Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........27
Whatsapp..............0613083801
iliyopita.......
Naisha alivyotoka kwa Doctor Tayler alienda moja kwa moja kwa rafiki wa doctor tayler ili amuulize kile kinachoendelea kati ya Doctor Tayler na mwanadada Diana......
ENDELEA NAYO.......
Naisha alifika kwa rafiki wa Doctor Tayler na kuanza kumhoji lakini hakuambulia chochote zaidi ya kuambiwa kuwa Doctor Tayler anafanya kazi ya kumtibu mwanadada Diana na hamna kingine kinachoendelea zaidi ya hicho, aliondoka huku akiwa na mpango wa kufatilia mwenyewe bira kusaidiwa na mtu yoyote yule.
Naisha aliamua kuishi karibu na nyumba ya wanaokaa, Doctor Tayler pamoja na Diana ili afatilie na kujua ni kipi kinachoendelea kati yao na alifanya vile bira kumshirikisha mtu yoyote yule.
Albert baada siku kadhaa kupita aliamua kwenda nyumbani kwa Mr.James ili ajue kipi kinachoendelea kwa Diana na alikili ndani ya nafisi yake kuwa Diana ni moja ya wanawake anaowapenda kwenye hii dunia ukimtoa mama yake mzazi.
Alimkuta Mr.James na siku hiyo hakumchangamkia kama ilivyo siku zote ila hakujali sana zaidi ya kufata kile kilichompeleka pale,
"Ningependa kujua hali ya Diana inaendeleaje sababu mimi nikimtafuta kwenye simu anijibu na nimejaribu kumtafuta kwenye mitandao karibu yote ya kijamii ila bado jibu ni lilelile la yeye kukaa kimya",Albert aliongea mbele ya Mr.James.
"Kijana pole sasa mimi najua unampenda sana binti yangu na upo tayali kufanya kila kitu kwa ajili yake, ata mimi miaka ya nyuma limeshawahi kunitokea hilo (Mr.James alimaanisha mama yake mzazi na Albert ambae ni mwanamama katalina)... lakini niliamua kuacha hatima iamue ndiyo mana mpaka leo sina mke mana nilimpoteza mwanamke niliyekuwa nikimpenda....
Cha kukushauli ni vyema ukamtoa Diana kwenye kichwa chako mana awezi kuolewa na wewe na ata yeye ameshakili kwa mdomo wake tafuta mwanamke utakayempenda kwa dhati na yeye kukupenda",Mr.James aliongea pasipo kumficha kitu Albert.
"Basi baba nimekuelewa naomba siku ukienda ufikishe salamu zangu kwa Diana mwambie namsalimia sana na apone haraka",Albert aliongea na kuagana na Mr.James.
Maneno ya Mr.James yalimwingia kwenye kichwa chake, na alikumbuka pia alishawahi kumtamkia Diana kuwa anampenda lakini hakupata jibu lolote lililo kamili kutoka kwa Diana, Albert alipanga kuanza maisha mapya na kumsahau kabisa Diana licha ya kuwa na upendo zidi yake.
Taratibu siku zilizidi kusogea na Albert alikuwa ameshaanza kumsahau Diana na alikuwa bize na kazi katika kampuni yao ya FNF, lakini haikupunguza urafiki wake na mwanadada Angelina na temu hii ukiwa mkubwa zaidi kwani walikuwa wakitembeleana mara kwa mara.
Siku moja mwanamama katalina aliitikia wito wa mwanamama Beatrice na aliamua kwenda ili asikilize kitu alichomwitia Mwanamama Beatrice rafiki wa enzi hizo,
"Katalina kuna kitu nahitaji nikiweke sawa na kiwe wazi ili na wewe ukifahamu",Mwanamama Beatrice alifungua mazungumzo mbele ya rafiki wake wa enzi hizo.
"Kitu gani rafiki yangu"
"Ni kuhusu Diana mtoto wa Mr.James nafikili unamfahamu",Mwanamama Beatrice aliongea.
"Kiukweli huwa sitaki kumsikia yule mtoto mana baba yake alinifanya nimchukie mpaka mtoto wake", Mwanamama Katalina aliongea bira kujua kama na yule ni mtoto wa mtu ambae anaongea nae hapo.
Beatrice aliamua kumweleza ukweli wote kuwa Diana ni mwanae na alimweleza kila kitu kilivyotokea mpaka kumzaa Diana, Mwanamama Katalina alimpa pole sana kwa kilichomtokea miaka hiyo ya nyuma na kusababisha ashindwe kuendelea na masomo yake.
"Nilikuwa namchukia bure yule mtoto sikujua kama atakuwa binti yako kwakweli leo umenifanya nikaujua ukweli".
Maongezi mengine yaliendelea na walikumbushiana mambo waliyowahi kuyafanya enzi hizo marafiki hao wawili.
Upande wa Albert baada ya Diana kuanza kutoka kwenye ubongo wa kichwa chake mwanamke aliyeanza kuteka hisia zake alikuwa ni Mwanadada Angelina na hii ni kutokana na wao kuwasiliana mara kwa mara,
"Mbona nikikaa karibu na Angelina najihisi mtu wa kitofauti, na nitofauti na zamani ilivyokuwa?,emu ngoja leo nimwambie tuonane, nione kama itanitokea tena kwa mara nyingi",Albert aliongea na kuchukua simu yake na kumtafuta Angelina na alimwomba waonane, upande wa Angelina hakuwa na pingamizi alikubali kuonana na Albert kwa ajili ya mazungumzo.
Albert alisubiri mda ufike kama walivyopanga na Angelina na hatimae masaa hayakuchelewa mda aliokuwa akiusubiri uliweza kufika wa kwenda kuonana na mwanadada Angelina.
Ndani ya hotel ya kifahari na sehemu iliyokuwa na utulivu wa hali ya juu Angelina alikuwa amekaa huku pembeni yake yupo Albert,
"Shemeji, anaendeleaje dada yangu mana najua wewe utakuwa na mawasiliano nae",Angelina aliweka utani wake kama ilivyokawaida kwa kumuita Albert Shemeji.
"Angelina naomba tu uelewe mimi na Diana hatuwezi kuwa pamoja tena na haitokuja kutokea, naomba uwe unaniita jina langu tu na sio shemeji",Albert aliongea.
"Kwani kimetokea kitu gani au mmekosana?".
Albert aliamua kumweleza Angelina kila kitu alichoambiwa na Mr.James kitu ambacho kilimsikitisha sana Angelina.
Albert aliamua kubadili mazungumzo na sasa alitaka kumpeleleza Angelina ajue ni mtu wa aina gani,
"Na wewe Miss Tanzania hujawahi kunitambulisha mwenza wako?",Albert aliongea.
"Kwa sasa sifikilii kuingia kwenye mahusiano labda miaka ya badae ila sio sasa ivi mana sipo kwenye mahusiano",Angelina alijibu
Jibu lile lilimfurahisha sana Albert kuona kuwa bado anaweza kupata nafasi ya kujaribu bahati yake ya kuwa na mwanadada Angelina japo alikiwa na upendo wa kawaida kwa mwanadada huyo tofauti na ilivyokuwa kwa Diana.
Wakati Albert yupo pamoja na Angelina wakipiga stori upande wa kijana Stewart aliamua kufata ushauli aliopewa na baba yake na usiku wa siku hiyo alimfata na kumuomba amuangalizie sehemu yoyote ile ya yeye kufanya kazi inayoendana na taluma aliyosomea,
Kitendo kile kilimfurahisha sana Mr.John nakuona mwanae sasa yupo tayali kwa ajili ya kutengeneza maisha.
Nchini Canada Diana alianza kutembea vizuri na alirudi katika hali yake na hii kumfanya sasa aweze kupata mda wa kuwa anaenda anakotaka na kurudi.
Mwanadada Naisha alikuwa akifatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea bira ya wao kujua na alipata viashilia vingi vilivyoonyesha Doctor Tayler na mwanadada Diana ni wapenzi na sio kama alivyoambiwa hapo mwanzo,siku hiyo Doctor Tayler ambae nae alikuwa ameshanogewa na mahusiano hayo walitoka pamoja wakiwa wameshikana mikono na kuanza kutembea barabarani,
Katika hiyohiyo barabara tunamuona Naisha akiwa ndani ya gari na aliweza kumuona Doctor Tayler kamshika mkono Mwanadada Diana, hasira zilimshika na kuwasha gari lake aliloliondoa kwa kasi akiwafata wao walipo tena wakiwa hawana habari kama kuna gari nyuma yao inayokuja kwa kasi.....ITAENDELA.
Nini ambacho amepanga kufanya mwanadada Naisha karibu katika sehemu ijayo..