PENZI LA MHALIFU 10
Kiukweli sikuwa na amani kwani niliamini kitumbua changu kipo kwenye hatari ya kuliwa mda wowote ule na mkuu wangu wa kazi, kuna mda niliwaza nimtafute Cyborg ila moyo mwingine uligoma kabisa kwa kuhisi nitazidi kuongeza matatizo.
Mimi na mkuu wangu wa kazi tuliweza kufika sehemu husika na aliniambia niteremke kwenye gari na mimi nilifanya kama alivyoniambia.
Tulielekea mpaka kwenye nyumba moja ya kawaida na Mkuu wangu aliingia kwenye chumba kimoja wapo huku akiniambia nimfate kitu ambacho sikutaka kufanya kabisa.
Nilisimama mlangoni na kugoma kuingia kwenye chumba hicho ndipo mkuu alipokasirika nakuongea.
"Acha ujinga wewe hapa upo kikazi usifikiri kila mda nataka nikutie tu, emu ingie huko" aliongea kwa ukali hivyo ilibidi niingie ndani ya chumba hicho.
Nilipoingia kwenye chumba hicho kitandani kulikuwa na nguo za kike wanazovaa machagudoa za kila aina, huku chini ya kitanda kukiwa na viatu vya kike.
Mkuu aliongea" vuaa hizo nguo zako uchague nguo moja wapo hapo, kuna kazi unayotakiwa kwenda kuifanya na hutakiwi kuonekana na vazi la kipolisi" mkuu aliongea na nilibaki nimemkodolea macho kwa kile alichokiongea.
Aliniambia kwa mara nyingine nivue sare zangu nilizokuwa nimevaa na mimi niliona ni ujinga hasa kuvua mbele yake.
"Toka nje nivue" nilimwambia na aliondoka huku akiwa kakunja sura kwani alitaka walau aone rangi ya chupi yangu inafananaje.
Nilibaki peke yangu nakuanza kutafakari kile nilichoambiwa na mkuu wangu na kilichokuwa kikiniumiza kichwa ni mavazi yaliyokuwa pale kitandani maana mimi ni mtu wa kuvaa suruali kwa sana na pensi tu.
Niliamua kuvua sare zangu nakuanza kuchagua nguo yenye uangalau kidogo, ila nguo zote hazikuwa na utofauti hivyo niliamua kuvaa moja wapo na niliangalia chini vyiatu vinachoendana na mimi ilibidi nilivua viatu vyangu vya kazi na kuamua kuvivaa viatu vilivyokuwa pale.
Baada ya kuvaa nilibaki nikimtukana mkuu wangu nikiwa mwenyewe ndani ya chumba hicho" huyu mkuu ni fala sana nguo gani hizi" niliongea kwani mpaja yote yalikuwa nje na mtu kama angetaka kunizagamua asingepata tabu kutokana na mavazi niliyokuwa nimevaa.
Nilitoka ndani ya chumba hicho huku nikiwa najiangalia kila mara na nilimkuta mkuu akinisubiri nje huku akitoa ulimi wake baada ya kuona mapaja yangu na nilipomtazama kwenye zipu yake ya suruali tayari alikuwa ameshasimamisha.
Kidogo nilijikuta nikishikwa na aibu nikiwa kama mwanamke.
Mkuu hakutaka kuongea kitu bali alienda kuchukua mfuko na aliporudi alinikabizi na kuniambia nikaweke sare zangu nilizokuwa nimevua kwenye mfuko alionipatia.
Nilifanya kama alivyoniambia na baadae aliniambia tuongozane wote kwenye gari lake, kiukweli hiyo siku nilishindwa kuelewa kabisa dhumuni na mpango wa mkuu wangu wa kazi ni upi.
Niliingia kwenye gari nikiwa na mfuko wangu niliokuwa nimeweka sare zangu za kazi pamoja na viatu.
Mkuu alianza kuendesha gari na safari yetu ilitufikisha kwenye klabu moja maharufu iliyokuwa na kila aina ya starehe.
Mkuu aliniambia kuwa natakiwa niingie ndani ya klabu hiyo na kuna kijana mmoja nitamuona kavaa tisheti nyekundu, nitatakiwa kumfata kijana huo.
Kijana huyo nitajitambulisha kwake kisha baada ya hapo atanipa mpango wa kumkamata tajiri mmoja aliyekuwa akiitwa James kwani alikuwa akipenda kwenda kwenye klabu hiyo kwa ajili ya kufanya biashara zake za madawa ya kulevya ndani ya klabu hiyo.
Nilijua tu kuwa mkuu kaamua kufanya hivyo ili anikomeshe hivyo nilimwangalia na kuamua kumwambia.
"Hii kazi ni ngumu kwangu siiwezi peke yangu"
Mkuu alikasirika baada ya mimi kumwambia vile.
"Hutaki kufata amri ya mkuu wako sio au unataka ufukuzwe kazi!?, nakupa dekika tano za kufikiria ufanye vile nilivyokwambia au nifanye maamuzi ya kukusimamisha" mkuu aliongea kwa kunitisha na mimi ilibidi nikubali kwenda kuifanya kazi yake.
Kwanza kilichokuwa kikiniuma ni mafunzo niliyoyapitia nilivyokuwa jkt na nilivyohangaika kutafuta kazi alafu anatokea mjinga na kutaka kuniharibia, ndiyo sababu iliyonifanya nikubali.
Niliondoka na kuingia ndani ya ukumbi huo huku nikimuacha boss akiniangalia kwa dharau.
Sikujua kama ilikuwa ni kazi au ulikuwa ni mpango wake tu kwani nilipofika ndani ya klabu hiyo niliwaona vijana wawili na nilipomwangalia kijana mmoja wao aliyekuwa na tisheti yenye rangi nyekundu.
Nilikumbuka jinsi mkuu wangu alivyoniambia kuwa nitakutana na kijana mwenye tishet nyekundu na inatakiwa nimfate na kujitambulisha kwake ili anipe maelezo kamili na jinsi kazi inavyotakiwa kufanyika.
Sikuwa na uhakika kama ndiye yeye ila niliamua kumsogelea na kwenda kutoa salamu kwake.
Kaka yule aliniangalia kwa kunipandisha na kunishusha kisha baada ya hapo alishika mkono kwenye kidevu chake na kuanza kukuna ndevu zake.
"Umetumwa na Mr Robert!?"
Aliniuliza akimaanisha mkuu niliyekuja nae na mimi nilimkubalia kuwa ndiye aliyeniagiza.
"Twende huku tukaongee" aliniambia na mimi nilianza kumfata. tulifika sehemu na kuingia kwenye chumba kimoja na ndani ya chumba hicho hakukuwa na mtu mwingine zaidi yetu.
Nilishuhudia kukiwa na vinywaji vya kila aina kwenye meza iliyokuwa ndani ya chumba hicho.
Mkaka yule alikaa kitandani na baadae aliniongelesha.
"Unatumia kinywaji gani!?"
Aliniuliza na kunifanya nishangae nakuamua kumjibu.
"Sijaja hapa kunywa vinywaji bali nimekuja kikazi" nilimjibu lakini nilishangaa kuona akinilazimisha ninywe kinywaji chochote kile ndipo tufanye maongezi.
Nikiwa kama asikari niligundua lazima kuna kitu kinachoendelea kwani tangu nifike hakuna chochote alichoniambia zaidi ya kunilazimisha ninywe kinywaji.
Sikutaka tena kuendelea kubaki ndani ya chumba hicho, nilinyenyuka kwa ajili ya kuondoka lakini aliniwahi na kunizuia.
"Unataka kwenda wapi mrembo!?" aliongea huku akijaribu kunivuta.
"Achia mkono wangu kabra sijakubadilikia" nilimwambia lakini alijifanya mjuaji.
Nilimpiga teke kwenye sehemu zake za siri na lilienda kumpata vyema kwenye korodani na kumfanya aniachie nakuanza kushika korodani zake kutokana na maumivu aliyokuwa akiyapata kwa wakati huo.....ITAENDELEA.
Inapatikana kwa Tsh 1000 tu.
Namba za malipo.????????????????
0613083801 HALOPESA Jina John Bugumba.
0755271203 M-pesa Jina John Bugumba..