Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........22
Whatsapp..............0613083801
ilipoishia.....
Angelina kitu kilichomfanya acheke ni kuona mtu ambae ata hamjui alafu anamtumia ujumbe wa kumwambia kuwa anampenda ila kwa kuwa ni Miss Tanzania wa mwaka huo jumbe kama zile aliona ni kitu cha kawaida tu kutumiwa........
ENDELEA NAYO.....
hakutaka kujibu ujumbe ule zaidi ya kuufuta na namba aliiblock kabisa nakuendelea na ratiba zigine.
Siku iliyofata asubuhi na mapema aliongozana na Manka mpaka mahakamani akiwa na karatasi zenye mikataba ya kazi ya kampuni aliyoingia nayo mkataba akipinga kwenda kufanya kazi nje ya makubaliano yao, alifungua kesi na baada ya kesi kufungulia manager alizipata zile tarifa na kuona sasa mambo yanaelekea pabaya aliamua amtafute Big Don,
"Unataka uingize kampuni katika matatizo makubwa sana ndugu yangu",manager alimwambia Big Don.
"Unamaana gani mbona hueleweki manager"
"Angelina kaenda mahakamani kufungua kesi ya sisi kutaka kumfanyisha kazi nje ya makubaliano tuliyowekeana", Manager aliongea na kumfanya Big Don kuelewa.
"Nisikilize kwa umakini manager, huyo mwanamke mimi nawaachia nyinyi sitaki kuchafua jina langu mana nilitumia juhudi sana kulifanya liwe juu alafu leo nilichafue kwa sababu ya Miss Tanzania",Big Don aliongea na aliamua kujitoa na hakutaka tena kumfatilia mwanadada Angelina.
"Huyu mjinga kweli kaniingiza katika matatizo alafu yeye anajitoa, na ikitokea Angelina akienda kuongea na waandishi wa habari alivyo na jina kubwa ataharibu sifa ya kampuni tuliyo ipambania kwa jasho na damu", Manager aliwaza afanya kitu gani na alipata njia aliyoona ni sahihi.
Alichukua simu yake na kumpigia mwanadada Angelina na kumuomba akaifute iyo kesi na ata mkataba yupo tayali kuvunja nae ili kila mtu aendelee na maisha yake.
Mwanadada Angelina alichana na kampuni hiyo maarufu na sasa alibakiwa na mikataba ya makambuni madogomadogo yaliyoingia nae kwa ajili ya kutangaza biashara zao.
Miezi mitatu ilipita na maisha yaliendelea ila Stewart alifanyikiwa kujiweka karibu na Mwanadada Angelina japo hakuwahi kumweleza kama ndiye yeye aliyetuma ule ujumbe wa kumwambia kuwa anampenda na tatizo kubwa alilokuwa nalo nikushindwa kumtamkia mwanamke kuwa anampenda akiwa nae,na upande wa Angelina yeye alimchukulia kama rafiki yake wa karibu.
Ahadi aliyompa dada yake Diana ya kuwa karibu na Albert na ahakikishe aingii kwenye mahusiano na mwanamke yoyote mpaka pale atakaporudi Tanzania ilimfanya Angelina atengeneze mazoea na Albert na ata upande wa kijana Albert alikuwa tayali ameshamzoea Angelina.
Siku hiyo walipanga kuonana kati ya Albert na Angelina kwa ajili ya mazungumzo,
"Angelina hali ya Diana inaendeleaje ni mda mrefu sana sijaongea nae na kila nikijaribu kumtafuta inakuwa ngumu kumpata",Albert aliongea.
"Ata mimi nini hivyohivyo sina mawasiliano naye zaidi siku ya mwisho kupata tarifa zake za yeye kuwa na uwezo wa kuanza kunyenyua miguu ila kutembea vizuri ndiyo bado mana miguu yake haijakaza vizuri"
"Nimemkumbuka sana Diana na amini ata yeye amenikumbuka huko aliko",Albert aliongea.
"Wewe ni shemeji yangu lazima ata yeye atakuwa amekukumbuka sana huko aliko"Angelina aliongea kiutani kidogo na kumfanya Albert atabasamu tu.
ila wakiwa katika mazungumzo maeneo yale Stewart nae alikuwa akipita ni kama bahati tu alishangaa kumuona Angelina maeneo yale akiwa anaongea na mwanaume aliyekuwa amemtegea mgongo nakushindwa kumuona vizuri, aliamua kusogea karibu ili atoe salamu kwa Angelina,alifika pale na kukutana uso kwa uso na kijana Albert.
"Angelina uko hapa naweza kukupa kampani?"Stewart aliongea kana kwamba kamkuta Angelina peke yake maeneo yale na hii ilimfanya Albert achukie sana mana aliona ni kama dharau.
"Ooh,Stewart sio kwa leo, nipo na mtu wangu wa mhimu tufanye siku nyingine itakuwa vizuri zaidi", Angelina aliamua kumtolea nje Stewart.
ila Albert alijaribu kukumbuka sura ya Stewart amewahi kuiona sehemu ngani ndipo alipoikumbuka vizuri,siku ya kwanza ni airport na siku ya pili ni hospital siku ambayo Diana amelazwa, alimtazama kwa macho ya kumdadizi Stewart aliyekuwa anaondoka maeneo hayo,
"Huyu rafiki yako watu wengine hatuoni, ata salamu tu anashindwa kutoa inaonekana anadharau sana",Albert aliongea na hakupenda kitendo kilichoonyeshwa na Stewart.
Upande wa Mary pesa alizokuwa nazo ziliisha kabisa na mbaya zaidi ata mpango alioupanga wa kwenda kumkamata Mwanamama katalina ulishindikana kabisa sasa alibadilisha mbinu na mbaya zaidi alikuwa akimshirikisha rafiki yake Faith bira kujua kama ndiye mtu anayeamua kumzunguka ili awasaidie watu anaopanga kuwafilisi,
"Faith nimepata mpango mpya temu hii nikipata tu pesa nasepa marekani kabisa kwenda kuishi huko na Tanzania hamtaniona tena", Mary aliongea.
"Mpango gani huo shoga yangu?, mama wewe kwa mipango rafiki yangu ni namba moja sioni wa kukufikia"
"Nataka nikafungue kesi mahakamani nikamshitaki Albert",Mary aliongea tena akiwa amethamilia kabisa.
"Kesi!!!"
"Ndiyo mbona unashangaa Faith mimi ndio Mary kwanza nitaenda kusema kuwa Albert alinibaka kisha baada ya hapo akanitoa mimba yake kwa lazima",Mary aliona ndio njia sahihi ya kujipatia pesa.
Na ata mwanadada Faith kwa mipango iyo ya Mary hakujua anaanzaje kumsaidia kijana Albert ili asiingie matatizoni
Nchini Canada Diana alikuwa akiendelea na matibabu na doctor aliyekuwa akimtibu alipata matatizo ivyo ikabidi doctor mwingine atafutwe ili amuangalie mwanadada huyo, ndani siku mbili tu doctor aliweza kupatikana na kutambulishwa mbele ya mwanadada Diana.
Diana alikili duniani kuna wanaume wazuri na moja ya mwanaume huyo ni doctor aliyekuja kwa ajili ya kumtibu na koti alilovaa lilikuwa na jina lililoandikwa doctor Tayler, macho ya Diana hayakuchoka kumwangalia mzungu huyo aliyemvutia na ata moyo wake ulikili kweli umetokea kumpenda doctor huyo,
"Habari mgonjwa naitwa doctor Tayler na nipo hapa kuendeleza kazi iliyoachwa na doctor mwenzangu",Doctor Tayler alijitambulisha kwa lugha ya kingeleza na lugha iyo haikuwa ngeni masikioni mwa Diana ila alikutwa na hali ya kupata ukakasi wa kujibu kutokana na kuzubaa kwake kumshangaa mzungu huyo.
Wiki moja iliweza kukatika huku doctor Tayler akiendelea kumtibu mwanadada Diana na ata doctor Tayler alianza kuvutiwa na urembo wa mwanadada Diana na ndani ya mda mfupi tu kila mtu alikuwa ameshamzoea mwenzake.
Siku moja doctor Tayler akiwa anamfanyisha mazoezi ya kutembea huku amemshika, alimshika sehemu ya kiunoni hali iliyomfanya mwanadada Diana awe na hisia kali na alishindwa kujiamini mbele ya mzungu huyu na bahati mbaya ilikuwa kwao, kwani wote walijikuta wakianguka chini huku doctor Tayler akimlalia Diana.
Mapigo ya moyo ya mwanadada Diana yalikuwa yakienda kasi isivyo kawaida na ata Doctor Tayler nae hali aliyokuwa nayo ni sawa na ya Diana.
Mara zote macho hutoa ishara ndicho kilichotokea kila mtu alikuwa akimtazama mwenzake na kushindwa kuongea lakini doctor Tayler alipeleka mdomo wake kwa mwanadada Diana ambae nae hakuwa na uwezo wa kukataa na wote wakaanza kubadilishana mate na kujikuta wakiingia kwenye ulimwengu mwingine.
Baada ya kila mtu kumjua mwenzake haikuwa siri tena kwa watu wale wawili mahusiano yalianzia hapohapo na kila mtu alikuwa na furaha kwa mwenzake hasa Diana aliyekuwa amempenda Doctor Tayler nakusahau Tanzania kama kuna mwanaume aliyekuwa anaitwa Albert akili zote zilikuwa kwa doctor Tayler.
Mr.James kama kawaida yake kila ifikapo mwisho wa mwezi lazima aende Canada kumjulia hali binti na ata temu hii alifika mpaka Canada lakini alisitaajabu kumkuta doctor tofauti na yule aliyekuwa anamjua yeye tena wa temu hii akiwa ni kijana na alishangaa pia kumuona binti yake ni mwenye furaha kuliko mwanzo,
"Binti yangu hongera sana sio mda utapona, mana sasa ivi unaweza wa kusimama japo kwa tabu,hongera sana miguu yako imeanza kukaza", Mr.James aliongea.
"Ni kweli baba ila natamani nikae hukuhuku kwanza ata kama nikipona sitawahi kurudi Tanzania",Diana aliongea kitu kilichomshangaza baba yake.
"Unamaanisha nini Diana kusema utabaki huku,Tanzania watu wengi wana kusubiri kwa hamu hasa Albert ambae kila siku anakuulizia na hachoki kunisumbua na mimi nafikilia kukuozesha yule kijana anakufaa sana na huwezi mpata mwanaume anayekupenda kama Albert japo mimi na mama yake tulikuwa na tofauti zetu ila haiwezi zuia nyinyi kuwa pamoja", Mr.James alijikuta akimpigia debe Albert na hii ni baada ya Albert kumjali sana Diana kipindi ambacho yupo kwenye magumu.
"Baba mume mimi ndiyo nitachagua yule atakayenifaa lakini naomba tu nikwambie ukweli uliopo siwezi kuolewa na Albert mimi", Diana aliongea na alimaanisha kile alichokiongea mana tayali alikuwa kwenye penzi zito kwa wakati huo na doctor Tayler....ITAENDELEA.
Diana anabadilisha mawazo yake tena ya kuwa na Albert na amepata mwanaume mwingine tukutane sehemu inayokuja.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k???????????????????????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..