PENZI LA MHALIFU 24
Sikujua alikuwa na mpango gani hivyo Cyborg aliondoka na kwenda kufanya kazi ya kuhubiri.
Baada ya masaa kadhaa kupita Cyborg alikuja nyumbani akiwa na mfuko uliokuwa na sadaka na baadae alizimwaga kwenye meza iliyokuwa sebleni kwetu.
"Leo nimehubiri sana sijui ata upako ulitokea wapi" Cyborg aliongea huku akifungua vishikizo vya shati lake.
"Kelvin ivi ni kweli unahubiri kwa ajili ya kutangaza neno la mungu au kwa ajili ya kujipatia pesa!?" Nilimuuliza sababu bado sikuona kama Cyborg kaamua kuokoka kutokana na baadhi ya matendo yake yaliyokuwa yakijionyesha.
Cyborg alinisogelea karibu na kuniambia.
"Wewe unajua kabisa mimi ni mpambanaji Malaika, acha nitangaze neno la mungu kwa mda na baadae nikichoka nitaacha na kufanya kazi nyingine ila sadaka lazima nizichukue" aliongea na kuanza kuhesabu sadaka alizokuja nazo.
Cyborg aliendelea na kazi hiyo ya kuhubiri na maisha yalikuwa yakiendelea ila kilichokuwa kinanishangaza hakuacha kutamka matusi ya kila aina wakati wa kufanya mapenzi.
Siku hiyo ilikuwa ni mida ya saa 5 usiku tukiwa tumelala tulisikia mtu akibisha hodi kwenye mlango wetu na mimi nilinyenyuka na kwenda kufungua mlango.
Nilikutana na mwanamke ambae ni mpangaji wetu aliyezoea kutupiga chapo wakati wa kufanya mapenzi na alikuwa kwenye hali ya wasi wasi mkubwa baada ya kuniona.
"Una shida gani jirani!?" Nilimuuliza na jirani yangu aliniambia.
"Na shida na mchungaji kuna tatizo kwenye chumba changu"
"Tatizo!?"
"Ndio kuna tatizo kubwa sana" Alinijibu na mimi nilimtazama machoni nione kama anachoongea kina ukweli wowote ule.
Jirani yangu alinielezea kuwa kuna mzimu ameuona kwenye chumba chake hivyo alikuwa anahitaji Cyborg aende akakiombee chumba chake.
Niliamua kumuita Cyborg na alikubali kwenda kuomba kwenye chumba cha jirani yetu japo nilikuwa na uhakika hakuna upako wowote ule aliokuwa nao Cyborg kwani mimi ndiye niliyekuwa nikiishi nae.
Cyborg alienda kwenye chumba cha jirani yetu na kuniacha ndani ya nyumba yetu.
Dekika 15 zilipita bira Cyborg kurudi na baadae machale yalianza kunicheza baada ya kujumlisha matukio ya jirani yangu hasa ya kumsifia Cyborg kuwa yupo vizuri kwenye mambo ya mizagamuo.
"Isije kuwa wanakulana hawa" niliongea mwenyewe na kuondoka na kwenda kwenye nyumba ya jirani yangu.
Nilifika na kweli nilisikia sauti ya Cyborg kwa mbali akiomba, kidogo nilipata uhakika kuwa kuna usalama hivyo niliamua kurudi kwenye nyumba yetu na kuendelea kumsubiri Cyborg.
Upande wa Cyborg yeye alikuwa akiomba kumbe jirani yangu alikuwa na mpango wake na kwakuwa alikuwa na makalio makubwa, alianza kuyabinua makusudi ili kumtamanisha Cyborg.
Jirani aliona haitoshi kwani alizidi kumsogezea makalio yake Cyborg kitu alichofanyikiwa maana Cyborg alisimamisha baada ya kugusishwa makalio na jirani.
Sijui ni hisia gani nilizokuwa nikizipata kwani nilijikuta nikiishiwa raha na gafra nilipata ujasili wa kwenda kwenye nyumba ya jirani yangu kwa mara nyingine. nilifika mlangoni na temu sikuisikia ata sauti ya Cyborg kuomba.
Moyo wangu ulihisi kutakuwa na kitu kinachoendelea hivyo nilijaribu kusukuma mlango na bahati nzuri ulikuwa wazi, niliingia kwenye nyumba ya jirani yangu na moja kwa moja nilielekea kwenye chumba walichokuwemo.
Ile nafungua mlango nilimkuta Cyborg akiwa kashika mwichi wake akijiandaa kuuweka na kuutwanga kwenye kinu cha jirani yangu.
"Cyborg!!!" nilimwita na kumfanya asitishe kile alichokuwa akitaka akifanye.
Jirani yangu aliokota kitenge chake haraka na kujifunga. Cyborg nae alipandisha suruali yake na kuvaa vizuri kwani mambo tayari yalikuwa yameharibika.
Niliondoka kwa hasira na kurudi kwenye nyumba yetu na nilipofika nilifunga mlango ili Cyborg asiingie ndani na ata mfanyakazi wetu aliyekuwa akishinda na mtoto nilimwambie asijaribu kumfungulia Cyborg.
Cyborg aligonga mlango ili nimfungulie lakini sikuta kabisa kwenda kumfungulia na nilikuwa kwenye hasira kwa wakati huo.
Cyborg baada ya kuona hatumfungulii alisogea kwenye dirisha la chumba chetu nilichokuwa nimelala na kuanza kuongea.
"Malaika naomba unisamehe kipenzi, jirani aliyagusisha makalio yake kwenye mhogo wangu na mimi nilijikuta nikitamani kumzagamua, nisamehe Malaika sitarudia tena" Cyborg aliongea maneno ya kila aina ila mimi nilijifanya simsikii kabisa.
Kumbe jirani alikuwa amedhamilia siku hiyo Cyborg amzagamue na ukizingatia mme wake hakuwepo aliona ndiyo nafasi ya pekee ya kufanikisha mpango wake.
Alikuwa akisikiliza jinsi Cyborg alivyokuwa akinibembeleza dirishani ili nimfungulie na baada ya kuona sitaki kumfungulia jirani alitoka kwenye nyumba yake na kumfata Cyborg.
"Samahani mchungaji, naomba ukalale kwangu na ilikuwa bahati mbaya tu" jirani aliongea.
"Mchungajiiii!! unaniita mchungaji sababu wewe ndio uliyenigusisha makalio yako mpaka nikashikwa na upwiru na kusababisha mke wangu akatae mpaka kunifungulia" Cyborg aliongea kwa kulalamika na mazungumzo yao nilikuwa nikiyasikia.
Haraka nilitoka na kwenda kufungua mlango sababu niliona nikizembea watatiana kweli, Cyborg baada ya kuniona nimefungua mlango aliingia ndani akiwa na bibilia yake mkononi utafikiri ni mtu wa mungu kweli.
Jirani yetu ilibidi aondoke baada ya kuona mpango wake umeharibika.
Cyborg siku hiyo alikuwa na kazi ya kuniomba msamaha na baada ya kuona nimemchunia na sitaki kumsamehe, Cyborg aliamua atumie mbinu yake ya siku zote.
Alianza kunipapasa kwa ajili ya kuniandaa ili tufanye mapenzi. kiukweli siku hiyo sikuwa na hisia kabisa licha ya kutumia utundu wake anaonifanyia siku zote bado sikuwa na hisia za kufanya nae mapenzi.....ITAENDELEA..