Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........25
Whatsapp..............0613083801
Doctor Tayler alishika mkono wake na kujaribu kuangalia kwa utaalamu anaojua yeye ndani ya mda mfupi tu aliweza kugundua kitu kilichomfanya ata yeye jasho lianze kumtoka huku akiwa na wasiwasi wa hali ya juu......
ENDELEA NAYO....
Doctor Tayler alikuwa na wasiwasi na ata Diana aliliona hilo,
"Tatizo nini kipenzi mbona umekosa raha gafra na umegundua kitua gani kinachonisibu",Diana alitamani kujua ni kitu gani kilichomfanya mpezi wake awe na wasiwasi kiasi hicho.
"Diana hamna tatizo lolote lile sema unahoma kali sana hapo ulipo na inatakiwa nikutafatie dawa haraka sana uweze kutumia",Doctor Tayler aliongea na mda huo alitoka na kwenda kuchukua dawa.
Upande wa Diana baada kipenzi chake kutoka alijiona mwenye bahati sana kumpata mwanaume wa kizungu anayemjali na kumpenda tena akiwa na mvuto,lakini hakuona dalili zozote za yeye kuwa na homa kama mpenzi wake alivyosema japo hakuwa na mashaka na kitu chochote kile.
Doctor Tayler alikuwa akitembea kwa kasi sana tena akiwa na wasiwasi wa hali ya juu alifika na kumkuta doctor mwenzake ambae ni rafiki yake na wanafanya kazi pamoja katika hospital hiyo,
"Njoo tuongee pembeni na maongezi na wewe doctor", aliongea huku akishika mkono wake na kumpeleka pembeni.
"Tatizo nini Doctor Tayler?, mbona unaonekana ni mtu mwenye wasiwasi sana?",swali kutoka kwa doctor mwenzake lilimfanya doctor Tayler kuangaza kila pande kama kuna mtu yoyote yule anayesikiliza mazungumzo yao alipohakikisha hamna alimgeukia rafiki yake nakuongea,
"Tatizo ni kuwa yule mgonjwa wa kiafrika aliyechini ya uangalizi wangu nilitengeneza nae mahusiano ndugu yangu", Doctor Tayler aliongea.
"Waafrika ni wazuri sana na ata mimi nataka niwe na mwanamke wa kiafrika",
"Sipo hapa kwa ajili yakuongea hayo mambo ila nimemwangalia na kwa utalamu atakuwa anamimba tayali japo yeye mwenyewe hajui isipokuwa mimi peke yangu ndiyo nafahamu",Doctor Tayler aliongea na kumfanya rafiki yake kushangaa.
Walikubaliana kufanya siri kati yao na Doctor Tayler hakutaka kuzaa na Diana kwasababu alikuwa na mwanamke mwingine waliyepanga kuoana, na kitu alichoshauliwa na doctor mwenzake ni kwenda kumpa dawa Diana itakayo mfanya mimba itoke na mambo mengine yaendelee kama walivyopanga.
Baada ya kupokea ule ushauli alichukua dawa na kwenda nazo, alifika na kumpatia Diana ambae nae alikunywa bira kujua kama anaua kiumbe kilicho ndani ya tumbo lake, na haikupita mda tumbo lilianza kuuma maumivu ya tumbo yalikuwa ni makali kwa mrembo Diana.
Doctor Tayler alienda kuchukua sindano na kuja kumchoma nayo iliyomfanya atulie na kulala usingizi wa kutokujitambua,Doctor Tayler alifurahi mana mambo yake yalienda kama alivyopanga na aliamua kumfanyia matibabu yatakayo mrudisha Diana kwenye hali yake ya kawaida.
Baada ya wiki moja kupita Albert akiwa bado gerezani na mwanamama katalina aligoma kabisa kutoa pesa kwa Mary hali iliyomfany mwanae aendelee kukaa gerezana na kusubiri siku ya kesi yake kusikilizwa ifike.
Nyumbani kwa Mwanamama katalina mme wake aliwasili baada ya kutoka nchi ya nje, ilikuwa ni furaha kwa Mwanamama katalina kumuona mmewe aliyeondoka Tanzania kwa miaka kadhaa iliyopita.
Cha kwanza alimuomba picha za binti anaye isumbua familia yake, Mwanamama Katalina alitafuta picha za Mary kwenye simu na kufanyikiwa kuzipata na kumuonyesha mmewe aliyeichukua simu ya mke wake na kuangalia picha za mke wake,
"Huyu binti anajifanya anaakili sana basi mimi nitamwonyesha, lazima nimuondoe duniani", mmewe aliongea kitu kilichomfaya Mwanamama katalina ashituke.
"Hapana usije ukafanya kitu kama hicho mme wangu mimi ninachotaka tu ni mwanangu aweze kurudi sihitaji kuona wewe ukijiingiza kwenye mambo yakuanza kumwaga damu za watu,naomba tutumie akili mme wangu ili tumpate Albert", Mwanamama Katalina alitoa ushauli kwa mme wake.
"Sawa nahitaji kuwatafuta vijana wachache watakaoweza kunifayia kazi na ndani siku mbili nakuahidi Albert atakuwa hapa na mtaishi nae tena kwenye hii nyumba"alijua nini atafanya mme wa Mwanamama katalina mda huohuo aliondoka pale nyumbani asimwambie Mke wake ni wapi anakoenda.
Na safari yake ilimpeleke kwenye vijiwe vya vijana wa mtaani na akaongea nao pia aliwaahidi atawapatia pesa endapo watakubali kufanya kazi yake.
Stewart hakukata tamaa ya kutompata Angelina bado aliamini ipo siku ata mkubali,aliamua atumie njia nyingine aliyoona ni sahihi kwake, na mtu peke aliyeona ni msaada kwake ni Manka ambae ni rafiki wa Angelina au ukipenda mwite Miss Tanzania.
Alimuahidi malipo mazuri endapo atafanyikiwa kumshawishi Angelina japo Manka alikuwa mgumu kukubali lakini aliposikia ahadi ile ya pesa aliamua kukubali,siku hiyo alienda kwao Angelina na alimkuta ni mtu mwenye mawazo sana,
"Angelina tatizo nini rafiki yangu mbona leo upo tofauti au unamfikilia Stewart wako", Manka aliongea huku akimsikiliza rafiki yake kuona atajibu kitu gani.
"Mimi namuwaza Albert na wala sio Stewart", Angelina aliongea, na mda huohuo alipigiwa simu na aliipokea mbele ya Manka,
"Angelina njoo nyumbani haraka sana huku",sauti ya upande wa mpigaji ilisikika kisha baada ya hapo simu ilikatwa na hii kumfanya Manka abaki njia panda na alitamani kujua mtu aliyempigia Angelina ni nani huyo.
Mda huohuo Mwanamama Beatrice alifika na kuwakaribisha chakula ila Angelina hakuwa na mda wa kula zaidi ya kuondoka pale nyumbani huku akimuacha mama yake akilalamika tu mbele ya Manka aliyebaki nae,
"Huyu mtoto tangu Albert aende gerezani safari kwenda kwa rafiki yangu katalina haziishi na ata sasa ivi naamini atakuwa anaenda hukohuko tu",Mwanamama Beatrice aliongea na kumfanya Manka aelewe ni wapi Angelina anapoenda.
Mawazo yao yalikuwa sahihi kwani Angelina alikuwa ameshafika kwa Mwanamama katalina baada ya kuitwa na siku hiyo alimwona baba mzazi wa Albert kwa mara ya kwanza,aliwakuta wote wakimsubiri yeye,
"Angelina samahani kwa usumbufu tumekuita hapa ili utusaidie kitu kimoja,ni wapi tutaweza kumpata Mary mana tangu afungue kesi anaishia kutupigia simu na kutoa vitisho na sasa ivi hapatikani kwenye simu", Mwanamama katalina aliongea na kumfanya Angelina avute kumbukumbu kipindi cha mashindano ni yupi aliyekuwa rafiki wa mwanadada Mary,
"Nimekumbuka kuna rafiki yake alikuwa anaitwa Faith ngoja nimtafute kwenye mtandao humu naweza kumpata",Angelina palepale alianza kumtafuta Faith na baada ya mda alifanyikiwa kuona picha zake na alituma jumbe mbalimbali na kilichokuwa kikisubiliwa kwa wakati huo ni Faith kujibu moja ya jumbe zile.
Bahati ilikuwa upande wao kwani Faith alijibu ndani ya dekika kadhaa tu na Angelina akamuomba namba kwa ajili ya mawasiliano ambae nae hakukataa kutoa namba.
Walimweleza Faith msaada wanaohitaji wa kujua alipo Mary na yeye hakusita kuwasaidia kwani aliwaelekeza mahari alipo mwanadada Mary,na baada ya kupata uhakika tu mme wa Mwanamama katalina aliondoka na kwenda kuwachukua vijana wake mpka alipo Mary kwa wakati huo.
Mary akiwa hana hili wa lile alishangaa kuona kazungukwa na vijana na hawakuwa na mda wa kupoteza moja kwa moja walimchukua na kumpeleka kwa mhusika aliyewatuma,
"Wewe nani na umepata wapi nguvu ya kunikamata mimi?",Mary aliongea na hakutaka kuonekana zaifu mbele ya watu waliokuwa wamemzunguka.
"Umemweka jela mwanangu alafu unaniuliza swali la kijinga hapa haya nileteeni sindano yenye sumu nimchome kwanza huyu akili zimkae sawa",Mary alivyosikia anataka kuchomwa sindano yenye sumu alitaka kukimbia lakini alikuwa ameshawekwa katikati na sindano ililetwa kwa ajili ya Mary kuchomwa...ITAENDELEA.
Mary atachomwa sindano?, karibu katika sehemu inayofata.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k???????????????????????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..