Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........20
Whatsapp..............0613083801
"Diana!!",Angelina aliuliza kwa mshangao na alishindwa kumuelewa mama yake anamuongelea Diana yupi na ata Stewart nae alishituka baada ya kusikia jina la Diana......
ENDELEA NAYO.......
Mwanamama Beatrice aliamua kumchukua mwanae Angelina na kwenda nae mpaka chumbani Ili wakafanye maongezi,
"Mwanangu najua unamjua vizuri sana Diana uliyekuwa ukishindana nae kwenye mashindano ya kumtafuta Miss Tanzania,naomba uamini maneno yangu yule ni dada yako na wote nyinyi ni ndugu",Mwanamama Beatrice aliongea na kumfanya Angelina asiamini kile alichoweza kukisikia.
"Mama utakuwa umekosea yule hawezi kuwa ndugu yangu mana mimi na yeye damu zetu haziendani ata kidogo",Angelina hakukubaliana na maneno ya mama yake.
Mwanamama Beatrice alimweleza kiundani zaidi mwanae hali iliyofanya aanze kuyaamini maneno yake na kutamani kwenda kuonana na ndugu yake huyo.
Stewart pamoja na mwanadada Manka baada ya wao kubaki peke yao,
"Diana gani aliyekuwa anamzungumzia?",Stewart aliamua kuvunja ukimya kwa kumuuliza Manka.
"Heeeeeh!!,wewe kaka umbea umezidi kwani lazima ujue ni mtu yupi waliokuwa wakimzungumzia mpaka uniulize mimi",maneno ya Manka yalimfanya Stewart anyamaze na kutulia kabisa mana Manka alionekana ni moja ya wanaoongea sana.
Angelina alitoka akiwa na mama yake mda huohuo na kumfata Manka aliyekuwa amekaa na Stewart,
"Manka kuna sehemu naenda nitakuja mda sio mrefu",alimuaga na kuondoka na alisahau kama Stewart alikuwa maeneo hayo ila akili zote za Anjelina kwa wakati huo zilikuwa ni kule alikokuwa akielekea yeye pamoja na mama yake.
"Kama mtu ambae nilikuja kwa ajili yake kaondoka na kuniacha hapa na mimi sioni haja ya kuendelea kubaki hapa acha niondoke",Stewart nae alinyenyuka na kuondoka akimuacha Manka peke yake.
Msanii maarufu aitwae Big Don alikuwa anapongezana na mtu aliyempa zile picha za manager wa kampuni aliyokuwa anafanya kazi Angelina na kwenda kumtishia Ili aweze kumwachia mwanadada Angelina aje katika mikono yake,
"Huyu mwanamke alijifanya mjanja sana kukataa million 50 nilizompa ili afanye kazi yangu sasa temu hii kazi yangu atafanya na malipo hatopata",Big Don aliongea.
"Lakini ni mwanamke mrembo yule ndiyo mana Kawa Miss Tanzania, kama inawezekana boss niachie mimi awe wangu",kijana aliongea mbela ya Big Don neno lilomkera,
"Yani nikuachie wewe alafu mimi nibaki na nani? unakichaa wewe?, kipi ambacho huelewi kazi lazima afanye na mapenzi nitafanya nae mimi ndiyo Big Don kwakuwa ni Miss Tanzania jina langu litazidi kuwa kubwa zaidi na watu kuniongelea kama tu nikiingia nae kwenye mahusiano",Big Don nae alikuwa na mpango wa kuingia kwenye mahusiano na mwanadada Angelina.
Big Don alichukua simu yake na kumpigia mwanadada Angelina ila iliita bira kupokelewa,
"Boss mbona hapokei simu au manager wa ile kampuni kakupa namba za mtu mwingine?",
"Hawezi kufanya kitu kama hicho yani huyu Miss Tanzania lazima awe mikononi mwangu, temu hii sitakubali kumuacha kama wa mwaka jana nilivyowaachia wao",Big Don aliongea.
Mwanadada Angelina sasa alikuwa kwenye vita ya kugombaniwa pasipo yeye kufahamu na temu hii ata masanii maarufu nae aliingia kwenye kinyanganyilo hicho cha kumtaka Miss Tanzania.
Angelina akiwa na mama yake walifanyikiwa kufika kwa Mr. James na unakuwa ni ugeni mwingine tena kwa mwanadada Diana aliyekuwa amekea kwenye kochi na hii ni baada ya kijana Albert kumtoa kwenye kiti cha wagonjwa na kumuweka kwenye kochi.
Angelina alisogea mpaka alipo Diana ili kujihakikishia kwa macho yake mwenyewe kama kweli yeye na Diana ni ndugu,
Wakati wote huo Mr.James na Mwanamama Beatrice walikuwa wakiwatazama tu mabinti zao na kijana Albert aliyekuwa amekaa pembeni,
"Angelina kwanini ndugu yangu asiwe mtu mwingine mpaka uwe wewe tena mtu niliyekuwa nakuchukia na sikutaka ata kukuona",Diana aliongea na alitoa ya moyoni pasipo ata kuficha kitu.
Angelina hakuwa na cha kuongea zaidi ya kumsikiliza ndugu yake aliyekiwa akilalamika.
"Kwanini Anjelina huu ulemavu nilioupata ni wivu niliokuwa nao baada ya wewe kunishinda kwenye mashindano ya Miss Tanzania na sijui lini nitapona, nimeharibu maisha yangu mwenyewe kwa kuwa na chuki na mtu ambae ni ndugu yangu",Diana alizidi kuongea na kumfanya Angelina amsogele karibu na kumkubatia.
"Wewe ni dada yangu kuanzia sasa nitafanya kile unachokitaka ata kujivua taji hili la uMiss Tanzania nipo tayali Diana ilimradi uwe na furaha, kwenye hii dunia nilijihisi nipo peke yangu na nilijua pia sina ndugu mwingine zaidi ya mama yangu na baba yangu mzazi, Diana wewe ni dada yangu na mimi ni mdogo wako",Angelina aliongea.
Mwanamama Beatrice alifurahi kuona watoto wake wamepatana na kumaliza tofauti zao na ata Albert nae alifurahi kuona ndugu wawili wamekuwa kitu kimoja.
Mr.James hakuwa na cha kusema lakini akiwa anaangalia tukio la binti yake Diana akiwa na ndugu yake gafra simu yake iliita na kukutana na namba ngeni iliyomlazimu kuipokea,
"Nimekutumia zile milion 4 ulizoniambia za taa ya gari lako niliyoiharibu",sauti ya upande wa pili ilisikika na hakuwa mwingine bali ni Mr.John au baba mzazi wa Stewart.
Mr.James alitaka kumjibu Mr.John ila mazingira hayakuruhusu akaamua kukata simu tu, kwanza alikuwa bado anamawazo kuhusu binti yake alafu Mr.John amechelewa kutuma ela tofauti na alivyomwambia alikuwa bado anakisasi na Mr.John cha kumchukulia Mwanamama katalina kipindi cha ujana wao kwa mawazo yake yalivyokuwa yakimtuma.
"Baba",Angelina alimwita Mr.James baba kitendo ambacho karibu kila mtu kilimfurahisha kuona binti huyo anamwita Mr.James baba kwa mara ya kwanza.
"Namu binti yangu",Mr.James nae aliitikia kuonyesha kufurahishwa na jinsi alivyoitwa.
"Baba mimi naona dada anaweza kupona kwanini tusimpeleke nchi za nje akatibiwe huko ni bora tuingie garama za kutosha ila apone na arudi kwenye hali yake", Angelina aliongea.
Albert nae aliona ni wazo zuri aliloongea Angelina,
"Kwanini hatukufikilia hili toka mwanzo",Albert aliongea.
Kila mmoja wao walikubaliana na wazo la Angelina na taratibu zilianza kufanyika za kumpeleka Diana nchi za nje ili kuangalia kama anaweza kupatiwa matibabu,na Mr.James aliamua kumpeleka Canada binti yake kwa ajili ya matibabu.
Siku iliyopangwa ya kumpeleka Diana kwa ajili ya matibabu ilifika na siku hiyo Angelina akiwa na mama yake mzazi walimsindikiza Diana aliyekuwa akiongozana na baba yake mzazi Mr.James kwenda Canada,
"Diana binti yangu mungu akutangulie huko uendako naamini utarudi Tanzania ukiwa tayali umeshatibiwa na umepona, nakupenda sana mwanangu",Mwanamama Beatrice aliongea akiwa amemkumbatia Diana.
"Niambie neno moja tu dada angu kabra hujaondoka", Angelina aliongea.
"Naomba uniangalizie Albert hakikisha haingii kwenye mahusiano na mwanamke yoyote yule mpaka pale nitakaporudi",Ndio neno alilotamka Diana kwa mdogo wake Angelina.
Waliekea kwenye ndege Diana akiwa na Mr.James na ata nyumba yao iliachwa chini ya uangalizi wa Angelina na Mwanamama Beatrice.....ITAENDELEA.
Diana anaenda kutibiwa nje ya nchi je? atafanyikiwa kupona karibu katika sehemu inayofata.
NB: Story hii NIYAKUTUNGA na haina ukweli wowote ule unaoendana na taratibu za nchi yetu????????????????.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k???????????????????????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..