Story……………….MMMMH...SHEMEJI HAPANA!!!?? 01
Mtunzi…………….SIMULIZI ZA ZOOPER
Whatsap………....0613083801
……………………….0748697173
Umri………………..18+
Kwa jina naitwa Fatuma karibu katika mkasa huu ili upate kujua yaliyonipata baada ya mimi kukutana na shemeji yangu aliyekuwa amemuoa dada yangu wa kumfata tuliyezaliwa nae tumbo moja.
Chondechondechondee..... story hii ni kwa wakubwa tu wale walio juu ya umri wa miaka 18 na kuendelea, na kwa wale walio na umri wa chini ya miaka 18 naomba mtupishe kidogo.
Ilikuwa ni mida ya asubuhi niliyokuwa nimelala kitandani, nilisikia sauti ya mama kwa mbali ikiniamsha lakini mimi sikutaka kuamka.
Mama baada ya kuona sitaki kuamka aliamua kuingia kwenye chumba changu na kuanza kuniamsha huku akiyapiga makalio yangu.
"Wewe Fatuma amka haraka uende nyumbani kwa dada yako, kanipigia simu nakuniambia kuwa shemeji yako anakusubiri umpeleke vyeti vyako"
"Mmmmh mama lakini!! mbona bado mapema sana niache niendelee kulala kwanza" nilimjibu mama na kujifunika shuka kwa ajili ya kuendelea kulala.
"Unaona sasa ujinga ulionao wewe mtoto!? ndiyo maana mpaka sasa ivi upo upo tu huna mwelekeo wa maisha, amka haraka huko" mama aliniambia kwa msisitizo hali iliyonifanya niamke na kukaa kitandani huku nikipiga miayo kutokana na chembe chembe za usingizi nilizokuwa nazo.
Baadae nilitoka kitandani na kwenda bafuni kuoga kwa ajili ya kujiandaa kuelekea kwenye nyumba ya dada yangu aliyekuwa akiitwa Aisha ili nikakutane na shemeji yangu aliyekuwa akiitwa Rashidi na lengo kubwa ni shemeji Rashidi anisaidie kunitafutia kazi kwenye hospital aliyokuwa akifanyia kazi.
Nilijiandaa na baada ya kumaliza nilibeba begi langu lililokuwa na nguo baadhi kisha baada ya hapo nilimuaga mama na kuondoka. Nilienda kupanda kwenye gari na nikiwa ndani ya gari niliishika simu yangu na kumtumia ujumbe Aisha nikimwambia kuwa nipo njiani nakuja nyumbani kwake.
Dada alijibu ujumbe niliomtumia kwa kuniambia kuwa shemeji Rashidi ndiye atakayenipokea kwani yeye alikuwa amebanana kidogo. Baada ya kuwasiliana na dada niliegemea kwenye siti ya gari niliyokuwa nimekaa na baadae nilijikuta nikipitiwa na usingizi, nilikuja kushituka baada ya masaa kadhaa kupita hasa baada ya kugundua kuwa gari imefika sehemu niliyokuwa nikielekea.
Niliteremka kwenye gari nililokuwa nimepanda na bahati nzuri kuna namba ngeni mda huo huo ilinipigia kwenye simu yangu hivyo niliamua kuipokea na sauti iliyosikika ilikuwa ni sauti ya shemeji Rashidi akiniuliza kama tayari nimeshafika.
Nilimwambia kuwa nimeshafika na shemeji Rashidi aliahidi atafika baada ya mda mfupi tu, nilimsubiri Shemeji Rashidi na baada ya mda aliweza kufika akiwa kavaa kanzu kama ilivyo tamaduni ya dini yetu.
Shemeji Rashidi alisogea mahali nilipokuwa mimi huku akiniangalia machoni na aliponifikia tulisalimiana kwa kushikana mikono lakini nilishangaa kumuona shemeji Rashidi akinitekenya kwenye kiganja changu cha mkono huku akiniambia.
"Umekuwa sana Fatuma"
"Mbona nipo vile vile tu Shemeji" nilimjibu huku nikiangalia pembeni kutokana na aibu niliyokuwa nayo.
"Mmmh basi mtu uliyenae atakuwa anakufaudu sana Fatuma"
Shemeji Rashidi aliongea hivyo na mimi ilibidi nimuulize.
"Kwanini unasema hivyo Shemeji..!?"
"Umejaliwa kuwa na umbo zuri Fatuma kuliko ata dada yako Aisha natamani mimi ndiye ningeipata hiyo bahati ya kuwa na wewe ila tayari nimeshamuoa dada yako" alinijibu na ndipo nilipotambua dhumuni la Shemeji Rashidi kuniambia kuwa nimejaliwa kuwa na umbo zuri.
"Shemeji hapana!! mimi nipo kawaida mbona!" nilimjibu na baadae niliamua kubadilisha mada ili asiendelee kuongea maneno yaliyokuwa yakinipa wakati mgumu kuyajibu.
Baadae tuliondoka na kuelekea nyumbani kwake na baada ya mda tuliweza kufika na kumkuta dada Aisha akiwa anafanya usafi kwenye nyumba tena akiwa kajifunga kitenge tu. Sikushangaa sana kumkuta akiwa amevaa vile kwani dada ndivyo alivyokuwa amezoea kuvaa toka tulivyokuwa tukiishi wote nyumbani.
Tulisalimiana na Aisha alinikaribisha nyumbani kwake na kuchukia mizigo yangu na kuipeleka chumbani. Nilibaki mimi pamoja na shemeji Rashidi lakini nilishangaa kwa jinsi alivyokuwa akiniangalia huku akichezesha miguu yake na baadae aliamua kuniuliza kama vyeti vyangu nimekuja navyo, nilimjibu nimekuja navyo hivyo nilienda kuvichukua na kumpatia.
Vyeti vyangu vilikuwa na ufaulu wa kawaida ila nilishangaa kumuona shemeji Rashidi akinisifia baada ya kuvikagua kwa kuniambia kuwa nilifanya vizuri shuleni kitu kilichonishangaza maana sikuwa na ufaulu wa kulizisha kiasi hicho kama aliyokuwa akinisifia shemeji Rashidi.
Baadae shemeji Rashidi aliniahidi atanisaidia ili niweze kupata kazi na siku mbili zilipita nikiwa naishi nyumbani kwa dada huku shemeji Rashidi akihangaika kunitafutia kazi kwenye hospital aliyokuwa akifanyia kazi yeye.
Siku moja nilipatwa na homa kali hivyo shemeji Rashidi aliingia kwenye chumba nilichokuwa nimelala na kupeleka mikono yake kwenye mashavu yangu kwa ajili ya kupima joto la mwili wangu.
"Hali yako ni mbaya sana shemeji ila nisubiri nije mara moja" Shemeji Rashidi aliongea na kutoka chumbani.
Baada ya mda alirudi huku akiwa kashika sindano kwenye mkono wake na kuufunga mlango kisha baada ya hapo aliniambia.
"Shemeji itabidi nikuchome sindano ya kutuliza hali uliyonayo kisha baada ya hapo nitakupeleka hospital ili uweze kuchukuliwa vipimo"
Baada ya shemeji Rashidi kuniambia kuwa anataka kunichoma sindano nilianza kuingiwa na hofu kwani nilikuwa mwoga sana wa kuchomwa sindano.
Ilibidi nimpe mkono wangu ili aweze kunichoma sindano lakini shemeji Rashidi alikataa kunichoma sindano kwenye mkono na badala yake aliniambia.
"Ingekuwa vizuri kama ungevua ili niweze kukuchoma kwenye makalio yako shemeji"
"Mmmh shemeji hiyo hapana kwanini usinichome kwenye mkono hapa!?" nilimjibu lakini shemeji Rashidi aliendelea kunitaka nivue nguo ili aweze kunichoma sindano kwenye makalio yangu huku akidai ni kwa ajili ya usalama wa afya yangu.....ITAENDELEA.
Aya sasa kazi kwenu ndiyo kwanza sehemu ya kwanza, nahitaji like 300 pamoja na komenti za kutosha ili nitupie kipande cha pili leo leo ?????????????????????.