Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya............29
Whatsapp..............0613083801
ilipoishia....
Nchini Canada tunamwona mwanadada Diana akiwa airport na akijiandaa kwa ajili ya kurejea Tanzania.....
ENDELEA NAYO......
Diana alipanda ndege kwa ajili ya kulejea Tanzania na akiwa ndani ya ndege kitu cha kwanza alichokiwaza ni kuonana na Albert na alikumbuka jinsi mwanaume yule alivyokuwa akimjali tangu wanasoma wote na ata alivyokuwa na matatizo ya kiafya ndani ya nafisi yake alikili maneno aliyowahi kuambiwa na baba yake siku ile kuwa Albert ni mwanaume anayetakiwa awe naye yalikuwa ni maneno ya kweli wa asilimia mia.
Diana alipanga kwenda kuweka mambo sawa ili aweze kufunga ndoa na Albert mwanaume aliyetokea kumuonyesha upendo wa kipekee.
Diana pia alitafakari jinsi DoctorTayler alivyomkimbia na kumuachia barua yenye maandishi ndani yake.
Akiwa amekaa na anamawazo alishangaa akiguswa na mtu,
"Hey sorry,is this your phone?(samahani hii ni simu yako)",sauti ilimtoa kwenye mawazo mwanadada Diana baada ya kupewa simu yake aliyoidondosha na mama wa kizungu aliyekuwa amekaa pembeni yake,aliichukua na kuiweka mahali pake huku safari ikiendelea.
Nyumbani kwa Mwanamama Beatrice akiwa amekaa na Mr.Gerald mmewe alionekana ni mwingi wa nawazo,
"Nilizoea kukaa na binti yangu, sikutegemea kama itakuja kutokea awe mbali na mimi kiasi hichi lakini kwa wakati huu hayupo karibu na mimi na yupo kwa mwenza wake",Mwanamama Beatrice aliongea kwa huzuni mbele ya mme wake baada ya Angelina kuolewa.
"ilikuwa ni lazima tutengane na mtoto wetu ni mda wake wa kutengeneza familia mke wangu, kumbuka ata sisi tulipitia magumu mengi na yenye kuumiza",Mmewe aliongea na kumtoa hofu Mkewe.
"Ni kweli bira wewe kunipokea na kukubali kuishi na mimi huenda nisingekuwa hapa nilipo"
Gerald na Mwanamama Beatrice ni watu waliopitia changamoto nyingi kipindi Beatrice anafukuzwa kwao alipokuwa na mimba ya Diana, Gerald ndiye aliyempokea na kuamua kuishi nae japo mwanzo waliishi kama marafiki ila baada ya kumzaa Diana na kumpeleka kwa Mr.James ndipo mahusiano yao yalipoanza na kufanyikiwa kumzaa Angelina,na maisha yao yalikuwa ya kawaida ila baada ya Angelina kukua na kufanyikiwa kufika mpaka chuo kikuu hali ya maisha ilizidi kuwa mbaya iliyomsababisha Mr.Gerald aingie kwenye kazi za wizi ili tu mwanae aweze kusoma,
Angelina alipobakiza miezi miwili amalize chuo Mr.Gerald alikamatwa kwa kosa la wizi na kukaa gerezani karibu mwaka mmoja na sehemu, hayo ndiyo maisha waliyoyapitia wapenda nao hao.
Albert na Angelina walipatiwa zawadi ya nyumba na mwanamama katalina akisaidizana na mmewe kuinunua nyumba hiyo tena ikiwa ya bei ya juu.
Upande wa wanandoa siku hiyo ilikuwa ni siku ya kihistoria kwao kwani walifurahia fungate lao na kila mmoja alilizika na mwenzake.
Angelina alikuwa kajilaza kwenye kifua cha mmewe,
"Albert umebadilisha mipango yangu gafra lakini ni mabadiliko yenye baraka kwangu,sikutegemea kama nitafunga ndoa mapema kiasi hichi", Angelina alimwambia mmewe.
"Nilikuwa mjinga sana kipindi cha nyuma sababu nilikuwa nakuchukia pasipo kuwa na sababu yoyote ya kunifanya nikuchukie,hakika mungu niwaajabu mtu niliyekuwa nikikuchukia ndiyo umekuja kuwa mke wangu",
"Najua yote yalitokea kwa sababu ya mimi kugombana na dada yangu Diana na wewe kipindi hicho ulikuwa upande wa Diana, hivyo ilikuwa ni lazima uwe upande wake na unichukie."
Albert alijikuta pia akimuuliza Angelina kama ana tarifa zozote kuhusu Diana lakini naye alijibu hakuna chochote alichokuwa akikifahamu kuhusu Diana.
Waliendelea kuongea mpaka pale kila mtu usingizi ulipomchukua.
Asubuhi na mapema sauti ya simu ilimfanya Albert awe wa kwanza kuamka na alivyoangalia kioo cha simu yake mpigaji alikuwa ni Mary na kwa wakati huo walikuwa wameshakuwa marafiki aliipokea na kuiweka sikioni,
"Bado umelala rafiki yangu mpaka sasa ivi emu amka, kwani umesahau kama leo ulinipa ahadi ya mimi kuja kwenye kampuni yenu kwa ajili ya kunipa kazi?",Mary aliongea.
"Kila kitu nilishaweka sawa unatakiwa uende ukaanze kazi leo hii", Albert aliongea na kumfanya Mary akate simu.
Albert alinyenyuka kitandani na hakutaka kumsumbua mke wake aliyekuwa bado kalala.
Stewart kwa upande wake alikuwa ameshaanza kumsahau Angelina na sasa alikuwa na mazoea na Manka rafiki wa Angelina na urafiki wako ulizidi kuongezeka siku hadi siku, na ukijumlisha na ubize wa kazi aliokuwa nao aliyotafutiwa na baba yake au Mr.John pia ulichangia kumfanya asahau kabisa kama aliwahi kumpenda mwanamke aliyekuwa akiitwa Angelina, akili zake zote kwa wakati huo zilikuwa kwa mwanadada Manka aliyeanza kuvutiwa nae kutokana na ucheshi aliokuwa nao binti huyo.
Diana aliweza kuwasili salama Tanzania na kitu cha kwanza alichotaka kukifanya ni kuonana na Albert, aliamua kwenda nyumbani kwao Albert tena akiwa na mabegi kwenye tax aliyoikodi ili amwone mwanaume anayempenda,
Alifika na kukalibishwa na Mlinzi wa nyumba ya Mwanamama Katalina,Diana alipelekwa mda ndani japo alikuwa na hali ya woga kutokana na yeye kutokupendwa na Mwanamama Katalina.
Diana alimkuta Mwanamama Katalina akiwa na Mmewe na kutoa salamu kwao na temu hii Mwanamama Katalina alimkaribisha bira kinyongo chochote kile mana tayali alikuwa ameshaambiwa ukweli kama Diana ni mtoto wa Mwanamama Beatrice,
"Mama samahani naomba kuonana na Albert",Diana alimwambia Mwanamama katalina.
"Yupo kwake kwa sasa ngoja nikuelekeze ni vyema ukaenda kwake kuongea nae"
Mwanamama Katalina alimwelekeza ni wapi Albert anapokaa na Diana alishukuru sana na aliamua kwenda mda huohuo mpaka kwa Albert akiwa na mtu wa tax aliyoikodi.
Ndani ya mda mfupi tu aliweza kufika kwenye nyumbani aliyoelekezwa na Mwanamama Katalina na kuingia ndani huku akishangaa kumkuta mdogo wake Angelina maeneo yale,
"Diana ni wewe!!!",Angelina alienda kumkumbatia ndugu yake baada ya kupita mda mrefu bira wao kuonana,
"Ndiyo ni mimi Angelina,Albert yupo wapi nimeelekezwa na kuambiwa anaishi hapa?",Diana aliongea.
Mda huohuo Albert nae alitoka chumbani na kwenda mahali walipo wao baada ya kusikia sauti ya Diana,
Diana alivyomwona Albert alienda kumkumbatia na kutaka kumpiga kiss mwanaume huyo ila alishangaa kuona mwenzake anakwepesha mdomo,
"Albert ni mimi Diana wako nisamehe kwa kukuacha peke yako nimerudi tuishi wote na tutengeneze familia, najua sijawahi kukuonyesha upendo wowote ule ila tambua moyo wangu upo kwako",Diana aliongea.
"Umeshachelewa Diana,it's too late", Albert aliongea.
"Unamaanisha nini Albert?"
Albert hakutaka kumjibu bali alisogea mahali alipokuwa Angelina na kumshika mkono upande wa Angelina wakati huo alikuwa na aibu na kushindwa kumtazama Dada yake usoni.
Diana hakuhitaji uthibitisho tena kwani alipowatazama kwenye mikono yao wote walikuwa na pete hii ilionyesha ni wanandoa tayali,
"Diana huyu unayemuona hapa ni mke wangu na tayali tumeshafunga ndoa samahani sana kwa hili lililojitokeza",Albert aliongea na kumfanya Diana masikio yake yasiamini kile alichokisikia.
"Haiwezekani huu ni utani,Angelina huwezi kunifanyia ivi mimi,kwanini unapenda kuchukua furaha yangu uMiss Tanzania umesababisha niukose na leo tena umemchukua mwanaume aliyekuwa ananipenda,nakuchukia Angelina...",
Diana aliondoka kwa hasira na kwenda kupanda kwenye tax aliyokuja nayo, nakuondoka akielekea nyumbani kwao, hakuamini kama Albert amemuoa Angelina kwake aliona ni kama ndoto.
Diana alifika mpaka nyumbani na kumfanya Mr.James ashangae kwa ujio wa binti yake tena wa bira kutoa tarifa zozote zile....ITAENDELEA.
Karibu katika sehemu inayofata ya mkasa huu wa kusisimua..