Story……………….MMMMH...SHEMEJI HAPANA!!!?? 17
Mtunzi…………….SIMULIZI ZA ZOOPER
Whatsap………....0613083801/0748697173
Umri………………..18+
ENDELEA.........
Shemeji Rashidi alikaa kimya kwa mda na baadae aliongea.
"Ni kweli kabisa nilimtaka Fatuma niwe muwazi kwako mama, kuna sababu zilizonifanya nimtake Fatuma licha ya kuwa nimemuoa ndugu yake" Shemeji Rashidi aliongea mbele ya mama pasipo kuwa na aibu.
Hiyo siku ndiyo niliamini kwenye hii dunia kuna watu wanaojiamini, Shemeji Rashidi pia ni mmoja wao kwani alikuwa akijiamini mbele ya mama labda kwakuwa alikuwa ni mwanamke maana ndiye mzazi pekee tuliyekuwa nae.
Mama alimuuliza sababu iliyomfanya atake kutoka na mimi kimapenzi na shemeji Rashidi alimwambia ni kwa sababu ya dada Aisha kutokushika mimba.
"Lakini hiyo ni mipango ya mungu!, hakukuwa na sababu ya kumtaka mdogo wake"
"Mama, mimi niliona bora nitembee na Fatuma na nizae kwenye familia hii kuliko kwenda kuzaa nje ya ndoa, huu ni mwaka wa tano sasa ivi Aisha hana dalili za kushika ujauzito" Shemeji Rashidi aliongea ila baadae mama alimuuliza.
"Wewe si doctor kwani unashindwa kujua mwanamke wako anasumbuliwa na tatizo gani!?"
"Nimejaribu kumwangalia ila sijaona tatizo lolote lile na kama huu mwaka hatashika mimba basi nitamrudisha nyumbani na kuoa mwanamke mwingine ata hivyo dini yangu inaniruhusu kuoa mwanamke mwingine" Shemeji Rashidi aliongea.
"Huko unaenda mbali mwanangu kwanini usiwe na subira tu, mtoto ni majaliwa na mkeo atashika ujauzito ila sio kutembea na shemeji yako!, kama angepata mimba wewe ungeilea hiyo mimba!?" mama alimuuliza shemeji Rashidi na alimjibu kuwa angeilea na sio kuilea tu angekubali kuitwa baba.
Mama aliona kama shemeji Rashidi kalukwa na akili hivyo alimwambia aondoke nyumbani kwetu akajifikirie upya kuhusu kile alichokisema, shemeji Rashidi aliondoka hivyo tulibaki wawili mimi pamoja na mama.
"Fatuma ivi huyu shemeji yako ana akili kweli!?"
"Nazani umejionea mwenyewe mama"
"Mbona Aisha ni binti mzuri tu kisura na huenda anakuzidi mpaka wewe kwanini asitulie na mwanangu akamvumilia! au jogoo wake hapandi mtungi vizuri ndiyo maana kashindwa kumpa mimba dada yako!?" Mama aliongea bira kujua kama jogoo wa shemeji Rashidi anapanda mtungi maana shahidi ni mimi mwenyewe sema niliamua kukaa na siri hiyo moyoni pasipo kumshirikisha.
"Sifahamu mama labda umuulize Aisha mwenyewe" nilimjibu na baadae mama alichukua simu yake na kumpigia dada Aisha akimtaka aje nyumbani.
Kwakuwa kulikuwa na kaumbali kutoka nyumbani kwetu mpaka alipokuwa akiishi dada Aisha pamoja na mme wake siku hiyo hakuja na siku iliyofata mida ya asubuhi na mapema dada Aisha alifika nyumbani na mama alimuuliza.
"Aisha mme wako analalamika kuwa unachelewa kushika ujauzito, unaweza kuniambia ni kitu gani kinachochelewesha!?"
"Mama mimi kiukweli sijui labda mda bado haujafika tu ila hamna mwenye tatizo kati yetu" dada Aisha alimjibu wakati huo mimi nilikuwa ni msikilizaji wa maongezi yao.
"Usinifiche mwanangu sema kama mme wako jogoo wake hapandi mtungi tuangalie namna ya kumsaidie"
"Wala!! yupo vizuri tu kwenye mambo hayo mama hana tatizo lolote lile" dada Aisha alimjibu na baada ya mda aliondoka.
Nilikaa nyumbani kwa siku kadhaa, maisha yangu yalianza kurudi nyuma kwa kasi kwani ata cent sikuwa nayo, Nilitoka nyumbani na kurudi kwenye nyumba niliyokuwa nimepanga na hapo ndipo kasheshe nyingine ilipoanzia kwani mpaka ile hela ya kula nilikuwa nakoswa.
"Mmmh sio kwa ugumu huu wa maisha hapa inatakiwa nifanye kitu tu!" niliongea mwenyewe huku nikipiga miayo kutokana na njaa niliyokuwa nayo, wanasema ukitaka kumuua nyani usimwangalie usoni.
Ugumu wa maisha ulinifanya niwaze kuwa na kazi na sio undugu tena hivyo nilimtumia ujumbe shemeji Rashidi nikiomba msaada wa kunitaftia kazi, niliona bora kumtafta shemeji Rashidi kuliko Kasimu maana mziki wa Kasimu hapana kwakweli! yule anakomesha kwenye kufanya mapenzi.
Shemeji Rashidi siku hiyo hakujibu ujumbe wangu na siku hiyo nililala njaa, asubuhi na mapema niliamka nikiwa na njaa nakuamua kwenda kwa dada Aisha huku lengo likiwa nikupata kifungua kinywa nikiwa huko. Nilimkuta Aisha peke yake na shemeji Rashidi alikuwa ameshaenda kazini.
"Mbona leo asubuhi ivi mdogo wangu!?" Dada Aisha aliniuliza na mimi pasipo kumficha nilimwambia ukweli kuwa usiku uliopita sikula.
"Duh wewe mjinga kweli dada yako niko hapa na shemeji yako yupo unashindwa kutujulisha!?" Dada aliongea kwa kulalamika, kutwa nzima nilishinda nyumbani kwake hiyo siku na nilipotaka kurudi nyumbani kwangu dada alinizuia na kuniambia natakiwa nimsubiri shemeji Rashidi aje kwa ajili ya kufanya nae maongezi.
Mda ulisogea na baadae Shemeji Rashidi alifika, alinitazama pasipo kuongea chochote na baadae walichukuana yeye pamoja na dada na kupelekana chumbani. sikujua ni mambo gani waliyoenda kuongea ila baadae waliporudi dada aliniambia kuwa natakiwa kulala nyumbani kwake na nilipomuuliza hakutaka kuniambia sababu.
Mda wa kulala ulifika hivyo nilienda kwenye chumba alichonielekeza kwa ajili ya kulala, nikiwa bado nautafuta usingizi ujumbe wa shemeji Rashidi uliingia kwenye simu yangu ukiniambia.
"Fatuma dada yako kanisimulia kila nipo tayari kukutafutia kazi kwa mara nyingine" niliusoma ujumbe na baadae niliamua kumjibu kwa kuandika "nitashukuru sana kama utanisaidia"
Baada ya kumjibu nilitaka kuitupa simu pembeni ya kitanda ili nilale lakini kuna sms iliingia ya muamala.
Niliifungua kwa ajili ya kuisoma, sikuamini baada ya kuona pesa imetumwa huku namba ya mtumaji ikiwa ni namba ya shemeji Rashidi.
"Hiyo ni kwa ajili yako Fatuma, usifunge mlango usiku nakuja kulala" shemeji Rashidi alinitumia ujumbe na mimi mapigo ya moyo yalianza kwenda mbio......ITAENDELEA.
Full Tsh1000 namba za malipo ???
0613083801 HALOPESA JINA JOHN BUGUMBA
0755271203 M-PESA JINA JOHN BUGUMBA.