Story......................MISS TANZANIA
Mtunzi...................Zooper
Sehemu..ya...........23
Whatsapp..............0613083801
Sehemu iliyopita.....
Diana aliongea na alimaanisha kile alichokiongea mana tayali alikuwa kwenye penzi zito kwa wakati huo na doctor Tayler.........
ENDELEA NAYO......
Mr.James hakuwa nacha kuongea tena kwa binti yake zaidi ya kumuacha afanye maamuzi mwenyewe aliyoona ni sahihi kwake, alikaa kwa siku kadhaa na ata yeye akiwa kama mtu mzima alikuwa ameshaanza kuona kuna kitu kinachoendelea kati ya Diana na doctor Tayler.
Mpaka anarejea Tanzania alikuwa ameshaona mabadiliko makubwa kwa binti yake hasa ukaribu aliokuwa nao kwa Doctor Tayler.
Diana penzi la doctor Tayler lilimnogea wakiwa wamekaa pamoja Diana aliamua kufunguka kile kilicho moyoni mwake mbele ya mwanaume huyo,
"Tayler naomba unioe",Diana alijikuta yeye ndiyo anaomba ndoa mbele ya mwanaume huyo.
Habari ile kwa Tayler ilikuwa ni mapema sana hakutaka kuingia kwenye ndoa kwa wakati huo na alikuwa anasababu zake binafsi Doctor Tayler,
"Give me time Diana and the only thing which I want to say I will marry you later (Nipe mda Diana na kitu pekee ningependa kusema nitakuoa hapo badae)"Doctor Tayler aliongea.
Diana hakutaka kupingana na maneno ya mpenzi wake aliyaamini kwa asilimia zote.
Miss Tanzania leo alipokea simu kutoka kwa Stewart,
"Angelina uliniahidi kuwa utatafuta mda maalumu wa kuongea na mimi",Stewart alisikika akimwomba Angelina atimize ahadi yake kama alivyokuwa amemuahidi.
"Ooh,Stewart mambo ni mengi na ratiba zinanibana sana ila kwakuwa umenikumbusha basi jioni ya leo naomba utafute sehemu nzuri ya mimi kuonana na wewe",Angelina aliongea na kukata simu.
"Oooh yes,safi kabisa kakubali",
Stewart alijikuta akishangilia kama mtoto na kujisahau kama yupo nyumbani kwao bira kujua kama maongezi yake yote Mr.John alikuwa akiyasikia.
"Nani huyo kakubali ??",ilikuwa ni sauti ya baba yake iliyomshitua na kumfanya akose cha kuzungumza.
ila Mr.John siku hiyo alikuwa na maneno ya kuongea na kijana wake kwanza alimkalisha chini ili amsikilize anachomwambia na alimsihi amsikilize kwa umakini sana,
"Wewe umeshakuwa sasa ndiyo mana sishangai kuona ukihangaika kutafuta mwenza wako wa maisha, ila kuna kitu kimoja tu umekisahau mwanangu",Mr.John aliongea.
"Kitu gani baba?",mwanae aliuliza.
"Umesahau kutengeneza future ya maisha yako tangu ulipotoka kusoma nje za nchi sijawahi kukuona ukiwa na juhudi za kutafuta kazi na mbaya zaidi, ata kujumuika na mimi katika biashara zangu huwa hujumuiki, na pia nafanya kazi na makampuni kadhaa ila Stewart hujawahi niambia nikufanyie mchakato wa kazi mwanangu kumbuka leo wazazi wako tupo hai kesho hatupo, inatakiwa utengeneze maisha yako Stewart kwanza wanawake utawapata tu huko badae",Mr.James alimwambia mwanae na kweli Stewart baba yake siku hiyo aliongea kitu cha mhimu sana kwa ajili ya kumkumbusha.
"Ni kweli baba nitafanyia kazi kile ulichoniambia"
Baada ya baba yake kuondoka aliona kweli kuna umhimu wa kufanya vile alivyoambiwa na Mr.John lakini haikumfanya asahau kama ana ahadi ya kuonana na mwanadada Angelina jioni ya siku hiyo.
Mwanadada Mary kama alivyopanga na ndicho alichokifanya alibadilisha mwonekano wake wa mavazi na kuvaa mavazi yaliyochoka na urembo wake kupotea kwa mda, kisha akenda kituoni na akiwa analia,
"Wewe dada tatizo nini mbona umekuja kituoni tena ukiwa na machozi",Afande alimuuliza mwanadada Mary.
"Afande nimefanyiwa ukatili, mimi nilikuwa nimshiriki katika mashindano ya kumtafuta mrembo wa taifa,nikiwa kama mshiriki kuna kijana aliyekuwa na nafasi kubwa kwenye ile kampuni ya FNF na mama yake ndiye aliyekuwa akitusimamia sisi katika mashindano, yule kijana kwa kuwa mama yake anafasi kubwa alinitishia na kunidanganya kuwa nitakuwa Miss Tanzania kama nikitembea nae kitendo ambacho nilikipinga ila badae alinitisha sana ikabidi nikubali na baada ya mda nikapata ujauzito......,
ukatili alionifanyia alinikamata akiwa na vijana wenzake nikapewa dawa ya kuitoa mimba bira ridhaa yangu mimi", Mary alitoa maelezo mengi mpaka yule asikari aliyekuwa anaandika maelezo alimpa pole mwanadada Mary.
Kwa maneno aliyozungumza Mary na kuifungua kesi palepale polisi waliongozana na Mary mpaka nyumbani kwa mwanamama katalina ili wakamuchukie kijana Albert.
Albert akiwa amekaa na mwanamama katalina palepale walishanga hodi ikigongwa kwa fujo hali iliyomlazimu Mwanamama Katalina akaangalie ni nani huyo anayegonga mlango,alifika na kufungua mlango mwanamama katalina alishangaa sana kuona asikari polisi katika nyumba yake,
"Karibuni Afande", Mwanamama Katalina aliongea kwa hofu licha ya ukubwa alionao ila hofu ya neno polisi alikuwa nayo.
"Albert yupo wapi?", ndio swali la kwanza aliloulizwa na moja ya Afande huku wakiingia ndani.
Kwakuwa Albert alikuwa amekaa palepale hawakupata shida kumpata,
"Wewe ndiyo unaitwa Albert?", Afande aliuliza kwa mara nyingine.
"Ndio ni mimi"
"Binti njoo na usogee huku", baada ya Afande kumwita Mary palepale aliingia ndani na hapo ndipo Albert na Mwanamama Katalina walijua ni mchezo wa Mary alioamua kuwachezea na temu hii akitumia njia nyingine.
"Binti ndio huyu mtu mwenyewe"
"Ndio afanye ni yeye",
Aliongea huku analia mwanadada Mary na hakukuwa na mda tena kwani Albert alichukuliwa na kupelekwa polisi.
"Afande mmekosea huyu ni mwanangu na hana kosa lolote huyu binti ni muongo, naombeni muamini maneno yangu",mwanamama katalina alijaribu kuongea kumtetea mwanae.
"Tunakuheshimu sana na ndiyo mana tumekuja kwako kistarabu maelezo yote yataenda kutolewa polisi,aya mchukueni huyo kijana twende",
hawakuwa na utani ata kidogo kwani Albert alichukuliwa na kupelekwa polisi.
Hatimae jioni ilifika na siku hiyo Stewart alivaa nguo za kitofauti kwani alivaa nguo ambazo hakuwahi kuzivaa hapo kabra na alimtafuta Angelina kumwelekeza ni sehemu gani wakutane ambae nae alikubali ila mda huo alikuwa na shoga yake Manka,
"Angelina usitake kuniambia wewe na Stewart tayali mambo yameshaanza kuiva",Manka aliongea.
"Nilijua tu yani ukisikia kitu wewe huachi kuongea,mimi na Stewart hamna chochote kile kinachoendelea kati yangu mimi na yeye aliniomba tuonane kwa ajili ya mazungumzo",Angelina aliongea na mda huo alikuwa akimalizia kujianda.
Kijana Stewart alikuwa ameshafika katisa sehemu husika na alikuwa akimsubiria tu Angelina aweze kuwasili pale,
"Leo lazima nimwambie ukweli wa moyo wangu ata kama sitaongea maneno mengi ila lazima nitamke neno nakupenda",Stewart aliongea na ndani ya dekika kadhaa tu aliweza kuona gari ya Angelina ikiwasili pale.
Stewart alinyenyuka na kuifata gari ya Angelina, baadhi ya watu waliokuwa maeneo yale waliweza kuwashuhudia na watu wengine wakianza kuchukua picha na kurusha kwenye mitandao kwa sababu ya uwepo wa Angelina maeneo yale.
Stewart alimpeleka Angelina mpaka sehemu aliyoichagua yeye kwa ajili ya maongezi,
"Stewart naomba tuzungumze haraka tuondoke maeneo haya wewe mwenyewe unaona jinsi watu wanavyotuangalia na kuchukua video",Angelina aliongea lakini kile kitendo Stewart yeye alikuwa anakifurahia tu.
"Stewart naomba uniambie ni kipi ulichoniitia?",Angelina alizidi kuongea.
Stewart akifikilia anzeje kumwambia mwanadada Angelina ili amwelewe lakini aliamua kujikaza kiume na kutoa kile kilicho moyoni mwake.
"Angelina moyo wangu haupo huru tangu nilipokuona mara ya kwanza ila leo nataka niuweke huru moyo wangu"
"Una maana gani Stewart?"
"Angelina mimi nakupenda sana zaidi ya kukupenda, nimeona wanawake wengi wenye kila sifa lakini sijaona mtu wa kukufikia wewe, na sio kwa sababu wewe ni Miss Tanzania ila nakupenda kwakuwa wewe ni Anjelina Gerald, naomba ukubali kuwa mke wangu",Stewart alimaliza kuongea huku akisubiri kuona Angelina ata chukua maamuzi gani.
Angelina hakuamini kusikia yale maneno kutoka kwa kijana Stewart na alipomtazama usoni macho ya stewart yalimaanisha kile alichokuwa akikizungumza kina ukweli, Angelina alifungua kichwa chake na kuongea....ITAENDELEA.
Angelina atamjibu nini Stewart na vipi kuhusu Albert aliyesingiziwa kesi na mwanadada Mary?,karibu katika sehemu inayofata.
Pata Story hii mpaka mwisho kwa Tsh 1000 za k???????????????????????? lipia kupitia namba,
0613083801 HALOPESA,John Bugumba..