Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........08
Whatsapp..............0613083801
ilipoishia.......
"Mara zote nilikuwa naitafuta hii nafasi ya kuongea vizuri na wewe baba angu uniambie kuhusu mama yangu mzazi yupo wapi?...
ENDELEA NAYO....
"Ni story ndefu sana binti yangu na siwezi kukwambia kwa leo ila unatakiwa ujue jina la mama yako mzazi ni Beatrice", Mr.James aliingia ndani baada ya kumtajia jina la mama yake mzazi binti yake pasipo kumweleza kiundani zaidi.
"Baba mbona ameniambia jina la mama angu na kuniacha njia panda",Diana aliongea huku akimfata baba yake aliyeelekea ndani ili amuulize vizuri lakini hakuambulia chochote kile zaidi ya kuambiwa asubiri mda mwafaka utakapofika .
"Ni siri gani baba anayonificha na hataki niijue kwa wakati huu?", Diana alijiuliza baada ya kutokuambulia chochote kutoka kwa baba yake mzazi zaidi ya kutajiwa jina la mama yake mzazi.
Aliamua kujianda ili aende katika kampuni ya FNF na siku hiyo Diana alitaka kupendeza na kuwa wakitofauti kabisa.
Nyumbani kwa kina Anjelina,
"Mwanangu mbona Leo sielewielewi?", Mama Angelina alimuuliza mwanae.
"Kwanini mama?"
"Umetumia mda mrefu kujipamba na sio kawaida yako,nahisi kutakuwa na tukio la mhimu siku ya leo huko uendako"
"Ni kweli mama hujakosea ila nyie ndio mmefanya mpaka nitumie mda mrefu kujipamba mana sikutaka kuingia kwenye haya mashindano kabisa", Angelina aliongea.
Mwanamama Beatrice alimsogelea binti yake nakuanza kumpa maneno ya kumtuliza na hakuacha kumkumbusha hatakiwa kukataa nafasi aliyopewa na Mwanamama katalina.
Lakini Angelina alikumbuka kitu cha mhimu na aliamua kumwambia mama yake,
"Mama ni mda mrefu umepita hatujaenda kumuona baba gerezani naamini atakuwa anajisikia vibaya sana kuona familia yake haiendi kumtembelea",Angelina aliongea kwa majonzi kidogo.
"Upo sahihi mwanangu kwa ulichosema ila hutakiwa kuwa na mawazo hayo kwa sasa, tutatafuta siku maalumu ya kwenda kumuona baba yako na hutakiwi kukaa sana mwanangu mda unazidi kwenda Angelina", Mwanamama Beatrice hakutaka kuendelea na zile stori za baba mzazi wa Angelina aliye gerezani kwa wakati huo.
Angelina alijiandaa na alipomaliza nae alielekea sehemu husika na siku iyo mavazi yake yalikuwa tofauti na siku zote na hakwenda kikazi kwani Mwanamama katalina alimpa likizo ya kutokufanya kazi yoyote ile zaidi ya kujumuika na wenzake kwenye tukio la siku hiyo.
Alifika ndani ya kampuni ya FNF na ata Mwanadada Diana nae aliwasili na alipendeza isivyo kawaida karibu kila mtu siku hiyo alikuwa tofauti na siku zote na wote walijumuika katika sehemu maalumu iliyo andaliwa kwa ajili ya tukio husika, Mwanamama Katalina aliyekuwa amewasili tayali akiwa na baadhi ya viongozi wenzake wanaowasimamia aliongea mbele ya warembo hao,
"Siku ya leo watu wote mtapatiwa namba na izo ndizo zitakazokuwa namba zenu za ushiriki mtakazo dumu nazo mpaka mwisho wa mashindano haya na kila mtu atakuja hapa mbele yetu kuonyesha kile kilichomfanya awe hapa", Mwanamama Katalina aliongea na kuwafanya wote warufahi.
Upande wa Angelina alikuwa na wasiwasi kidogo mana alikuwa sio mzoefu wa maswala hayo ya kutembea kimiss na wala hakuwahi kufanyia mazoezi kama wenzake hali iliyozidi kuongeza hofu kiupande wake.
Mwanamama katalina alisimama kwa mara nyingine nakuongea
"na kingine, ni siku ya leo peke yake tutakayofanya ili zoezi asubuhi, siku zingine zote zinazokuja zoezi hili litakuwa likifanyika usiku........
Cha mwisho kampuni yetu ya FNF tumeingia makubaliano ya washiriki wote kuvaa viatu vitakavyotoka kwenye kampuni tuliloingia nalo makubaliano,kila mmoja wenu mda mtakaokuwa mnapatiwa namba zenu za ushiriki mtachagua viatu vitakavyo wafa na hii ni lazima ndugu zangu,na mkumbuke kuwa imebaki miezi miwili tu mashindano yaweze kufanyika ya kumtafuta mshindi kati yenu nyinyi", Mwanamama alimaliza kuongea na kila mshiriki aliyashika maneno yaliyotamkwa na Mwanamama huyo.
Zoezi lilianza kufanyika na kila mshiriki alipatiwa namba na kuchagua kiatu atakachotumia katika zoezi hilo,Mary na Faith nao hawakuwa mbali kwani kila mtu alipatiwa namba ya ushiriki na ata kwa mwanadada Angelina nae alipatiwa namba 30 ikiwa kama namba yake ya ushiriki tatizo lilikuwa kwenye aina ya viatu alivyopewa vilikuwa ni size yake lakini kwenye maisha yake yote hakuwahi kuvaa viatu vyenye visigino virefu na huo ukawa mtihani mwingine kwa mwanadada Angelina.
Diana alipatiwa namba 25 ya ushiriki na sasa kila mtu alijipanga kwa ajili ya zoezi kuanza huku tukio hilo likirecordiwa.
Albert nae alifika kwa ajili ya kushuhudia mazoezi ya warembo waliokuwa pale.
Zoezi lilianza na mshiriki namba Moja alianzia kutembea kwa miondoko iliyomvutia Karibu kila mtu aliyekuwa pale na watu walipiga makofi wakimpongeza kwa kazi nzuri, na wengine pia walianza kupita japo asilimia ya wote waliokuwa wakipita wengi walikuwa na miondoko iliyowavutia watazamaji wa zoezi lile.
"Huu mwaka itakuwa kazi sana kumpata mshiriki mana wengi wanaonekana wako vizuri", mwanamama katalina aliongea akimwambia kiongozi mwenzake waliokuwa wamekaa wote maeneo yale.
washiriki walizidi kupita na kufanya vizuri akiwemo Mary pamoja na rafiki yake Faith nae alijitahidi kwa kiasi chake, ilifika zamu ya mshiriki namba 25 kupita na hakuwa mwingine bali ni Diana,
Albert alivyomwona Diana kwa mbali ndipo alipozidi kudata kabisa kwani siku hiyo Diana alipendeza utasema ndio siku husika ya mashindano yenyewe,
"Diana leo lazima nikutamkie kitu ambacho nilikisubiri kwa mda mrefu kukwambia,leo ni lazima nitamke neno nakupenda ", yalikuwa ni maneno ya kijana Albert aliyekuwa akimtazama Diana.
Mwanamama Katalina alivyomwona Diana alikasilika ila hakuwa na cha kufanya zaidi ya kutazama tu na alikuwa hatazami kwa umakini ushiriki wake kama ni mzuri au mbaya,alijikuta akiwa na mawazo ya chuki kuliko kufatilia kile kilichokuwa kikiendelea pale,lakini alishangaa watu wakipiga makofi ya kumpongeza Diana.
Karibu kila mtu alifurahishwa na kile alichokionesha Diana na ata baadhi ya washiriki wenzake walimpongeza kwa kile alichokionyesha.
Baada ya Diana washiriki wengine wanine walipita sasa ilifika zamu ya mshiriki namba 30 ambae ni Angelina licha ya kuwa ni mazoezi waliyokuwa wakifanya lakini alikuwa na hofu ya hali kitu kilichomfanya apoteze kujiamini, alisogea mpaka stegini na kujaribu kutembea kama wenzake walivyokuwa wanafanya lakini bahati haikuwa kwake siku hiyo kutoka na hofu aliyokuwa nayo alijikuta akitembea vibaya na kuanguka mpaka chini,
"Hahahahahahahaha!!!", ni vicheko tu ndio vilikuwa vikisikika kwa watu waliokuwa pale Karibu kila mtu alicheka isipokuwa Mwanamama katalina peke yake.
Watu waliofurahi zaid ni Diana pamoja na Albert aliyeshindwa kuzuia kicheko chake kwa tukio aliloliona pale.
Mwanamama Katalina alisimama na kwenda mpaka alipokuwa Angelina alimyenyua kwa kutumia mikono yake yake,
"Mwanangu hii ni kama changamoto kwako dhahabu ili ing'ae lazima ipite kwenye moto, mwanzo siku zote huwa mgumu sana na ndiyo tunafanya mazoezi hapa ili ikifika siku ya tukio kila mtu awe na uwezo wa kupambana kupigania taji",Mwanamama katalina aliongea lakini upande wa Angelina ni maneno machache aliyoyasikia kwani mawazo yake yalikuwa kwenye aibu aliyoipata mbele ya umati ule na ata Mwanamama katalina alilitambua hilo ikabidi apaze sauti yake kuwatuliza watu waliokuwa pale,
"Wote naomba mtulie, hapa tunafanya mazoezi tu Ili tulekebishane na ata nyie washiriki wengine mliopita hapa na hamjaanguka kama mwenzenu ilivyomtokea bado mnavitu vya kulekebisha,huyu ni mshiriki mwenzenu na hamtakiwi kumdhihaki ata kidogo kwani hii ni kama changamoto kwake", Mwanamama katalina alimaliza kuongea na kidogo ilisaidia watu kutulia na kuendelea kuangalia washiriki wengine waliokuwa wanapita mpaka pale walipomaliza.
Kila mtu alitowanyika na ata Angelina ambae kila mtu aliyekuwa akikutana nae anamwangalia na kumcheka kutokana na tukio lililotokea,akiwa anatembea kutoka katika kampuni hiyo ya FNF alisikia akiitwa ikabidi ageuke kutazama ni nani anayemuita,
Hakuwa mwingine aliyekuwa anamwita bali alikuwa Diana aliyeamua kumfata baada ya yeye kusimama,
"Duuuuuh pole sana kwa kuanguka si bora uache tu kushiriki kama huwezi, yani mbele za watu unaanguka, hii ajabu sana",Diana aliongea lakini Angelina hakutaka kumjibu zaidi ya kugeuka nakuanza kuondoka kitendo kile Diana aliona kama ni dharau anayofanyiwa na Angelina.
"Unakiburi mimi naogea wewe unaenda?"
"Ata kama nikikujibu haitasaidia kitu kama kuanguka nilianguka mimi na sio wewe".
Wakiwa bado na majibishano yale Albert aliweza kuwaona na kuamua kuwafata huku moyoni akiwa na dukuduku la kuongea mbele ya Angelina,kabra hajawafikia alishika simu yake na kuanza kutabasamu kwa kile alichokiona kwenye simu aliwasogelea huku akiwa anakitu cha kuongea kwa Angelina.....ITAENDELA.
Nini atafanya Albert atakapo wafikia karibu katika sehemu inayokuja.
NB: Story hii NIYAKUTUNGA na haina ukweli wowote ule unaoendana na taratibu za nchi yetu????????????????.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k???????????????????????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..