka kumuona Albert mida hii mama nini tufanye tuwezi kumsaidia?", Angelina aliogea na alikuwa ameshazoea kumuita mwanamama katalina mama.
Katalina alimweleza alivyoambiwa na mmewe au mzazi mwenzake na hii kidogo ikamfanya Angelina aweze kuwa na matumaini ya Albert kuachiwa huru kwani kwa upande wake alikuwa anamchukulia Albert kama shemeji yake kama alivyoambiwa na dada yake Diana amchunge mpaka atakapo rudi.
Nchini Canada mahusiano kati ya Diana na doctor Tayler yalikuwa kwa kiasi kikubwa sana na Diana hakutaka kuifanya iwe siri tena aliamua kutuma picha zao kwenye mitandao ya kijamii na alifanya ivi bira kumshirikisha doctor Tayler.
Akiwa ameka na akijaribu kunyoosha miguu yake kama moja ya mazoezi aliyoambiwa na doctor Tayler kufanya, alishangaa mpenzi wake amekuja tena akiwa na sura ya kitofauti kabisa,
"Tatizo nini kipenzi mbona unaonekana haupo sawa?", Diana alimuulizi huku akiendelea kumdadisi machoni doctor Tayler.
"Nakupenda sana Diana lakini kwa hichi ulichokifanya umenikera sana na najisikia vibaya sana kwenye hili, haiwezekani utume picha kwenye mitandao ya kijamii bira ruhusa yangu mimi Diana",Doctor Tayler aliongea.
Diana alishangaa na hakuona ubaya wowote ule wa yeye kutuma picha tena akiwa na mtu anayempenda kwa dhati lakini maneno aliyozungumza Doctor Tayler yalimfanya awe na maswali mengi kichwani.
"Diana naomba ufute picha zote ulizotuma mitandaoni tafadhali, nielewe kwa hilo kipenzi", Doctor Tayler aliamua apunguze hasira zake mbele ya mwanadada Diana.
"Unaweza ukanipa sababu ya kwanini hutaki nitume picha kwenye mitandao ya kijamii?",Diana aliuliza
"Kwa sababu mimi sio mtu wa kuamini mitandao, na ata ivyo nilishaweka ahadi na mama yangu kuwa sitakuwa mtu wa mtandaoni kamwe",Doctor Tayler aliamua kuongea maneno ambayo Diana alikubaliana nayo kishingo upande.
Wakiwa bado na maongezi Diana alishikwa na kichefuchefu cha gafra alichoshindwa kukizuia na kujikuta akitapika hapohapo mana hakuwa na uwezo wa kutembea vizuri,
"Tatizo nini Diana emu kaa hapa nikuangalia",akiwa kama doctor alimkalisha Diana ili amwangalie tatizo nini.
Doctor Tayler alishika mkono wake na kujaribu kuangalia kwa utaalamu anaojua yeye ndani ya mda mfupi tu aliweza kugundua kitu kilichomfanya ata yeye jasho lianze kumtoka huku akiwa na wasiwasi wa hali ya juu....ITAENDELEA.
Nini alichogundua doctor tayler karibu katika mwendelezo.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k?????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..