Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........19
Whatsapp..............0613083801
Ilipoishia......
Mr.James alimweleza Beatrice hali ya mwanae Diana ya ulemavu alionao na hii kumfanya Mwanamama aumie sana ndani ya moyo wake baada ya kupokea tarifa hizo na aliamua mda huohuo waongozane ili akamuone mtoto wake Diana....
ENDELEA NAYO......
Mwanamama Beatrice aliamua kuongozana na Mr.James akiwa pamoja na kijana Albert na mda ambao walitoka tu mwanae Angelina aliweza kuwasili akiwa na rafiki yake Manka,
Ajabu alivyofika ndani hakumkuta mama yake ikabidi aende kumuuliza mlinzi aliyemwambia kila kitu juu ya mama yake kuondoka na watu waliokuwa wamekuja pale mda sio mrefu.
Mwanadada Angelina alirudi ndani alimomwacha rafiki yake Manka,
"Mama kaondoka na Kuna watu alioondoka nao"
"Angelina isije kuwa mama yupo matatizoni, kumbuka wewe ni mtu mkubwa sasa ivi watu wanajua unapesa kwakuwa ni mtu maarufu",Manka aliongea na kuzidi kumpa wasiwasi rafiki yake.
"Huo ni wasiwasi wako ngoja nimpigie simu",alichukua simu yake ili ampigie mama yake ajabu simu iliita humohumo ndani kumaanisha kuwa simu iliachwa na mama yake.
Maneno aliyoongea Manka kidogo yalianza kumpa wasiwasi mwanadada Angelina ya kutokumuona mama yake na pia kitendo cha kuacha simu yake mle ndani.
Upande wa Mary sasa alikuwa mtu tofauti baada ya kupata pesa kutoka kwa Albert aliamua kumtafuta Faith siku hiyo baada ya kutengana nae kwa mda na kila mtu kuendelea na mambo yake.
yalikuwa ni kama maajabu kwa Faith baada ya kupita mda kidogo bira kutafutwa na Mary lakini siku hiyo alimtafuta ilibidi apokee simu, Mary alimwambia waonane kwa ajili ya mazungumzo.
Faith alijiandaa haraka na kwenda mpaka sehemu aliyoelekezwa na Mary kwanza alikuta meza yote imejaa vyakula na pia kulikuwa na vivywaji vya kila aina maeneo yale napesa baadhi zimewekwa juu ya meza,
"Faith nilikwambia hapo kabra Mary is genius always, kunywa chochote unachotaka na kula chochote unachotaka tajiri niko hapa",Mary aliongea na tayali pombe zilikuwa zimeshaanza kumtawala mwanadada.
Faith hakutaka ata kuuliza kwa wakati huo alikaa na kuanza kufakamia vyakula vilivyokuwa pale, na baada ya kuanza kushiba ndipo alipofungua kinywa chake,
"Umetoa wapi pesa zote hizi Mary?",Faith alimuuliza.
"Hahahaahaha, hiki ni kisasi cha mimi kukoswa uMiss Tanzania na hii ni kama adhabu kwa yule mpuuzi ninayompatia", Mary aliongea kilevi.
"Mpuuzi unamaanisha Albert".
"Huyohuyo katoa million 100 hapa najiandaa kesho kutwa tu natinga kwake temu hii nataka nichukue kila kitu kutoka kwao", Mary aliongea aliongea kwa kujiamini tena bira wasiwasi wowote ule.
"Lakini hii ni hatari rafiki yangu unaweza kuingia kwenye hatari Mary",Faith aliongea kama kumpa ushauli rafiki yake huyo.
"Naona umeshalizika na maisha mpaka unaanza kunitisha, aya nyenyuka na uondoke",Mary alibadilika gafra na kumtaka Faith aondoke mahali pale.
Faith aliamua kujishusha mbele ya Mary na kuanza kumpamba Mary ili asiweze kutolewa mahali pale.
Faith hakutegemea kama rafiki yake amebadilika kisa hicho kisa kukoswa taji la uMiss Tanzania, kuna mda alimuhurumia mana aliitamani sana ile nafasi ila bahati haikuangukia kwa mwanadada huyo na iliangukia kwa Angelina.
Siku hiyo kama ni maisha Faith aliyafaidi mana pia alipatiwa pesa za kutosha kitendo kilichomfanya ata yeye aone kumbe kutajirika ni vyepesi kama ukiwa na akili za kukufanya utajiriki.
Mr.James aliweza kuwasili nyumbani kwake akiwa kaongozana na Mwanamama Beatrice na kijana Albert,na waliingia mpaka ndani na kumkuta Diana amekaa kwenye kiti chake anachotumia kutembelea.
Mwanamama Beatrice hakuamini kumuona binti yake akiwa kwenye hali ile alimsogelea na kuchuchumaa mbele yake huku Diana yeye akimuangalia tu akiwa haelewi kinachoendelea,
"Diana binti yangu unakumbuka mda sio mrefu tulikuwa tukimuongelea mama yako basi huyo unayemuona ni mama yako mzazi",Mr.James aliongea na kumfanya Diana aelewe.
"Hapana huyu sio mama yangu mzazi",Diana alimjibu baba yake.
"Unaongea nini wanangu yote yameshapita na Mimi baba yako nimeshakueleza mwanangu kila kitu naomba uelewe kile nilichokwambia",Mr.James aliongea kwa mara nyingine.
Albert alijua ni kitu gani kinachomtia hasira Diana alimsogelea na kushika mikoni yake,
"Diana najua una machungu mengi sana ya wewe kupoteza nafasi ya kuwa mshindi katika mashindano ya Miss Tanzania lakini kila kitu kinatokea kwa sababu, naomba ukubaliane na hiki kilichotokea Diana na usamehe kila kitu",Albert aliongea.
Mwanamama Beatrice alianza kutoa machozi mbele ya binti yake na hakuamini kuwa kitendo cha mwanae huyo kukoswa ushindi wa Miss Tanzania ndio kilipelekea yey kupata ajali,
"Mimi sikuwa mama mazuri ata kidogo nilimuimiza sana mwanangu Angelina ashiriki mashindano hayo ya Miss Tanzania na nilitoa baraka zote za yeye kushinda katika mashindano hayo, kumbe pia kulikuwa na mwanangu mwingine aliyekuwa akishiriki huenda nisingemlazimisha Angelina kushiriki basi wewe ungeibuka mshindi na yasingetokea haya yote",Mwanamama Beatrice aliongea kwa uchungu sana,Albert akimsogelea na kumtia moyo.
Mwanamama Beatrice alikuwa na kazi kubwa ya kujieleza kwa binti yake na badae mama na mtoto walipatana huku Mr.James na Albert wakifurahi kuona Diana akitoa chuki alizokuwa nazo kwa mama yake.
Stewart sasa aliamua kwenda kwao Angelina baada ya kuona imekuwa kazi kuonana nae ili aongee nae, alifika na kukutana na nyumba yenye hadhi ambayo ata yeye ilimvutia alibisha hodi na mlinzi akaja,
"Mambo vip, Angelina nimemkuta?",Stewart alitoa salamu kwa Mlinzi aliyekuja kumfungulia.
"Ndio yupo",Mlinzi alimruhusu kuingia mpaka ndani.
Alimpeleka mpaka kwa mwanadada Angelina aliyekuwa na mawazo yake siku hiyo ya kutokumuona mama yake tangu alipofika hapo nyumbani.
"Boss kuna mgeni wako huyu hapa", mlinzi aliongea na kuondoka huku mda huo akimuacha Stewart maeneo hayo.
"Ni wewe tena?", Manka aliongea aliyekuwa maeneo hayo na kumfanya Angelina avute kumbukumbu ya wapi amewahi kumuona Stewart na alifanyikiwa kukumbuka tu.
"Kuna kitu cha mhimu sana kimenileta hapa",Stewart aliongea huku akikaa kwenye kochi mda huo tena bira kukalibishwa na alianza kuwaelezea kila kitu kuhusu kampuni anayofanyia kazi Angelina kwa wakati huo.
Na alikuwa amejipanga mana alikusanya tarifa zote za warembo waliowahi kushinda taji la Miss Tanzania na waliochukuliwa na kampuni hilo kwenda kufanya kazi na niukweli usiopingika kuwa wanadumu kwa mda mfupi tu katika kampuni iyo ya uigizaji,
"Hapo kidogo nimeaanza kukuelewe lakini wewe ni nani na kwanini umeamua kuja kumpa tarifa hizi Angelina?",lilikuwa ni swali la Manka lililomfanya Stewart awe na kigugumizi cha kujibu kile alichoulizwa.
Wakiwa bado wanaendelea na maongezi Mwanamama Beatrice aliingia ndani tena akionekana hayupo sawa,
"Mama,Mwanadada Angelina alimwita mama yake.........
ulikuwa wapi mama mda wote huo nimekaa kusubiri hapa?".
"Nilikuwa kwa dada yako Diana",Mwanamama Beatrice alijibu bira kujali kama kuna mgeni maeneo yale ambae ni Stewart na pia Manka aliyekuwa maeneo yale.
"Diana!!",Angelina aliuliza kwa mshangao na alishindwa kumuelewa mama yake anamuongelea Diana yupi na ata Stewart nae alishituka baada ya kusikia jina la Diana....ITAENDELEA.
Angela atagundua ni Diana yupi anayemwongelea mama yake anayedai ni ndugu yake Karibu katika sehemu inayofata.
NB: Story hii NIYAKUTUNGA na haina ukweli wowote ule unaoendana na taratibu za nchi yetu????.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k?????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..